Maskini Tanzania Yetu

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,015
Jana nilipata ban baada kumuita Magufuli d*****a. Siwezi kuwalaumu wamiliki wa Jamii Forums maana najua nanyi mnafuatiliwa sana kuhusu yanayoandikwa humu ndani na si ajabu kuna mkakati tayari unaandaliwa wa kuifunga Jamii Forums kitu ambacho wanachama wote hapa na hata ambao si wanachama hatutapenda kitokee.

Nchi yetu sasa hivi inapitia kipindi kigumu sana na kama hali itaendelea hivi basi siku za usoni tutaingia katika giza nene sana la kutisha kama hali itaendelea kuwa hivi na Viongozi wastaafu mbali mbali nchini wakiwemo Salim Ahmed Salim, Joseph Sinde Warioba, Ali Hassan Mwinyi na Watanzania wote tukiamua kukaa.

Nasema tutaingia kwenye giza nene maana tunaona mchana kweupe kabisa jinsi katiba ya nchi inavyosiginwa Bungeni na hata uraiani. Bungeni tunaona Wabunge wa vyama vya upinzani wanavyozuiliwa bila ya kuwepo sababu zozote za msingi kuikemea Serikali pale inapokosea au kusoma hotuba zao kupitia Mawaziri Vivuli wa UKAWA kwa sababu tu hotuba hizo zina masuala ambayo Serikali haitaki Watanzania tuyasikie.

Pia tumeona jinsi Serikali ilivyokuja na sababu ambazo haziingii akilini na kuamua kutoonyesha Bunge live. Kwanza Serikali ilidai kwamba gharama ya kurusha matangazo hayo ya bilioni 4 kwa mwaka ni kubwa sana, hivyo katika zama hizi za "kubana matumizi" Serikali haiwezi kuendelea kuingia gharama kubwa kiasi hicho. Zikatokea TV za watu binafsi ambazo ziliomba zirushe matangazo hayo na wao hawakuona shida kulipia hizi gharama za shilingi bilioni 4 kwa mwaka. Serikali ikaona hoja yake ya gharama kubwa haina nguvu tena kama TV za watu binafsi ziko tayari kurusha Bunge live bila matatizo yoyote yale pamoja na gharama za mwaka kufikia bilioni nne. Ndipo Serikali ikaja na sababu mpya ambayo mwanzo hawakuizungumzia kwamba Bunge live linasababisha Watanzania waangalie kipindi hicho na hivyo kushindwa kufanya kazi, sababu ambayo haina ukweli wowote.

Hivi karibuni pia tumeona Bungeni wale Wabunge mahiri katika kuichachafya Serikali Bungeni wakiwemo Halima Mdee, Esther Bulaya, Msigwa, Heche, Lissu, Lema, Sugu, Zitto n.k. wakitafutiwa sababu zisizo na kichwa wala miguu na kamati inayodaiwa ni kamati ya bunge ya maadili. Sababu hizo zisizo na kichwa wala miguu zimesababisha wabunge hawa mahiri wafungiwe kuingia Bungeni kwa vipindi mbali mbali.

Pamoja na jitihada kubwa za kuwanyima Wabunge wa upinzani haki yao ya kikatiba Bungeni kujadili chochote kile Bungeni bila pinganizi la CCM, sasa tunaona juhudi hizo zikifanyika hadi uraiani ambapo vyama vya upinzani vimezuiwa kufanya mikutano ya hadhara, kuandamana, kuongea na Watanzania kupitia vyombo vya habari mbali mbali nchini na pia kukatazwa kufanya shughuli zozote zile za kisiasa mpaka mwaka 2020. Kwa maneno mengine vyama vya upinzani haviruhusiwi kupita huku na kule kutafuta wanachama wapya wa kujiunga na vyama vyao, kutangaza sera zao ili kuvutia wanachama wapya, kukusanya michango toka kwa wanachama wao wa zamani na wapya ili kusaidia katika gharama mbali mbali za kuviendesha vyama hivyo.

Tanzania kama tujuavyo ni nchi ya vyama vingi, na hakuna kipengele chochote ndani ya katiba kinachompa nguvu yoyote yule au taasisi yoyote ile nchini kuzuia kwa kila hali vyama vya upinzani kufanya shughuli zao za kisiasa nchini. Hili linaloendelea sasa la kuvizuia vyama vya upinzani kufanya shughuli zao nchini si jambo jema hata kidogo na lipigwe vita na Watanzania wote wanaoitakia nchi yetu amani.

