Muziki wa taarabu....!!

Muziki wa taarabu....!!

Hapo sasa,

Hivi taarabu huwa inagusa theme moja tu....???

Karibu sana B!!

Taarab inaimba theme nyingi tu

kuna huu unasema "kunionya sikatai, kusengenywa haifai" .......kaimba Fatma Issa "Uso wa Basi" :]

Inasemakana huko kwao Zanzibar alikuwa akisemwa sana kisa anakunywa pombe nae mwanamke...akawarushia mziki huo akiwaambia "nami ni mja mwenzenu, kunionya sikatai, kusengenywa haifai"

 
Last edited by a moderator:
Ama kweli,

Lugha ya huu muziki si kama ile ya ubongo wa fleva!!

Hivi under 18 huwa wanaelewa kweli?


Na uzee wangu bado nahitaji msaada hapa na pale!!

huu mziki kwa muda mfupi ambao nimeji devote kwake nimegundua ni mwalimu mzuri sana wa kiswahili
 
Asante Gee, ni kweli nilikuwa najaribu kukumbuka hata kuna mmoja sijui nani kaimba unaenda hivi...."mamaa aah mama aah, kilio umeniachia"... bibie alikuwa akieleza hisia zake baada ya kuondokewa na bi mkubwa wake.
Kwa hiyo kuna theme mbali mbali kwenye huu muziki
 
Asante Gee, ni kweli nilikuwa najaribu kukumbuka hata kuna mmoja sijui nani kaimba unaenda hivi...."mamaa aah mama aah, kilio umeniachia"... bibie alikuwa akieleza hisia zake baada ya kuondokewa na bi mkubwa wake.
Kwa hiyo kuna theme mbali mbali kwenye huu muziki

Zipo za siasa pia

Modern politics ilikuja na hii "kitandawili natega" http://www.youtube.com/watch?v=vyqDkLv9QJk

Na old politics ilikuja na hii "Abedi nenda tunakutuma" lol (niwawekea link soon)
 
huu mziki kwa muda mfupi ambao nimeji devote kwake nimegundua ni mwalimu mzuri sana wa kiswahili

Sasa unaonaje tukianzisha NGO ya kuukweza huu muziki??

Walau tuondoe hii dhana kwamba ni muziki wa ngono kwa kwenda mbele....

Pia ukumbuke kuwa kuna dimension nyingine aliidokeza The Boss...Kwamba mabwabwa wanajaa sana kwenye huu muziki!!
 
  • Thanks
Reactions: bht
"wengi wamenihasimu na thamani kunitoa
mwapita kumwaga sumu kila ovu kutupiwa
bure mna nituhumu ya fitina kuyagawa
nami ni mwanaadamu, si vyema kunibagua

nami ni mja mwenzenu, hata mkinichukia
aibu yangu ndo yenu, kama mtafikiria




Maana kwa nyimbo kama hiyo "mabwabwa" lazima waipende wanaona inawahusu! ...🙁

Ila mie leo najitolea kukurushia taarab zisizolenga mapenzi moja kwa moja, japo zinalenga kwenye jamii
 
Sasa unaonaje tukianzisha NGO ya kuukweza huu muziki??

Walau tuondoe hii dhana kwamba ni muziki wa ngono kwa kwenda mbele....

Pia ukumbuke kuwa kuna dimension nyingine aliidokeza The Boss...Kwamba mabwabwa wanajaa sana kwenye huu muziki!!


hilo la NGO ngoja kwanza.

kuhusu hao mabwabwa, vipi kama hao ni wapenzi tu wa muziki huu kama mimi na Gee tulivyo? ina maana huko kwenye rhumba na salsa na bongo fleva hawapo hao? ni hivyo walivyo ndio kuna wasukuma kupenda taarab? kuna dhana potofu sana mwanaume anayependa sana huu muziki ana walakini
 
@Gaijin....asante sana kwa huo wimbo wa Issa Matona......ndio nasuuza nao moyo wangu saa hii....
 
"wengi wamenihasimu na thamani kunitoa
mwapita kumwaga sumu kila ovu kutupiwa
bure mna nituhumu ya fitina kuyagawa
nami ni mwanaadamu, si vyema kunibagua

nami ni mja mwenzenu, hata mkinichukia
aibu yangu ndo yenu, kama mtafikiria




Maana kwa nyimbo kama hiyo "mabwabwa" lazima waipende wanaona inawahusu! ...🙁

Ila mie leo najitolea kukurushia taarab zisizolenga mapenzi moja kwa moja, japo zinalenga kwenye jamii

Unajua watu wamakariri sana kuhusu huu muziki...Kiasi kwamba zile nyimbo za kuonya na kushauri zimerushwa kapu moja na hizo nye upupu wa ngono!!

