Mwakyembe umechemka, acha kujing'ata ulimi.....

Mwakyembe umechemka, acha kujing'ata ulimi.....

Crucifix

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2011
Posts
1,655
Reaction score
593
KLM wanaposema ndege itaruka saa 11:45 basi tegemea saa11:40 ndege itaanza kutembea tayari kuelekea njia ya kurukia. Haya ndio matarajio ya kizazi hiki. Kama kuna hitilafu, tutatangaziwa ndani ya muda wa kutosha kuwa ile ndege iliyokuwa iruke saa 11:45 sasa itaruka saa 12:45...hakuna longolongo.

Mwakyembe ulisema treni zako zitaanza 'kuruka' Oktoba. Sasa kwa akili ya haraka, kama hujataja tarehe sisi tunachukulia Oktoba mosi. Leo unasema, "Nipeni muda wa miezi sita ili muweze kuona sekta ya reli itakavyokua imekamilika nchini.... "Unataka kutuzuga kuwa sio Dar bali nchi nzima hivyo tuendelee kusubiri kwa matumaini. Hii lugha haipishani na ile ya kiranja wako Pinda ambaye kila siku anakariri, ”tumejipanga........”

Tena unaongeza bila aibu, ”Tuacheni tufanye kazi na nyie endeleeni kutunga ngojera kuhusiana na usafiri wa reli lakini sisi tunajua tunachokifanya kwani niliposema usafiri wa reli unaanza mwezi Oktoba sikumaanisha utaanza Oktoba Mosi kwani hata Oktoba 15 ipo ndani ya mwezi huo huo Ndio lazima tuchonge ngonjera kwa sababu umekuwa mwongo!!! Kama hukumaanisha Oktoba mosi, sema sasa Oktoba ngapi na uache kujing’ata ulimi kwani heshima yako inaanza kushuka kwa kasi.
 
Kikwete na familia yake wanahodhi kampuni kubwa sana ya uchukuzi, je reli ikipona atakula wapi?
 
KLM wanaposema ndege itaruka saa 11:45 basi tegemea saa11:40 ndege itaanza kutembea tayari kuelekea njia ya kurukia. Haya ndio matarajio ya kizazi hiki. Kama kuna hitilafu, tutatangaziwa ndani ya muda wa kutosha kuwa ile ndege iliyokuwa iruke saa 11:45 sasa itaruka saa 12:45...hakuna longolongo.

Mwakyembe ulisema treni zako zitaanza 'kuruka' Oktoba. Sasa kwa akili ya haraka, kama hujataja tarehe sisi tunachukulia Oktoba mosi. Leo unasema, "Nipeni muda wa miezi sita ili muweze kuona sekta ya reli itakavyokua imekamilika nchini.... "Unataka kutuzuga kuwa sio Dar bali nchi nzima hivyo tuendelee kusubiri kwa matumaini. Hii lugha haipishani na ile ya kiranja wako Pinda ambaye kila siku anakariri, ”tumejipanga........”

Tena unaongeza bila aibu, ”Tuacheni tufanye kazi na nyie endeleeni kutunga ngojera kuhusiana na usafiri wa reli lakini sisi tunajua tunachokifanya kwani niliposema usafiri wa reli unaanza mwezi Oktoba sikumaanisha utaanza Oktoba Mosi kwani hata Oktoba 15 ipo ndani ya mwezi huo huo Ndio lazima tuchonge ngonjera kwa sababu umekuwa mwongo!!! Kama hukumaanisha Oktoba mosi, sema sasa Oktoba ngapi na uache kujing’ata ulimi kwani heshima yako inaanza kushuka kwa kasi.
so? ina maana hukumuona alivyohangaika kuhakikisha hiyo tarehe treni zinatembea? au hujui kuwa kutotembea kumetokana na matatizo yaliyo nje ya uwezo wake! btw hizo wiki mbili ndo zinakutoa povu namna hiyo au ufuasi wako wa makundi pinzani yasiyolala kuona Mwakyembe akitekeleza ahadi zake za maendeleo
 
mie nakushangaeni siku zote mlikuwa hamjajua kama huyu ni HOT AIR?