Sasa imefikia hata wakuu wa mikoa na wilaya nao kupata nguvu za kutisha na kutamka hadharani kwamba watavisambaratisha vyama vya upinzani ambavyo vitafanya shughuli za kisiasa katiika maeneo yao husika. Hawa wanapata wapi nguvu na ujasiri kiasi hiki cha kuweza kuisigina katiba ya nchi mchana kweupe? Mbona hali hii ya kuvizuia vyama vya upinzani kufanya shughuli zao za kisiasa kwa miaka mitano, kunyimwa kujadili chochote wakitakacho bungeni, kukataliwa kusoma hotuba za mawaziri vivuli kwa mpaka waondoe masuala ambayo CCM haitaki Watanzania tuyasikie hatukuiona katika awamu ya pili na ya tatu? Kwanini hali hii ijitokeze katika awamu hii ya tano? Kulikoni?

Tamko la Rais la kuzuia siasa hadi 2020 laanza kutolewa mwangwi na wakuu wa Mikoa.
"Marufuku mikutano ya siasa katika mkoa wangu, wasubiri hadi 2020 kama watakuwa hai. Kama wanataka kujifunza siasa watafute pahali pengine. Nitawafuata hata wakiwa watatu ndani". - Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Daktari Steven Kebwe akiongea na wazee

Polisi nao katika awamu ya tatu na ya nne hawakuwahi kutumika kiasi hiki katika kukandamiza haki ya kikatiba ya vyama vya. Kumetokea nini katika awamu ya tano hadi polisi watumike kiasi hiki katika kuisigina katiba ya nchi yetu? Lini nchi yetu imebadilika kuwa ya chama kimoja badala ya vyama vingi hadi vyama vya upinzani vizuiliwe kufanya shughuli zao za kisiasa nchini? Kwanini basi isitangazwe rasmi hadharani kwamba awamu ya tano imeamua kuvifuta vyama vyote vya upinzani na kurudi zama za kale za Tanzania kuwa nchi ya chama kimoja!?

Kutoka gazeti la Mwananchi:

Friday, July 8, 2016

MAONI YA MHARIRI: Kwa hali ilivyofikia polisi watoe kauli inayoeleweka

Katiba ndiyo inatoa haki na uhuru wa wananchi kujumuika bila kuvunja sheria. Ibara ya 18 ya Katiba Sehemu ya (1) inasema bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati.

Jeshi la Polisi linakabiliwa na swali jepesi kwamba katika utumishi wake linamtumikia nani? Majibu ya swali hili yatawasaidia wananchi kujua kwanini limekuwa likijichanganya linapotoa sababu za kufuta mikutano ya vyama vya siasa.

Katiba ndiyo inatoa haki na uhuru wa wananchi kujumuika bila kuvunja sheria. Ibara ya 18 ya Katiba Sehemu ya (1) inasema bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati.

Sehemu ya (2) inasema kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi, na pia juu ya masuala muhimu kwa jamii.

Mbali ya Ibara hiyo ya 18 ya Katiba, sura ya 258 ya Sheria ya Vyama vya Siasa sehemu ya IV inatoa haki kwa chama chochote cha siasa kuandaa mkutano au maandamano. Ibara ya 11 (1) inasema chama chochote chenye usajili wa muda au wa kudumu; (a) kinaruhusiwa kuandaa mikutano yake eneo lolote katika Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kujitangaza au kutafuta wanachama baada ya kuwapa taarifa polisi wa eneo husika; (b) kinastahili kupewa kinga na msaada wa ulinzi ili kiweze kufanya mkutano wake kwa amani.

Ili shughuli hizo za kisiasa ziweze kufanyika kwa amani, vyama vya siasa vinapaswa kulijulisha Jeshi la Polisi ili uwepo ulinzi kwa usalama wao.

Sheria ya Jeshi la Polisi kifungu cha 43 sehemu ya (1) inasema yeyote anayetaka kuandaa mkutano au mkusanyiko au kufanya maandamano atapaswa kuwajulisha polisi katika muda usiopungua saa 48 kabla ya siku ya mkutano, muda na mahali kujulisha kwamba siku ya mkutano au maandamano imekaribia.

