Mungu yuko wapi?

Mungu yuko wapi?

1. Mola muumba yuko juu ya mbingu ya saba juu ya Arshi(hiki ndiyo kiumbe kikubwa zaidi kati ya viumbe alivyo viumba Mola wetu mlezi) yake chini ya Arshi kuna maji na juu ya Arshi kuna kiti cha enzi amestawi huko.

2. Dunia na ulimwengu ni katika viumbe vya mwishoni mwishoni kuumbwa na Mola ila kiumbe cha mwisho kabisa kuumbwa ni sisi wanadamu.

3. Kwa jinsi alivyo jielezea na alivyoelezewa na mitume wake ni kuwa amestawi huko ila hajajielezea kama ameketi kwa namna gani

4. Kuhusu sayari nyingine hakuna mahali katika vitabu vyake vinaonyesha hilo ila tunafahamu ya kuwa kuna viumbe ameumba ambavyo hatuvijui na vyenyewe viko katila uwili. Kwahiyo kama imethibitika kweli sayari zipo basi nazo zimeumbwa na Mola muumba.

5. Yeye ndiyo amejaalia uhai katika dunia, na si pengine. Kwa upande wangu mimi binafsi siamini kama kuna uhai katika sayari nyingine kama zipo lakini, na kama kungekuwa na uhai basi mitume wangetuambia.

Shukrani.

Mungu ameketi yaan anamatako kama
Ww
 
Wakiwa wanakujibu, wanajibu pia je hadithi ya mnara wa baberi ni kweli au si kweli. Maana ndio hadithi inayozungumzia chimbuko la lugha.

Je huo mnara ulikua na urefu gani hadi Mungu aone binadamu watamfikia?.. maana vyombo vya usafiri vinatoka hadi nje ya dunia

Story za uongo zile
 
Katika tumbo la mama kulikuwa na watoto wawili. Mmoja akamuuliza mwenzake: “Je, unaamini maisha baada ya kujifungua?” Yule mwingine akajibu, “Kwa nini, bila shaka. Lazima kuwe na kitu baada ya kujifungua. Labda tuko hapa kujitayarisha kwa kile tutakachokuwa baadaye.”

"Upuuzi," wa kwanza alisema. "Hakuna maisha baada ya kujifungua. Je, hayo yangekuwa maisha ya aina gani?” Wa pili akasema, "Sijui, lakini kutakuwa na mwanga zaidi kuliko hapa. Labda tutatembea kwa miguu yetu na kula kutoka kwa midomo yetu. Labda tutakuwa na hisia zingine ambazo hatuwezi kuelewa sasa.

Wa kwanza akajibu, “Huo ni upuuzi. Kutembea haiwezekani. Na kula kwa midomo yetu? Kichekesho! Kamba ya umbilical hutoa lishe na kila kitu tunachohitaji. Lakini kamba ya umbilical ni fupi sana. Maisha baada ya kujifungua yanapaswa kutengwa kimantiki.” Wa pili alisisitiza, "Nadhani kuna kitu na labda ni tofauti na ilivyo hapa. Labda hatutahitaji kamba hii ya mwili tena." Wa kwanza akajibu, “Upuuzi. Na zaidi ya hayo, ikiwa kuna uhai, basi kwa nini hakuna mtu aliyewahi kurudi kutoka huko? Kujifungua ni mwisho wa maisha, na katika baada ya kuzaa hakuna ila giza na ukimya na usahaulifu. Haitupeleki popote.” “Sawa, sijui,” akasema wa pili, “lakini hakika tutakutana na Mama naye atatutunza.

” Wa kwanza akajibu “Mama? Unamwamini Mama kweli? Hiyo inachekesha. Kama mama yupo, yuko wapi sasa hivi?" Wa pili akasema, “Anatuzunguka pande zote. Tumezungukwa naye. Sisi ni wake. Ni ndani Yake tunaishi. Bila Yeye, ulimwengu huu haungekuwepo na tusingekuwepo." Alisema wa kwanza:

"Kweli, simuoni, kwa hivyo ni sawa kwamba Yeye hayupo." Ambayo wa pili alijibu, "Wakati mwingine, unapokuwa kimya na ukizingatia na kusikiliza, unaweza kuona uwepo Wake, na unaweza kusikia sauti Yake ya upendo, ikiita kutoka juu." Labda hii ilikuwa moja ya maelezo bora ya dhana ya MUNGU.
You nailed it in a very understandable way.

Wajinga acha tuendelee kuwa wajinga wa kisomi na hekaya za anunnaki na planet nibiru

Sent from my SM-J610F using JamiiForums mobile app
 
Kama unamzungumia Mungu wa kweli ambae ni mmoja Allah basi jibu hili hapa
 
Katika tumbo la mama kulikuwa na watoto wawili. Mmoja akamuuliza mwenzake: “Je, unaamini maisha baada ya kujifungua?” Yule mwingine akajibu, “Kwa nini, bila shaka. Lazima kuwe na kitu baada ya kujifungua. Labda tuko hapa kujitayarisha kwa kile tutakachokuwa baadaye.”

"Upuuzi," wa kwanza alisema. "Hakuna maisha baada ya kujifungua. Je, hayo yangekuwa maisha ya aina gani?” Wa pili akasema, "Sijui, lakini kutakuwa na mwanga zaidi kuliko hapa. Labda tutatembea kwa miguu yetu na kula kutoka kwa midomo yetu. Labda tutakuwa na hisia zingine ambazo hatuwezi kuelewa sasa.

Wa kwanza akajibu, “Huo ni upuuzi. Kutembea haiwezekani. Na kula kwa midomo yetu? Kichekesho! Kamba ya umbilical hutoa lishe na kila kitu tunachohitaji. Lakini kamba ya umbilical ni fupi sana. Maisha baada ya kujifungua yanapaswa kutengwa kimantiki.” Wa pili alisisitiza, "Nadhani kuna kitu na labda ni tofauti na ilivyo hapa. Labda hatutahitaji kamba hii ya mwili tena." Wa kwanza akajibu, “Upuuzi. Na zaidi ya hayo, ikiwa kuna uhai, basi kwa nini hakuna mtu aliyewahi kurudi kutoka huko? Kujifungua ni mwisho wa maisha, na katika baada ya kuzaa hakuna ila giza na ukimya na usahaulifu. Haitupeleki popote.” “Sawa, sijui,” akasema wa pili, “lakini hakika tutakutana na Mama naye atatutunza.

” Wa kwanza akajibu “Mama? Unamwamini Mama kweli? Hiyo inachekesha. Kama mama yupo, yuko wapi sasa hivi?" Wa pili akasema, “Anatuzunguka pande zote. Tumezungukwa naye. Sisi ni wake. Ni ndani Yake tunaishi. Bila Yeye, ulimwengu huu haungekuwepo na tusingekuwepo." Alisema wa kwanza:

"Kweli, simuoni, kwa hivyo ni sawa kwamba Yeye hayupo." Ambayo wa pili alijibu, "Wakati mwingine, unapokuwa kimya na ukizingatia na kusikiliza, unaweza kuona uwepo Wake, na unaweza kusikia sauti Yake ya upendo, ikiita kutoka juu." Labda hii ilikuwa moja ya maelezo bora ya dhana ya MUNGU.
Hao watoto wakiwa tumboni walijuaje kama kuna kitu kinaitwa kuzaliwa?
Who certainly informed them about birth?
How did the awareness of birth came to them?
kuwa ipo siku watazaliwa baada ya miezi tisa?

Huenda sijaelewa, naona hiyo nadharia yako Ina ukakasi...ukuilinganisha na suala la mwanadamu kujua kuwa ipo siku atakufa.

