Hammaz
JF-Expert Member
- May 16, 2018
- 7,019
- 15,234
Kwani ni nini maana ya Hammaz?Akhi unabishana na mtu anayejiita hammaz? Huyo jamaa anawasingizia wanazuoni tu wala haweki marejeo yao humu.Wapo watu wengi sana watakutajia majina lukuki na rejea nyingi za uongo za wanazuoni wengi waliotangulia . Aqidah ya ahlul sunna wal jamaa ipo wazi kabisa kuwa ALLAH yupo juu ya arshi..ipo hivyo na itaendelea kuwa hivyo.
Hao wanaosema kuwa ALLAH hayupo juu ya arshi yake wanaficha tu aqidah zao , mwisho wa siku atajifunua na kusema ALLAH yupo kila sehemu.
Hata mwanangu mdogo wa mwaka mmoja nikimuuliza suali kuwa ALLAH yupo wapi ,atanijibu kuwa ALLAH yupo juu!!
Unajua kupinga/kubisha ni rahisi sana! Na ndiyo kazi ambayo inahitaji zero qualifications, ni kwa sababu kila mtu anaiweza.
"Majina lukuki na rejea za uongo za wanawazuoni." Hapa hujajibu, bali umetuhumu na ukifanya hivi hujengi bali unabomoa zaidi na kwa watu wanaohitaji manufaa kwenye mjadala wataona unafanya malumbano yasiyo na msingi. Maadamu umetuhumu sipo sawa ni jukumu lako kuleta kilicho sahihi.
Bw. Mkubwa uliyemkoti na kuzingumzia mimi amesema Mungu yupo juu ya Arsh, akaleta na uthibitisho wa aya kuwa baada ya uumbaji wa mbingu na ardhi kisha Mungu aka stawaa alal arshi. Aya ipo wazi kabisa na imeelezea kwa uwazi kabisa. Kwa namna hii Hammaz akaja na hadithi za wazi na niliziandika kwa haraka nyengine hazijakaa sawa kiuandishi lakini maudhui yake yapo wazi.
Mtume amesema mmoja wenu akiswali, asiteme mate mbele kwani Allah yupo mbele yake. Mwisho wa kunukuu.
Hadithi ambayo Allah akimuuliza mja wake kwa nini hakuenda kumzuru kipindi alipokuwa mgonjwa. Mja akauliza Allah nawe huumwa? Mungu akajibu fulani aliumwa, laiti ungelimzuru ungenipata kwake. Mwisho wa kunukuu.
Mtume anasema unaposujudu unakua karibu na Mungu. Mwisho wa kunukuu.
Hadithi hizo chache zipo wazi kabisa mithili ya aya aliyoitoa Bwana Mkubwa. Swali ni hili!
-Mungu ametajwa yupo juu ya Arshi
-Mungu yupo kwa wagonjwa
-Mungu yupo mbele unaposwali.
-Mungu huyu huyu ambaye ametajwa sehemu hizo zote nilizonukuu ukisujudu upo nae karibu.
Sasa Mungu yupo wapi?


,