Na hata kama ingekuwa hivyo...sioni tatizo kwa sababu na hayo mambo ni sehemu ya maisha!!

Ngoja nizidi kuwa denti mwenye nidhamu!!
 
DC kuna hii inazungumzia bahati

"Bahati ikenda kombo, mwerevu huwa mjinga
Huwa mjinga wa mambo, bahati ikikuchenga
jambo mzuri wa umbo, wabaya humsimanga

mwenzetu umeshapewa bahati usiitupe
Mungu akiiondoa, fikiri itakuwaje

 
Last edited by a moderator:
Unajua watu wamakariri sana kuhusu huu muziki...Kiasi kwamba zile nyimbo za kuonya na kushauri zimerushwa kapu moja na hizo nye upupu wa ngono!!

Na hata kama ingekuwa hivyo...sioni tatizo kwa sababu na hayo mambo ni sehemu ya maisha!!

Ngoja nizidi kuwa denti mwenye nidhamu!!

Hii ya Bahati ina maneno mazito


anasema bahati ikipotea unakuwa kama "ng'ombe kasoro mchunga", hata ndugu wanaweza kukutenga

Taarab inazungumza sana mapenzi kwa sababu ndio sehemu kubwa ya maisha yetu, lakini tusisahu kuwa pia inazungumza na vitu vyengine.



Hii inawazungumza wale watu "nawatende wao, wakitenda wenzao huwa mwao"

 
Last edited by a moderator:
kuna mambo mengine huwa ni ya kufikirika tu halafu watu tunataka kuyafanya ndo uhalisia...gays na taarab, wapenda taarab ni watu wa kurushiana maneno/usutwe nk.

hebu Gee enedelea kutuonyesha upande mwingine wa taarab, muziki bila jasho!!!

Hivi wale mabwabwa wa marekani na ulaya na wao wanahusikaje na taarab??
 
kuna mambo mengine huwa ni ya kufikirika tu halafu watu tunataka kuyafanya ndo uhalisia...gays na taarab, wapenda taarab ni watu wa kurushiana maneno/usutwe nk.

hebu Gee enedelea kutuonyesha upande mwingine wa taarab, muziki bila jasho!!!

Hivi wale mabwabwa wa marekani na ulaya na wao wanahusikaje na taarab??

Unajua labda gays wanapenda taarab kutokana na historia yake. Zamani ulikuwa ukichukuliwa ni muziki wa kike. Sio wasikilizaji, ila wachezaji pamoja na matumizi yake. Wanawake wakitaka kutuma ujumbe kuwa sasa ana mpenzi anatumia taarab, akitaka kusema anaonewa, anatumia huo huo. So umekuwa mziki ambao wanwake wanautumia kisawa sawa kama meneno kwenye khanga-lolz

Sawa wao wakitumia taarab wanajiona na wao wanawake kweli kweli


Anyway leo acha tuangalie na pande nyengine ya taarab

Tena kwa matao, vingi huvi beza, bila ya kuwaza
wapendacho wao, kikiwapendeza, sifa hueneza
mikononi mwao, chongo ni kengeza, huipa na tunza
zile ila zao, ukiwasemeza, hima huzimeza

Na watende wao, kitenda wenzao, ati huwa mwao
na watende wao, ati huwa mwao, kitenda wenzao
 
hii "ushoga" (meaning urafiki wa wanawake wawili")
mwanamme anashangazwa na ushoga wa wanawake.....unafiki mtupu ..........LOLZ

 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: bht
Gee naipenda sana hii nyimbo ya ''ushoga"
 
One of the best of Malika's ....Subira

Kiri moyo wangu kiri, hebu acha kusonona
mema na ovu kujiri, kwa waja hili ni sana
shetwani asikughuri, ingawa dhiki naona
subiri moyo subiri, lisilo mwisho hakuna

Moyo silete majuto, ukavunja wako utu
wala usifanye joto, hayo yafanye si kitu
na dunia ni mapito, na ulimwengu si wetu
si wewe pekee mazito, humfika kila mtu



 
Last edited by a moderator:
Bibi kaombwa mwisho kaingia line .....hahaha some things are just too funny



Hii inawasema wale "wapenda umaarufu"........Kioo kimemcheza


 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom