Mwakyembe anasikitisha! Walaaniwe wanaohusika!

Mwakyembe anasikitisha! Walaaniwe wanaohusika!


Kama ilivyosemwa hapo awali, ugonjwa wa mtu ni siri yake na daktari wake. Kuhusu jinsi Mhe. Mwakyembe anavyoonekana katika picha, hata kama anaonyesha amezeeka, hatuwezi kutegemea mtu aliyelazwa hospitali kwa muda, na labda akilishwa vyakula asivyozoea, aonekane na sura yake ya kiafya, mara anapotoka hospitali.

WanaJF tuendelee kumtakia afya njema huyu mpinga mafisadi; na mimi binafsi nakutakia mapumziko mema, Mheshimiwa, wakati huu wa Siku Kuu ya Krisimasi na Mwaka Mpya; ukijiandaa kwa mapambano na mafisadi.
 
wakuu,ni kweli jamii forums imeshinwdwa kutambua nini jamaa kimemzeesha? hapana bwana ngoja nilifuatilie kwa ukaribu hili swala nitakuja baadae tena!
 
attachment.php
Ugonjwa wa kisasa!!!
Babu kashindwa sasa wanaelekea India kuhusisha sumu!!!!!!!!!!
 
whatever the case, ninachojua Bwana atawapigania nasi tutanyamaza kimya, anayejiita Maflme basi na Aishi milele ili auone mkono wa Bwana wa Mwakyembe! Halleluya!!!!.
 
iiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii nalia mimi,huyo ndio basi tena,swala la kupona halipo hapo Madaraka jamani matamu,ila watu hawamwogopi mungu bana

Potea na uchuro wako!Mheshimiwa Mwakyembe amepona,yupo nyumbani TZ:lol:
 
Naamini kabisa kwamba Dr. Mwakyembe aliongoza Kamati Teule ya Bunge dhidi ya Richmond & Dowans huku akijua kwa hakika kwamba anajiweka katika hatari kubwa. Alifanya uamuzi wa kusema ukweli mwingi (hata kama si ukweli wote) dhidi ya Richmond & Dowans na wahusika wake akijua hakika kuwa anajitoa muhanga. Mnaweza kunisahihisha ktk usemi huu - [Kelele dhidi ya Richmond&Dowans ndiyo ilikuwa kelele kubwa ya kwanza dhidi ya Ufisadi hapa Tanzania. Hapakuwahi kuwa na kelele kubwa hapa TZ dhidi ya Ufisadi kwa kiwango cha sakata la Richmond+Dowans'. Rich+Dowans ilipigiwa kelele na watu mbalimbali tangu bungeni hadi mitaani bila kujali dini, kabila wala ushabiki wa vyama vya siasa. Upinzani dhidi ya Richmond&Dowans ndio umetupa wa-TZ funguo za kupiga kelele kubwa dhidi ya ufisadi mwingine. Kabla ya Richmond&Dowans wa-TZ wengi sana tulikuwa waoga na wakimya wa kusema dhidi ya Ufisadi na wasiokuwa na taarifa (yaani wajinga) kuhusu Ufisadi uliokuwa ukiendelea nchini]. Baada ya usemi huu, napenda kusema kuwa Dr. Mwakyembe amekuwa Icon, Alama, Banner ya vita dhidi ya Ufisadi Mkubwa Mkubwa hapa TZ. Amekuwa Revolutionalist dhidi ya Ufisadi Papa.

Ili kupambana na uovu duniani iko haja ya mtu au watu kujitoa muhanga (knowingly or unknowingly). Mabadiliko hayaji isipokuwa kwa kujitoa muhanga. I am not a historian but remember Martin Luther King Jr, Nelson Mandela, Edward Moringe Sokoine, Horace Kolimba, Samora Machel, etc. (For Christians - Na katika ulingo wa kiroho ilipasa mtu/watu kujitoa sadaka kuleta mabadiliko - remember Jesus Christ-who died for change, Stephen of the Book of Acts who died of stoning, and many other prophets in and out of the bible.

In my opinion, Dr Mwakyembe na wote walio naye ktk vita hii walijitoa muhanga kuleta mabadiliko. Na baada ya wao kujitoa muhanga maisha yao ni HAKIKA mabadiliko yatakuja. Pasipo kujitoa muhanga HAKUNA MABADILIKO yanayoweza kufanyika.

Naomba tusifanye mzaha ktk suala la afya ya Dr. Mwakyembe na pia ktk hatari inayowakabili walio mstari wa mbele kuleta mabadiliko e.g. Samwel Sitta, Dr. Slaa, Wanaharakati e.g. Lugemeleza Nshala, na wengi wengineo-siwafahamu wote.

