min -me
JF-Expert Member
- Jul 20, 2022
- 47,838
- 132,258
jukwaa huru mkuu furahia siku yako.Mwisho wa siku wote mtakufa tajiri na maskini. Sasa hata wewe utamwambia nini?
jukwaa huru mkuu furahia siku yako.Mwisho wa siku wote mtakufa tajiri na maskini. Sasa hata wewe utamwambia nini?
Elimu ya mjinga ni Majungu...mtu humjui una anzaje kumuita mpumbavu na maskini au kwa vile anaenda kinyume na imani yako na mawazo yako? Wewe ndio mjinga kudhani kila mtu anafikiria sawa na kichwa chako...Kama huna hoja tulia,nyamaza usikashifu watu kwa matusi si kwamba hatuwezi tumia hayo matusi ila tunataka Hoja fikirishi...wewe kama huna cha kusema toka humu jukwaani!unaongelea size unadhani nani anashindana na huyo mpumbavu na maskini
Wewe baki na imani yako inavyo kuaminisha na Atheist pia wana Imani zao pia za kutokuwepo Mungu... usihalalishe imani zako kwa watu maana na wewe huna uthibitisho wa ku prove zaidi ya kuegemea maandiko yako ya KIDINI...Wanadamu na sayansi yetu ndogo hapa duniani ya Technology kama ya mtu aliyeanzishaa internet ni ndogo sana, ila sisi tumeona kubwa na kwavile tuliumbwa kwa mfano wa Mungu roho zetu basi tunajikuta wajuaji kama Shetani na kujiona miungu watu.
Kosa lile lile walilolifanya Israel na mataifa Mengine kuabudu miungu..
Na mwisho wa Dhambi hiyo ni mauti.
Athiest wanajikutaga wanajua kinoma na kutegemea akili zako ndio Mwanzo na Mwisho wa hekima hapa duniani hawajui wala kuamini Yupo mwenye hekima zaidi Yetu na Akili zake hazichunguziki.
mkuu hili ni jukwaa huru hongera pia kwa uhuru wakoElimu ya mjinga ni Majungu...mtu humjui una anzaje kumuita mpumbavu na maskini au kwa vile anaenda kinyume na imani yako na mawazo yako? Wewe ndio mjinga kudhani kila mtu anafikiria sawa na kichwa chako...Kama huna hoja tulia,nyamaza usikashifu watu kwa matusi si kwamba hatuwezi tumia hayo matusi ila tunataka Hoja fikirishi...wewe kama huna cha kusema toka humu jukwaani! Sio kukashifu mawazo ya watu....ndio maana ya "JF where we dare to talk openly"....sasa Mawazo yako mgando acha huko huko njoo na Hoja......
mkuu nimechagua kuwasilisha nilichowasilisha kwa uhuru kabsa bila kupangiwa na mtu kwa hyo ata ww usinipangie nisemejeElimu ya mjinga ni Majungu...mtu humjui una anzaje kumuita mpumbavu na maskini au kwa vile anaenda kinyume na imani yako na mawazo yako? Wewe ndio mjinga kudhani kila mtu anafikiria sawa na kichwa chako...Kama huna hoja tulia,nyamaza usikashifu watu kwa matusi si kwamba hatuwezi tumia hayo matusi ila tunataka Hoja fikirishi...wewe kama huna cha kusema toka humu jukwaani! Sio kukashifu mawazo ya watu....ndio maana ya "JF where we dare to talk openly"....sasa Mawazo yako mgando acha huko huko njoo na Hoja......
Sawa sawa Mkuu...mkuu nimechagua kuwasilisha nilichowasilisha kwa uhuru kabsa bila kupangiwa na mtu kwa hyo ata ww usinipangie nisemeje


Kijana kila siku huwa nakwambia kadhia ya kumjadili Mola ishakushinda na hutawahi kuja kuwa na hoja.Mimi binafsi maongezi yangu niliyoyafanya JF miaka yote kuhusu uwepo wa Mungu hayajafikia hata 5% ya maongezi ninayoweza au ninayotaka kuyafanya.
Kwa sababu watu wengi wanajadili dhana hii kwa upeo finyu wa dini zao. Na inakuwa vigumu kuendeleza mazungumzo ngazi ya tatu wakati hata ya kwanza hatujamaliza. Inakuwa sawa kutaka kujadiliana hesabu za Poincare's Conjecture level ya Grigori Perelman na mtu ambaye hajui kujumlisha na kutoa.
Hivyo hatujafikia kuzungumzia hata dhana kama pantheism, deism, na nyingine nyingi.
Mara nyingi watu huanzia na Mungu anayetajwa kwenye dini kubwa. Maana huyo ndiye anayetajwa sana.
Mfano, mimi mara nyingi ninapopinga uwepo wa Mungu, humtambulisha kwa sifa kama kusema "Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote".
Huyu ndiye Mungu anayetajwa kwenye misahafu ya Uyahudi, Ukristo, Uislamu na mingine mingi tu.
Mungu huyu ni dhana tu, hayupo kwenye uhalisia.
Dhana ya kuwepo Mungu huyu inapingana na ulimwengu unaoruhusu mabaya. Ama una ulimwengu unaoruhusu mabaya na Mungu huyu hayupo, ama Mungu huyu yupo na ulimwengu unaoruhusu mabaya haupo.
Ulimwengu unaoruhusu mabaya upo.
Hivyo, Mungu huyo hayupo.
This is basic logical consistency.
Mungu huyo kuwepo ni contradiction kama kuwepo kwa pembetatu ambayo hapo hapo ni duara katika planes za Euclidian geometry.
Ni contradiction kama 10 kuwa square root ya 2 katika base 2 mathematics.
