Salaam wanabodi,
Very simple. Swali linajieleza hapo juu. Je Mungu yuko wapi? Kabla ya Mungu kuumba ulimwengu/dunia na vitu vyoooote vilivyopo, yeye binafsi alikuwa wapi? Alikuwa kwenye nini? Aliketi au kusimama kwenye kitu gani? Je ni yeye aliyeumba sayari nyingine zaidi ya 9 zinazofahamika? Kwanini amemuweka mwanadamu kwenye sayari moja tu ya DUNIA?
Swali zuri japo ukishaelewa msingi linakuwa la kijinga sana. Kwa hiyo nitakusaidia kuuona msingi na kuona kwa nini ni swali lisilo na maana.
Kitu cha msingi hapa ni kuwa yote nitakayoongelea ni kwa mujibu wa Biblia na kwa sababu naamini, kwa sababu nzito tu, kuwa Biblia ni Neno la Mungu na kuwa Mungu aliyejifunua ndiye Mungu muumba mbingu na nchi. Kwa hiyo jibu ni very specific. Kama unataka majibu juu ya jumla sina na wala sitawajibika kujibia miungu.
Biblia inafungua na mstari huu:
"Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi" - Mwanzo 1:1
Hapo maneno ya msingi ni Mwanzo, Mbingu na Nchi. Mstari huu unatuonesha kuwa kuna kipindi kulikuwa na mwanzo yaani muda haukuwepo ziku zote ulianza katika "kipindi" fulani. Kabla ya mwanzo hakukuwa na muda.
Pili tunaona Mungu akiumba mbingu na nchi. Mbingu na nchi au ulimwengu (universe) kama unavyofahamika kisayansi ni nafasi. Tunajua kuwa Ulimwengu upo katika muda na nafasi. Muda unatuambia wakati kitu kimefanyika au kimekuwepo na nafasi inatuambia mahali tukio lilifanyika. Huwezi kuwa na muda bila nafasi, kwa sababi ili kitu kifanyike au kiwepo kwenye ulimwengu huu lazima kiwe katika nafasi fulani na huwezi kusema nafasi ni nafasi mpaka iwepo ndani ya muda.
Kwa sababu wakati-nafasi sio mada niishie hapa. Ila ili ulimwengu wetu uwepo ni lazima wakati na nafasi viwepo kwa wakati mmoja. Na hapa Biblia inatuambia Mungu aliumba wakati na nafasi.
Tunajuaje? Kwa sababu Biblia si tu inatuambia Mungu aliumba mbingu na nchi "hapo mwanzo", bali pia inatuambia kuwa huyu Mungu alikuwako tayari kabla ya huo mwanzo. Kwa lugha rahisi kabla ya huo mwanzo (muda) kuwepo, Mungu alikuwepo!
"Hapo mwanzo
kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika" Yohana 1:1-3
Na ndio maana jina lake anaitwa NIKO. Yaani baada ya muda Yeye yuko, "hapo mwanzo" Yeye yuko na kabla ya muda Yeye yuko!
"Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n’nani? Niwaambie nini? Mungu akamwambia Musa, MIMI NIKO AMBAYE NIKO; akasema, Ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli; MIMI NIKO amenituma kwenu" - Kutoka 3:13-14
Kwa hiyo msingi hapa ni kuwa
1. Ulimwengu na vyote vilivyomo, vinavyoonekana na visivyoonekana viliumbwa hapo mwanzo
2. Muda na Nafasi havikuwepo milele, kuna wakati hakukuwa na wakati wala nafasi.
3. Mungu Yehova Yeye Yuko, kabla ya wakati na wakati utakapokoma.
Tukirudi swali la msingi, ambalo lina sehemu mbili:
Kuuliza Mungu yupo wapi maana yake unadhania Mungu anafungwa na muda na nafasi. Maana ukisema yuko wapi unaongelea muda na nafasi. Mfano tukisema Mwanyuma yuko wapi, jibu litakuwa linaambatana na nafasi na muda. Kwa hiyo jibu la swali hili lina dhahania ndani yake kuwa "wapi" hiyo itakuwa ndani ya huu ulimwengu uliofungwa kwa muda na nafasi.
Basi Jibu lake ni kuwa Mungu yupo kila mahali, katika ulimwengu wetu huu. Lakini kwa sababu Mungu hafungwi na muda na nafasi, basi kuna jibu ambalo linapaswa kufafanuliwa hapa kwamba nje ya ulimwengu huu wa muda-nafasi Mungu Yuko! Kwa sababu nje ya huu ulimwengu hakuna kitu kinaitwa wapi, kwa sababu ili kuwe na wapi unahitaji uwe na muda na nafasi.
Kujibu swali lako kwa ukamilifu ni kuwa Mungu YUKO! iwe ni mahali popote, muda wowote au iwe nje ya muda, Yeye Yuko!
Kabla ya Mungu kuumba ulimwengu/dunia na vitu vyoooote vilivyopo, yeye binafsi alikuwa wapi?
Kabla ya kuumba vyote, hakukuwa na muda wala nafasi. Kwa hiyo kusema alikuwa wapi ni swali la kijinga kwa sababu hakukuwa na wapi bado. Au ukisema Mungu alianza lini ni swali la kipuuzi pia kwa sababu ukirudi nyuma kabla ya mwanzo hakuna muda na hivyo kuanza (muda) hakupo!
Kwa hiyo jibu rahisi ni kuwa kabla ya vyote kuumbwa Yeye alikuwepo. Siku zote Yehova Yuko na ndio maana jina lake ni MIMI NIKO!