Mungu hayupo? Atheist njooni mthibitishe

Mungu hayupo? Atheist njooni mthibitishe

mm sio mtu wa dini usinihusishe huko, unatamn usfe kwa nn? ni sawa na mtoto anae tamn asizaliwe , jinsi mtoto alie tumbon kwa namae hamna tofauti na sisi tulivyo kwa Mungu , sku ukitoka apa utaelewa kila kitu kma mrotonanavyozaliwa anamjua mama yake na ndivyo ukitoka kwenye huo mwili utamjua mama yako, mtoto alie tumbon hutambua hisia za ***** na sisi tunatambua hisia za mungu juu yetu.
Kama sio mtu wa dini we unaabudu Mungu gani?

Mungu wako unayemuamini wewe hana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote?
 
Atheism ni kukataa kuwepo Mungu nje ya dhana na fikra, hivyo ukiniuliza atheists tunaielewaje dhana ya Mungu, tunaielewa kama kitu cha kufikirika ambacho hakipo katika uhalisia nje ya kufikirika.

Ni kama dhana ya "pembetatu ambayo pia ni duara" katika Euclidean geometry planes.Unaweza kuisema, unaweza kuifikiria, lakini haipo katika uhalisia.

Kuhusu dhana ya Mungu kwa upana wake, nakuomba usome hiki kitabu "Philosophy of Religion: An Anthology".

Kimeelezea vizuri sana, kisomi, kutoka pande zote, za watu wanaoamini uwepo wa Mungu na wasioamini uwepo wa Mungu. Nakiambatanisha.
ili kitu kiwepo kwenye uhalisia kitu hicho kinatakiwa kiweje , je dhani ya kuwa mtu ana akili ni dhana ya kufikirika isiyo na uhalisia?
 
kwa maelezo yako unautofauti mkubwa na scar , nmekuelewa kuwa unapinga Mungu alie elezwa kwenye dini , ila una uelewa mkubwa zaidi kumueleza Mungu katika dhana nyingne kabsa tofauti na dhana iliyopotoshwa ya kwenye din, yan hauridhiki na Mungu aliyesemwa ana upendo wakati duniani kuna majanga ya kila namna , yan unataka Mungu aondoe shida zote ndio ujue kuwa yeye yupo aliejieleza ana upendo na huruma , yan umemaanisha sifa zake haziendani na uhalisia uliopo , Au unamaanisha hakuna nguvu yoyote iliyoanzisha uhai ? yaani hamna chanzo cha yote haya,kama anavyoamini scar ?
Hujanielewa vizuri.

Labbda niandike kwa point form.

1. Mazungumzo mengi ya hapa ni very basic na hayagusi aspects nyingi za falsafa ya kuwepo, kutokuwepo Mungu.

2. Kwa kuanzia (msisitizo ni kwa kuanzia) mazungumzo mengi yanatokana na Mungu aliyeandikwa misahafuni, Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, kama alivyoandikwa kwenye Torati, Biblia, Quran na vitabu vingine.

3.Umenisoma vibaya kwamba napinga Mungu huyu na nataka Mungu fulani, mimi sitaki Mungu yeyote, mimi nataka logical consistency, si kwenye hoja ya Mungu tu, kwenye hoja yoyote. Maana yake ni kwamba, mtu akija na kuniambia Mungu yupo ila ni mshenzi anapenda kutesa watu, hoja yake kuhusu kuwapo Mungu huyo itakuwa na mashiko na logical consistency kubwa kwa kuangalia dunia hii ilivyo, kuliko Mungu aliyeandikwa kwenye misahafu hiyo niliyoitaja hapo juu. Bado nitakuwa na maswali mengi sana kuhusu huyo Mungu, pamoja na imekuwaje Mungu akawa mshenzi na mtesi wa viumbe wake, lakini hiyo dhana itakuwa na logical consistency kubwa zaidi ya hii ya Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, halafu anaumba ulimwengu ambao unawezekana kuwa na mabaya mengi.

