Mwakyembe anasikitisha! Walaaniwe wanaohusika!

Mwakyembe anasikitisha! Walaaniwe wanaohusika!

Mimi simuelewi Dr. Mwakyembe anaogopa nini kusema kile walichomtenda mafisadi wakati wameshammaliza? Wao wamemwaga ugali naye amwage mboga kwani kwa hali aliyofikia ni bora wammalizie kuliko mateso anayoyapata.
 
Wewe ongea kama umechanganyikiwa ila LAANA ya Watanzania millioni 45 ni kubwa sana! Hata mkimsingizia EL haisaidii. TUBUNI kwa waTanzania.
WAUAJI ndio wanapaswa KUTUBU. Na hakika laana itawaangukia wakati wowote kuanzia sasa. Take my word.
 
Dr, hatimaye inafaa iuambie umma wa waTz kile kinachokusumbua, iwe ni sumu, au vinginevyo.
Wewe una maadui wengi wafujaji wa mali na maliasili zetu.
Ni muhimu kuwaambia waTz kuhusu ugonjwa wako ili hata ikitokea ukaondoka (nasali ili isitokee, ila sote tutaondoka hatimaye) uwe umetuachia urithi kwa kutueleza ukweli, ili hao waliokuhujumu wasifaidi matunda ya ubaya wao.
 
tulisikia anajua kila kitu kinachoendelea,kama ameamua kukaa kimya kulinda chama chake na kujipendekeza kama ilivyo kawaida yetu ataenda kusemea huo ukweli kaburini
Ninawasiwasi na wewe ni mmojawapo wa wahusika wa kumzuru shujaa wetu!, lakini huwajui wazee wa kyela.
 
mi naamini tiba za hospital zimegonga mwamba kulingana na hii taarifa ya sasa, mi namwomba mh. Mwakyembe atumie tiba hii AENDE KWA MZEE WA UPAKO natumaini atapona mapema.
Lakini ni swala la kiimani zaidi kama hapendezwi na wazo langu sio mbaya.
 
MUNGU amponye dr Mwakyembe,ili aeleze aliyo yaficha kwenye ripoti ya RICHMOND,"Kwa heshima ya serikali"
Pole sana mheshimiwa
 
WAUAJI ndio wanapaswa KUTUBU. Na hakika laana itawaangukia wakati wowote kuanzia sasa. Take my word.

Niambia mpaka sasa LAANA imempata nani? aliyewadanganya watanzania millioni 45 au anayesingiziwa mambo asiyohusika?
LAANA mnayo TUBUNI.
 
Nimetokwa machozi nilipoona picha ya Mh Mwakyembe gazeti la mwananchi ya leo akizungumza na Sitta akiwa bado hosipitalini. Mwli wake umekuwa kama nyoka. Kama ni watu walimpa sumu ili watu wapate madaraka walaaniwe

Picha kubwa: https://www.jamiiforums.com/attachment.php?attachmentid=41762&d=1321869350

sasa unatoka na machozi yanini???kama sio unafiki>>>nenda muhimbili pale uone zaidi na ulie kama unavyojifanya ulilia hapa.....acheni unafiki....uko mkavu hapo ulipo
 
Mara nyingi UONGO hausemwi hadharani tena mbele ya Waheshimiwa miatatu na ushei hivi. Uongo, kama yalivyo MAOVU mengine yote hayafanyiki hadharani.

Wildcard nawe sometimes unachekesha.

Marais au wabunge wakiomba kura wakati wa UCHAGUZI si huwa wanawadanganya wananchi? UONGO wao wanasemea chumbani?. Kampeni zinafanyika chumbani?
 
Tanzania hatuna sense of privacy wala dignity kwa wagonjwa, mtu unaenda kumuangalia mgonjwa halafu unakuja kuwaambia waandishi wa habari "jamaa kanyonyoka nywele, kope, ndevu mpaka...." na waandishi wanaandika.

Ndiyo maana wengine wanaona gozigozi, hamna mtu zaidi ya close friends and family kujipendekeza.

Where is Right to Privacy, Right to dignity??? or Right to access and freedom of expression prevailed over the former rights?
Censorship obligation is upon whom???
 