Suala la Dr. Mwakyembe ni suala la Ki-Mungu. Ni wangapi kati yetu tulitarajia Dr. Mwakyembe angerudi hai - whatever the condition of his body? Waliomfanyia walichomfanyia watakuwa wametaharuki kwa yeye kurudi hai. Mtu mmoja mnyakyusa aliye karibu na'inner cycle' ya CCM aliyemwona Dr Mwakyembe kabla hajakwenda ktk matibabu alisema 'Dr Mwakyembe hawezi kurudi hai'. Lakini karudi. Kama atarejesha afya yake ya awali au la sijui lakini angalau anaweza kutumia ulimi na akili yake.

Nawaonya wanaopambana na Dr. Mwakyembe na wanaokandamiza haki za walio wengi ya kwamba mnapambana na nguvu za Mungu aliye Hai, hampambani na nguvu za kibinadamu. Na hamtaweza kushinda ktk hili. Siku baada ya siku, your grip on power is being eroded. And in the end you will fall down.

Ile mvua iliyojaza ma-bwawa mwaka 2005 (kama sijakosea) na kusababisha watu kuhoji kwa uchungu dhidi ya mkataba wa Richmond/Dowans ilikuwa mvua ya Ki-nabii (sorry to non-christians). I repeat 'Ilikuwa mvua ya ki-nabii'. Serikali ilitangaza kuwa kutakuwa na njaa Tanzania kwa sababu ya ukame lakini after sometime the rains came and the whole country was turned 'green'.

God is with you Dr. Mwakyembe and all who love and practice righteousness.

WATCH OUR FOR NEXT ARTICLES.
 
kwa mwonekano huu, anafaa kuwa rais, utadhani sata, zuma na wenzao wakongwe?
Umeona eeh? Halafu atakuwa anasalimu watu akiwa kavaa gloves. Majamaa wali m time vibaya. Mungu amsaidie.
 
Mwakyembe(18).jpg

Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe.



SerikaliI imekataa kutoa taarifa ya ripoti iliyopewa na madaktari bingwa wa Hospitali ya Apolo, India ambao walimtibu Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Blandina Nyoni, alipoulizwa kuhusiana na ripoti hiyo, alisema kuwa suala hilo haliwahusu na kama wameipokea hawezi kuzungumzia suala hilo.

Alisema Dk. Mwakyembe ndiye anaweza kuzungumzia na hajui kama imepokelewa au la.
“Hata kama tumeipokea sina ruhusu ya kuzungumza na kama hiyo ripoti yake mfuate mwenyewe Dk. Mwakyembe akueleze

kwani sisi hatuwezi kutaja ugonjwa uliokuwa unamkabili,” alisema Nyoni.
Akizungumzia hali ya Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Cyril Chami. ambaye alikuwa India kwa matibu, alisema kuwa hali yake inaendelea vizuri, lakini alisema hana taarifa za kurejea kwake.

Hivi karibuni, Dk. Mwakyembe alisema hospitali ya Apollo alikokuwa amelazwa alikuwa, imetuma ripoti kwa serikaali ya Tanzania kueleza walichobaini baada ya kumfanyia uchunguzi.



CHANZO: NIPASHE
 
Kuumwa aumwe Mwakyembe, halafu ripoti ya ugonjwa itoe serikali! nadhani hizi tamthilia nyingine Mwakyembe atafute pa kuzipeleka, kwahiyo yeye Mwakyembe mpaka leo hajui alikuwa anatibiwa nini India? unafki mwingine mbaya sana.
 
Kuumwa aumwe Mwakyembe, halafu ripoti ya ugonjwa itoe serikali! nadhani hizi tamthilia nyingine Mwakyembe atafute pa kuzipeleka, kwahiyo yeye Mwakyembe mpaka leo hajui alikuwa anatibiwa nini India? unafki mwingine mbaya sana.

Ukweli utabaki kuwa ukweli. Na mojawapo ya sifa za uaminifu ni kusema ukweli daima. Mwakyembe siyo mkweli na hivyo siyo mwaminifu, kila kitu kinachomhusu hawezi kuweka wazi kama kilivyo, rejea ripoti ya richmond hakusema ukweli wote. Mambo mengi aliyaficha yanayoligharimu Tz mpaka kesho. Kutosema ukweli kwake unadhihirisha namna huyu bwana asivyokuwa mwaminifu wala mzalendo. Mwakikyembe aache mambo ya siasa uchwari awaambie Watz sumu aliyolishwa ni ya aina gani, na kwa nini hasa alilishwa, aweke mambo hasarani ili wanasiasa wengine wachukue tahadhari kabla ya hatari!
 