Sijawahi kuona mkana mungu ana hoja. Shida yenu huwa waoga na mnakimbia jukumu la kuthibibitisha na liacha jukumu Hilo kwa mwenye kusadili. Ukisoma vitabu vya Elimu ya mijadala husema hivi mara nyingi mwenye kukanusha hutangulizwa katika kuthibitisha jambo husika sababu hudhaniwa ya kuwa yeye ana Elimu zaidi ya yule anae sadikisha na mara chache mwenye kusadiki hutangulizwa.Unasema kikombe kipo na Mimi ninasema hakipo halafu unanitaka Mimi ninaesema hakuna kikombe ndio nithibitishe, badala ya wewe unaesema kipo.
Wewe unaesema mungu yupo thibitisha na sio athibitishe anaesema mungu Hayupo.
Umejuaje kama hayupo ? Kitu ambacho hakipo unajuaje kama hakipo ? Je ni lazima kitanguliwe na kutokuwepo kwake ? Au si lazima ? Kama si lazima umejuaje Mola hayupo ?Mungu hayupo
Thibitisha hili.Achana na stori za mungu, ni hadithi za alinacha, hadithi za kutunga, mungu hayupo.
Muelezee huyu na utuambie kwanini aitwe mungu au anaitwa mungu.Acidalia
Hawana uthibitisho Wala hawajawahi kuwa nao na wala hawatakuja kuwa nao.
Kama asili ya Mungu ni Upendo kwa nini tena aruhusu mabaya yawepo? Maandiko ya kidini yanadai Mungu asili yake ni mwenye upendo, huruma, mwingiii wa Rehema...iweje tena aruhusu ubaya na uovu u exist duniani? Huo upendo wake na huruma viko wapi?Kijana kila siku huwa nakwambia kadhia ya kumjadili Mola ishakushinda na hutawahi kuja kuwa na hoja.
Kila siku unarudia yale yale, maswali hujibu hapa unakuja kujifaragua kwamba tangu uanze kujadili hili ni 5% tu umetumia. Kwanini unaandika uongo ? Mara ngapi najadiliana na wewe unakimbia maswali.
Umeandika suala la dhana ambazo hujawahi kuziongelea hizo siyo hujawahi kuziongelea Bali hazi jibu hoja katika kadhia hii.
Uwepo wa Mola ni uhalisia, ndiyo maana mpaka unakufa hutaweza walau kuharibu tu kukana kutokuwepo kwa Mola.
Nilishakwambia siyo kila unachokiona kina uta (contradiction) basi kina uta kweli, utata mara nyingi husababishwa na ujinga wa Mtu husika. Mfano wako ni wewe kuwa mjinga na usiye tumia akili unaona utata ila kiuhalisia hakuna utata.
Mfano nikikuuliza swali, tuthibitishie ya kuwa Mola hayupo na kwamba hii ni dhana. Dhana tamko hili Lina maana zaidi ya Moja Kuna wakati humaanisha hakika ya jambo baada ya ithibati na maana nyingine ni wazo tu. Sasa tujadili kwa maana hii ya pili. Thibitisha ya kuwa Mola kuwepi kwake ni dhana. Kisha utuambie dhana hii ilianzishwa na nani na lini.
Kuwepo kwa mabaya kunathibitisha juu ya uwepo wa Mola mwenye uwezo wote ndiyo maana akaruhusu mabaya yawepo. Sasa unapo mfasili Mola kwa upande mmoja huo ni uchachefu wa akili na Mola hufanya kila jambo kwa hekima.
Unajua ubaya uko wapi? Upo brainwashed toka mdogo, kwaiyo ubongo wako umeshalishwa sumu hutaweza kuchambua kiyakinifu,Umejuaje kama hayupo ? Kitu ambacho hakipo unajuaje kama hakipo ? Je ni lazima kitanguliwe na kutokuwepo kwake ? Au si lazima ? Kama si lazima umejuaje Mola hayupo ?
Maswali gani hayo? Je uko tayari kwa majibu au ndo tayari una majibu?Hawana uthibitisho Wala hawajawahi kuwa nao na wala hawatakuja kuwa nao.
Najua kupitia vitu vya asili alivyoumba. Uwezo huo bado haujawahi kufanywa na mwingine,huo ndio upekee wakeSawa.
Tuseme napenda kukubaliana na wewe. Mimi pia kimsingi ningependa sana Mungu awepo. Ulimwengu ambao una Mungu ungenipunguzia matatizo mengi sana, hivyo ningefurahi sana kujua kwamba fikra zangu kwamba Mungu hayupo zina makosa, na kiukweli Mungu yupo.
ila nina tabia ya kuhakiki mambo kabla ya kuyakubali.
Hivyo, sina tatizo kukukubalia, ila nataka kuhakikisha mambo tu kabla sijakubali.
Unajuaje uwezo huo upo kweli, na si kitu ulichokifikiria tu mawazoni kwako wewe na watu mnaoamini uwepo wa Mungu, aghalabu kwa kurithishana kwenye hadithi, mapokeo, vitabu, uvivu wa kufikiri unaofanya kutojua jibu kufanywe kuwa ni kujua jibu, kuwa jibu la kisichojulikana ni Mungu huyo, wakati kiukweli uwezo huo haupo na hata huyo Mungu hayupo?
Unazunguka palepale.Najua kupitia vitu vya asili alivyoumba. Uwezo huo bado haujawahi kufanywa na mwingine,huo ndio upekee wake
Kwanza nani amekwambia asili ya Mungu ni upendo ? Haya mambo mlitakiwa myasome na myajue kwanza Kisha myakanushe.Kama asili ya Mungu ni Upendo kwa nini tena aruhusu mabaya yawepo?