Mimi namjua sana toka enzi zake za pale mnazi mmoja alipokuwa na na ofisi jengo la ushirika na mwenzie aliyeamua kurudi kufundisha UD bwana MVUNGI

Sasa wakati sisi tunaletewa upuuzi wa treni isyo na kichwa wala miguu tazama kule Nairobi na commuter trains zao zilivyo safi na kueleweka

Nairobi-Commuter-Train-Route-Map-rev2.jpg

MTW7h.png

AuDWM9QCIAEnUEM.jpg:large

scaled.php

AuDlaUlCAAIwVYo.jpg:large



[youtube]http://www.youtube.com/watch?feature=player_embedded&v=FbwS8mWJT6U[/youtube]

Syokimau Railway Revolution - YouTube

[youtube]FbwS8mWJT6U[/youtube]


Halafu mnaanzisha thread kuuliza eti wakewnya wamewazidi nini
 
Tafadhali elewa pia Oktoba inaweza kuwa 2013, au hata 2015!
Usafiri ni zaidi ya mabehewa.......miundombinu inabidi iwe tayari na huduma itolewe kwa faida. Stay tuned
 
KLM wanaposema ndege itaruka saa 11:45 basi tegemea saa11:40 ndege itaanza kutembea tayari kuelekea njia ya kurukia. Haya ndio matarajio ya kizazi hiki. Kama kuna hitilafu, tutatangaziwa ndani ya muda wa kutosha kuwa ile ndege iliyokuwa iruke saa 11:45 sasa itaruka saa 12:45...hakuna longolongo.
.

Kizazi hiki cha wapi? Bongo? Wapi kunatokea hivyo?
 
Ni kweli aliahidi October na bado hajafanikiwa kutimiza alichoahidi, lakini angalau tumeona jitihada alizoweka na nia ya dhati aliyonayo. Inawezekana anakwamishwa au amekwama lakini hata jitihada kidogo alizofanya ni sawa na bure? Mawaziri wangapi wamekaa pale kwenye wizara husika hata wazo wahakuwa nalo? Mnyonge mnyongeni lakini ujira wake mpatieni.
 
Mhh mimi sitaki hata kuchangia kuhusu lini inaanza!! Maandalizi tu yanatosha kutuonyesha kuwa hizo ni ndoto!! Maana hatakwenye ile reli iliyopo hatujaona vituo wala platform kwa ajili ya abiria!!!

Mimi nilidhani wanakarabati reli, pamoja na kuweka miundo mbinu japo kiasi ya kuwezesha "commuter train" All we see mabehewa yanapakwa rangi ya nyumba tu, na wanasiasa wana-test route isiyokuwa na vituo!!!

Jamaa zangu walioko bongo wanansema ni maneno tu, kama kawaida!!!
 
Mwacheni wazirir afanye kazi yake. Nadhani wewe ni kati ya wale waliofukuzwa.
 
Mwakyembe nia anayo ila uwezo ndo tatizo.
sema,mwakyembe nia anayo ila riz one yale malori ya mafuta yatafanya kazi gani?
Ezekieli maige naye anamalori yanaenda mpaka kongo nayo je
?
 
Ni kweli aliahidi October na bado hajafanikiwa kutimiza alichoahidi, lakini angalau tumeona jitihada alizoweka na nia ya dhati aliyonayo. Inawezekana anakwamishwa au amekwama lakini hata jitihada kidogo alizofanya ni sawa na bure? Mawaziri wangapi wamekaa pale kwenye wizara husika hata wazo wahakuwa nalo? Mnyonge mnyongeni lakini ujira wake mpatieni.

Hatutaki jitihada, tunataka matokeo ya jitihada! Jitihada bila matokeo ni maneno matupu hayavunji mfupa. Kuna tofauti gani katika maisha ya watu kutokana na jitihada hizo?
 
Mbona jamaa Alishachemsha tokea akatae kusema kuhusu ule ungonjwa wake wa kumomonyoka!!!
anasubiri mda mwafaka wa kutangaza yaliyomkuta [ugonjwa]. naskia anasubiri mpaka 2014 kuelekea 2015 ili amwaribirie mtu ambaye anautaka urais 2015.
 
Kama Mkulu aliyemteua alitoa ahadi ambazo alijua hatoweza kutekeleza unategemea Mwakyembe ataona haya kutupiga kalenda kuhusiana na huu usafiri wa treni?!! Think again.
 
Mbona jamaa Alishachemsha tokea akatae kusema kuhusu ule ungonjwa wake wa kumomonyoka!!!

Huyu jamaa ni mchemfu wa siku nyingi, mnakumbuka hata kwenye ile riport ya Richmond iliyompa umaarufu alikiri kuwa kuna UKWELI ALIOUFICHA ili kuinusuru serikali, tangu hapo mi najua si msemakweli, na hata huko kwa makanisa anakoenda kuomba ni kama kuzuga tu! Kama alishindwa kusema ukweli akiwa nje ya serikali kwa akili ya kawaida ataweza kweli kusema ukweli akiwa ndani ya serikali?
 
Ni mapema mno kuanza kumshutumu Dr Mwakyembe kwa kutoanza kwa usafiri wa treni Dar. Mambo mangapi yamepangwa kufanyika lakini hata dalili hatuioni? Naamini watendaji wengine serikalini wakimpa ushirikiano Dr Mwakyembe soon tutaona matunda ya jitihada zake.
 
Back
Top Bottom