Japokuwa Katiba iko wazi na sheria ya vyama vya siasa pamoja na ya Jeshi la Polisi zote zinatoa uhuru kwa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu na wa muda kufanya mikutano yao wakati wowote, mahali popote ili kunadi sera na kupata wanachama, Jeshi la Polisi limekuwa likivunja na kusambaratisha mikutano ya vyama vya upinzani pekee lakini linalinda ya chama tawala.

Kila polisi walipozuia mikutano ya upinzani walitoa sababu nyingine hazina mashiko. Mfano, walipozuia mahalafi ya wanafunzi wa vyuo vikuu wafuasi wa Chadema mjini Dodoma walidai kuna ugonjwa usiojulikana na walipozuia mkutano wa Chadema mjini Kahama walidai ni kuzuia vurugu baada ya CCM kusema itafanya mikutano ya kufuta nyayo za Chadema.

Sasa vijana wa Chadema wanajihamasisha kwenda Dodoma kuvuruga mkutano wa CCM, je, polisi watazuia kama walivyofanya CCM waliposema wataandaa mikutano ya kufuta nyayo za Chadema?

Sisi tunadhani, jeuri hii ya vijana wa Chadema inatokana na polisi wenyewe kujichanganya kutokana na sababu walizokuwa wanatoa walipokuwa wanafuta mikutano ya Chadema.

Tunaamini kuwa polisi wanaweza kuepusha vurugu hizi za vyama kama wangekuwa wanatoa sababu za msingi, lakini kufuta mkutano wa chama fulani kutokana na kauli ya chama kingine haikuwa muafaka.

Yaliyotokea Zanzibar na yanayoendelea kutokea kule wote tunayajua sasa imefikia mpaka mawakili wanatishiwa kuwatetea watuhumiwa na kuambiwa kufanya hivyo kutasababisha na wao waunganishwe kwenye kesi husika na hivyo kukamwatwa na kuswekwa lupango.

Natumai hekima na busara vitatumika ili kuepusha nchi kuingia katika giza nene kama uhuru wa kikatiba uliopewa vyama vya upinzani utaendelea kuminywa bila sababu zisizo na mashiko hata chembe.

Mungu ibariki Tanzania.

12472600_590442954439402_3258901789086524724_n-jpg.364341




 
Kheeee! Mi nilidhani Tanzania hakuna madhila yoyote yale...kwamba mambo yote ni mswano tu!

Sasa haya manung'uniko ya nini tena?
 
Mkuu umelalamika sana we ni kamanda usife moyo wa kukata tamaa . Mapambano yanaendelea mods akili zao zimeshikwa.
 
Kheeee! Mi nilidhani Tanzania hakuna madhila yoyote yale...kwamba mambo yote ni mswano tu!

Sasa haya manung'uniko ya nini tena?

Mkuu upo salama ? Maana police officers wanafanya Yao. Karibu Scandinavia.
 
Shukrani Mkuu hakuna mwenye hati miliki ya Tanzania, nchi hii ikiingia kwenye giza nene basi gharika litakuwa ni kwa Watanzania wote bila kujali itikadi zao au kama wana vyama au la.

Mkuu umelalamika sana we ni kamanda usife moyo wa kukata tamaa . Mapambano yanaendelea mods akili zao zimeshikwa.
 
Kuwabana polisi kuwauwa Negros Mara kwa Mara.

Kama hawezi kuwabana negroes kuwaua negroes wenzao ndo ataweza kuwabana polisi wasiofaa kuwaua watu?

La msingi ni nini kinachotokea baada ya uhalifu kufanywa!

Halafu Marekani siyo kama huko mavumbini. Hakuna polisi wa nchi nzima huko.

Kila eneo lina mapolisi wake locally ambao bosi wao siyo Obama.
 
Jana nilipata ban baada kumuita Magufuli d*****a. Siwezi kuwalaumu wamiliki wa Jamii Forums maana najua nanyi mnafuatiliwa sana kuhusu yanayoandikwa humu ndani na si ajabu kuna mkakati tayari unaandaliwa wa kuifunga Jamii Forums kitu ambacho wanachama wote hapa na hata ambao si wanachama hatutapenda kitokee.

