FIKRA MBADALA
Senior Member
- Jun 30, 2008
- 167
- 16
Hali ya mambo ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), bado si shwari baada ya kuibuka mvutano wa kuwania nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa ambayo kwa sasa inashikiliwa na FREEMAN MBOWE.
Habari za uhakika zilizopatikana kutoka ndani ya chama hicho zinaeleza kuwa, mvutano uliopo hivi sasa ni wa kuwania nafasi ya Mwenyekiti wa CHADEMA katika uchaguzi mkuu wa chama hicho unaotarajiwa kufanyika Mwezi Machi mwaka 2009. Awali uchaguzi huo ulipangwa kufanyika mwezi Desemba 2008, kabla ya kuahirishwa kwa kile kinachoelezwa na wafuatiliaji wa siasa ndani ya chama hicho kuwa ni kutokana na mvutano wa uongozi unaofukuta.
Kimsingi, mvutano wa uongozi ndani ya CHADEMA ni mkubwa kiasi cha kusababisha kuibuka kwa makundi matatu yanayogombea kushika wadhifa wa Mwenyekiti. Makundi hayo yana nguvu na kila moja limejiandaa kupigana kwa nguvu zote ili kuhakikisha kuwa linatwaa Uenyekiti wa chama hicho.
Makundi hayo ni lile linalomuunga mkono Mwenyekiti wa sasa, FREEMAN MBOWE na ambalo kwa sehemu kubwa linaundwa na viongozi na wanachama wenye nyadhifa na uhusiano mzuri na Makao Makuu ya CHADEMA. Kundi hili limeanza kujiandaa kuhakikisha kuwa MBOWE anarejea tena katika uongozi wa chama hicho, na ndiye atakuwa mgombea wa Urais wa chama katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.
Taarifa inaeleza kuwa, wafuasi wa kundi hili, wanajua MBOWE amepoteza umaarufu ndani na nje ya chama lakini wanajua kuwepo kwake katika uongozi ni jambo la kheri kwao. Kundi hili, bado linamuona MBOWE kuwa ni kiongozi mwenye mvuto na anaweza kuendelea na uongozi wa chama hicho pamoja na kuwepo kwa tuhuma na migogoro iliyochafua wasifu wake katika siku za hivi karibuni.
Hata hivyo, wafuatiliaji wa mambo ndani ya CHADEMA wanaamini kuwa, MBOWE amepoteza umaarufu hasa kutokana na kutajwa kuwa ndiye chanzo cha migogoro ambayo imekuwa ikijitokeza ndani ya chama hicho.
Kundi la pili na lililoibuka na ambalo linaelezwa kuwa na nguvu zaidi, ni lile linalomuunga mkono katibu wa chama hicho, DR. WILBROAD SLAA. Kundi hili linaloaminika kuwa na ngome yake katika Kanda ya Ziwa, linajenga hoja kuwa DR. SLAA ndiye mtu pekee ndani ya chama hicho ambaye anaonyesha sifa ya kukiongoza chama hicho na kukiletea tija kisiasa.
Kundi la DR. SLAA linaonekana kuwa na nguvu zaidi kwa sababu linaungwa mkono na wanachama wengi ambao wanataka kuona chama kikipata mafanikio zaidi na kurejesha imani yake kwa wananchi. Wafuasi wa DR. SLAA wanamuona kuwa hana kashifa kama alivyo Mwenyekiti wa chama, MBOWE na ndiyo maana wanataka ashike usukani ili kuokoa chama kisisambaratike.
Kambi hii, inadai kuwa CHADEMA inahitaji kupata mtu msafi (ambaye hajachafuka) anayeungwa mkono na wanachama wa kawaida na ndiye atakisadia chama hicho kuimarika katika ngazi za chini badala ya kuwa cha Makao Makuu.
Mbali na makundi hayo mawili ambayo kwa sehemu kubwa ndiyo yanaonekana kuwa na mchuano mkali, lipo kundi la tatu ambalo linaelezwa kuungwa mkono na watu wenye pesa ndani na nje ya chama hicho. Kundi hili ambalo limepachikwa jina la kundi la wenye fedha kutokana na kujumuisha wafanyabiashara matajiri, linaamini kuwa chama kinapaswa kuongozwa na watu wenye umri mkubwa kama MZEE PHILEMON NDESAMBURO.