Tunajua tutakufa kwa sababu tunaona watu wakifa.
Mapacha waliotungwa mimba, na kujikuta ndani ya mji wa uzazi, wana habari gani kuhusu kuzaliwa? Wanajuaje kama wao ndio mimba ya kwanza au ya pili? Wanaexperience gani ya kuwafanya wapate kujadili afterbirth?

Labda nimekuwa too literal.....huenda pengine ni tafakuri tu kama tafakuri nyingine kuhusu maisha.
 
Salaam wanabodi,

Very simple. Swali linajieleza hapo juu. Je Mungu yuko wapi? Kabla ya Mungu kuumba ulimwengu/dunia na vitu vyoooote vilivyopo, yeye binafsi alikuwa wapi? Alikuwa kwenye nini? Aliketi au kusimama kwenye kitu gani? Je ni yeye aliyeumba sayari nyingine zaidi ya 9 zinazofahamika? Kwanini amemuweka mwanadamu kwenye sayari moja tu ya DUNIA?

Tusaidiane kujua majibu ya haya maswali muhimu kwenye historia ya ulimwengu.
🤣🤣🤣
Yaani ni sawa na kinyago,kinajiuliza alienitengeneza alikua wapi?Aliketi kwenye
nini?
God dwells in the light!..you can not vote him in,you can not vote him out.
 
Sayari ya dunia pamoja na na galaxy yetu yenye sayari 9 (solar system) ni changa sana kiumri ukilinganisha na galaxy zingine. Kwenye uumbaji basi solar system ni ya Karibuni.
 
1. Mola muumba yuko juu ya mbingu ya saba juu ya Arshi(hiki ndiyo kiumbe kikubwa zaidi kati ya viumbe alivyo viumba Mola wetu mlezi) yake chini ya Arshi kuna maji na juu ya Arshi kuna kiti cha enzi amestawi huko.

2. Dunia na ulimwengu ni katika viumbe vya mwishoni mwishoni kuumbwa na Mola ila kiumbe cha mwisho kabisa kuumbwa ni sisi wanadamu.

3. Kwa jinsi alivyo jielezea na alivyoelezewa na mitume wake ni kuwa amestawi huko ila hajajielezea kama ameketi kwa namna gani

4. Kuhusu sayari nyingine hakuna mahali katika vitabu vyake vinaonyesha hilo ila tunafahamu ya kuwa kuna viumbe ameumba ambavyo hatuvijui na vyenyewe viko katila uwili. Kwahiyo kama imethibitika kweli sayari zipo basi nazo zimeumbwa na Mola muumba.

5. Yeye ndiyo amejaalia uhai katika dunia, na si pengine. Kwa upande wangu mimi binafsi siamini kama kuna uhai katika sayari nyingine kama zipo lakini, na kama kungekuwa na uhai basi mitume wangetuambia.

Shukrani.
Hadithi iliyopokelewa na Ibn Jarud, Imam Al Bayhaqii na Bukhari Mtume anasema: "Kana llahu walam ghayrahu shay'aa"
Yaani; alikuwepo Mungu pasipo chochote kuwepo. Kwa maana pasipo Mbingu, Arshi, na kila chochote kuwepo alikuwepo.

Katika msingi wa sheria ya Kiislamu Mungu habadiliki! kama alivyokuwa ndivyo alivyo. Kwa maana; hatuwezi kusema kabla ya Mungu kuanza kuumba haimaanishi kuwa hakuwa na uwezo wa kuumba na alivyoupata ndivyo akaanza kuumba. Msingi wa sheria ya Kiislamu unakataa, unasema Mungu kama alivyokuwa ndivyo alivyo(Tazama aqida katika kitabu cha Imam Tahawi).

Ikiwa hiyo ndiyo hali, kipi kimemfanya abadilike? Yaani; alikuwepo kabla ya chochote na kisha baada ya kuumba akawa juu ya Arshi kama unavyosema. HAYA NI MABADILIKO! Ikiwa hiyo ndiyo hali basi msingi wa sheria ya Kiislamu si sahihi kwani utakuwa umeongopa kwa kusema Mungu habadiliki.
 
