Mwakyembe anasikitisha! Walaaniwe wanaohusika!

Mwakyembe anasikitisha! Walaaniwe wanaohusika!

Mara nyingi UONGO hausemwi hadharani tena mbele ya Waheshimiwa miatatu na ushei hivi. Uongo, kama yalivyo MAOVU mengine yote hayafanyiki hadharani.

Hivi yale yoote JK alipohutubia bunge ambayo hajayatekeleza sio alisema UONGO?
 
Kuumwa aumwe Mwakyembe, halafu ripoti ya ugonjwa itoe serikali! nadhani hizi tamthilia nyingine Mwakyembe atafute pa kuzipeleka, kwahiyo yeye Mwakyembe mpaka leo hajui alikuwa anatibiwa nini India? unafki mwingine mbaya sana.

siyo kwamba anaogopa watammalizia? Siri apeleke benki,au kwa mwanasheria,au mkewe. Iwe katika mfumo wa CD. Na itolewe siku atakayoona ye Mwakyembe inafaa.
 
Hivi siku anatua toka India hakuna aliyeweza hata kumpiga picha? maana haya maneno yakuwa nimesikia nimesikia, majungu mengiu hapa JF, tuleteeni tumuone na tuteme cheche kama dalili ni za kkuwekewa sumu au kakanyaga high voltage who knows? Isije kuwa wanasingiziwa watu bila sababu
 
Kusema ukweli, ufisadi umeimaliza si nchi tu bali pia watu wake... Bado tuna kazi kubwa ya kuwang'oa mafisadi hawa.
 
....Halafu cha kushangaza hadi sasa Serikali haijatia hata neno kama inachunguza ugonjwa huu wa ajabu unaosemekana umetokana na kupewa sumu au la. Kama inachunguza kwanini inaogopa hata kuwafahamisha Wananchi kwamba uchunguzi wa yaliyompata Mwakyembe unaendelea? Kwa nini kumekuwa na kimya kizito toka Serikalini?
Mkuu BAK,

Tatizo hapa kwaukweli si kuchunguza, tatizo hapa ni taarifa za madaktari zenye kuonyesha nini haswa kinamsibu ama kilimsibu.

Tatizo la huyu mwanasiasa, ni siasa kwenye kila kitu hadi maisha yake.

Kutupiana mpira na serikali kuhusu utoaji taarifa za daktari kuhusu yanayomsibu ni tatizo kubwa zaidi kwa Mwakyembe yeye binafsi, familia yake na wafuasi wake.

Wewe mtu maisha yako yako kwenye hati hati halafu bado unatupiana mipira ya kisiasa na serikali?

I feel bad for him, but on the other hand sorry for him...
 
hivi unajua ni kwa nini amerushwa nchini??
Either atakuwa amepata nafuu na hivyo madaktari kuona kwamba anaweza kurudi nyumbani na kuendelea na prescriptions bila uhitaji wa daktari

OR pia inawezekana kwamba wamemrudisha kusubiri kifo, it can be either or...

Or the combination of both.
 
Tanzania hatuna sense of privacy wala dignity kwa wagonjwa, mtu unaenda kumuangalia mgonjwa halafu unakuja kuwaambia waandishi wa habari "jamaa kanyonyoka nywele, kope, ndevu mpaka...." na waandishi wanaandika.

Ndiyo maana wengine wanaona gozigozi, hamna mtu zaidi ya close friends and family kujipendekeza.
Ndo consuquences za a public office, people will always demand every bit of information pertaining those public figures.

This has been going on for centuries now.
 
Wale watu wa upako ndo mnapaswa kuonesha cheche zenu, Wanene kwa lugha, ili Mungu amponye mtumishi wake, otherwise, wana maombi huyu mtu asipopona tuna jua huwa mnafanya usanii
 
Dr bdo mda unao, mungu pekee ndio kimbilio lako kwa sasa, jina la Yesu limejaa uponyaji hakuna kinachoshndkana kwake, hebu thubutu kuliitia jina hlo.
 
Kuumwa aumwe Mwakyembe, halafu ripoti ya ugonjwa itoe serikali! nadhani hizi tamthilia nyingine Mwakyembe atafute pa kuzipeleka, kwahiyo yeye Mwakyembe mpaka leo hajui alikuwa anatibiwa nini India? unafki mwingine mbaya sana.

