Mwakyembe awamaliza CHADEMA Bungeni!

Mwakyembe awamaliza CHADEMA Bungeni!

Asieee! nimeona mbele giza tu wala hatuwezi kuendelea kwa madharau ya viongozi wetu hawa, inakuaje ata Bungeni Mh Mwakyembe anaweza kumwita Mbunge mwenzie "Msanii kutoka Mbeya"? je nje ya Bunge anaweza kushirikiana na wengine kwa manufaa ya wengine?.

Kweli hatuwezi kuendelea kwa uongozi wa akina Mh Mwakyembe na kampani yake.
 
Kauli ya Dr. imekaa vizuri sana. Kimsingi ndio imezaa debate duniani kote juu ya uhalali wa baadhi ya wasomi. Jiulize Barclays wanajiondoaje Africa wakati tayari wana investments za muda mrefu na za kutosha, ni kwa sababu ya uncertainty yetu na so called wasomi.
Kwamba mtu alimaliza darasa la 12 na mwingine ana degree 10, je ni sahihi kuziangalia hizo degree na leaving certificate yake au tuangalie anachokifanya na kukisimamia!? Jamani tusisahau Daktari huyu naye ni miongoni mwa waliopitisha katiba ya chenge kwa mbwembwe.
 
Mbunge anahitajika kujua kusoma na kuandika. Mnasema ooh hana shule. Tumeona phd za kina Mrema. Uprofesa wa china na korogwe! Hayo ni mapambo tu ya kujikombea leo hii mnaruhusu waalimu waache kufundisha watoto wetu wanakuja kupayuka kwenye siasa. Hiyo phd ya mwakyembe ina tija gani kwenye siasa?
 
Mwakyembe yule wa mabehewa feki nae anajinasibu tumuone mwanasheria mbobezi wakati alikana mpaka alichoandika kwenye Phd yake nimeamini huyu jamaa ni Lumbesa.
 
Kwanza kabisa hakuna shule inayofundisha busara, alafu pia kigezo cha mtu kuongoza watu sio elimu bali ni hekima. Hivi kati ya sugu na mwakyembe nani anayewaongoza wajinga?


Tusibishe tu bwana, sugu karopoka sana
 
Sugu ni lijinga moja lililochaguliwa na baadhi ya wahuni wa mjini, baada ya kuwafanyia vurugu watu wenye hekima ili wasiende kupiga kura.
Duh kumbe watu laki moja waliomchagua sugu ni wahuni basi CCM imeharibu taifa,Mbeya mjini tu wahuni laki moja ndio kusema Tanzania nzima ina wahuni karibu milioni 40 kati ya watanzania milioni 50
 
Mwakyembe amehamishia njaa tumboni,atuambie pia alichomfanyia yule mzee Wa kigamboni
 
Mwalimu wa sheria asiye jua sheria,
rejea posho za wabunge wa Ukawa ukilaza wake ulipojitojeza

Atakumbushwa suala la vichwa vya treni na madai yake CCM walitaka kumkolimba
Jamaa feki
tuliza ball..sio unaandika na hasira. unaona sasa umeandika ugoro. eti unamdharau mwanasheria mahiri kama mwakyembe!
 
Duh kumbe watu laki moja waliomchagua sugu ni wahuni basi CCM imeharibu taifa,Mbeya mjini tu wahuni laki moja ndio kusema Tanzania nzima ina wahuni karibu milioni 40 kati ya watanzania milioni 50
Bangi hizo!
 
Problem is not PHD, standard seven or whatever but the basic problem is PHD ACTIONS are not yet realized than mind-driven, personal interest-driven and slave-serving. I can only pick one action of which was revealed during NBC scandal.
Hivi akisema hivyo akina Lusinde na Stephen Ngonyani wanajisikiaje. Ebu Mwakyembe acha kuwaonea wenzio
 
Sugu hana phd lakini anaweza kuongea la maana kuzidi huyo mwakyembe. Hiv si wale wale waliosoma chemistry kwa kiswahili? Na wana phd? Tofauti iko wap? Bureeee kabisa
 
Asieee! nimeona mbele giza tu wala hatuwezi kuendelea kwa madharau ya viongozi wetu hawa, inakuaje ata Bungeni Mh Mwakyembe anaweza kumwita Mbunge mwenzie "Msanii kutoka Mbeya"? je nje ya Bunge anaweza kushirikiana na wengine kwa manufaa ya wengine?.

Kweli hatuwezi kuendelea kwa uongozi wa akina Mh Mwakyembe na kampani yake.

Hivi anaposema msanii kwa maana ya dharau, anasahau kwenye uchaguzi mkuu CCM ilikuwa inazunguka na wasanii mpaka wa bongo movie nchi nzima?

Mwakembe asisahau kwamba alitaka kugeuzwa kenge akaponea uzi wa sindano
 
Acha mbwembwe Msikilize tena Mwakyembe vizuri halafu linganisha Msigwa, Kubenea, Lema, Mbowe, Mnyika - kwa miaka 8 walihubiri na walituaminisha kuwa Lowasa ni mwizi na fisadi leo kipo wapi?
Ujinga kweli kipaji. Hivyo wewe unaweza kushangaa kuona January hadi April mvua kubwa inanyesha na kuleta mafuriko lakini July hadi November jua Kali linawaka hadi kuleta ukame na maji ya kunywa kukosekana?
Dunia inabadilika kulingana na wakati hivyo hivyo hata watu wake. Kama huwezi kubadilika kulingana na hali halisi wewe ukabaki na msimamo eti nilisema vile nwaka 1980 wewe ni bonge la mpu.mbavu
 
Anamshangaa Mbunge Sugu wa Mbeya ambaye hata Shule hajamaliza na anahoji umahiri wa PhD holder!

Kwa kweli hawa Wabunge wa chadema sijui hiki Chama kinawatoa wapi ni shiida hasa Sugu, Msigwa halafu eti ndiyo diplomat wa chadema!


Sihitaji ushabiki hapa, nami pia nahoji PhD ya waziri wa sheria na katiba, hivi kweli wakati anatoa mwongozo zidi ya wabunge wanaotoka bungeni wakati bunge likiwa linaongozwa na NS kulipwa mishahara na posho....hivi alitoa mwongozo bila kusoma kanuni za bunge? Nahisi hata NS alimshangaa maana wakati akijibu huo mwongozo msomi wetu wa sheria na PhD holder alionekana kama hakuwa anajua kuwa kanuni za bunge hazisemi hayo alokuwa akiyataka.
Nashawishika kukubaliana na Mh Sugu.
 
kubali ukatae Dr Slaa alinunuliwa na pesa ya NIDA na marehemu Gadafi toka kwa Membe, madalali wa Dili walikuwa January Makamba na Nape ambao hawana PhD , wewe ndiyo Umekariri habari za vijiweni na Usomi wako kama Jesca, mbona mkiwa bungeni mnamtumia kibajaji darasa la saba? Kwa taarifa yako wabunge wengi wa ccm wamechukizwa na Kauli ya Mwakyembe maana ni kama amewatukana kijanja.[/QUO Kwa akili hizo mtaendelea kuwa nyumbu tu maana hakuna namna sasa
 
mwakyembe toka aukane ule utafiti wake kuhusu muungano haaminiki tena...
 
Naangalia marudio ya dk45 ITV ya Mh. Lema. Anadai wabunge wana hadhi za kidiplomasia lakini haziheshimiwi. Nadhani hawatambui kwamba wamepewa hadhi hiyo kama kilemba cha ukoka, ili wasahau kwamba chini ya ICCPR (International Convention on Civil and Political Rights) raia wote hawastahili kupigwa au kuzuiwa kushiriki katika masuala ya kisiasa kwa amani.
Kuhusu wabunge wa ukawa kupokea posho wakiwa kwenye mgomo. Ni halali kabisa kwasababu wanafanya walichotumwa na wananchi waliowachagua. Kama CCM hawataki walipwe posho zao wafute vyama vya upinzani. Wabunge wa Ukawa hawapo bungeni kwa posho wala mishahara, wapo pale kwa maslahi ya wananchi, wakati wale wa chama tawala wanajiwakilisha wenyewe, serikali na chama chao. Na ndiyo mana hawaungi mkono hoja ya mawaziri wasiwe wabunge.
 
Back
Top Bottom