Mmh hili swali hata ma Prof Hawana majibu..
 
Hadithi iliyopokelewa na Ibn Jarud, Imam Al Bayhaqii na Bukhari Mtume anasema: "Kana llahu walam ghayrahu shay'aa"
Yaani; alikuwepo Mungu pasipo chochote kuwepo. Kwa maana pasipo Mbingu, Arshi, na kila chochote kuwepo alikuwepo.
Sasa nani amesema amebadilika ? Swali lililo ulizwa ni kuwa Mola yuko wapi ? Hapa hakuna mahusiano na kunadilika.
Katika msingi wa sheria ya Kiislamu Mungu habadiliki! kama alivyokuwa ndivyo alivyo. Kwa maana; hatuwezi kusema kabla ya Mungu kuanza kuumba haimaanishi kuwa hakuwa na uwezo wa kuumba na alivyoupata ndivyo akaanza kuumba. Msingi wa sheria ya Kiislamu unakataa, unasema Mungu kama alivyokuwa ndivyo alivyo(Tazama aqida katika kitabu cha Imam Tahawi).
Sasa kipi kimekuonyesha amebadilika ? Yaani kuwepo juu ya Arshi yake kimabadilika nini au kimebadilisha nini ?

Kitabu hicho ulichokinukuu cha Imam Abuu Jaffar at-Tahawiy kilicho sehereheshwa na Imam Abul Izz al-Hanafi ni kitabu bora katika vitabu bora vinavyoleezea itikadi yetu sisi Waislam.

Muandishi hukumuelewa wala hakuna sehemu aliyo kanusha kwamba Allah hayuko juu ya Arshi yake, Allah, kisicho badilika kwa Allah ni ile mienendo yake na mambo yake.

Anasema Allah aliye juu :

23. Huo ndio mwendo wa Mwenyezi Mungu ulio kwisha pita zamani, wala hutapata mabadiliko katika mwendo wa Mwenyezi Mungu. (al-Fath : 23)


Ikiwa hiyo ndiyo hali, kipi kimemfanya abadilike? Yaani; alikuwepo kabla ya chochote na kisha baada ya kuumba akawa juu ya Arshi kama unavyosema. HAYA NI MABADILIKO! Ikiwa hiyo ndiyo hali basi msingi wa sheria ya Kiislamu si sahihi kwani utakuwa umeongopa kwa kusema Mungu habadiliki.
Kubadilila vipi ? Kwanza hoja yangu umeisoma, nionyeshe katika hayo niliyo yaandika kinamfanya Mola au kinaonyesha Mola amebadilika ?

Kingine mkiwa mnasoma vitabu vya Wanazuoni mnatakiwa msome kwa undani yaani msisome nusu nusu.
 
Sasa nani amesema amebadilika ? Swali lililo ulizwa ni kuwa Mola yuko wapi ? Hapa hakuna mahusiano na kunadilika.
"Kana llahu walam ghayrahu shay aa"

"Kana llahu wala qablahu shay aa"

-Alikuwepo Mungu pasipo chochote kuwepo.

-Alikiwepo Mungu kabla ya chochote kuwepo.

Ni hadithi za Mtume.

Kisha baada ya kuumba thumma stawaa al arshi. Kwa hili ukasema Mungu yupo juu ya Arshi.

-Tunafafanuaje hapa?
Ufafanuzi ni kuwa kuna hali mbili: (1)Pasipo/kabla ya chochote
Kwa maana uwepo wake haukutegemea chochote.

