Mwai Kibaki awadharau watanzania!

Mwai Kibaki awadharau watanzania!

Katika kile ambacho nahisi ni hotuba ya kuishukuru serikali ya Tanzania kwa Barabara moja ya kihistoia kufutwa jina lake la awali na kupewa jina la kiongozi huyo wa Kenya ambaye nahisi bado Kiswahili kwake ni tatizo japo nchi yake imeonekana kama moja ya nchi inayoongea Kiswahili kwa ufasaha hali iliyopelekea taasisi nyingi za kimataifa kupeleka kazi za tafsiri nchini Kenya. Katika hotuba yake ya shukrani raisi huyo wa Kenya amewataja tena bila hofu kwamba watanzania huwa hawasafiri hivyo amewaomba watanzania wajifunze kusafiri. Sikumuelewa alimaanisha kusafiri kwa namna gani..
 
Lo! yatakushinda ZIPUWAWA!!!!!!! Kama wewe ni mwanamume katu hutaishi na mke! kama we mwanamke basi siku moja utasutwa!
Watu wote tumemsikia huyo mzee lakini wewe na negativity zako, umesikia unayoyawaza kichwani mwako. Kazungumza kiswahili hukumwelewa, angezungumza kiingereza sijui ungetoa thread gani!!!!!!!!!!!

Tuseme alimaanisha ulivyosema, je wewe hata mikumi ulishatembelea? pengine hata coco beach hupajui[/QU akili zingekuwa pesa ungekuwa level za bakhresa.unaakili sana,mleta uzi ajifikirie....
 
Alisemaje Hatujui kutembea wakati alikuwa na bingwa la kukata anga JK?

Bora angemwambia JK apeane zamu na wananchi wake 'kutembea'!

JK ni aibu ya Tanzania.
 
Pili mkutano wake wa pili alikuwa anawahutubia Wazee wa CCM wa Mkoa wa Dr es salaam na si Watanzania wote, alikuwa sahihi kabisa kuwaambia watembee maana wote pale ni watu wa pwani na hata Arusha hawapajui sembuse Nairobi?

Hivi JK siyo mzee na pia mtu wa pwani?

zomba umepata ujumbe? Uwe unatembetembea bana.

Anataka Mwai Kibaki Road iwe na watembeaji.
 
Rais wa kenya Mwai Kibaki leo akiwahutubia wazee wa Dar kwa niaba ya Watanzania amesema ''Watanzania hamjazoea kutembea'' maana yake kuwa watanzania wengi wanaishi Tanzania tu Je hi si dharau kwa Watanzania? Inamaana Watanzania huushi pwani tu na hatutoki nje ya nchi hivyo akasisitiza tuende kenya.

Hata hivyo kitendo cha serikali ya Tanzania ikiongozwa na Rais JK Kikwete kuipa barabara ya Old Bagamoyo yenye historia ya Tanzania na kumpa Mwai kibaki, ikumbukwe Mwai kibaki aliingia kwa nguvu Kenya na kusababisha mauaji ambayo leo hii hatosaulika kenya. Sisi Watanzania ni kipi kilichotufanya barabara ya kihistoria kupewa Kibaki?

Source ITV habari saa 2000hrs usiku

huna hoja
 
hiyo barabara bora ingeitwa Bakulutu. Au Ulimboka road
 
Last edited by a moderator:
Kwa upeo wako mdogo utaona hii si hoja....ila kwa mtu anayefikiria kwa makini na kuushugulisha ubongo wake. Hi si hoja ya kupuuza

Wewe nawe hiyo nayo ni hoja? inahusu nini?
 
Sijui kama maelezo ya mleta mada ni sahihi ama siyo lakini lazima tukubali jambo moja Watanzania wengi tumebweteka,hatusafiri,hata tukisafiri hatujifunzi!!
 
Kuna wakenya wangapi ambao hata Nairobi hawapajui, tujiulize hivo.
Kenya ni nchi masikini sana, ila wakenya wanajipamba sana, kivile wanapamba nyumba rangi nje wakati ndani ni vumbi na wanalala chini.

Utakuta mkenya kavaa suti na shati limepasuka mgongoni. Chupi ya kupasuka, soksi za kupasuka, alafu anajifanya anauwezo nzuri.

Huyo Mwai Kibaki utakuta anao jamaa kibao ambao hata pesa ya kununua unga wa sembe hawana, je pesa ya nauli kwenda nchi nyingine wataitoa wapi?

kha, kama kikwete kamtuma aseme hivo kwa wazee wa pwani ama watanzania au wazee wa ccm kakosea.

Kikwete awaongezee mshahara wazee wetu ili waweze kutembea.

Unyanyasaji wa watu masiki kwa vile wao wanatembea na ndege private.

mara ya mwisho kusafiri kutoka hapo unapoishi ni mwaka gani?
 
Ni kweli hamna exposure ndio maana mpaka leo mnapigania dini za uongo hadi kuua wengine!
 
kwa nini hawakumpa barabara ya Arusha-Namanga?