MUNGU amponye dr Mwakyembe,ili aeleze aliyo yaficha kwenye ripoti ya RICHMOND,"Kwa heshima ya serikali"
Pole sana mheshimiwa

mpaka sasa anaweza kuongea vizuri tu...naweza hata kunyanyuka na kuweka cd yake jinsi alivyokuwa anatibiwa huko india kwenye dvd player...anaongea vizuri tena kwa sauti safi kabisa......kwa sasa anaweza kabisa kusema hizo siri kama zipo..awaite waandishi wa abari kwake ili aseme......lakini kwa aliofikia hapo hatasema tena kitu maana alishakosea tangu wakati ule kukaa kimya....

hivi unajua ni kwa nini amerushwa nchini??
 
tulisikia anajua kila kitu kinachoendelea,kama ameamua kukaa kimya kulinda chama chake na kujipendekeza kama ilivyo kawaida yetu ataenda kusemea huo ukweli kaburini

Ndo ukweli. Kwa vyovyote anajua matokeo ya hali yake kuwa yatakuwaje. Ikiwa asilimia kubwa anajua kuwa ni sumu na hatapona ni vizuri kuikubali hali hiyo. Na ukishakuikubali hali hiyo ni kujitangaza hadharani kuwa chanzo cha shida yako nini au ni akina nani.
Mbona tunahimiza waathirika wa ukimwi wajotangaze kuwa ni waathirika.Vivo naye ajitangaze rasmi kwa kuuambia Umma sababu ya ugonjwa wake, chanzo cha ugonjwa wake, na nani wanahusika na ugonjwa wake.
Hapo hata kama ikitokea amekufa atakuwa amekifa kizalendo zaidi na kama alisema mwenzetu atabaki kuwa mtu shujaa na tutavaa tishet zenye picha yake n.k.
Asiogope, dawa ni kujilipua hadharani, mimi niko hivi kwa sababu ya hivi kwa vile wale wametaka niwe hivi.
 
Wildcard nawe sometimes unachekesha.

Marais au wabunge wakiomba kura wakati wa UCHAGUZI si huwa wanawadanganya wananchi? UONGO wao wanasemea chumbani?. Kampeni zinafanyika chumbani?
Hizi scenario mbili hazifanani kabisaa. Bungeni ni wakali sana kwa anayeongopa. Lowasa na uimara wake na nguvu zake asingeunyamazia au kuukimbia uongo.
 
Ni wakati muafaka kwa mwakyembe kuondoa mzigo mzito ulio moyoni mwake!
 
Hizi scenario mbili hazifanani kabisaa. Bungeni ni wakali sana kwa anayeongopa. Lowasa na uimara wake na nguvu zake asingeunyamazia au kuukimbia uongo.

Naomba nikuulize, unaamini Dr alisema ukweli kuhusu Richmond bungeni bila kuficha taarifa muhimu kama mmiliki na mhusika mkuu?

Nijibu hilo ili nijue niendelee na mjadala au niachie hapa. Usije ukawa ndo Dr mwenyewe!
 
Mungu atamtetea kutoka katika mikono ya wadhalimu waliomtenda.

Sijui hizi pilipili msio kula sijui zinawawashia nini Mwakembe mwenyewe anajijua health status yake na kakaa kimya ,nyie kutwa kuchonga ati katendwe .Mnadhani yeye ni mtoto mdogo na asiye jua hatari ni nini? , kama kaisha jua wanataka kumuua na wamesha mdamage unadhani angerudi Tz? Kwa afya aliyo nayo kama ni sumu teari imeshafanya kazi na safari imekua delayed tuu unadhani anaweza kubali kufa kiiwoga kwa kukaa kimya bila hata ya kukimbia nchi na kusema wazi kilicho msibu?

Halafu watu wengine wana bahati sana , wanaweza kua wamecheza na sana maisha ,halafu wame kwaa gonjwa lile , halafu kila mtu anasikitika nakudhani kawekewa sumu na kulaani wengine. Sisemi kama ni ana ukimwi maana sijui chochote kuhusu tabia yake wala naisha yake.

Naungana na mdau aliye sema kuhusu kodi zetu , once zimetumika kibinafsi nivema tukajua zimetumikaje na kivipi .Aseme anaumwa nini ili kunusuru taifa kwa kuonekana ni la wauaji .
 
............Ni zaidi ya social network..hapa jamvini anatumia jina gani?
 
Back
Top Bottom