(2) Yupo juu ya Arshi
Kutoka katika pasipo au kabla ya chochote mpaka kuwa juu ya chochote ambacho ni Arshi: Haya ni mazingira au hali mbili tofauti. Pengine tuseme "walam ghayrahu shay aa na kqbla huu shay aa tuipe herufi A. Na juu ya Arshi tuipe herufi B. Hivyo, Mungu alikuwa herufi A kisha akawa herufi B. Huko ni kubadilika.

Tuje kwenye msingi wa sheria ya Kisslamu kuwa Mungu habadiliki. Tukikusanya hadithi za Mtume na maneno yako wewe yanaonyesha Mungu yupo herufi B baada ya kutoka herufi A. Swali linakuja; Haya kwako unayaitaje?
 
Kitabu hicho ulichokinukuu cha Imam Abuu Jaffar at-Tahawiy kilicho sehereheshwa na Imam Abul Izz al-Hanafi ni kitabu bora katika vitabu bora vinavyoleezea itikadi yetu sisi Waislam.

Muandishi hukumuelewa wala hakuna sehemu aliyo kanusha kwamba Allah hayuko juu ya Arshi yake, Allah, kisicho badilika kwa Allah ni ile mienendo yake na mambo yake.
Hiki kitabu kipo ukihitaji tukipitie tutakipitia hapa hapa na hakuna shaka Mkuu ni kuelimishana tuu!
 
"Kana llahu walam ghayrahu shay aa"

"Kana llahu wala qablahu shay aa"

-Alikuwepo Mungu pasipo chochote kuwepo.

-Alikiwepo Mungu kabla ya chochote kuwepo.

Ni hadithi za Mtume.

Kisha baada ya kuumba thumma stawaa al arshi. Kwa hili ukasema Mungu yupo juu ya Arshi.

-Tunafafanuaje hapa?
Ufafanuzi ni kuwa kuna hali mbili: (1)Pasipo/kabla ya chochote
Kwa maana uwepo wake haukutegemea chochote.

(2) Yupo juu ya Arshi
Kutoka katika pasipo au kabla ya chochote mpaka kuwa juu ya chochote ambacho ni Arshi: Haya ni mazingira au hali mbili tofauti. Pengine tuseme "walam ghayrahu shay aa na kqbla huu shay aa tuipe herufi A. Na juu ya Arshi tuipe herufi B. Hivyo, Mungu alikuwa herufi A kisha akawa herufi B. Huko ni kubadilika.

Tuje kwenye msingi wa sheria ya Kisslamu kuwa Mungu habadiliki. Tukikusanya hadithi za Mtume na maneno yako wewe yanaonyesha Mungu yupo herufi B baada ya kutoka herufi A. Swali linakuja; Haya kwako unayaitaje?
Hivi unakielewa unachokoandika ? Hujaonyesha mabadiliko yako wapi ?

Mola habadiliki katika nini ? Hili hujafafanua ?

Hayo siyo mabadiliko, sababu Allah anafanya analo litaka.
 
Hivi unakielewa unachokoandika ? Hujaonyesha mabadiliko yako wapi ?

Mola habadiliki katika nini ? Hili hujafafanua ?

Hayo siyo mabadiliko, sababu Allah anafanya analo litaka.
Mungu anafanya anachotaka lakini si mwenye kuvunja/ku- violet sheria alizoziweka.

مَا زَالَ بِصِفَاتِهِ قَدِيمًا قَبْلَ خَلْقِهِ لَمْ يَزْدَدْ بِكَوْنِهِمْ شَيْئًا لَمْ يَكُنْ قَبْلَهُمْ مِنْ صِفَتِهِ

وَكَمَا كَانَ بِصِفَاتِهِ أَزَلِيًّا كَذَلِكَ لَا يَزَالُ عَلَيْهَا أَبَدِيًّا
Na kama sifa zake zilikuwa kabla ya uumbaji ndivyo zitakavyobakia.

