Mwai Kibaki awadharau watanzania!

Mwai Kibaki awadharau watanzania!

Kwahili naungana mkono na babu Kibaki! Jamani kwani uongo kuwa watanzania hatutembei sana nje ya nchi?
 
Hivi tumekosa watu wa kuwaenzi mpaka tunamuenzi Kibaki, mtu aliyesababisha watu kupoteza maisha kwa sababu ya uroho wake wa madaraka?
 
tokea lini kutotembea kukawa tusi? sioni kama kamtusi mtu, ukweli watanzania tokea miaka wameridhika na kwao, sababu ziko nyingi tu za watanzania kuwa miomgoni mwa wasiopenda kutembea, wala si aibu wala tusi.
 
Mi sioni tatizo la alilosema Rais Kibaki. Hapa katupatia changamoto kama wana wa Afrika Mashariki, mtu anaibuka na kuita ni dharau. Udhaifu wa fikra utaliangamiza taifa.
 
Sifa ya kumpa kibaki jina la barabara hapa Tz amewapatia CCM mafunzo ya kuchakachua uchaguzi 2015.
 
tafsiri ni kitu cha ajabu sana. hutokana na upeo wa anayetasfiri jambo fulani. wakati mwingine tafsiri ya mambo mbalimbali huathiriwa na hisia fulani alizonazo muhusika juu ya jambo fulani. ndio maana kitu kimoja kinaweza kutafsiriwa tofauti tofauti na watu tofauti.

sishangai mtoa mada kutafsiri alivyofanya juu ya kauli ya watanzania hamjui kutembea.
 
Rais wa kenya Mwai Kibaki leo akiwahutubia wazee wa Dar kwa niaba ya Watanzania amesema ''Watanzania hamjazoea kutembea'' maana yake kuwa watanzania wengi wanaishi Tanzania tu Je hi si dharau kwa Watanzania? Inamaana Watanzania huushi pwani tu na hatutoki nje ya nchi hivyo akasisitiza tuende kenya.

Hata hivyo kitendo cha serikali ya Tanzania ikiongozwa na Rais JK Kikwete kuipa barabara ya Old Bagamoyo yenye historia ya Tanzania na kumpa Mwai kibaki, ikumbukwe Mwai kibaki aliingia kwa nguvu Kenya na kusababisha mauaji ambayo leo hii hatosaulika kenya. Sisi Watanzania ni kipi kilichotufanya barabara ya kihistoria kupewa Kibaki?

Source ITV habari saa 2000hrs usiku

Hivi kwa nini sisi watanzania tukielezwa ukweli tunakasirika na kusema ni zarau,hiyo siyo zarau ila ni kweli kabisa hatutembei
 
sijui kahonga ili jina lake ipewe barabara! mtu kuingia ikulu damu ilgmwagika ndo tumuenz hvo? au hatujali damu za wakenya zilizomwagika? au tunapenda ukabila kama wao?
 
Hivi tumekosa watu wa kuwaenzi mpaka tunamuenzi Kibaki, mtu aliyesababisha watu kupoteza maisha kwa sababu ya uroho wake wa madaraka?

Ni sawa Kibaki kuenziwa manake hapo ameenziwa kama mtu aliyesababisha watu kupoteza maisha kwa sababu ya uroho wake wa madaraka itakua kumbukumbu nzuri kwa vizazi vijavyo,ili wajifunze wasiibe kura wajue wakiiba itatokea machafuko
 
ni kweli... idadi ya wa k hapa tz ni kubwa kuliko ya wa Tz huko Kenya
SO many Tanzanians in mombasa.In kongowea market alot of the food comes from tanzania. people have relatives in tanga and in tanga people have relatives in mombasa.Mombasa pia kuna wantanzania wengi sana wa biashara.
 
Rais wa kenya Mwai Kibaki leo akiwahutubia wazee wa Dar kwa niaba ya Watanzania amesema ''Watanzania hamjazoea kutembea'' maana yake kuwa watanzania wengi wanaishi Tanzania tu Je hi si dharau kwa Watanzania? Inamaana Watanzania huushi pwani tu na hatutoki nje ya nchi hivyo akasisitiza tuende kenya.

