Kaka mshana, kwanza kabisa nikupinge, kimwili hatujaumbwa na Mungu Kwa maana Mungu ni mwili, ila kinadharia mtu ni kweli ameumbwa na Mungu, na Mungu ni neno, consider dualism, man and animal.
Kimwili sisi ni wanyama, na wanyama wote wanatokana na asili ambayo ndani yake imejaa njama ya kuangamiza maisha, ndio maana sisi wanyama tuna silka ndani yetu kwaajili ya kulinda uhai,
Baada ya mnyama mtu kuzungumza, alijuwekea utaratibu wa kuiheshimu lugha anayozungumza kwakua ndio yenye kumpa ukuu nguvu na ndoto, au Mungu
Wakristo walimuwua Mungu Kwa kumpa Mungu utu, ndio maana Leo utawasikia wakitamba kuwa mbinguni ndipo alipo baba, huku wakinyoosha vidole mawinguni, ila Mungu ni neno kama yalivyo maneno mengine,
Mfano, Plato aliunda neno gap ambalo ndani yake Kuna guardian auxiliary na producer ndivyo ilivyo na neno God ambalo ndani yake Kuna Greatness power na dream
Maneno yana tabia ya kujenga illusion, ipo siku neno Sababu litakuwa mtu pia, usishangae wajukuu wako wakipiga goti kumuomba Sababu awalinde, kama tuu neno Mungu lilivyobadilika na kuwa mtu, Leo Imani limekuwa mtu, msalimie upendo na baraka, ahsante
Kama utanielewa ntashukuru, wako mpendwa zaidi ya mtu