Mwai Kibaki awadharau watanzania!

Mwai Kibaki awadharau watanzania!

Hakuna dharau yeyote mkuu! Ni ukweli usio pingika kuwa Watanzania tu waoga sana wa kuthubutu.
Takwimu ziko wazi, ni watanzania wangapi wanao thubutu kuulizia walau kibarua tu, pale Nairobi?
 
Rais wa kenya Mwai Kibaki leo akiwahutubia wazee wa Dar kwa niaba ya Watanzania amesema ''Watanzania hamjazoea kutembea'' maana yake kuwa watanzania wengi wanaishi Tanzania tu Je hi si dharau kwa Watanzania? Inamaana Watanzania huushi pwani tu na hatutoki nje ya nchi hivyo akasisitiza tuende kenya.

Hata hivyo kitendo cha serikali ya Tanzania ikiongozwa na Rais JK Kikwete kuipa barabara ya Old Bagamoyo yenye historia ya Tanzania na kumpa Mwai kibaki, ikumbukwe Mwai kibaki aliingia kwa nguvu Kenya na kusababisha mauaji ambayo leo hii hatosaulika kenya. Sisi Watanzania ni kipi kilichotufanya barabara ya kihistoria kupewa Kibaki?

Source ITV habari saa 2000hrs usiku

Tulizidi kuonyesha kumbabaikia!!
Ilikuwa aibu tupu, magufuli anapiga tumba..JK anakatika!! kwani yule nani? mbona mchovu tu!!...alisababisha vita vya wenyewe kwa wenyewe alipolazimisha kujitangaza kushinda uraisi!!!
Wapuuzi sana hawa ndie mtu wa kumpa heshima huyu?
Au kwakuwa anawapa mbinu za kuiba ushindi 2015? au kuficha uhalisia wa "Mkenya" alimteka ulimboka!?
 
Hakuna dharau yeyote mkuu! Ni ukweli usio pingika kuwa Watanzania tu waoga sana wa kuthubutu.
Takwimu ziko wazi, ni watanzania wangapi wanao thubutu kuulizia walau kibarua tu, pale Nairobi?

Mkuu wakenya hawa hawa enzi za mwalimu walikuwa wakituheshimu mno, na hata kuiga mambo yetu mengi...rejea TANU..KANU...
Nini kimefanya wageuke?
 
Kama Kibaki kasema hivyo ni ukweli na sijui wa Tz tuna tatizo gani daima hatupendi kuambiwa ukweli naona CCM imetudumaza kwani inapenda kujisifia na kukosolewa haitaki,si siri Watanzania tunaogopa sana kutembelea nchi nyingine,sijui ni tatizo la lugha au ni kutojiamini tu,kidogo siku hizi akina dada ndio wanaenda China/Thailand na Dubai ingawa wengi wao wanaenda si kwa kwenda kutaka kujifunza mambo yafaayo,hapa Tanzania wamejaa Wakenya lakini Watanzania hata Namanga hawajui,wakwetu tembea uone,na si tumekaa tu kama sanamu ya Bismini(Askari monument) ya pale IPS
 
Oh nchi yangu Tanzania! watoto wako wamekuwa wa aina gani? hatumu APPRECIATE mtu yeyote? kwa nini lakini?

Mie nimeshangaa ! Hivi wanaona ni jambo dogo sana mtu kufanya usuluhishi na watu wakaelewana ? Yule Akkufor wa Ghana si alishidwa !
 
umeongea vizuri sana mkuu! hawa watu wanataka sisi watanzania tumchukie mwai kibaki bila sababu. hii kasumba ya kuwachukia wakenya ililetwa na mtu ambaye sasa yupo kaburini. hawa watu bado wantawaliwa na kaburi lake. tanzania ndio maana haina maendeleo kwa sababu kuna watu bado wanendeshwa hisia zao na kaburi la mtu badala a ya akiri zao.

we naona huna akili mpaka unamuongea marehemu naona umeishiwa sera sasa we una wazo gani basi hata leo ukifa familia yako itakumbuka ndio nyie msio na adabu huna ladhi wewe ongea mengine.ila Mungu akusamehe bure
 
Kibaki amwmpandisha chati jk kwa kusulihisha mgogoro wa uchaguzi ana heshima sana kwa watz
 
Kutembea ni msemo tu lakini ukilinganisha wakenya waliopo nchini kwetu kwa nafasi mbalimbali na watz waliopo Kenya unaweza kugundua kuwa wakenya wanachangamkia fursa kwa haraka zaidi. kwa hiyo Mzee Kibaki yuko sahihi na kwamba ametoa changamoto kwa wa tz kugundua fursa nje ya Tz na kuzichangamkia. Yote hayo pia yanahitaji ujuzi na maarifa.
 
Kutembea ni msemo tu lakini ukilinganisha wakenya waliopo nchini kwetu kwa nafasi mbalimbali na watz waliopo Kenya unaweza kugundua kuwa wakenya wanachangamkia fursa kwa haraka zaidi. kwa hiyo Mzee Kibaki yuko sahihi na kwamba ametoa changamoto kwa wa tz kugundua fursa nje ya Tz na kuzichangamkia. Yote hayo pia yanahitaji ujuzi na maarifa.

Kauli ya Kibaki inaukweli ndani yake, iwe kwenye kutafuta fursa or safari kama za baba Ridhiwani. Wakenya wanasafiri zaidi kuliko watanzania. Waliokua nje ya nchi wanaweza kutusaidia hili wapi ambako wamepita hawajakuta mkenya. Ni ukweli mchungu lakini tuwe waungwana kukubali kwamba tuko nyuma ktk masuala ya safari na kuchangamkia fursa.
 
Back
Top Bottom