Katika siku za karibuni, kumekua na watu kadhaa ambao wamekua wakimzulia KIFO Naibu Waziri wa Ujenzi na Mbunge wa Kyela, mpambanaji Dk. Harrison Mwakyembe. Baada ya taarifa hizo, watu wa karibu na mwanasiasa huyo ambaye ugonjwa wake umehusishwa na madhara yatokanayo na sumu, wamezungumza naye mara kadhaa jana na leo na kubaini kama ni mzima na afya yake inazidi kuimarika na kuwa bora zaidi ya siku anakwenda India kwa matibabu. Mmoja wa aliyezungumza naye alisema;
"Kuna post imetumwa jamii forums kwamba dr mwakyembe amefariki sio kweli, nimeongea naye kama dk ishirini zilizopita." "Dk. Anasema kwa sasa ukimuona utashangaa maana amepata nafuu ajabu."
Moani yangu: Wana JF, Mwakyembe ni binadamu na kama kiumbe yeyote hawezi kuishi milele duniani, lakini hiyo si sababu ya kumzushia mtu mauti angali hai. Wale wote wanaofanya hivyo kwa nia mbaya wajue hakuna aliye juu ya Mwenyezi Mungu na kwamba kila nafsi itaonja mauti na tumekuja kwa udong na tutarudi kwa udongo. Taarifa za msiba hazipaswi kuwa hisia bali kutoka kwenye vyanzo mahsusi.
Kwa nini aliisoma nusu report ya Richmond? . Shame on him.
Acha kupima upepo! Nikisema muniyo munyokwe utaanza kulalamika. Tumeshaukataa huu upumbavu wa kupost taarifa zisizo na source!
Haya ni matusi makubwa sana! jamani JF inaelekea wapi?
Acha kupima upepo! Nikisema muniyo munyokwe utaanza kulalamika. Tumeshaukataa huu upumbavu wa kupost taarifa zisizo na source!
kweli Pasco,sasa hivi makapi yamekuwa mengi! Lkn pia naona itakuwa ngumu kidogo maana JF sasa imefahamika zaidi na yanaingia makundi ya aina mbali mbali! Halisi asante kwa taarifa Mungu azidi kumrejesha Mwakyembe
Mwakyembe ni MNAFIKI MKUBWA, HANA TIJA KWA TAIFA LETU.Pengine tunaweza kumshukuru Mungu, Mbunge wa Kyela Dr. Harrison Mwakyembe anaweza kutinga ofisini Jumatatu kupiga Mzigo. Mwakyembe sasa umepona njoo toa nusu ripoti ya Richmond iliyobaki, tumechoshwa na tambo za mafisadi.
Wana JF, Nimepost hiyo thread kwa nia nzuri, Chanzo cha habari ninacho, kama mtu alikuwa anahitaji angeweza kuomba nikarudi kuleta taarifa zaidi. Ila KWA MATUSI MAZITO ALIYONITUKANA MWANA JF MWENZANGU MUNGI....... Ninafikiri zaidi uamuzi wangu wa kuendelea kutumia JF, Maana itakuwa haijengi watanzania badala yake wote tunaonekana wahuni tu. Watu makini fuatilieni magazeti ya kesho kama hamtaiona habari hiyo kwenye kurasa za mbele. MUNGI UMENITOLEA MATUSI KUTUKANA MATUSI MPAKA YA WAZAZI...... KWA BUSARA NAKUSAMEHE, NAJUA IPO SIKU MUNGU ATAKULIPA.
Habari njema kwa kuwasili huyu MNAFIKI?Kama amerejea na afya yake imeimarika hii ni habari njema. Tunashukuru kwa taarifa.