Mwakyembe awamaliza CHADEMA Bungeni!

Mwakyembe awamaliza CHADEMA Bungeni!

Anamshangaa Mbunge Sugu wa Mbeya ambaye hata Shule hajamaliza na anahoji umahiri wa PhD holder!

Kwa kweli hawa Wabunge wa CHADEMA sijui hiki Chama kinawatoa wapi ni shiida hasa Sugu, Msigwa halafu eti ndiyo diplomat wa CHADEMA!


Ile tu kutoa na kuanza kubishana ni ukosefu wa weledi na ujinga!! Hoja iko pale pale hasa mwaki-embe alipokana makala yake ya kisomi kuhusu serikali tatu. Wasomi wanakuwa UDSM ila wakiingia bungeni wanageuka zumbukuku wa kawaida tu. Heko Sugu kwa kumpa za chembe huyu msomi mchumia tumbo!!
 
[QUOTE ung'o boy, post: 16434460, member: 160761] Huyo msomi kagundua nin cha maana au katuletea nin cha maana, usikute hata ki IQ kazidiwa basi tu alipata bahati ya kusoma
Msomi huyu aligundua kuwa, Taifa letu laweza kunawiri kwa kukubali kuwa na mfumo wa serikali tatu. Bahati mbaya sana hamkumuunga mkono. Tafuta maandishi yake utalikuta hili.[/QUOTE]
Alilikana andiko lake huyu Mchumia tumbo!!
 
Mwakyembe yupi, au ni Harrison huyu waziri wa sheria aliyeomba mwongozo wa hovyo juzi kuhusu wabunge wa upinzani kunyimwa posho? Kama ni yeye afadhali hata ya Sugu ana uwezo wa kujenga hoja. Mawaziri walio wengi wa CCM ni mizigo.
Mkuu si mawaziri tu ccm wote huwa hawajengi hoja na siyo kwamba hawajui bali hawataki kwa sababu ya kudekezwa na chama dola. Wanajua kuwa watakuwa na back up ya chama na selekali
 
CCM MBONA WANATUZINGUA KWANI SIFA YA ELIMU KUGOMBEA UBUNGE NI KUJUA KUSOMA NA KUANDIKA SASA MASWALI HAYA YANATOKA WAPI
 
Dawa yake ni lissu tu huwa anajificha chini ya viti akisikia saut ya lissu

Siku zote huwa nahoji Udaktari wa Harrison Mwakyembe kama kweli aliupta kihalali au ni kihiyo tu kama alivoingia Jesca binti wa Baba Jesca! Hivi huyu Mnyakyusa anaposema kuwa mtu hakumaliza shule ana maanisha nini? Mbona hajawasema Wabunge wa CCM wenye elimu ya Std VII na wako Bungeni na hoja zao wakizitoa Mwakyembe na Udaktari wake wa kuungaunga ana ziunga mkono???

Mwakyembe huyuhuyu na Kamati yake ya Richmond alilidanganya Bunge kuwa Edo Lowassa(rtd PM)ni Fisadi lakini mpaka leo hii ameshindwa kuwathibitishia Watanzania kuwa Edo Lowassa ni FISADI!!!!
JPM kaingia na gear ya kutumbua Majipu akimkamia EL lakini matokeo yake ameishia KUWATUMBUA MACCM wenzake.
EL bado anapeta na hana hata harufu ya Ufisadi.
Mwakyembe hana lolote baali ni daktari fake!!!!!
 
Hana lolote huyo kasoma nini Yeye? Usomi huo wa kifisadi una faida gani kwa Taifa? Kule Airport alipiga 10% Ujenzi wa majengo mapya na Treni toka mjini hadi Airport, Bandarini alipiga Dili kibao akapenyeza Ukabla akawaajili ndugu zake kibao, PhD za kununua mabehewa Feki, kuchakachua reports ya Richmond hizo zina manufaa gani? Mbona Dr Slaa na prof Lipumba ni Wasomi lakini walirubuniwa na Div four Nape Nnauye pia Div zerooo form six January Makamba, Wanaojiita Wasomi CCM wote ni Mafisadi angalia tabia za Chenge, werema, Tibaijuka, Kapuya, mbilinyi, ngereja na wenzao zinafanana na Tabia za Ally kessy?
Big up mkuu umewaza kwa akili kubwa
 
image.jpeg
image.jpeg
Huyu ndio Daktari wa sheria,mtu aliyeyakimbia machapisho yake juu ya Katiba
Miaka kadhaa iliyopita alikuwa na ngozi kama ya kenge na kupoteza nywele kwa sbb anasema walitaka kumuua "kwa kusema ukweli"
Baadae akaja na ngano za kuwa walitaka kumuuaa pale Ihemi Iringa,akatuambia kuwa kuna Mganga wa kienyeji katikati ya pori la Selous anatumika kumaliza "wapinzani" wa "Mfumo" na yeye wanamuwinda

Baadae akaja kasema anawindwa auwawe.....,Leo anakuja analeta dharau wakati ubunge kashinda kwa nguvu za dola.Booker Washington aliwahi kusema maneno hayo hapo juu.Hivyo kwa vikwazo alivyopitia Sugu katika harakati za maisha na leo wanakutana bungeni wakiwa na Mwakyembe,tena Sugu akiwa mbunge wa Mbeya Mjini toka Chama cha Upinzani ambapo ili uwe mbunge unahitaji kupitia vikwazo vingi vya dola na vyombo vya ulinzi na usalama.Sugu ndio mwenye mafanikio makubwa zaidi ya huyo Dr aliyekana maandiko yake mwenyewe.Booker anasema "Mafanikio ya mtu hayapimwi kwa nafasi aliyonayo,bali kwa kuhimili vikwazo kufikia nafasi aliyonayo"
 
Anamshangaa Mbunge Sugu wa Mbeya ambaye hata Shule hajamaliza na anahoji umahiri wa PhD holder!

Kwa kweli hawa Wabunge wa CHADEMA sijui hiki Chama kinawatoa wapi ni shiida hasa Sugu, Msigwa halafu eti ndiyo diplomat wa CHADEMA!


Teeeeeeeeh teeeeeeeeh, vipi kuhusu maji marefu alimaliza wapi?
 
Kwanza kabisa hakuna shule inayofundisha busara, alafu pia kigezo cha mtu kuongoza watu sio elimu bali ni hekima. Hivi kati ya sugu na mwakyembe nani anayewaongoza wajinga?
Mwakyembe
 
PhD ukiwa CCM, huwa haifanyi kazi..!!! Wengi ni wachumia tumbo
 
Mwakyembe ni JIPU Sugu lililomshinda Magufuli, hana Taaluma kichwani bali kutokana na kukaa mda mwingi na wanasheria kakariri vifungu muhimu muhimu ili kujikinga na wachambuzi wasimshitukie kuwa Elimu yake ni ya kuunga unga, PhD feki iliyonunua mabehewa feki.
 
Back
Top Bottom