4. Kuhusu dhana ya chanzo cha yote, hiyo dhana yenyewe tu inatokana na umasikini wa mawazo unaotupata sisi kama watu. Kimsingi unaongelea causality.Dhana ya kwamba kuna chanzo, kinaleta matokeo. Matokeo hayawezi kuja bila chanzo kuanza. Dhana hii ni potofu, tumeona katika quantum physics kwamba inawezekana kukawa na mzunguko wa chanzo na matokeo kwa namna ambayo hatuwezi kusema chanzo kimeleta matokeo au matokeo yameleta chanzo. Kwa hivyo, kwa mujibu wa Quantum Physics, causality is not fundamentally linear. Tunahitaji kujifunza kuelewa zaidi, si kurukia kutaja Mungu.

Kwa sababu hata ukiambiwa kwamba kuna chanzo, na chanzo ni quantum probability, utasema quantum probability ndiyo Mungu? What if there is something weirder than quantum probability that we still don't know and that has no resemblance to any of our current notions of God?
 
ili kitu kiwepo kwenye uhalisia kitu hicho kinatakiwa kiweje , je dhani ya kuwa mtu ana akili ni dhana ya kufikirika isiyo na uhalisia?
Mtihani wa kwanza wa kitu kuwepo kwenye uhalisia ni logical consistency.

Ingawa si kila cheney logical consistency kipo kwenye uhalisia, hakuna kilicho kwenye uhalisia kisicho na logical consistency.

Ukitaka kuijadili dhana ya mtu kuwa na akili kwa mapana, itakubidi ui define akili kwanza.

Lakini,kwa namna inavyoeleweka kiurahisi kila siku, dhana ya mtu kuwa na akili haina tatizo la kuwa ya kufikirika, kwa sababu haina tatizo la logical consistency.

Dhana za "pembetatu lililo duara" , "square root ya namba iliyo kubwa kuliko hiyo namba yenyewe" au "mtu mzima wa miaka 40 ambaye muda huo ana miaka 40 mama yake mzazi ni mtoto mchanga wa miezi 6" ni za kufikirika tu bila ya uhalisia nje ya kufikirika, kwa sababu zina tatizo la logical consistency.
 
Kama sio mtu wa dini we unaabudu Mungu gani?

Mungu wako unayemuamini wewe hana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote?
kwanza kabsa tambua mimi maisha nayaona ni mchezo ya kuigiza , nipo nje kabsa ya mfumo uliowashika watu wengi wanaishi maisha wanatafuta kitu ambacho tayari kipo kwaajili yao , kimwili mimi ndio nijue natumiaje nguvu ilyo ndan ili nijue nacheza vip mchezo wangu katika haya maumbile ya kuonekana

nipo apa katika haya maumbile ili kuendeleza uumbaji katika maumbile yanayoonekana Ukisikia mungu aliumba akapumzka Mungu anaumba kila sekunde ya nukta kupitia maumbile yanayoonekana nayasionekana, uwezo alionao ni kuweka vitu katika hali ya usawa na uwiano sahihi .
 
kwanza kabsa tambua mimi maisha nayaona ni mchezo ya kuigiza , nipo nje kabsa ya mfumo uliowashika watu wengi wanaishi maisha wanatafuta kitu ambacho tayari kipo kwaajili yao , kimwili mimi ndio nijue natumiaje nguvu ilyo ndan ili nijue nacheza vip mchezo wangu katika haya maumbile ya kuonekana , nipo apa katika haya maumbile ili kuendeleza uumbaji katika maumbile yanayoonekana Ukisikia mungu aliumba akapumzka Mungu anaumba kila sekunde ya nukta kupitia maumbile yanayoonekana nayasionekana, uwezo alionao ni kuweka vitu katika hali ya usawa na uwiano sahihi .
Vipi kama hata dhana ya uwepo wa Mungu ni muendelezo wa maigizo tu?

