Mume wake dada hataki kunipa mtaji

Mume wake dada hataki kunipa mtaji

Mbona kilimo umeacha sasa mkuuu [emoji90] vipi hapo

na umeacha kwa muda gani?

Na kwann umeacha?

Hapo kwa dada ako umekaa kwa muda. Gani?

Umejishughulisha na nn tangia ufike hapo?

Umemshawishi vipi huyo shemeji akupe mtaji?

Kilimo sikupenda kuacha, kiligoma. Wao wenyewe wakaniita mjini, sasa walichoniitia mjini hakijafanikiwa wananiambia nirudi kijijini, hiyo ni haki?
 
Mimi ni kijana mdogo mwenye miaka 29, nimesoma diploma ya masuala ya afya, baada ya kuhitimu nilikaa sana kijijini bila ajira. Dada na mume wake wakaamua kuniita mjini nijaribu bahati yangu.

Ila huku nako hali imezidi kuwa mbaya, kazi hakuna. Cha ajabu siku hizi wamenianzishia visa, dada na mume wake wanataka na mm niwe nafanya kazi za hapa nyumbani, wakati wafanyakazi wapo. Nilivyokataa kutumikishwa, mume wake dada anataka kunirudisha kijijini. Nimemwambia kijijini siendi, labda anipe mtaji. Amekataa kata kata, na sio kwamba hela hana. Hela anazo maana kila mwisho wa wiki anapendaga kutoka yeye na dada.

Wanashindwa kujibana hata mwezi ili mimi nipate mtaji? Leo tumezozana sana, walivyo na tabia mbaya, wameanzisha haya malumbano wakati wa kula. Hapa nipo na msongo wa mawazo, pia njaa ni kali maana nimegoma kula chakula chao usiku.

Naombeni ushauri, sielewi nifanye nini.
Unapoishi kwa watu kuwa mnyenyekevu
 
Mkuu umefanya vema sana kutushirikisha yanayousumbua wako mtima.

Kwenye suala la kuomba,jitahidi kutumia mbinu shawishi zitakazomuibua mtu kukusaidia kuipiga hatua kufika utakapo.

Usitake jilinganisha na dadako au shemeji,kwa kigezo kuwa Wana uwezo wa kukusaidia.

Fanya kazi za nyumbani ambazo sioni shida we kufanya kwani hata ungekuwa kwako Bado ungefanya.

Jitahidi kuwa na malengo na kuyasimamia,Bado unaweza Toka na kwenda kutafuta walau vibarua vya muda kwa kada uliyonayo au hata nje ya taaluma.

Kumbuka ,kile moyo na nafsi inachokipa muda kukifiria ndicho hicho akili huvutia na kukipa nafasi kubwa.

Amini hapo upo kwa muda,na na dhamiria kutafuta vyako kwa kujiongezea japo kaujuzi Fulani mfano udereva ,ufundi sofa ,bodaboda nk.

Kutoka na kwenda sehemu kwa lengo la kutafuta pia kuna baraka nyingi zitokazo kwa Muumba.
Maeneo kama kwenye miradi ya ujenzi mfano reli,mabomba ya maji nk.Watu wa kada ya afya wanahtajika sana.
Ni kazi za kusotea kwani hakuna kazi inayopatikana kirahisi.

Iambie akili yako unaweza fanikiwa nje ya hapo ulipo,nje ya kada yako au hata watu uliowazowea.

Amini shemeji si adui kwako,Fikisha mawazo yako kwa lengo la kusaidiwa na si kulazimisha ,kubali kujishusha na kuomba msamaha kwani mwisho wa siku ukisaidiwa n kwa manufaa yako na si.ya yeyote jamii forums.

Nashkuru kwa ushauri wako kaka, unanipa mwanga. Ila kazi za nyumbani siwezi kufanya tamaduni za kwetu mwanaume hatakiwi kuingia ingia jikon au kufanya kaz za kike. Mume wa dada yy ni mtu wa Pwani kwao ni kawaida
 
Mimi ni kijana mdogo mwenye miaka 29, nimesoma diploma ya masuala ya afya, baada ya kuhitimu nilikaa sana kijijini bila ajira. Dada na mume wake wakaamua kuniita mjini nijaribu bahati yangu.

Ila huku nako hali imezidi kuwa mbaya, kazi hakuna. Cha ajabu siku hizi wamenianzishia visa, dada na mume wake wanataka na mm niwe nafanya kazi za hapa nyumbani, wakati wafanyakazi wapo. Nilivyokataa kutumikishwa, mume wake dada anataka kunirudisha kijijini. Nimemwambia kijijini siendi, labda anipe mtaji. Amekataa kata kata, na sio kwamba hela hana. Hela anazo maana kila mwisho wa wiki anapendaga kutoka yeye na dada.

Wanashindwa kujibana hata mwezi ili mimi nipate mtaji? Leo tumezozana sana, walivyo na tabia mbaya, wameanzisha haya malumbano wakati wa kula. Hapa nipo na msongo wa mawazo, pia njaa ni kali maana nimegoma kula chakula chao usiku.

Naombeni ushauri, sielewi nifanye nini.
Bwege kweli wewe
 
Nashkuru kwa ushauri wako kaka, unanipa mwanga. Ila kazi za nyumbani siwezi kufanya tamaduni za kwetu mwanaume hatakiwi kuingia ingia jikon au kufanya kaz za kike. Mume wa dada yy ni mtu wa Pwani kwao ni kawaida
Karibu sana mkuu,

Jitahidi yale utakaoona yanawezekana uweke bidii na juhudi za vitendo kuyatekeleza.

Ukipambana hasaa,kuna siku haya unipitia yatabaki historia.

Muda ni sasa
 
Mimi ni kijana mdogo mwenye miaka 29, nimesoma diploma ya masuala ya afya, baada ya kuhitimu nilikaa sana kijijini bila ajira. Dada na mume wake wakaamua kuniita mjini nijaribu bahati yangu.

Ila huku nako hali imezidi kuwa mbaya, kazi hakuna. Cha ajabu siku hizi wamenianzishia visa, dada na mume wake wanataka na mm niwe nafanya kazi za hapa nyumbani, wakati wafanyakazi wapo. Nilivyokataa kutumikishwa, mume wake dada anataka kunirudisha kijijini. Nimemwambia kijijini siendi, labda anipe mtaji. Amekataa kata kata, na sio kwamba hela hana. Hela anazo maana kila mwisho wa wiki anapendaga kutoka yeye na dada.

Wanashindwa kujibana hata mwezi ili mimi nipate mtaji? Leo tumezozana sana, walivyo na tabia mbaya, wameanzisha haya malumbano wakati wa kula. Hapa nipo na msongo wa mawazo, pia njaa ni kali maana nimegoma kula chakula chao usiku.

Naombeni ushauri, sielewi nifanye nini.
NAona umeamua kuwapima watu upepo kwa kuwachota akili
 
Ushauri wewe komaa hapo hapo kwa Dada na Shemeji yako, waambie Kijijini hurudi kama kulima rahisi wakalime wao wakuachie nyumba,
Kwanza wewe bado kijana mdogo sana kwanini wanataka kukuzeesha na maisha ya kijijini,

Kuanzia sasa anza na wewe kuwafanyia visa, Kojoa kitandani.
Indeed.

Kama mbwai iwe mbwai tu. Alaaah!
 
Back
Top Bottom