Hata hivyo kitendo cha serikali ya Tanzania ikiongozwa na Rais JK Kikwete kuipa barabara ya Old Bagamoyo yenye historia ya Tanzania na kumpa Mwai kibaki, ikumbukwe Mwai kibaki aliingia kwa nguvu Kenya na kusababisha mauaji ambayo leo hii hatosaulika kenya. Sisi Watanzania ni kipi kilichotufanya barabara ya kihistoria kupewa Kibaki?

Source ITV habari saa 2000hrs usiku
Sioni ubaya!! Huyu ndiye Rais pekee Afrika kufanya maendeleo yakaonekana!! Barabara Kenya hasa Nairobi ni za kisasa kupita baadhi ya vinchi vya Ulaya.
Ndiyo kaingia kimtafaruku kwenye urais lakini tujiulize ni nani Afrika mashariki ameingia kihalali? Huyo fast jet ndiyo usiseme! Mus_eveni ndiyo janga kuu! Dictator Kagame?
Huyu ni kama wengine lakini kaleta maendeleo! By the way mimi huyu mzee alinikosha pale alipokataa misaada ya nje na akaendesha nchi bila kutembeza bakuli hadi mijamaa ikaja kumuombea "tunaomba tukusaidie". Wazungu hawapendi Rais stable kama huyu. Hata sasa wameshapania Uhuru akose ili apate puppet wao Raila. tegeni masikio na macho
 
Rais wa kenya Mwai Kibaki leo akiwahutubia wazee wa Dar kwa niaba ya Watanzania amesema ''Watanzania hamjazoea kutembea'' maana yake kuwa watanzania wengi wanaishi Tanzania tu Je hi si dharau kwa Watanzania? Inamaana Watanzania huushi pwani tu na hatutoki nje ya nchi hivyo akasisitiza tuende kenya.

Hata hivyo kitendo cha serikali ya Tanzania ikiongozwa na Rais JK Kikwete kuipa barabara ya Old Bagamoyo yenye historia ya Tanzania na kumpa Mwai kibaki, ikumbukwe Mwai kibaki aliingia kwa nguvu Kenya na kusababisha mauaji ambayo leo hii hatosaulika kenya. Sisi Watanzania ni kipi kilichotufanya barabara ya kihistoria kupewa Kibaki?

Source ITV habari saa 2000hrs usiku

Ana kila sababu ya kutudharau maana inaonekana hata yeye hakutegemea na hakustahili kupewa heshima kubwa kiasi hiki. Anawahurumia watanzania na kuwashauri watembee kiakili waone wenzao wanafanya nini kutunza na kuthamini vitu vyao.
 
Sekta ya utalii ya Kenya inatangaza kwamba mlima Kilimanjaro upo Kenya. Kiongozi wa nchi hiyo inayotangaza kwamba mlima wetu ni wao, anakuja kututembelea, halafu sisi tunamtukuza sana na kuweka kumbukumbu yake kwa kubadilisha jina la barabara muhimu ya kihistoria kwa kuiita: MWAI KIBAKI ROAD!

Only in Tanzania weird things happen!
 
lo! Yatakushinda zipuwawa!!!!!!! Kama wewe ni mwanamume katu hutaishi na mke! Kama we mwanamke basi siku moja utasutwa!
Watu wote tumemsikia huyo mzee lakini wewe na negativity zako, umesikia unayoyawaza kichwani mwako. Kazungumza kiswahili hukumwelewa, angezungumza kiingereza sijui ungetoa thread gani!!!!!!!!!!!

Tuseme alimaanisha ulivyosema, je wewe hata mikumi ulishatembelea? Pengine hata coco beach hupajui

ni kama shati la mzee vifungo vimekosewa ati au macho yangu???
 
Mbona kuna watu wamebatizwa "Fastjet" kwa ajili ya kusafiri nje ya TZ!
 
Kama kweli amesema hayo maneno hajakosea kabisa,kama unaona katudharau subiri Jumuiya ya Afrika Mashariki ikamilike halafu utaona nan anatembea sana!
 
Back
Top Bottom