Nchi yetu sasa hivi inapitia kipindi kigumu sana na kama hali itaendelea hivi basi siku za usoni tutaingia katika giza nene sana la kutisha kama hali itaendelea kuwa hivi na Viongozi wastaafu mbali mbali nchini wakiwemo Salim Ahmed Salim, Joseph Sinde Warioba, Ali Hassan Mwinyi na Watanzania wote tukiamua kukaa.

Nasema tutaingia kwenye giza nene maana tunaona mchana kweupe kabisa jinsi katiba ya nchi inavyosiginwa Bungeni na hata uraiani. Bungeni tunaona Wabunge wa vyama vya upinzani wanavyozuiliwa bila ya kuwepo sababu zozote za msingi kuikemea Serikali pale inapokosea au kusoma hotuba zao kupitia Mawaziri Vivuli wa UKAWA kwa sababu tu hotuba hizo zina masuala ambayo Serikali haitaki Watanzania tuyasikie.

Pia tumeona jinsi Serikali ilivyokuja na sababu ambazo haziingii akilini na kuamua kutoonyesha Bunge live. Kwanza Serikali ilidai kwamba gharama ya kurusha matangazo hayo ya bilioni 4 kwa mwaka ni kubwa sana, hivyo katika zama hizi za "kubana matumizi" Serikali haiwezi kuendelea kuingia gharama kubwa kiasi hicho. Zikatokea TV za watu binafsi ambazo ziliomba zirushe matangazo hayo na wao hawakuona shida kulipia hizi gharama za shilingi bilioni 4 kwa mwaka. Serikali ikaona hoja yake ya gharama kubwa haina nguvu tena kama TV za watu binafsi ziko tayari kurusha Bunge live bila matatizo yoyote yale pamoja na gharama za mwaka kufikia bilioni nne. Ndipo Serikali ikaja na sababu mpya ambayo mwanzo hawakuizungumzia kwamba Bunge live linasababisha Watanzania waangalie kipindi hicho na hivyo kushindwa kufanya kazi, sababu ambayo haina ukweli wowote.

Hivi karibuni pia tumeona Bungeni wale Wabunge mahiri katika kuichachafya Serikali Bungeni wakiwemo Halima Mdee, Esther Bulaya, Msigwa, Heche, Lissu, Lema, Sugu, Zitto n.k. wakitafutiwa sababu zisizo na kichwa wala miguu na kamati inayodaiwa ni kamati ya bunge ya maadili. Sababu hizo zisizo na kichwa wala miguu zimesababisha wabunge hawa mahiri wafungiwe kuingia Bungeni kwa vipindi mbali mbali.

Pamoja na jitihada kubwa za kuwanyima Wabunge wa upinzani haki yao ya kikatiba Bungeni kujadili chochote kile Bungeni bila pinganizi la CCM, sasa tunaona juhudi hizo zikifanyika hadi uraiani ambapo vyama vya upinzani vimezuiwa kufanya mikutano ya hadhara, kuandamana, kuongea na Watanzania kupitia vyombo vya habari mbali mbali nchini na pia kukatazwa kufanya shughuli zozote zile za kisiasa mpaka mwaka 2020. Kwa maneno mengine vyama vya upinzani haviruhusiwi kupita huku na kule kutafuta wanachama wapya wa kujiunga na vyama vyao, kutangaza sera zao ili kuvutia wanachama wapya, kukusanya michango toka kwa wanachama wao wa zamani na wapya ili kusaidia katika gharama mbali mbali za kuviendesha vyama hivyo.

Tanzania kama tujuavyo ni nchi ya vyama vingi, na hakuna kipengele chochote ndani ya katiba kinachompa nguvu yoyote yule au taasisi yoyote ile nchini kuzuia kwa kila hali vyama vya upinzani kufanya shughuli zao za kisiasa nchini. Hili linaloendelea sasa la kuvizuia vyama vya upinzani kufanya shughuli zao nchini si jambo jema hata kidogo na lipigwe vita na Watanzania wote wanaoitakia nchi yetu amani.

Sasa imefikia hata wakuu wa mikoa na wilaya nao kupata nguvu za kutisha na kutamka hadharani kwamba watavisambaratisha vyama vya upinzani ambavyo vitafanya shughuli za kisiasa katiika maeneo yao husika. Hawa wanapata wapi nguvu na ujasiri kiasi hiki cha kuweza kuisigina katiba ya nchi mchana kweupe? Mbona hali hii ya kuvizuia vyama vya upinzani kufanya shughuli zao za kisiasa kwa miaka mitano, kunyimwa kujadili chochote wakitakacho bungeni, kukataliwa kusoma hotuba za mawaziri vivuli kwa mpaka waondoe masuala ambayo CCM haitaki Watanzania tuyasikie hatukuiona katika awamu ya pili na ya tatu? Kwanini hali hii ijitokeze katika awamu hii ya tano? Kulikoni?

