Muziki wa taarabu....!!

Muziki wa taarabu....!!

Mzee DC, Mie sio mtaalam wa Taarab but the little I know I Love and appreciate... hii ni moja ya Music hapa JF inakua rarely listed to or discussed, hopefully hii thread itaendelea na Music ya taarabu Worthwhile zitazidi miminika....

Inatia moyo kuona kwamba kuna walau watu wachache wanaotambua kuwa huu muziki ni muhimu sana na unabeba utambulisho wetu kama watu wa A Mashariki....Hili ni muhimu sana kulitambua.

Naomba tundelee kupata maoni ya wadau!!
 
Mwanaume mzima anaongea pumbaaaaaaa
At na yeye anaweza kujiita baba! au mume!! lol
sijui kama maisha atayaweza kwa mtazamo alonao
Ndio maana Malkia wa taarabu alishaimbaga kwamba.......
"........Wengine si wanaume......ila magumegume......." - hadija kopa

Mama D,

Hebu tumwagie mistari zaidi basi...Usitunyime uhondo wenzio!
 
Hapo sijajua kama ni Sodium Chloride kweli au chenginecho ........ila mie nimeamua kuitafsiri kwa chenginecho 😛

Ngoja niusikilize kwanza, then nitarudi na reflection yangu,

Ila huu muziki ni hatari sana kwa jinsi unavyocheza na lugha!

I wish people knew!!!
 
Nilaumu macho yangu au moyo nambieni

Moyo umesalitika, kwa sababu macho yangu
Tena nna yakinika, nidirikini wenzangu
Mwisho nitafedheheka, kupenda kitu sichangu
Nilaumu macho yangu, au moyo nambieni

Umeulizwa suali, jawabu nakuletea
Uamuzi wa halali, hukumu iso hatia
Itakuwa ni muhali, kimoja kukionea
Laumu vyote viwili, usilaumu kimoja

NILAUMU MACHO YANGU AU MOYO - YouTube
 
Sikiliza hii kisha unambie linazungumzwa kasha la kuwekea mizigo! lol


Kasha langu la zamani, kasha lisilo tunguu
Kitasa ndani kwa ndani, na ufunguo ni huu
Alolifungua n'nani, amenifunza makuu

Kasha muundo wa kale, si muondo wa kisasa
Ni kazi ya watu wale, si fani ya kiMambasa
Usifanye makelele, melipa mengi mapesa

Mafundi wote wa kale, kwa hivi sasa hakuna
Na walobaki wa vile, kabisa hutawaona
Ulobaki mkulele, na kazi sijaiona

http://www.youtube.com/watch?v=ANKznuG0Vas
 
Mpewa hapokonyeki, aliyepewa kapewa
wewe ukifanya chuki, bure unajisumbua

Aliyepewa kapewa, naapa hapokonyeki
Kwa alicho jaaliwa, Wallah hapunguziki
Kwake ukilia ngoo, unajipatisha dhiki


Wa tisa humpa tisa, wa moja haongezeki
Alomnyima kabisa, pindi akitaharuki

Mola mtoa hidaya, mambo yote kamiliki
Kwa anomtunukia, huwa ndio yake haki
Na asiye mtakia, huwa si yake laiki

MPEWA HAPOKONYEKI. - YouTube
 
Kukupenda sana, ndilo kosa langu
Sitofanya tena, naapa kwa Mungu
Niliyoyaona, yanatosha kwangu

Nikikumbukia, naona uchungu
Nimekupokea, kwa khiari yangu
Kumenichongea, kukupenda kwangu


kukupenda sana ndio kosa langu - YouTube

Kweli Gee,

Ni kosa kubwa kumpenda sana mtu naye akalijua hilo...Mara nyingi utajuta kumpenda!

Ni ukweli unaoumiza sana!
 
Kweli Gee,

Ni kosa kubwa kumpenda sana mtu naye akalijua hilo...Mara nyingi utajuta kumpenda!

Ni ukweli unaoumiza sana!

Apendwaye akajua haachi kujizuzua. Lazima u-make sure anakupenda yeye sana kuliko unavyompenda wewe 😛
 
Apendwaye akajua haachi kujizuzua. Lazima u-make sure anakupenda yeye sana kuliko unavyompenda wewe 😛

Kwa hiyo unapendekeza mchezo wa kutegeana???

Ila kuna watu wanakuwa malimbukeni kiasi kwamba wanapoteza akili, busara na hekima wapojidai wanapenda!

Sijui ndiyo hayo mambo ya Zumbukuku???
 
Kwa unapendekeza mchezo wa kutegeana???

Ila kuna watu wanakuwa malimbukeni kiasi kwamba wanapoteza akili, busara na hekima wapojidai wanapenda!

Sijui ndiyo hayo mambo ya Zumbukuku???

Sijui ndo tuseme binaadamu binaadamu tumeumbwa tofauti! Maana kuna wengine wakipenda kama wagonjwa!

Atafikia hadi kupigwa, lakini humuelezi kitu.......

Mungu asituonyeshe huuuh
 
Hii kwa wale wala "makombo" lolz

Chungu kaona kivuno, ganda la mua la jana
Kwa mbwembwe na majivuno, apita aking'ong'ona
Tele alama za meno, halina utamu tena
Wa leo huna maneno, lilofaidiwa jana

GANDA LA MUWA LA JANA - YouTube
 
Sijui ndo tuseme binaadamu binaadamu tumeumbwa tofauti! Maana kuna wengine wakipenda kama wagonjwa!

Atafikia hadi kupigwa, lakini humuelezi kitu.......

Mungu asituonyeshe huuuh

Nadhani wakati mwingine ni usanii au matatizo na hofu ya kuachwa!

Ila pia kuna watu wanakuwa kama vichaa vile. Mfano mtu anapokuwa na wivu wa kupitiliza/

Hivi ule wimbo wa, "wivu ni kidonda" unaweza kutuwekea hapa ndugu yangu?

Babu DC
 
Back
Top Bottom