Nijuavyo Mwakyembe alipelekwa na serikali tena kwa wadhifa wake wa uwaziri. Kudhihirisha hilo, hao wana - Apollo majibu wakatoa kwa Serikali na hiyo haimaanishi Mwakyembe hajui alichotibiwa. Sasa kwa kuwa serikali ilimpeleka waziri wetu, basi wananchi tunataka tupewe taarifa ya ugonjwa na mustakabali wa hali yake. Usisahau kuwa jambo hili ni muendelezo wa matukio kadhaa yenye utata yaliyomhusu Mwakyembe na ambayo mengine aliyaripoti polisi. Kwa hiyo jambo hili lina public interest, kukaa kimya na kujifanya hawajui au hawawajibiki hiyo si dalili nzuri kwa image ya serikali mbele ya jamii. Naipenda mno nchi yangu, ila huku tuendako kuna dalili ya kiza kinene.
 
DR. Na dr waziri waligonga kikombe semunge
na prof. Pia manake kama siri ni hii kunywa ya magonjwa sugu bila kusema unaumwa nini mpaka mkimbilie dawa,
 
Jamii yote ya watanzania inajua kwamba serikali ina mkono katika lile lililomkuta Dr.Mwakyembe,kwa hiyo haiwezi kutoa taarifa ya ugonjwa unaomsibu.itakuwa aibu kubwa.Ni bora shari kidogo kuliko shari kamili.Naomba mkumbuke kwamba sasa Mwakyembe anaiogopa serikali kama ukoma,kwahiyo hawezi tena kuwa kinyume nayo.
Mwakyembe(18).jpg

Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe.



SerikaliI imekataa kutoa taarifa ya ripoti iliyopewa na madaktari bingwa wa Hospitali ya Apolo, India ambao walimtibu Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Blandina Nyoni, alipoulizwa kuhusiana na ripoti hiyo, alisema kuwa suala hilo haliwahusu na kama wameipokea hawezi kuzungumzia suala hilo.

Alisema Dk. Mwakyembe ndiye anaweza kuzungumzia na hajui kama imepokelewa au la.
“Hata kama tumeipokea sina ruhusu ya kuzungumza na kama hiyo ripoti yake mfuate mwenyewe Dk. Mwakyembe akueleze

kwani sisi hatuwezi kutaja ugonjwa uliokuwa unamkabili,” alisema Nyoni.
Akizungumzia hali ya Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Cyril Chami. ambaye alikuwa India kwa matibu, alisema kuwa hali yake inaendelea vizuri, lakini alisema hana taarifa za kurejea kwake.

Hivi karibuni, Dk. Mwakyembe alisema hospitali ya Apollo alikokuwa amelazwa alikuwa, imetuma ripoti kwa serikaali ya Tanzania kueleza walichobaini baada ya kumfanyia uchunguzi.



CHANZO: NIPASHE
 
Shangazi yangu wakati ameugua ugonjwa wa U.K.I.M.W.I alikua anafanana hivyo hivyo,kutoka unga,nywele,mba etc mpaka mauti yanamkuta.
 
sasa kama Mama Nyoni anasema kuwa habari za ugonjwa wa Dr. aulizwe yeye mwenyewe Dr. wewe Dr unaona ugumu gani kusema? si uweke wazi tu? ama unasubiri hadi waje tena kukupa kitu kingine na kukumaliza ndio utasema?

sema Dr wakati ndio huu,kumbuka kuwa pale muhimbili walidanganya wakakueleza kuwa unakisukari,ingawaje Daktari mmoja tu ndie aliyeweza kusema kuwa aliona chembechembe za sumu ktk damu yako,sasa unaogopa nini kusemaaaaaaaaaaaa?

sema Dr semaaaaaaaaaaaaa
 
Serikali Tawala itakaa kimya kweli? inaogopesha kupata cheo ndani ya serikali ya Kikwete
 
ugonjwa wa mtu ni suala personal, haina uhusiano na siasa.
 
ndugu zangu mmemwona mwakyembe huo ndoo mtandao wa mafisadi masikini ndugu yangu mwakyembe anasikitisha sana rani sisi sote tutaonja mauti kama kweli kunamtu anamsababishia mwezie hiyo hali amini nawambieni hiyo rana itamrudia mwenyewe alio fanya hicho kitendo na araniwe chadema oheeeeee😛oa
 
Siasa imemfanya mbaya Dr.

Baadhi ya watu ni nyang'au kabisa yani wanadiriki kujaribu kuua mwenzao sababu ya siasa. Malipizi yao ni hapa hapa duniani.
 
Back
Top Bottom