Tamko la Rais la kuzuia siasa hadi 2020 laanza kutolewa mwangwi na wakuu wa Mikoa.
"Marufuku mikutano ya siasa katika mkoa wangu, wasubiri hadi 2020 kama watakuwa hai. Kama wanataka kujifunza siasa watafute pahali pengine. Nitawafuata hata wakiwa watatu ndani". - Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Daktari Steven Kebwe akiongea na wazee

Polisi nao katika awamu ya tatu na ya nne hawakuwahi kutumika kiasi hiki katika kukandamiza haki ya kikatiba ya vyama vya. Kumetokea nini katika awamu ya tano hadi polisi watumike kiasi hiki katika kuisigina katiba ya nchi yetu? Lini nchi yetu imebadilika kuwa ya chama kimoja badala ya vyama vingi hadi vyama vya upinzani vizuiliwe kufanya shughuli zao za kisiasa nchini? Kwanini basi isitangazwe rasmi hadharani kwamba awamu ya tano imeamua kuvifuta vyama vyote vya upinzani na kurudi zama za kale za Tanzania kuwa nchi ya chama kimoja!?

Kutoka gazeti la Mwananchi:

Friday, July 8, 2016

MAONI YA MHARIRI: Kwa hali ilivyofikia polisi watoe kauli inayoeleweka

Katiba ndiyo inatoa haki na uhuru wa wananchi kujumuika bila kuvunja sheria. Ibara ya 18 ya Katiba Sehemu ya (1) inasema bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati.

Jeshi la Polisi linakabiliwa na swali jepesi kwamba katika utumishi wake linamtumikia nani? Majibu ya swali hili yatawasaidia wananchi kujua kwanini limekuwa likijichanganya linapotoa sababu za kufuta mikutano ya vyama vya siasa.

Katiba ndiyo inatoa haki na uhuru wa wananchi kujumuika bila kuvunja sheria. Ibara ya 18 ya Katiba Sehemu ya (1) inasema bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati.

Sehemu ya (2) inasema kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi, na pia juu ya masuala muhimu kwa jamii.

Mbali ya Ibara hiyo ya 18 ya Katiba, sura ya 258 ya Sheria ya Vyama vya Siasa sehemu ya IV inatoa haki kwa chama chochote cha siasa kuandaa mkutano au maandamano. Ibara ya 11 (1) inasema chama chochote chenye usajili wa muda au wa kudumu; (a) kinaruhusiwa kuandaa mikutano yake eneo lolote katika Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kujitangaza au kutafuta wanachama baada ya kuwapa taarifa polisi wa eneo husika; (b) kinastahili kupewa kinga na msaada wa ulinzi ili kiweze kufanya mkutano wake kwa amani.

Ili shughuli hizo za kisiasa ziweze kufanyika kwa amani, vyama vya siasa vinapaswa kulijulisha Jeshi la Polisi ili uwepo ulinzi kwa usalama wao.

Sheria ya Jeshi la Polisi kifungu cha 43 sehemu ya (1) inasema yeyote anayetaka kuandaa mkutano au mkusanyiko au kufanya maandamano atapaswa kuwajulisha polisi katika muda usiopungua saa 48 kabla ya siku ya mkutano, muda na mahali kujulisha kwamba siku ya mkutano au maandamano imekaribia.

Japokuwa Katiba iko wazi na sheria ya vyama vya siasa pamoja na ya Jeshi la Polisi zote zinatoa uhuru kwa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu na wa muda kufanya mikutano yao wakati wowote, mahali popote ili kunadi sera na kupata wanachama, Jeshi la Polisi limekuwa likivunja na kusambaratisha mikutano ya vyama vya upinzani pekee lakini linalinda ya chama tawala.

Kila polisi walipozuia mikutano ya upinzani walitoa sababu nyingine hazina mashiko. Mfano, walipozuia mahalafi ya wanafunzi wa vyuo vikuu wafuasi wa Chadema mjini Dodoma walidai kuna ugonjwa usiojulikana na walipozuia mkutano wa Chadema mjini Kahama walidai ni kuzuia vurugu baada ya CCM kusema itafanya mikutano ya kufuta nyayo za Chadema.