Dr. Mwakyembe atuambie ripoti ilipelekwa serikalini ili iweje? Je, ni serkali ilihitaji ripoti kwa sababu iligharimia matibabu yake au ni utaratibu wa kawaida? Kama yeye ana nakala ya ripoti aitumie kuteleza sisi Watanzania ( kama ataona kwamba ni sawa). Njia nyingine awape waandishi wa habari watajua namna ya kutufikishia ujumbe.

Kikubwa tunachojua ni kuwa ugomjwa ni siri ya mgonjwa na daktari sasa kama serikali imepewa taarifa na kukaa nayo kimya basi ujue kuna makubwa katika hilo ambalo serikali haitaki tulijue na hakuna maana kwa Dr. Mwakyembe kutupiana mpira na serikali. Kama ndiyo hiyo sumu basi yanawahusu yeye na mafisadi wenzake.
 
Mambo mengine tunachokonoa ambayo hata kwa akili ya kawaida si kitu cha kumwaga hadharani. Ugonjwa huwa siri ya mtu na madaktari wake. Na watu wengine wenye nafasi ya kupewa taarifa ya ugonjwa ni ndugu wa mgonjwa kama daktari ataona inafaa, na mara nyingi hili halifanyiki isipokuwa kama ni mtoto kwa vile anakuwa chini ya uangalizi wa wazazi wake. Mwakiembe ni mtu mzima na kuambiwa kiini cha ugonjwa wake ni busara ya doctor wake, na serikali kupewa taarafa ya ugonjwa kama mwajiri wake ni jambo ka kawaida po pote.

Mwakiembe mwenyewe kwa taadhima ya kazi yake hakupaswa kuirushia kombora serikali kwa kuujulisha umma kwamba riporti ya ugonjwa wake imetumwa serikali ni makosa, hakupaswa kufanya hivyo. Na kama ugonjwa wake umeingilia au kuhusisha mfumo wa usalama au baadhi ya usalama nchini kuhusishwa na kiini cha matatizo ya ugonjwa wake basi ingekuwa ni busara ya Dotor kuwaeleza waajiri wake, na ni jukumu la mwajiri wake kuchukulia hatua kama itafaa, na kama Mwakiembe mwenyewe amepata taarifa hiyo kwa ridhaa yake binafsi na kama anaona shaka mazingira ya kuugua ana haki ya kutoboa siri si kwa kushinikizwa na watu. Wagonjwa wengi tu wamepelekwa India kutibiwa nakuna riporti iliyoainishwa kwa wananchi, maana mambo ya matibabu ni siri za mjonjwa na doctor pamoja na wauguzi na kupewataarifa mwajiri wake ni dhana inayoeleweka.

Doctor hawezi kuanika siri za ugonjwa wa mtu hadharani, na hata inapobidi kutoa taarifa kwa wahusika kama waajiri ambao ni serikali huwa ni siri inayotumwa kwa sealed emvelope. Kuna mambo mengi ya muhimu kujadili, lakini hili la kutangaza au kutoboa siri za ugonjwa wa Mwakiembe ni kuingilia mambo ambayo ni siri za kitaalam kwa wauguzi na tunajaribu kupenya ndani ya mwajiri aanike siri za waajiriwa ni kosa linalotakiwa kuepukika. Si kila kitu kianikwe hadharani, kuna mengi ambayo ni siri za kiofisi, maana mengie ambayo si skendo za hadharani ni siri za ofisi na wanataratibu zao.
 
Dr.Mwakyembe ana siri nzito ndio ujumbe niliousikia ktk vichwa vya habari leo magazetini

Dr.weka wazi kabla chochote kile hakija tokea

maana wanadai sio makyembe yule tumjuaye
1.kucha zake ni nyeusi
2.miguu na mikono ina magaga ambayo hutoa damu na kusababisha maumivu makali
3.kope hazina nywele zote zimepunyuka
4.kichwani hana nywele zimepukutika zote
5.anaongea vizuri sana kama mzima lakini mda wote kava kofia,suruali,shati mikono mirefu,groves na soksi miguuni

HUJAFA HUJAUMBIKA
 
Basi kama ni siri abaki nayo mwenyewe...Asithubutu kuivujisha..Hata mkewe asijaribu kumtonya!
 
Back
Top Bottom