Habari zinadai kuwa, kundi linalomuunga mkono NDESAMBURO ni lile ambalo limekuwa likinufaika na chama katika kufanya biashara zao. Hata hivyo, wanachama wasiolitaka kundi la NDESAMBURO wanadai kuwa katika kikundi chochote watu hawawi na malengo ya kufanana, wengine wanataka kutumia kikundi kujinufaisha binafsi na wengine wanataka kuona kikundi kikifanikiwa. Hivyo, hata ndani ya CHADEMA kuna wachache ambao wapo humo lakini wanataka kuhakikisha mambo yao yakifanikiwa kupitia chama na hawa ndio wanaounga mkono watu wenye pesa na walio na mawazo ya kibiashara ndani ya chama hicho.
Kuna madai kuwa kuibuka kwa kundi la tatu ni ishara ya kuwa waasisi wa chama hicho hawako tayari kuona chama kikiondoka mikononi mwao na kuwaachia wageni kutoka CCM kama ilivyo kwa DR SLAA. Hata hivyo, watu wanaojenga dhana kuwa kundi hili halina madhara kwa makundi mengine, kwa maana kwamba watu wenye umri mkubwa kama NDESAMBURO hawana jipya linaloweza kuwashawishi na kuwavutia wapiga kura ambao wengi wao ni vijana.
Aidha, kuna kundi la aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Marehemu CHACHA WANGWE. Kundi hili, linajumuisha wanaCHADEMA waliokuwa wanamtaka CHACHA WANGWE kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa (CHADEMA). Baada ya kifo cha WANGWE, kambi hii haijaamua mgombea wa kumuunga mkono kati ya kundi la MBOWE, DR SLAA na NDESAMBURO. Hata hivyo, kundi hili limeweka wazi kwamba halitamuunga mkono Mwenyekiti wa sasa, FREEMAN MBOWE.
Habari zaidi zinaonyesha kuwa kuibuka kwa mvutano huu wa kuwania uongozi wa CHADEMA, kumetokana na kubaini kuwa Mwenyekiti MBOWE amechafuka kiasi cha kuwa mzigo kwa chama, viongozi wenzake na Watanzania waliokuwa wakiunga mkono sera za CHADEMA.
Wanaopinga MBOWE wanasema kuwa, baadhi ya kashifa ambazo zinamwandama ni pamoja na ya kuacha majina yaliyopendekezwa na chama kuwa wabunge wa viti maalum na kujaza ya watu aliowataka yeye.
Kashfa nyingine ni ya chama kukimbiwa na viongozi wa juu kwenda CCM au kuanzisha chama kingine kama ilivyotokea kwa aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, DR AMANI WALID KABOUROU ambaye alihamia CCM na PAUL KYARA aliyekuwa Mweka Hazina wa CHADEMA Taifa ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa chama cha Sauti ya Umma.
Miongoni mwa kashifa hizo, ipo pia ya matumizi mabaya ya pesa za ruzuku ikiwemo kulipa madeni yaliyotokana na matumizi ya Helkopta katika kampeni za Urais kwenye uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005.
Kashfa ambayo imemchafua zaidi MBOWE katika siku za karibuni ni ya kuhusishwa na Kifo cha aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wake CHACHA WANGWE ambaye pamoja na mambo mengine alikuwa akihoji masuala tajwa hapo juu. Kifo cha WANGWE kimesababisha MBOWE kushambuliwa kwa mawe huko Tarime wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo hilo uliofanyika hivi karibuni. Ikumbukwe pia kuwa MBOWE hakwenda kumzika WANGWE kutokana na sababu hizo hizo.
Kutokana na mlolongo wa matukio haya wana-CHADEMA wanaona ni kwa nini MBOWE asikae pembeni ili kutoa nafasi kwa watu wasio na kashfa?
Wana JF, habari hii inatupa changamoto ya kuanzisha mdahalo (debate) wa kuchanganua mipaka ya kuwajibika kwa viongozi wa kisiasa nchini. Imekuwa ni kawaida na mazoea kwa vyama vya upinzani nchini kudai viongozi wa chama tawala CCM wawajibike wakati wao hawafikirii kufanya hivyo kwa wanachama wao waliowachagua. Nimekuwa sipati jibu ni kwa nini viongozi wa kisiasa wawe wa upinzani au chama tawala ni wagumu kuwajibika ili kuonyesha mfano wa kuigwa? Je, ni udikteta au ni kukosa sifa za uongozi?