Halafu swali hujajibu, Mungu unayemuamini wewe hana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote?
 
Sawa mkuu nimekuelewa.

Hivyo kwa mujibu wako ni kwamba;
Hakuna Mungu, na ulimwengu huu pamoja na vyote vilivyomo, tuvijuavyo na tusivyovijua- haijulikani vimekuaje vile vilivyo. Utafiti zaidi unahitajika.
Nimekupata vizuri sana.



Sijui vimetokana vipi (na hakuna anayejua) hilo ni swala la kutafiti, sio kutolea maoni kwa jinsi unavyo imagine kichwani mwako.

Hata dini haina majibu ya swali hilo, dini ndio imeacha loopholes ya maswalo mengi tata ila imeweka kitisho cha zuio ili watu wasihoji.
Lakini Mkuu kama hujui vitu hivyo vilikujaje lakini waumini dini wanadai wanajua na wanaeleza kila leo juu ya uwepo wake na kueleza kwanini vipo mahali hapa vilipo, na nani alivileta.

Swali ni kuwa kwanini kwako inakuwa ngumu kukubali madai yao ilhali wewe mwenyewe hauna majibu?
 
Atheism ni kukataa kuwepo Mungu nje ya dhana na fikra, hivyo ukiniuliza atheists tunaielewaje dhana ya Mungu, tunaielewa kama kitu cha kufikirika ambacho hakipo katika uhalisia nje ya kufikirika.
Sawa kabisa.
Ni kama dhana ya "pembetatu ambayo pia ni duara" katika Euclidean geometry planes.Unaweza kuisema, unaweza kuifikiria, lakini haipo katika uhalisia.
Nimekupata vilivyo.
Kuhusu dhana ya Mungu kwa upana wake, nakuomba usome hiki kitabu "Philosophy of Religion: An Anthology".

Kimeelezea vizuri sana, kisomi, kutoka pande zote, za watu wanaoamini uwepo wa Mungu na wasioamini uwepo wa Mungu. Nakiambatanisha.
Shukrani, ama kwa hakika nitakipitia 🙏.

Swali la mwisho la kufunga huu mjadala;
Kama kwa Atheists dhana ya Mungu ni ya kufikrika tu je mnayaelezaje haya yaliyomo hapa duniani na Ulimwenguni kote? Kwamba yalitoka wapi ama kutengenezwa na nani? (Kama yupo) Kwaajili ya nini?
 
Sawa mkuu nimekuelewa.

Hivyo kwa mujibu wako ni kwamba;
Hakuna Mungu, na ulimwengu huu pamoja na vyote vilivyomo, tuvijuavyo na tusivyovijua- haijulikani vimekuaje vile vilivyo. Utafiti zaidi unahitajika.
Nimekupata vizuri sana.




Lakini Mkuu kama hujui vitu hivyo vilikujaje lakini waumini dini wanadai wanajua na wanaeleza kila leo juu ya uwepo wake na kueleza kwanini vipo mahali hapa vilipo, na nani alivileta.

Swali ni kuwa kwanini kwako inakuwa ngumu kukubali madai yao ilhali wewe mwenyewe hauna majibu?
Kwasababu sio mimi nisieamini Mungu ndio naye pingana na madai yao

Hata wao kwa wao hawakubaliani na madai yao.

Hili swala nilishalitolea ufafanuzi


Thread 'Philosophy of Religion: Uthibitisho wa uwepo wa Mungu kwa hoja ya Ufunuo na maandiko matakatifu' Philosophy of Religion: Uthibitisho wa uwepo wa Mungu kwa hoja ya Ufunuo na maandiko matakatifu
 
Sawa kabisa.

Nimekupata vilivyo.

Shukrani, ama kwa hakika nitakipitia 🙏.

Swali la mwisho la kufunga huu mjadala;
Kama kwa Atheists dhana ya Mungu ni ya kufikrika tu je mnayaelezaje haya yaliyomo hapa duniani na Ulimwenguni kote? Kwamba yalitoka wapi ama kutengenezwa na nani? (Kama yupo) Kwaajili ya nini?
Atheism si dini, hakuna kanisa la atheists, hakuna kikao cha kuwaunganisha atheists wote.

Atheists ni kukataa kuwepo Mungu. Zaidi ya hapo, kila mtu anaweza kufikiri anachotaka kuhusu chanzo cha ulimwengu na maswali mengine.

Hivyo, mimi naweza kujibu kama mimi, si kwa niaba ya atheists, maana atheists hatuna msahafu useme nimesoma kwenye msahafu wetu wamesema hivi.

Haya yaliyomo duniani na ulimwenguni kote ni mengi, inabidi ufafanue vizuri.

Ama kuhusu ulimwengu umetoka wapi, swali lenyewe linajikita katika causality, ambayo nimeizungumzia hapo juu. Hivyo, kabla ya kutafuta jibu la swali, inabidi tulihoji hilo swali kama ni swali sahihi.

Nimezungumzia causality na kutoa links kwenye posts namba 124

Maana, inawezekana tukawa kama mtu kipofu, ambaye hajui rangi, anajua sauti tu, akawa anauliza, nasikia kuna bendera ya taifa ina rangi nzuri sana, ningependa kujua sauti za rangi za hii bendera ya taifa zinafananaje? Je, nyeusi ni kama tarumbeta au filimbi? kijani ni kama gita au marimba? Kwa mtu huyu kipofu, swali lake analiona ni la msingi, kwa sababu anachojua yeye ni sauti, hajui rangi, lakini kiuhalisia, swali lake halina maana, kwa sababu bendera ya taifa ina rangi ambazo hazina sauti.
 
Kwasababu sio mimi nisieamini Mungu ndio naye pingana na madai yao

Hata wao kwa wao hawakubaliani na madai yao.

Hili swala nilishalitolea ufafanuzi


Thread 'Philosophy of Religion: Uthibitisho wa uwepo wa Mungu kwa hoja ya Ufunuo na maandiko matakatifu' Philosophy of Religion: Uthibitisho wa uwepo wa Mungu kwa hoja ya Ufunuo na maandiko matakatifu
Nimesoma hoja zako na nimezielewa mashaka yako.

Kwa mada yangu hii toka kwako bwana Scars natoka na majibu kuwa;

“Tafiti ziendelee kuujua ukweli kuhusu Ulimwengu wetu”

Shukran sana ‘and I appreciate it’🙏
 
Hujanielewa vizuri.

Labbda niandike kwa point form.

1. Mazungumzo mengi ya hapa ni very basic na hayagusi aspects nyingi za falsafa ya kuwepo, kutokuwepo Mungu.
2. Kwa kuanzia (msisitizo ni kwa kuanzia) mazungumzo mengi yanatokana na Mungu aliyeandikwa misahafuni, Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, kama alivyoandikwa kwenye Torati, Biblia, Quran na vitabu vingine.
3.Umenisoma vibaya kwamba napinga Mungu huyu na nataka Mungu fulani, mimi sitaki Mungu yeyote, mimi nataka logical consistency, si kwenye hoja ya Mungu tu, kwenye hoja yoyote. Maana yake ni kwamba, mtu akija na kuniambia Mungu yupo ila ni mshenzi anapenda kutesa watu, hoja yake kuhusu kuwapo Mungu huyo itakuwa na mashiko na logical consistency kubwa kwa kuangalia dunia hii ilivyo, kuliko Mungu aliyeandikwa kwenye misahafu hiyo niliyoitaja hapo juu. Bado nitakuwa na maswali mengi sana kuhusu huyo Mungu, pamoja na imekuwaje Mungu akawa mshenzi na mtesi wa viumbe wake, lakini hiyo dhana itakuwa na logical consistency kubwa zaidi ya hii ya Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, halafu anaumba ulimwengu ambao unawezekana kuwa na mabaya mengi.
4. Kuhusu dhana ya chanzo cha yote, hiyo dhana yenyewe tu inatokana na umasikini wa mawazo unaotupata sisi kama watu. Kimsingi unaongelea causality.Dhana ya kwamba kuna chanzo, kinaleta matokeo. Matokeo hayawezi kuja bila chanzo kuanza. Dhana hii ni potofu, tumeona katika quantum physics kwamba inawezekana kukawa na mzunguko wa chanzo na matokeo kwa namna ambayo hatuwezi kusema chanzo kimeleta matokeo au matokeo yameleta chanzo. Kwa hivyo, kwa mujibu wa Quantum Physics, causality is not fundamentally linear. Tunahitaji kujifunza kuelewa zaidi, si kurukia kutaja Mungu. Kwa sababu hata ukiambiwa kwamba kuna chanzo, na chanzo ni quantum probability, utasema quantum probability ndiyo Mungu? What if there is something weirder than quantum probability that we still don't know and that has no resemblance to any of our current notions of God?

