Mwaka 2009 nilichorwa kwa wembe alama hii kwenye dole gumba la mkono wa kulia, maana yake nini?

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Sep 4, 2013
36,063
40,724
Ilikuwa ni miaka takriban 13 Iliyopita, mwaka 2009, siku moja niliamka na kukuta nimechorwa alama hiyo ya kujiviringisha, na alama hiyo ilichorwa kwa kutumia kitu chenye ncha kali (nilihisi ni wembe), ambapo alama hiyo ilikuwa imechongwa juu kwenye dole gumba la mkono wa kulia, kwenye ile ngozi ya juu juu (dead skin).

Nilipoiona alama hii nilihisi labda niko usingizini naota, hivyo nikarudi tena kulala, ila nilipoamka ngoma bado ipo, bayana.

Niliogopa mno! Nikawa najaribu kukataa kwamba haiwezekani hiki kitu kimechanjwa mubashara kabisa kidoleni mwangu. Nilijiaminisha hii si kweli, ni ndoto tu, hata hata kama nashindwa kuamka usingizini. Baada ya siku kadhaa ile ngozi ya juu ilibanduka na alama ikapotea.

Ila hadi leo najiuliza, hii alama maana yake nini?

6B549DB3-6C6E-4358-963E-96B6A244B019.png
 
Mwaka 2009 sikuwa na smart aisee..,
Kuchanjwa usingizini ni matukio maarufu kutokea hasa Singida, unaweza hata kutahiriwa usingizini, kuchanjwa chale au kunyolewa upande mmoja kichwani...bila shaka na maeneo ya Kondoa na Tabora lkn zaidi Singida.

Hiyo alama ni namba 666.
Kama unakumbuka ilitumika kama brand name ya Zain Tanzania kipindi flani.
 
Kuchanjwa usingizini ni matukio maarufu kutokea hasa Singida, unaweza hata kutahiriwa usingizini, kuchanjwa chale au kunyolewa upande mmoja kichwani...bila shaka na maeneo ya Kondoa na Tabora lkn zaidi Singida.

Hiyo alama ni namba 666.
Kama unakumbuka ilitumika kama brand name ya Zain Tanzania kipindi flani.
Aloooo, natafuta usingizi hapa halafu unanitisha hivyo, sio poa bhanaaa. 666?!
 
Muda mwingine una akili...muda mwingine huna! kitaalamu inaitwa maji kupwa,maji kujaa...au mchicha mwiba
 
Haya matukio ni ya kawaida mkuu iliwahi nitokea na miimi kuchanjwa chale tano usingizini kwenye dole gumba nikiwa bweni miaka 19 iliyopita. Tukio hilo lilinishangaza sana mpaka sasa bado najiuliza lilikuwa na maana gani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom