Mungu yuko wapi?

Kabla ya uuambaji..Mungu alikuwepo katikati ya Giza Totoro na huko alitambulika kam "ELOHIM"
 
Nani amekwambia anashindana, wewe si ulisema hili jambo la kielimu ? Sasa tulijadili kielimu, usitafute udhuru. Kijana dini yetu haitaki ujanja ujanja, nikichokiona kwako huenda hata hivyo vitabu huna yaani hujasoma bali una copy mahali kisha unakuja kubwaga humu. Sasa unatakiwa usome haya mambo na usomeshwe.

Mimi nakupa muda wa kutosha nenda katafute, na nakupa kazi nyingine kayasome haya mapote Jahmiya, Ashaaira/Ashaariya, Muutazila, Kullabiya hawa ndiyo waliathiriwa na Falsafa na wakaingiza fikra za kikafiri katika itikadi ya Uislamu.
 
Naona Mzee unaleta ligi!

Anaitwa Nafii Ibn Mawla ambaye mwalimu wake ni ibnu Umar (Abdallah Ibn Umar).
Jalia ni Mawla siyo jina la mtu, Mawla kwa maana ya asili yake au mzazi au yeye alikuwa mjakazi, na si jina lake kwa maana ya jina.

Hapa hakuna ligi, shida ulianza na ujuaji mwingi katika hili jambo, hapo ndipo ulipo kosea. Sasa sisi hivi vitu wenzako tumeshomeshwa hatujaanza navyo mitandaoni. Siku nyingine ukiwa unakuja unakuja vizuri na usijitie mjuaji na hoja huna.
Ushahidi wa aya nitakupatia tu nitakupigia na picha na usikimbie humu. Kesho au kesho kutwa nitakupatia humu Inshaallah! Na Uzuri Imam Qurtubi ndivyo alivyotafsiri Aya!
Sasa nikimbie ili iweje wewe niletee maana ya aya kwa mujibu wa waja wema. Hizo fikra tunajua asil yake ni wapi, Wanazuoni wetu walishafanya kazi ya kutuwekea wazi fikra hizi na makundi haya yaliyo kuwa yanajinasibisha na Uislamu.

Kwa ufupi huwezi kupata ushahidi unao onyesha ya kuwa Allah hayupo juu. Zaidi ya hizo falsafa na mambo ya Logic.

Kisha kawasome Wanazuoni kama Abul Maali al Juweni naye alikuwa na fikra kama hizo za kutumia falsafa na Kalamu pasi na kurejea kwa waja wema, ila alikuja kurejea katika Haki kadhalika tafuta kitabu cha Imam Al Harawi kiitwacho "Dham al Kalam wa ahlihi" uone asili ya hiyo mitazamo.

Wewe utaleta na mimi nitakuwekea alicjokisema Imam Al-Qurtubiy katika Tafsiri Jamiul ahkaam al Qur'aan.
 
Kuwa na mipaka!

Mwenye elimu huwa anasema mimi kwangu haikunifikia, kama unaelimu nalo tupatie ushahidi.

Inshaallah nitakueletea ushahidi ila usikimbie humu! Tuwekane wazi kabisaaa usikimbie humu!
Ina maana unaposema sanadi hukuwa unamaanisha ? Maana ya Isnaad kwa umoja ni hiyo lazima turudi kwenye "Primary Source" kisha tunakuja kwa hawa walio wafata maswahaba na walio kuja baada yao.

Kijana naanzaje kukimbia ? Kwa lipi yaani ? Haya mambo yana wenyewe, mimi ile siku ya kwanza tu kunijibu nikajua weww mweupe katika hili jambo, nikawa nakusubiri uje. Yaani kuna vitu vingi ulionyesha kwamba hujui na hivyo vitabu huna wala huenda hujawahi kuviona.

Kuna mtu mwingine nikawa naona anakusifia sasa sijui ulikuwa unajisifia mwenyewe kwa ID yaki nyingine (hili siyo la msingi, ni mtazamo wangu) nikasema ujinga ni ugonjwa mbaya sana, yaani mjinga fulani anamsifia mjinga mwenzake, haya ndiyo aliyo yabashiri mtume.
 
Hakuna haja ya kukaa chini sababu haya ni mambo mepesi na madogo sana, tena sisi Waislamu mizani tunayo.

Kukusanya zote siyo hoja, sababu elimu ilikuwa imesambaa zama zile na maswahaba walikuwa wamehama miji na wengine kufariki, kwahiyo huenda kuna mengi hakuyadiriki wakaja kuyadiriki walio kuja kabla yake. Hili lipo sana.

Hoja hapa ni kupatia.
 
Uwe najibu kwanza swali ulilo ulizwa kisha unauliza swali.
Umeleta ushahidi kila anapotajwa Allah yupo!

-Kisha akawa istawaa juu ya Arshi: Jawabu lako Mungu yupo juu ya Arshi.

Swali langu linakuja nahitaji msaada:

-Mtume anasema mmoja wenu akiswali asitupe mate mbele, kwani yupo Mungu.

-Hadithi ya Mtume inasema Mungu anamwambia mja: Mja wangu mimj nimeumwa hukuja kunitembelea! Mja akauliza Mola wangu kwani wewe huumwa? Mungu akajibu; lau ungeenda kunitembelea ungenipata kwake!

Sasa nisaidie Mungu yupo wapi?
-Yupo juu ya Arshi?
-Yupo mbele unaposwali?
-Yupo kwa wagonjwa?

Subiri kidogo pia!
-Hata Nabii Ibrahim alipoulizwa unaenda wapi? akajibu naenda(naelekea) kwa Mola wangu! Sikumbuki ni aya gani ila ukipata muda utaiweka mwenyewe sana!

Ila mwisho wa siku Nabii Ibrahim (kama kumbukumbu yangu ipo sawa) aliishia Palestina!

Mtumé kasema ukisujudu upo karibu na Mungu. Haya maeneo yote Mungu katajwa yupo! Sasa yupo wapi?

-Yupo juu ya Arsh?
-Yupo kwa wagonjwa?
-Yupo mbele unaposwali?
-Yupo Palestina?
-Yupo kwenye sijda?

Ikiwa kama kila eneo takapotajwa basi yupo tuambie Mungu yupo wapi? Ila ukumbuke tunaposwali ni ardhini!

Nisaidie yupo wapi?
 
Hueleweki!
 
Biblia imesema walitaka kujenga mnara kuelekea juu alipo Mungu, wewe unakuja na hekaya za siyo mnara wa kawaida ila ni mnara wa ibada!!!!!
 
Wakristo huwa mnanichekesha sana mkiulizwa Mungo yuko wapi mnasema kuwa hamjui ,mara sijui mungu ni niko!!!

Si mumwambie kwa mujibu wa imani yenu kuwa Mungu wenu ni YESU!! Na ameshawahi kuonekana hapa duniani alikuwa akila,akinywa,akilala na kwenda msalani kujisaidia!! Mungu wenu alizaliwa na Mariam, infact Mungu wenu ana mama na amenyonya maziwa ya mama yake.


Kwa Mujibu wa dini yetu ya Kiislam ni kuwa MUNGU hajazaliwa wala hajazaa, yupo mmoja tu na yeye ndiye anayetegemewa na kila kitu na hakuna afananae nae hata mmoja.

Mungu ametufunulia majina yake matukufu 99 na ametufundisha kuwa pindi tunapokuwa na shida tumuombe kupitia majina hayo naye atajibu.

Miongoni mwa majina hayo matukufu ni.

Al-Awwal (MWANZO) - Mungu ndiye mwanzo kabla yake hakuna mwanzo kila jambo unaloliona lina anzia kwake, yeye ndie originator wa unavyovijua na vile usivyovijua.

Al-Akhir (MWISHO) - Mungu ndie wa mwisho yaani baada yake hakuna mwisho.

Haya ni majina yake mawili matukufu miongoni mwa majina yake 99 aliyotufunulia sisi wanaadamu kupitia kwa mtume wake Muhammad (sala na amani ziwe juu yake).

Mungu ndiye mmiliki wa muda (nyakati), Katika mkono wake amemiliki usiku na huu mchana na ameumba usiku na mchana kama alama mbili kuonesha kuwa yupo ila hizi alama mbili ni kwa ajili ya watu wenye akili bimaana kuna wengine ni mazezeta kila siku wanaona usiku na mchana vinapishana ila wanakwambia kuwa hakuna Mungu.

Pia muda ameuumba ili tu utusaidie sisi hapa duniani tujue majira, hesabu za siku,miezi na miaka. Katika ulimwengu ujao baada ya kufa na kufufuliwa kutakuwa hakuna usiku wala mchana. Na maisha yatakuwa ni ya milele hakuna tena kufa.
 
Mungu yupo everywhere.
ndio maana anayetenda dhambi hapa Tz ama Marekani au Japan anawaona at the same time
 
Hakika huu ni mfano bora sana ila hawataelewa haya ila wenye akili!! Kuna wanaadamu wanavichwa ila akili hawana licha ya kuwa na vyeti vingi kuonesha wamehitimu elimu za juu!!,

leo hii ukimwambia kuwa kuna maisha ya kaburini hawezi kukuelewa ,atakuona umechanganyikiwa na ukimwambia kuwa mara baada ya mwili kusagika na kuwa mchanga ,Mungu atatufufua sote na kuturudisha ktk maumbile ya awali ,vilevile atakuona umechanganyikiwa na maisha.


Mwanadamu ameumbwa akiwa na asili ya ubishi, mwanadamu ni mtu wa kupinga vitu hata kama hana elimu au ujuzi navyo.
 
Akhi unabishana na mtu anayejiita hammaz? Huyo jamaa anawasingizia wanazuoni tu wala haweki marejeo yao humu.Wapo watu wengi sana watakutajia majina lukuki na rejea nyingi za uongo za wanazuoni wengi waliotangulia . Aqidah ya ahlul sunna wal jamaa ipo wazi kabisa kuwa ALLAH yupo juu ya arshi..ipo hivyo na itaendelea kuwa hivyo.

Hao wanaosema kuwa ALLAH hayupo juu ya arshi yake wanaficha tu aqidah zao , mwisho wa siku atajifunua na kusema ALLAH yupo kila sehemu.

Hata mwanangu mdogo wa mwaka mmoja nikimuuliza suali kuwa ALLAH yupo wapi ,atanijibu kuwa ALLAH yupo juu!!
 
Kama umeamua kujivika mamlaka ya kujibia Wakristo basi acha longolongo, jibu Mungu yuko wapi? Huyohuyo Yesu uliyemkebehi hapo yuko wapi? Jibu swali acha taralila
 
Kwa Mujibu wa dini yetu ya Kiislam ni kuwa MUNGU hajazaliwa wala hajazaa, yupo mmoja tu na yeye ndiye anayetegemewa na kila kitu na hakuna afananae nae hata mmoja.
Kwa hiyo huyo mungu wa kiislam yupo wapi?
Maana umekimbilia kujibu swali ambalo hujaulizwa. Hujaulizwa kama huyo mungu wako kazaa au kazaliwa. Umeulizwa yuko wapi? Badala ya kujibu mungu wako mwenye mikono miwili na yote ni ya kulia na ana mguu mmoja yuko wapi umekurupuka na kuwa msemaji wa Mungu wa wakristo.

Jibu swali Allah yuko wapi?
 
Soma maandiko, usituchoshe!!
 
Quran 7:54

Hakika Mola Mlezi wenu ni Mwenyezi Mungu aliye ziumba mbingu na ardhi katika siku sita. Kisha akatawala juu ya Kiti cha Enzi. Huufunika usiku kwa mchana, ufuatao upesi upesi. Na jua, na mwezi, na nyota zinazo tumika kwa amri yake. Fahamuni! Kuumba na amri ni zake. Ametukuka kabisa Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote.
 
Allah yuko wapi? Kwani ni swali gumu sana hili? Mbona unazunguka? Kumbe ni rahisi kurukia kwenye kukashifu imani zingine ilhali ya kwako mwenyewe huna hata idea?

Allah yuko wapi, shaikh?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…