wewe unasema Mungu hayupo kwa sababu anatesa watu , akija mtu wa dini akakuambia hayo mateso ni mitihani tu huoni anavunja hoja yako? akakupa mfano kuwa unapofanya mtihani ukakutana na maswali magumu yanayotesa kichwa mpka kinauma , huoni mwanafunzi huyo akikurupuka nakusema baraza la mitihani halipo kisa ameumwa kichwa wakati anafanya huo mtihani , hauoni watu watamwona ni mwehu?

unaposema kila kitu unataka kiwe na logic na logic ni good argurment , huoni wanaosema Mungu ypo wana good argurment au ukisema hayupo unakuaje na good argurment ambayo huwa logic?
 
wewe unasema Mungu hayupo kwa sababu anatesa watu , akija mtu wa dini akakuambia hayo mateso ni mitihani tu huoni anavunja hoja yako? akakupa mfano kuwa unapofanya mtihani ukakutana na maswali magumu yanayotesa kichwa mpka kinauma , huoni mwanafunzi huyo akikurupuka nakusema baraza la mitihani halipo kisa ameumwa kichwa wakati anafanya huo mtihani , hauoni watu watamwona ni mwehu? unaposema kila kitu unataka kiwe na logic na logic ni good argurment , huoni wanaosema Mungu ypo wana good argurment au ukisema hayupo unakuaje na good argurment ambayo huwa logic?
Unaonekana ni mgeni kwenye hii mijadala

Hoja unayo i-prefer kama defense dhidi ya atheist, hakuna muamini Mungu ambaye ni mzoefu kwa hii mijadala akaitumia hoja mbovu kama hiyo
 
Atheism si dini, hakuna kanisa la atheists, hakuna kikao cha kuwaunganisha atheists wote.
Naam hii ni kweli.
Atheists ni kukataa kuwepo Mungu. Zaidi ya hapo, kila mtu anaweza kufikiri anachotaka kuhusu chanzo cha ulimwengu na maswali mengine.

Hivyo, mimi naweza kujibu kama mimi, si kwa niaba ya atheists, maana atheists hatuna msahafu useme nimesoma kwenye msahafu wetu wamesema hivi.

Haya yaliyomo duniani na ulimwenguni kote ni mengi, inabidi ufafanue vizuri.

Ama kuhusu ulimwengu umetoka wapi, swali lenyewe linajikita katika causality, ambayo nimeizungumzia hapo juu. Hivyo, kabla ya kutafuta jibu la swali, inabidi tulihoji hilo swali kama ni swali sahihi.

Nimezungumzia causality na kutoa links kwenye posts namba 124
Nimeipitia na nimeona majibu.
Maana, inawezekana tukawa kama mtu kipofu, ambaye hajui rangi, anajua sauti tu, akawa anauliza, nasikia kuna bendera ya taifa ina rangi nzuri sana, ningependa kujua sauti za rangi za hii bendera ya taifa zinafananaje? Je, nyeusi ni kama tarumbeta au filimbi? kijani ni kama gita au marimba? Kwa mtu huyu kipofu, swali lake analiona ni la msingi, kwa sababu anachojua yeye ni sauti, hajui rangi, lakini kiuhalisia, swali lake halina maana, kwa sababu bendera ya taifa ina rangi ambazo hazina sauti.

Sasa kutokana na maelezo yako kuhusu swali la “Dunia imetoka wapi?” Na majibu yako ya ‘causality’ kwenye ‘post’ yako namba 124, je tunaweza hitimisha kuwa kwako wewe Bwana Kiranga dhana ya Mungu (ikimaanisha Muumba wa vyote) ni batili na kiumbe, nguvu, mtu au chochote kinachinasibishwa na dhana hiyo si halisi ila uzushi???
 
wewe unasema Mungu hayupo kwa sababu anatesa watu , akija mtu wa dini akakuambia hayo mateso ni mitihani tu huoni anavunja hoja yako? akakupa mfano kuwa unapofanya mtihani ukakutana na maswali magumu yanayotesa kichwa mpka kinauma , huoni mwanafunzi huyo akikurupuka nakusema baraza la mitihani halipo kisa ameumwa kichwa wakati anafanya huo mtihani , hauoni watu watamwona ni mwehu? unaposema kila kitu unataka kiwe na logic na logic ni good argurment , huoni wanaosema Mungu ypo wana good argurment au ukisema hayupo unakuaje na good argurment ambayo huwa logic?
Kwanza, sijasema Mungu hayupo kwa sababu anatesa watu. Akitesa watu atakuwa yupo, si hayupo.

Nasema Mungu hayupo kwa sababu dhana ya Mungu kuwapo inajipinga yenyewe. Mara unaambiwa Mungu ana upendo mkuu, mara unaona vitoto vichanga masikini vinakufa kwa utapiamlo.

Watu wametunga dhana ya Mungu.

Wakampa Mungu tabia za watu. Ndiyo maana unasikia Mungu anatoa mtihani, Mungu anakasirika, Mungu anaghairi mambo aliyopanga na kuleta mafuriko duniani.

Mungu anakasirikaje wakati anajua kila kitu kitakavyokuwa? Anaghairi nini wakati anajua kila kitu kitakavyokuwa?

Anatoa mtihani ili iweje wakati yeye anajua yote yatakavyokuwa?

Mtihani ni sehemu ya maisha ya dunia ya watu wasio na nguvu zote, uwezo wote wala upendo wote. Kupimana ili kujua nani anajua zaidi. Na hata katika dunia hii, kuna baadhi ya jamii zinaondokana kwenye mifumo ya mitihani.

Sasa Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, kwanza kwa nini aweke mitihani mibaya sana inayoweza kuumiza watu wake anaowapenda?

Hivi, kuna baba mwenye akili zake timamu, anayewapenda watoto wake, anayesema leo najenga nyumba, naitegeshea mabomu ndani yake, ili wanangu wapate kujua kukwepa mabomu, wakati anaweza kujenga nyumba ambayo haina mabomu?

Hivi, msichana wa miaka 10 anayejiuza mjini Manila Philippines ili apate kula tu, anapewa mtihani wa maisha hayo na Mungu mwenye mapenzi?

Wale Wahutu na Watusti waliochinjana kama kuku, yani Mungu hata kama tunasema anatoa mitihani, alishindwa kuwapa mtihani mzuri ambao hauna mauaji ya kinyama?

Kwa nini Mungu anayejua kila kitu na kuweza kila kitu na mwenye upendo wote ahitaji kuwepo na mtihani, hususan kama mtihani wenyewe unaumiza sana viumbe wke anaowapenda?

Usiongelee mtihani kama kitu ambacho hakiepukiki katika dunia hii tunayoiona, ongelea mtihani kutoka perspective ya Mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wote.
 
Vipi kama hata dhana ya uwepo wa Mungu ni muendelezo wa maigizo tu?

Halafu swali hujajibu, Mungu unayemuamini wewe hana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote?
sijajibu hilo swal kwasababu kumuamini haitaathiri yeye kuwepo , nikisema hana uwezo nimemshusha zaidi ya kinyonga kenye uwezo wa kubadilika rangi kinapohisi hatari , unaposema upendo ni namna unavyotafsi upendo kwako ni nini , mimi ata nikiumwa ni upendo wa Mungu ili madaktari wanitibu wapate pesa , nikifa kuna watu watapa pesa kuuza mageneza ni upendo , nikiwa kilema nitanunua wheel chair watu watapata pesa wasomesha ni upendo pia
 
Naam hii ni kweli.

Nimeipitia na nimeona majibu.


Sasa kutokana na maelezo yako kuhusu swali la “Dunia imetoka wapi?” Na majibu yako ya ‘causality’ kwenye ‘post’ yako namba 124, je tunaweza hitimisha kuwa kwako wewe Bwana Kiranga dhana ya Mungu (ikimaanisha Muumba wa vyote) ni batili na kiumbe, nguvu, mtu au chochote kinachinasibishwa na dhana hiyo si halisi ila uzushi???
Si hivyo tu.

Leo nikikaa na kuangalia angani naona nyota ambazo hazipo, zimetoweka mamilioni ya miaka iliyopita, lakini mwanga wake nauona leo. Naweza kukuonesha ile pale nyota ipo, na wewe unaiona na kukubali kwamba ipo, kwa sababu unaiona. Lakini nyota ishalipuka na kutoweka mamilioni ya miaka iliyopita.

Je, hizo nyota zipo, kwa sababu nauona mwanga wake, au hazipo kwa sababu zimetoweka mamilioni ya mika iliyopita?

Kuna sehemu ya ulimwengu hatuijui na daima hatutakuja kuijua, kwa sababu ulimwengu unapanuka kwa kasi kubwa kuliko mwanga wa hiyo sehemu unavyosafiri na kuweza kutufikia.

Je, tunaposema "vyote" huko nako tunakuhesabu? Tunakujuaje?

Unaposema vyote unamaanisha nini? Na unajuaje hivyo ndivyo vyote?

Inawezekana hii dhana ya "vyote" nayo ni mauzauza ya kufikirika tu?

Vyote kwa wapi, lini, na msingi gani?

Vyote kwa wapi, lini, na msingi gani?

Kama siyo, utajuaje hapa umemaliza vyote?

Kama ndiyo, ikiwa hatujui vyote ni nini, tutasemaje huyu ni Mungu muumba vyote?
 
sijajibu hilo swal kwasababu kumuamini haitaathiri yeye kuwepo , nikisema hana uwezo nimemshusha zaidi ya kinyonga kenye uwezo wa kubadilika rangi kinapohisi hatari , unaposema upendo ni namna unavyotafsi upendo kwako ni nini , mimi ata nikiumwa ni upendo wa Mungu ili madaktari wanitibu wapate pesa , nikifa kuna watu watapa pesa kuuza mageneza ni upendo , nikiwa kilema nitanunua wheel chair watu watapata pesa wasomesha ni upendo pia
Huelewi sifa za Mungu ni kigezo kikubwa kumtofautisha na mtu?

Mungu ambaye hana uwezo wote na upendo wote unamtofautishaje na mtu?
 
Unaonekana ni mgeni kwenye hii mijadala

Hoja unayo i-prefer kama defense dhidi ya atheist, hakuna muamini Mungu ambaye ni mzoefu kwa hii mijadala akaitumia hoja mbovu kama hiyo
kama umeona hyo hoja ni mbovu wewe ndio umeona hvyo kwangu mimi ni hoja sahihi onyesha ubovu wake nikupe usahihi wake, kwasababu imetoka kwangu kama chanzo cha hoja hyo apa.
 
Back
Top Bottom