Sasa vijana wa Chadema wanajihamasisha kwenda Dodoma kuvuruga mkutano wa CCM, je, polisi watazuia kama walivyofanya CCM waliposema wataandaa mikutano ya kufuta nyayo za Chadema?

Sisi tunadhani, jeuri hii ya vijana wa Chadema inatokana na polisi wenyewe kujichanganya kutokana na sababu walizokuwa wanatoa walipokuwa wanafuta mikutano ya Chadema.

Tunaamini kuwa polisi wanaweza kuepusha vurugu hizi za vyama kama wangekuwa wanatoa sababu za msingi, lakini kufuta mkutano wa chama fulani kutokana na kauli ya chama kingine haikuwa muafaka.

Yaliyotokea Zanzibar na yanayoendelea kutokea kule wote tunayajua sasa imefikia mpaka mawakili wanatishiwa kuwatetea watuhumiwa na kuambiwa kufanya hivyo kutasababisha na wao waunganishwe kwenye kesi husika na hivyo kukamwatwa na kuswekwa lupango.

Natumai hekima na busara vitatumika ili kuepusha nchi kuingia katika giza nene kama uhuru wa kikatiba uliopewa vyama vya upinzani utaendelea kuminywa bila sababu zisizo na mashiko hata chembe.

Mungu ibariki Tanzania.

12472600_590442954439402_3258901789086524724_n-jpg.364341




Mkuu kwa thread hii, kama hawajakuelewa basi wa subiri kueleweshwa na "NGUVU" ya Mungu.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Jana nilipata ban baada kumuita Magufuli d*****a. Siwezi kuwalaumu wamiliki wa Jamii Forums maana najua nanyi mnafuatiliwa sana kuhusu yanayoandikwa humu ndani na si ajabu kuna mkakati tayari unaandaliwa wa kuifunga Jamii Forums kitu ambacho wanachama wote hapa na hata ambao si wanachama hatutapenda kitokee.

Nchi yetu sasa hivi inapitia kipindi kigumu sana na kama hali itaendelea hivi basi siku za usoni tutaingia katika giza nene sana la kutisha kama hali itaendelea kuwa hivi na Viongozi wastaafu mbali mbali nchini wakiwemo Salim Ahmed Salim, Joseph Sinde Warioba, Ali Hassan Mwinyi na Watanzania wote tukiamua kukaa.

Nasema tutaingia kwenye giza nene maana tunaona mchana kweupe kabisa jinsi katiba ya nchi inavyosiginwa Bungeni na hata uraiani. Bungeni tunaona Wabunge wa vyama vya upinzani wanavyozuiliwa bila ya kuwepo sababu zozote za msingi kuikemea Serikali pale inapokosea au kusoma hotuba zao kupitia Mawaziri Vivuli wa UKAWA kwa sababu tu hotuba hizo zina masuala ambayo Serikali haitaki Watanzania tuyasikie.

Pia tumeona jinsi Serikali ilivyokuja na sababu ambazo haziingii akilini na kuamua kutoonyesha Bunge live. Kwanza Serikali ilidai kwamba gharama ya kurusha matangazo hayo ya bilioni 4 kwa mwaka ni kubwa sana, hivyo katika zama hizi za "kubana matumizi" Serikali haiwezi kuendelea kuingia gharama kubwa kiasi hicho. Zikatokea TV za watu binafsi ambazo ziliomba zirushe matangazo hayo na wao hawakuona shida kulipia hizi gharama za shilingi bilioni 4 kwa mwaka. Serikali ikaona hoja yake ya gharama kubwa haina nguvu tena kama TV za watu binafsi ziko tayari kurusha Bunge live bila matatizo yoyote yale pamoja na gharama za mwaka kufikia bilioni nne. Ndipo Serikali ikaja na sababu mpya ambayo mwanzo hawakuizungumzia kwamba Bunge live linasababisha Watanzania waangalie kipindi hicho na hivyo kushindwa kufanya kazi, sababu ambayo haina ukweli wowote.