(Al-Aqidah al-Tahawiyyah)​


Allah anasifa 6 zinazoitwa Assifat adh-dhaatiya: (1) Al wujuud (kuwepo), (2) Al Qidam (kutokua na mwanzo), (3) Al Baqaa (kutokua na mwisho na kuwepo milele), (4) Al wahdaaniyya (kutokua na mshirika), (5) Al mukhaalafatu lil hawaadith (kuwa tofauti na viumbe wote kwa namna yoyote), (6) Al Qiyaamu bi nafsihi (kutotegemea kitu katika uwepo wake).

Sifa ya 6 ni kutotegemea kitu katika uwepo wake. Al Aqidah al Tahawwiyah inasema "na kama sifa zake zilikuwa kabla ya uumbaji ndivyo zitavyobakia." Na katika sifa zake ni kutotegemea kitu katika uwepo wake: Uwepo wake hautegemei chochote. Hautegemei nguvu, Mahali au eneo au upande (juu, chini, kulia, kushoto, mbele, nyuma). Anajitosheleza yeye mwenyewe.

Hii sifa inaingia kwenye "alikuwepo Mungu pasipo chochote kuwepo". Hakukuwa na chochote ila yeye alikuwepo! Ina maana uwepo wake haukutegemea chochote. Inarudi kulekule kwenye sifa ya 6.

Wewe unasema yupo juu ya Arshi. Unasema sijakielewa kitabu cha Imam Tahawi. Kwenye mafungamano niliyoyaweka juu kutoka kwa Imam Tahawi hayakubaliani na wewe.
 
Salaam wanabodi,

Very simple. Swali linajieleza hapo juu. Je Mungu yuko wapi? Kabla ya Mungu kuumba ulimwengu/dunia na vitu vyoooote vilivyopo, yeye binafsi alikuwa wapi? Alikuwa kwenye nini? Aliketi au kusimama kwenye kitu gani? Je ni yeye aliyeumba sayari nyingine zaidi ya 9 zinazofahamika? Kwanini amemuweka mwanadamu kwenye sayari moja tu ya DUNIA?

Tusaidiane kujua majibu ya haya maswali muhimu kwenye historia ya ulimwengu.
Yupo sinza
 
Sifa ya 6 ni kutotegemea kitu katika uwepo wake. Al Aqidah al Tahawwiyah inasema "na kama sifa zake zilikuwa kabla ya uumbaji ndivyo zitavyobakia." Na katika sifa zake ni kutotegemea kitu katika uwepo wake: Uwepo wake hautegemei chochote. Hautegemei nguvu, Mahali au eneo au upande (juu, chini, kulia, kushoto, mbele, nyuma). Anajitosheleza yeye mwenyewe.
Kwani kuwepo kwake Allah juu, kumetegemea nini ? Kadhalika kuwepi juu ni katika sifa gani ? Dhaatiya au ?

Sababu Arshi ni katika viumbe vya Allah, na katika viumbe vya Allah Arshi ndiyo kiumbe kikumba zaidi. Sasa ndiyo maana nasema hivi hujamuelewa Imam Tahawi, sababu kuumba ni katika sifa zake.

Ndiyo maana nimekuuliza swali hivi, kuwepo kwake Allah juu ya Arshi yake ni kwamba unata useme Allah amegemea Arshi kuwepo kwake ? Sasa sijui unaandika nini na unajenga hoja gani ? Ndiyo maana nakwambia hujaelewa maneno hayo.

Ngoja nikuulize swali, Allah yupo wapi ? Sababu Allah baada ya kuumba akajiwekea mwenyewe akastawi juu ya Arshi yake.

