NYENJENKURU
JF-Expert Member
- Feb 11, 2011
- 1,067
- 299
Ilikuwa ni October 1994 ndipo Mutungirehi alipogaragazwa pale Nkrumah Hall. Soma headline ifuatayo: [UDSM wanaamriwa kuondoka kurudi makwao: {UHURU: November 07, 1994, pg. 1}].
Walioongoza kumtwanga Mutungirehi pale Jukwaani ni kweli mmemtaja Harold Mushi alikuwa Engineering. Mwingine ni Gasper Tracers aliyekuwa 3rd year Electrical Engineering. Huyu ninajua kuwa hadi 1998 alikuwa ni Engineer pale ITV ingawa sasa sijui yuko wapi.
Ila kuna moja wengi mnalisahau na hamlisemi. Wakati Mutungirehi anasulubiwa katibu wake wa DARUSO alikuwa Godwin Ngwilimi. Godwin alipoona Mutungirehi kaparamiwa na kuangushwa chini akachukua kiti na kumponda Harold Mushi ndipo fujo ikazidi...
Baada ya hapo wale vijana wa FOE second year wakati huo wakaenda mbele kufanya fujo...Umenikumbusha mbali sanaaaa.