Naomba kutoa hoja.
Habari za uhakika zilizopatikana kutoka ndani ya chama hicho zinaeleza kuwa, mvutano uliopo hivi sasa ni wa kuwania nafasi ya Mwenyekiti wa CHADEMA katika uchaguzi mkuu wa chama hicho unaotarajiwa kufanyika Mwezi Machi mwaka 2009. Awali uchaguzi huo ulipangwa kufanyika mwezi Desemba 2008, kabla ya kuahirishwa kwa kile kinachoelezwa na wafuatiliaji wa siasa ndani ya chama hicho kuwa ni kutokana na mvutano wa uongozi unaofukuta.
Kimsingi, mvutano wa uongozi ndani ya CHADEMA ni mkubwa kiasi cha kusababisha kuibuka kwa makundi matatu yanayogombea kushika wadhifa wa Mwenyekiti. Makundi hayo yana nguvu na kila moja limejiandaa kupigana kwa nguvu zote ili kuhakikisha kuwa linatwaa Uenyekiti wa chama hicho.
Makundi hayo ni lile linalomuunga mkono Mwenyekiti wa sasa, FREEMAN MBOWE na ambalo kwa sehemu kubwa linaundwa na viongozi na wanachama wenye nyadhifa na uhusiano mzuri na Makao Makuu ya CHADEMA. Kundi hili limeanza kujiandaa kuhakikisha kuwa MBOWE anarejea tena katika uongozi wa chama hicho, na ndiye atakuwa mgombea wa Urais wa chama katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.
Taarifa inaeleza kuwa, wafuasi wa kundi hili, wanajua MBOWE amepoteza umaarufu ndani na nje ya chama lakini wanajua kuwepo kwake katika uongozi ni jambo la kheri kwao. Kundi hili, bado linamuona MBOWE kuwa ni kiongozi mwenye mvuto na anaweza kuendelea na uongozi wa chama hicho pamoja na kuwepo kwa tuhuma na migogoro iliyochafua wasifu wake katika siku za hivi karibuni.
Hata hivyo, wafuatiliaji wa mambo ndani ya CHADEMA wanaamini kuwa, MBOWE amepoteza umaarufu hasa kutokana na kutajwa kuwa ndiye chanzo cha migogoro ambayo imekuwa ikijitokeza ndani ya chama hicho.
Kundi la pili na lililoibuka na ambalo linaelezwa kuwa na nguvu zaidi, ni lile linalomuunga mkono katibu wa chama hicho, DR. WILBROAD SLAA. Kundi hili linaloaminika kuwa na ngome yake katika Kanda ya Ziwa, linajenga hoja kuwa DR. SLAA ndiye mtu pekee ndani ya chama hicho ambaye anaonyesha sifa ya kukiongoza chama hicho na kukiletea tija kisiasa.
Kundi la DR. SLAA linaonekana kuwa na nguvu zaidi kwa sababu linaungwa mkono na wanachama wengi ambao wanataka kuona chama kikipata mafanikio zaidi na kurejesha imani yake kwa wananchi. Wafuasi wa DR. SLAA wanamuona kuwa hana kashifa kama alivyo Mwenyekiti wa chama, MBOWE na ndiyo maana wanataka ashike usukani ili kuokoa chama kisisambaratike.
Kambi hii, inadai kuwa CHADEMA inahitaji kupata mtu msafi (ambaye hajachafuka) anayeungwa mkono na wanachama wa kawaida na ndiye atakisadia chama hicho kuimarika katika ngazi za chini badala ya kuwa cha Makao Makuu.
Mbali na makundi hayo mawili ambayo kwa sehemu kubwa ndiyo yanaonekana kuwa na mchuano mkali, lipo kundi la tatu ambalo linaelezwa kuungwa mkono na watu wenye pesa ndani na nje ya chama hicho. Kundi hili ambalo limepachikwa jina la kundi la wenye fedha kutokana na kujumuisha wafanyabiashara matajiri, linaamini kuwa chama kinapaswa kuongozwa na watu wenye umri mkubwa kama MZEE PHILEMON NDESAMBURO.
