Naungana na mleta uzi Geita pamebadlika kiasi chake, mim nimezaliwa na kukulia geita toka miaka ya 90s, Elim yang ya msingi nimesoma hapo pia
Kipind hiko hakukua na soko zuri kama linalojengwa sasa,hakukua na maji kama sasa wala miundombinu ya barabara haikua rafk sana. Ilituchua hadi masaa manne kutembea kwa basi la Lushanga au Nyehunge toka Mwanza mpk Geita umbal wa km90 tu
Zaman mji uliishia Maili moja (Gerage ya Lushanga) upande wa kaskazin na Mbugani upande wa kusini ila kwa sasa ni habari nyingne kabisa
Kaz bado ipo kipind hiki ambacho imekua Mkoa maendeleo ya kijamii yanapaswa kufanana na yale tunayo yaona mikoa mingne mipya kama Njombe na Simiyu/Bariadi