Hivi karibuni pia tumeona Bungeni wale Wabunge mahiri katika kuichachafya Serikali Bungeni wakiwemo Halima Mdee, Esther Bulaya, Msigwa, Heche, Lissu, Lema, Sugu, Zitto n.k. wakitafutiwa sababu zisizo na kichwa wala miguu na kamati inayodaiwa ni kamati ya bunge ya maadili. Sababu hizo zisizo na kichwa wala miguu zimesababisha wabunge hawa mahiri wafungiwe kuingia Bungeni kwa vipindi mbali mbali.

Pamoja na jitihada kubwa za kuwanyima Wabunge wa upinzani haki yao ya kikatiba Bungeni kujadili chochote kile Bungeni bila pinganizi la CCM, sasa tunaona juhudi hizo zikifanyika hadi uraiani ambapo vyama vya upinzani vimezuiwa kufanya mikutano ya hadhara, kuandamana, kuongea na Watanzania kupitia vyombo vya habari mbali mbali nchini na pia kukatazwa kufanya shughuli zozote zile za kisiasa mpaka mwaka 2020. Kwa maneno mengine vyama vya upinzani haviruhusiwi kupita huku na kule kutafuta wanachama wapya wa kujiunga na vyama vyao, kutangaza sera zao ili kuvutia wanachama wapya, kukusanya michango toka kwa wanachama wao wa zamani na wapya ili kusaidia katika gharama mbali mbali za kuviendesha vyama hivyo.

Tanzania kama tujuavyo ni nchi ya vyama vingi, na hakuna kipengele chochote ndani ya katiba kinachompa nguvu yoyote yule au taasisi yoyote ile nchini kuzuia kwa kila hali vyama vya upinzani kufanya shughuli zao za kisiasa nchini. Hili linaloendelea sasa la kuvizuia vyama vya upinzani kufanya shughuli zao nchini si jambo jema hata kidogo na lipigwe vita na Watanzania wote wanaoitakia nchi yetu amani.

Sasa imefikia hata wakuu wa mikoa na wilaya nao kupata nguvu za kutisha na kutamka hadharani kwamba watavisambaratisha vyama vya upinzani ambavyo vitafanya shughuli za kisiasa katiika maeneo yao husika. Hawa wanapata wapi nguvu na ujasiri kiasi hiki cha kuweza kuisigina katiba ya nchi mchana kweupe? Mbona hali hii ya kuvizuia vyama vya upinzani kufanya shughuli zao za kisiasa kwa miaka mitano, kunyimwa kujadili chochote wakitakacho bungeni, kukataliwa kusoma hotuba za mawaziri vivuli kwa mpaka waondoe masuala ambayo CCM haitaki Watanzania tuyasikie hatukuiona katika awamu ya pili na ya tatu? Kwanini hali hii ijitokeze katika awamu hii ya tano? Kulikoni?

Tamko la Rais la kuzuia siasa hadi 2020 laanza kutolewa mwangwi na wakuu wa Mikoa.
"Marufuku mikutano ya siasa katika mkoa wangu, wasubiri hadi 2020 kama watakuwa hai. Kama wanataka kujifunza siasa watafute pahali pengine. Nitawafuata hata wakiwa watatu ndani". - Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Daktari Steven Kebwe akiongea na wazee

Polisi nao katika awamu ya tatu na ya nne hawakuwahi kutumika kiasi hiki katika kukandamiza haki ya kikatiba ya vyama vya. Kumetokea nini katika awamu ya tano hadi polisi watumike kiasi hiki katika kuisigina katiba ya nchi yetu? Lini nchi yetu imebadilika kuwa ya chama kimoja badala ya vyama vingi hadi vyama vya upinzani vizuiliwe kufanya shughuli zao za kisiasa nchini? Kwanini basi isitangazwe rasmi hadharani kwamba awamu ya tano imeamua kuvifuta vyama vyote vya upinzani na kurudi zama za kale za Tanzania kuwa nchi ya chama kimoja!?

Kutoka gazeti la Mwananchi:

Friday, July 8, 2016

MAONI YA MHARIRI: Kwa hali ilivyofikia polisi watoe kauli inayoeleweka

Katiba ndiyo inatoa haki na uhuru wa wananchi kujumuika bila kuvunja sheria. Ibara ya 18 ya Katiba Sehemu ya (1) inasema bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati.

