Mvua kubwa jijini Dar - Mei 8, 2017

Mvua kubwa jijini Dar - Mei 8, 2017

Bagamoyo....daa hii ni balaa aisee, na TMA ndo wanazidisha utata.

We unawaamini hao TMA mkuu, kwani wao ndio wanaratibu mvua,,,,tangu enzi na enzi mvua za masika zipo,,,,mi nitawamini kama watatabiri mvua kunyesha mwezi August
 
Hii mvua sasa too much! Ikanyeshe vijijini huko watu walime.....Huku mjini riziki ziko miguuni
 
Still working from home mana hamna namnaaa...km na kesho ndo hv basi itakua hamna namnaaaaaaaa....
 
Still working from home mana hamna namnaaa...km na kesho ndo hv basi itakua hamna namnaaaaaaaa....
Naomba nije tufanye wote kazi. Working from home alone is kinda boring....
 
jamani hii mvua sasa balaa hapa nimejibaza mahali hatali sana kitunda
 
Duh sasa huku mvua inatuletea madimbwi tu hamna wakulima.
Yaani hapa ndipo ninapomkumbuka Comred Ghadafi (R.I.P); aliamisha maji kutoka mitoni na bahari na kuyapeleka jangwani kwa idadi kubwa ya kilometa za umbali na watu wakaanza kulima kilimo cha maana. Wakajitosheleleza...! Yaani we acha.
 
Watu walikuwa wanasema mkulu kaingia kwenye uongozi na laana hadi ukame unataka kuua watu.
Sasa naona laana imeisha, tayari tunalia hatuitaki au ndo bado laana inaendelea nini.
(Tunadhambi sana sisi yaani ukame tunamlaumu binadamu mwenzetu!!)
 
Mkuu mimi nimezaliwa chini ya km kutoka jangwani. Wakati huo kulikuwa viwanja vya mpira hapo, vingi sana. Hata Simba walikuwa wanafanya mazoezi mara moja moja tena hapo ilipo Udart na maji yalikuwa hayafuriki viwanjani hata mvua inyeshe vipi.

Kabla ya udart kulikuwa na yard ya Kajima (japanese construction company) wamekaa miaka mingi sana. Sababu ya hayo mafuriko ni mto kujaa uchafu na kina kupungua. Upande wa muhimbili hapo palikuwa plain na mchanga mweupe kama wa bahari ndio maji yakizidi mtoni yanakaa hapo sasa hivi kuna takataka na magugu kibao.

NEMC inabidi wafanye kazi sana.
Hata Ally Mufuruki aliandika wakati Fulani kuhusu mafuriko na bomoa bomoa. Lilikuwa andiko zuri sana kuhusu chanzo cha mafuriko. Najaribu kulitafuta nitalibandika hapa
 
Back
Top Bottom