Kuna uwezekano mkubwa ikawa sababu UBALOZI WA KENYA umejengwa inapopia hiyo barabara,au ni heshima wanyopeana;JK alisuluhisha mgogoro wa wizi wa matokeo ya uchaguzi,KIBAKI akapendekeza apewe Udokta(Phd)
 
Mimi bado naitambua hiyo barabara kwa jina lile lile la zamani , Bagamoyo Road ! ( silitambui hili jina la Mwai Kibaki ) , Unaweza kushangaa , inaruhusiwa , lakini Habari ndiyo hiyo ! Huyu Kibaki ndiye aliyesababisha mauaji na wizi wa kura Kenya , Mimi kama Great Thinker Najitambua , hivyo sikubaliani so
 
We acha tu nasikitika sana barabara hiyo kuitwa jina la kiongozi alietakiwa kuwa mshitakiwa wa kwanza wa vurugu za mauaji ya Kenya baada ya uchaguzi wa mwaka 2007. Shame on us, hata angesema chochote juu yetu ni swa kabisa.Mi ntaendelea kuiita Old Bagamoyo Road na kama vipi tuna watu wamefanya makubwa kwenye jamii yetu lakini hawatambuliki hata hawajawahi kupewa hata jina la mtaa

Ni maneno ambayo nilipanga kuyasema kwa kuyaandika humu ndani ya jamii aksante bornagain chr..airforceone.Nimezipenda sentence zako ndio zilikuwa kichwani mwangu,Utawala ukibadilika tunabadilisha na kurudisha jina la zamani.Ni aibu kwa watanzania kumpa jina hila mtu aliyejiapisha mwenyewe na kusababisha mauaji
 
Ukiambiwa ukweli-dharau,unapenda kusifiwa eeh!
 
Mimi bado naitambua hiyo barabara kwa jina lile lile la zamani , Bagamoyo Road ! ( silitambui hili jina la Mwai Kibaki ) , Unaweza kushangaa , inaruhusiwa , lakini Habari ndiyo hiyo ! Huyu Kibaki ndiye aliyesababisha mauaji na wizi wa kura Kenya , Mimi kama Great Thinker Najitambua , hivyo sikubaliani so
Mgomo wetu utashinda kwa sababu hata watu wanaoheshimika kweli kweli nchi hii bado bara bara zao watu wanatumia majina ya zamani kwa mazoea mfano Nyerere road wapo ambao mpaka leo wamezoea kuita Pugu road, na Mandela road, wapo ambao wamezoea jina la Port access.

Mimi kulitamka tu jina la Mwai Kibaki naona kama kinyaa, hivi hawa viongozi wetu wanatufanyia kipima joto cha uvumilivu au nini hasa? Kenya haitakaa itokee eti Kikwete apewe barabara Never.
 
482484_507276975982805_1605657235_n.jpg

Naona mkuu wa mkoa kajitutumua kavaa suti na tai leo. Angesema pia watz hatujazoea kuvaa suti na tai
 
Mtanzania amka acha blanget la umaskini kwani tunaposema nchi imeuzwa kwa jamaa mwingine tuna maana ghani?.tujiulize kwanza kisha ukipata jibu jiulize tena juu ya mali za nchi zinavyo taifishwa .cfa kukuki tanzania nchi ya amani baada ya kusema tanzania nchi ya mafisadi na matapeli !!!.jamani hee mwai kibaki kaja kumalizia makombo yaliyo baki hapa nchini na kama amta ckia yakwamba tanzania imeingia ubia na nchi ya kenya juu ya sekta fulani cjui.lakini jamani maisha yetu ndivyo yalivyo toka zamani, kwahiyo tusishangae sana kwani alivyo kuja joji bush nyerere road iliitwaje?ahsanten sana.
 
Kwani Kikwete aliingia kihalali kama si kuwachafua wenzake na kuiba pesa ya EPA? Show me your friends I will tell you who you are. Sikuona mantiki ya kumpa hadhi ya jina la barabara wakati mtu mwenyewe anamaliza muda wake. Yeye atakupa nini? Anyways, kwa vile aliyefanya hivyo ni Kikwete hamna neno. Wakati mwingine kutumia zeero braiin inalipa au siyo?
Rais wa kenya Mwai Kibaki leo akiwahutubia wazee wa Dar kwa niaba ya Watanzania amesema ''Watanzania hamjazoea kutembea'' maana yake kuwa watanzania wengi wanaishi Tanzania tu Je hi si dharau kwa Watanzania? Inamaana Watanzania huushi pwani tu na hatutoki nje ya nchi hivyo akasisitiza tuende kenya.

Hata hivyo kitendo cha serikali ya Tanzania ikiongozwa na Rais JK Kikwete kuipa barabara ya Old Bagamoyo yenye historia ya Tanzania na kumpa Mwai kibaki, ikumbukwe Mwai kibaki aliingia kwa nguvu Kenya na kusababisha mauaji ambayo leo hii hatosaulika kenya. Sisi Watanzania ni kipi kilichotufanya barabara ya kihistoria kupewa Kibaki?

Source ITV habari saa 2000hrs usiku
 
Back
Top Bottom