Jeshi la Polisi linakabiliwa na swali jepesi kwamba katika utumishi wake linamtumikia nani? Majibu ya swali hili yatawasaidia wananchi kujua kwanini limekuwa likijichanganya linapotoa sababu za kufuta mikutano ya vyama vya siasa.

Katiba ndiyo inatoa haki na uhuru wa wananchi kujumuika bila kuvunja sheria. Ibara ya 18 ya Katiba Sehemu ya (1) inasema bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati.

Sehemu ya (2) inasema kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi, na pia juu ya masuala muhimu kwa jamii.

Mbali ya Ibara hiyo ya 18 ya Katiba, sura ya 258 ya Sheria ya Vyama vya Siasa sehemu ya IV inatoa haki kwa chama chochote cha siasa kuandaa mkutano au maandamano. Ibara ya 11 (1) inasema chama chochote chenye usajili wa muda au wa kudumu; (a) kinaruhusiwa kuandaa mikutano yake eneo lolote katika Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kujitangaza au kutafuta wanachama baada ya kuwapa taarifa polisi wa eneo husika; (b) kinastahili kupewa kinga na msaada wa ulinzi ili kiweze kufanya mkutano wake kwa amani.

Ili shughuli hizo za kisiasa ziweze kufanyika kwa amani, vyama vya siasa vinapaswa kulijulisha Jeshi la Polisi ili uwepo ulinzi kwa usalama wao.

Sheria ya Jeshi la Polisi kifungu cha 43 sehemu ya (1) inasema yeyote anayetaka kuandaa mkutano au mkusanyiko au kufanya maandamano atapaswa kuwajulisha polisi katika muda usiopungua saa 48 kabla ya siku ya mkutano, muda na mahali kujulisha kwamba siku ya mkutano au maandamano imekaribia.

Japokuwa Katiba iko wazi na sheria ya vyama vya siasa pamoja na ya Jeshi la Polisi zote zinatoa uhuru kwa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu na wa muda kufanya mikutano yao wakati wowote, mahali popote ili kunadi sera na kupata wanachama, Jeshi la Polisi limekuwa likivunja na kusambaratisha mikutano ya vyama vya upinzani pekee lakini linalinda ya chama tawala.

Kila polisi walipozuia mikutano ya upinzani walitoa sababu nyingine hazina mashiko. Mfano, walipozuia mahalafi ya wanafunzi wa vyuo vikuu wafuasi wa Chadema mjini Dodoma walidai kuna ugonjwa usiojulikana na walipozuia mkutano wa Chadema mjini Kahama walidai ni kuzuia vurugu baada ya CCM kusema itafanya mikutano ya kufuta nyayo za Chadema.

Sasa vijana wa Chadema wanajihamasisha kwenda Dodoma kuvuruga mkutano wa CCM, je, polisi watazuia kama walivyofanya CCM waliposema wataandaa mikutano ya kufuta nyayo za Chadema?

Sisi tunadhani, jeuri hii ya vijana wa Chadema inatokana na polisi wenyewe kujichanganya kutokana na sababu walizokuwa wanatoa walipokuwa wanafuta mikutano ya Chadema.

Tunaamini kuwa polisi wanaweza kuepusha vurugu hizi za vyama kama wangekuwa wanatoa sababu za msingi, lakini kufuta mkutano wa chama fulani kutokana na kauli ya chama kingine haikuwa muafaka.

Yaliyotokea Zanzibar na yanayoendelea kutokea kule wote tunayajua sasa imefikia mpaka mawakili wanatishiwa kuwatetea watuhumiwa na kuambiwa kufanya hivyo kutasababisha na wao waunganishwe kwenye kesi husika na hivyo kukamwatwa na kuswekwa lupango.

Natumai hekima na busara vitatumika ili kuepusha nchi kuingia katika giza nene kama uhuru wa kikatiba uliopewa vyama vya upinzani utaendelea kuminywa bila sababu zisizo na mashiko hata chembe.

Mungu ibariki Tanzania.

12472600_590442954439402_3258901789086524724_n-jpg.364341



Pole sana! JF kama ulivyosema, nao wanabanwa sidhani kama wanapenda kufanya hayo. Hilo neno d........ta lilikuwa halina zuio humu of very recent, nadhani wamezuiwa.
 
tunataka mwenyekiti chadema awe na ukomo, katiba ya chama ibadilishwe!! wanachama tumechokaa, IPO Siku haki itapatkana!!
 
Back
Top Bottom