Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,720
- 21,779
SERIKALI imesema hali ya afya ya Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe, inaendelea vizuri na bado yupo nchini India akiendelea na matibabu.
Hayo yalisemwa Dar es Salaam jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Blandina Nyoni mara baada ya kuulizwa na waandishi wa habari juu ya hali ya Waziri huyo.
Kila siku huwa naongea naye kwa njia ya simu na amenihakikishia mwenyewe kuwa anaendelea vizuri na matibabu yake na kwamba hali yake ni nzuri, alisema Nyoni.
Hata hivyo, aligoma kuzungumzia nini hasa kinamsumbua Waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Kyela na kueleza kuwa hairuhusiwi kimaadili kuweka hadharani ugonjwa wa mtu kwani ni siri yake na familia yake.
Pamoja na hayo, Dk. Mwakyembe anadaiwa kusumbuliwa na ugonjwa wa ngozi unaomsababishia uvimbe katika baadhi ya maeneo mwilini mwake na kitaalamu ugonjwa huo unajulikana kama Exfoliative Dermatitis.
Ugonjwa huo unadaiwa kuathiri wanaume na wanawake wenye umri kuanzia miaka 55 na dalili zake ni kuwashwa, mwili kuishiwa nguvu na sehemu ya juu ya ngozi kupukutika.
Dk. Mwakyembe aliondoka takribani wiki moja iliyopita kwenda Hospitali ya Apollo iliyopo Chenai nchini India kwa ajili ya matibabu kufuatia hali yake kuzidi kuwa tete.
Hayo yalisemwa Dar es Salaam jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Blandina Nyoni mara baada ya kuulizwa na waandishi wa habari juu ya hali ya Waziri huyo.
Kila siku huwa naongea naye kwa njia ya simu na amenihakikishia mwenyewe kuwa anaendelea vizuri na matibabu yake na kwamba hali yake ni nzuri, alisema Nyoni.
Hata hivyo, aligoma kuzungumzia nini hasa kinamsumbua Waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Kyela na kueleza kuwa hairuhusiwi kimaadili kuweka hadharani ugonjwa wa mtu kwani ni siri yake na familia yake.
Pamoja na hayo, Dk. Mwakyembe anadaiwa kusumbuliwa na ugonjwa wa ngozi unaomsababishia uvimbe katika baadhi ya maeneo mwilini mwake na kitaalamu ugonjwa huo unajulikana kama Exfoliative Dermatitis.
Ugonjwa huo unadaiwa kuathiri wanaume na wanawake wenye umri kuanzia miaka 55 na dalili zake ni kuwashwa, mwili kuishiwa nguvu na sehemu ya juu ya ngozi kupukutika.
Dk. Mwakyembe aliondoka takribani wiki moja iliyopita kwenda Hospitali ya Apollo iliyopo Chenai nchini India kwa ajili ya matibabu kufuatia hali yake kuzidi kuwa tete.