Swali lingine ushawahi kumsikia mtu mmoja anaitwa Jahm bin Safwaan aliye fariki mwaka 128H ?
Hii sifa inaingia kwenye "alikuwepo Mungu pasipo chochote kuwepo". Hakukuwa na chochote ila yeye alikuwepo! Ina maana uwepo wake haukutegemea chochote. Inarudi kulekule kwenye sifa ya 6.
Unakubali kwamba Arshi imeumbwa na Allah ? Sasa haya maelezo mengine unayotoa hayana ulazima na hayajibu hoja.
Wewe unasema yupo juu ya Arshi. Unasema sijakielewa kitabu cha Imam Tahawi. Kwenye mafungamano niliyoyaweka juu kutoka kwa Imam Tahawi hayakubaliani na wewe.
Siyo kweli maelezo ya Imam yako wazi kabisa na sivyo ambavyo weww unaelezea, ndiyo maana nasisitiza ya kuwa hujamuelewa Imam.

Allah mwenyewe katika Qur'aan amesema haya :

Hakika Rabb wenu ni Allaah Ambaye Ameumba mbingu na ardhi katika siku sita, kisha Akawa juu (Istawaa) ya ‘Arsh [Al-A’raaf: 54]

Sasa wewe hoja yako iko wapi ?
 
Hakika Rabb wenu ni Allaah Ambaye Ameumba mbingu na ardhi katika siku sita, kisha Akawa juu (Istawaa) ya ‘Arsh [Al-A’raaf: 54]
Hii ni tafsiri ya tarjama/subtitle lete tafsiri ya wafasiri wa Quran walivyotafsiri.

Tafsiri ya Imam Qurtubi imeelezea vyema maana ya hiyo aya na ameweka wazi kuwa wanawazuoni wa karne 3 bora msimamo wao ni kuwa Allah ameepukana na upande. Iwe juu, chini, mbele, nyuma, kulia ama kushoto hivyo vyote Allah ameepukana navyo. Kusema Allah yupo juu ya ni makosa. Kwa usahihi na uelewe zaidi na huu si msimamo wangu bali ni Aqida ndivyo inavyosema kwa maelezo ya kina na ya usahihi kaangalie tafsiri ya Imam Qurtubi Juz.7 ukurasa wa 196 ambao ndiyo kauli niliyokupatia.

Kauli yangu inakwenda sambamba na ya Imam Abu Hanifa kwenye kitabu chake cha Al Wasiyya na utapata kwenye Sharh Al Fiqhul Akbar (Mullah Ali Qaari) ukurasa wa 37.

Kauli yangu inakwenda sambamba na Imam Hafiz ibn Katheer (Tafseer ibn Katheer Juz. 2 ukurasa 220.

Kauli yangu inakwenda sambamba na kitabu cha Ma ariful Quran Juz. 3 ukurasa 598. Humo Qadhi Mufti Muhammad Shafii ameweka wazi.

Kauli yangu inakwenda sambamba na Imam Mansoor Al Baghdadi kwenye kitabu cha Al Faraq baynal Firaq juu ya Allah yuko wapi?

Kauli yangu inakwenda sambamba na aqida ya Imam Tahawi ambayo wewe unang'ang'ania kuwa sijamuelewa ila haubainishi.

List ni ndefu naishia hapo!

Sasa vipitie vitabu vya juu hivyo vyote kisha utajua ya kuwa sijamuelewa Imam Tahawi ama la!
Sasa wewe hoja yako iko wapi ?
Msingi wa hoja yangu ni kuwa Allah hayupo juu ya Arsh.

-Mungu hayupo juu ya Arshi, na kama yupo juu ya Arshi jiulize kabla ya kuiumba hiyo Arshi alikuwa wapi?

Wanawazuoni wa Sunnah wal Jamaa wanasema kuwa: Alikuwepo Mwenyezi Mungu bila ya sehemu (juu ya Arshi). Na kama alivyokuwepo bila ya sehemu basi yupo bila ya sehemu. Hii kauli utaipata kwenye kitabu cha Sheikh Mansoor Al Bakhdadi cha Al Farqu baynal Firaq. Ni mwanawazuoni mkubwa wa madhheb ya Imam Shafii. Na huo ndio msingi katika sheria ya Kiislamu kuwa Allah habadiliki.
 
Back
Top Bottom