Siku 1 nilikua nakwenda Rwanda, mpakani pale nikawa na kazoezi kakubadiri hizi pesa zetu za madafu kwenye kwenye currency yao, wale jamaa wa bolder walinambia, mkuu, hii pesa yenu ya Tanzania ukituachia hapa itakaa sana, nyie Watanzania hua hamsafiri! Nakubaliana na Mwai Kibaki kwamba Wabongo wengi hatusafiri though kutokusafiri haina maana kwamba hatuna akili ingawa pia kusafiri kunakupa Exposure ya kinachoendelea sehemu nyingine, inawezekana hatusafiri kwasababu linchi letu likubwa mno, so mtu akitoka Mbeya kwa mfano na akaeenda Mwanza, au Mwanza kwenda Mtwara, kwa baadhi ya nchi hiyo distance ni kama kutembea zaidi ya nchi 4!
Bado sijaelewa, kwanini Mwai Kibaki amepewa barabara? Au kwasababu barabara hiyo inaenda Bagamoyo kwa mkuu, mwenye uelewa wa hilo tafadhari!?