Habari zinadai kuwa, kundi linalomuunga mkono NDESAMBURO ni lile ambalo limekuwa likinufaika na chama katika kufanya biashara zao. Hata hivyo, wanachama wasiolitaka kundi la NDESAMBURO wanadai kuwa katika kikundi chochote watu hawawi na malengo ya kufanana, wengine wanataka kutumia kikundi kujinufaisha binafsi na wengine wanataka kuona kikundi kikifanikiwa. Hivyo, hata ndani ya CHADEMA kuna wachache ambao wapo humo lakini wanataka kuhakikisha mambo yao yakifanikiwa kupitia chama na hawa ndio wanaounga mkono watu wenye pesa na walio na mawazo ya kibiashara ndani ya chama hicho.
Kuna madai kuwa kuibuka kwa kundi la tatu ni ishara ya kuwa waasisi wa chama hicho hawako tayari kuona chama kikiondoka mikononi mwao na kuwaachia wageni kutoka CCM kama ilivyo kwa DR SLAA. Hata hivyo, watu wanaojenga dhana kuwa kundi hili halina madhara kwa makundi mengine, kwa maana kwamba watu wenye umri mkubwa kama NDESAMBURO hawana jipya linaloweza kuwashawishi na kuwavutia wapiga kura ambao wengi wao ni vijana.
Aidha, kuna kundi la aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Marehemu CHACHA WANGWE. Kundi hili, linajumuisha wanaCHADEMA waliokuwa wanamtaka CHACHA WANGWE kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa (CHADEMA). Baada ya kifo cha WANGWE, kambi hii haijaamua mgombea wa kumuunga mkono kati ya kundi la MBOWE, DR SLAA na NDESAMBURO. Hata hivyo, kundi hili limeweka wazi kwamba halitamuunga mkono Mwenyekiti wa sasa, FREEMAN MBOWE.
Habari zaidi zinaonyesha kuwa kuibuka kwa mvutano huu wa kuwania uongozi wa CHADEMA, kumetokana na kubaini kuwa Mwenyekiti MBOWE amechafuka kiasi cha kuwa mzigo kwa chama, viongozi wenzake na Watanzania waliokuwa wakiunga mkono sera za CHADEMA.
Wanaopinga MBOWE wanasema kuwa, baadhi ya kashifa ambazo zinamwandama ni pamoja na ya kuacha majina yaliyopendekezwa na chama kuwa wabunge wa viti maalum na kujaza ya watu aliowataka yeye.
Kashfa nyingine ni ya chama kukimbiwa na viongozi wa juu kwenda CCM au kuanzisha chama kingine kama ilivyotokea kwa aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, DR AMANI WALID KABOUROU ambaye alihamia CCM na PAUL KYARA aliyekuwa Mweka Hazina wa CHADEMA Taifa ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa chama cha Sauti ya Umma.
Miongoni mwa kashifa hizo, ipo pia ya matumizi mabaya ya pesa za ruzuku ikiwemo kulipa madeni yaliyotokana na matumizi ya Helkopta katika kampeni za Urais kwenye uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005.
Kashfa ambayo imemchafua zaidi MBOWE katika siku za karibuni ni ya kuhusishwa na Kifo cha aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wake CHACHA WANGWE ambaye pamoja na mambo mengine alikuwa akihoji masuala tajwa hapo juu. Kifo cha WANGWE kimesababisha MBOWE kushambuliwa kwa mawe huko Tarime wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo hilo uliofanyika hivi karibuni. Ikumbukwe pia kuwa MBOWE hakwenda kumzika WANGWE kutokana na sababu hizo hizo.
Kutokana na mlolongo wa matukio haya wana-CHADEMA wanaona ni kwa nini MBOWE asikae pembeni ili kutoa nafasi kwa watu wasio na kashfa?
Wana JF, habari hii inatupa changamoto ya kuanzisha mdahalo (debate) wa kuchanganua mipaka ya kuwajibika kwa viongozi wa kisiasa nchini. Imekuwa ni kawaida na mazoea kwa vyama vya upinzani nchini kudai viongozi wa chama tawala CCM wawajibike wakati wao hawafikirii kufanya hivyo kwa wanachama wao waliowachagua. Nimekuwa sipati jibu ni kwa nini viongozi wa kisiasa wawe wa upinzani au chama tawala ni wagumu kuwajibika ili kuonyesha mfano wa kuigwa? Je, ni udikteta au ni kukosa sifa za uongozi?
Naomba kutoa hoja.