Kupatikana na kubadilika kwa usiku na mchana mwanga na giza ni ishara tosha za kuthibitisha kuwepo Mwenyezi Mungu (s.w) kwa wenye akili.
"Hakika katika kuumbwa kwa mbingu na ardhi, na kukhitalifiana usiku na mchana, na marikebu ambazo hupita baharini kwa viwafaavyo watu, na maji anayo yateremsha Mwenyezi Mungu kutoka mbinguni, na kwa hayo akaihuisha ardhi baada ya kufa kwake, na akaeneza humo kila aina ya wanyama; na katika mabadiliko ya pepo, na mawingu yanayo amrishwa kupita baina ya mbingu na ardhi, bila shaka zimo Ishara kwa watu wanao zingatia". (Qur'an 2:164)
"Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi na kukhitalifiana usiku na mchana ziko Ishara kwa wenye akili"Qur'an 3:190.
Rejea Qur’an (17:12) na (28:71-72)