JS nitakupa hadithi yangu
Kulikuwa na mtoto (I call him mtoto kwa sababu he sounded like one) alikoseaga namba siku moja akapiga kwangu. Sikuwa namfahamu so nikamsalimia na kumwuliza nimsaidie nini. Akanambia anamhitaji mwenye simu nikamwambia ni mie, akajibu mbona si kama sauti ya Aunt Leila, nikamwambia basi umekosea namba. Akanijibu kistaarabu tu samahani dada yangu aksante. Akakata. Baada ya siku moja akanipigia tena- safari hii usiku wa saa tano-- akaanza na samahani dada najua nimekosea namba (eti anajua amekosea but bado akapiga!!) naomba kujua unaitwa nani na unakaa wapi? Nikamwambia samahani sasa hivi ni usiku na ningependa kupumzika. (sikuona sababu ya kumjibu naitwa nani wakati keshajua amekosea!!). Huweziamini akawa anabeep (kila dakika) kila siku usiku kuanzia saa tano sita. Mr akawa anakuja juu sana na hata nikimweleza story ilivyokuwa hakuwa anaamini nikawa naulizwa swali la Barnaba .....haiwezekani akosee namba wakati wenye simu ni wengi"... huyo ni mtu wako na mnajuana.
Ilikuwa inaniumiza kichwa sana na bahati mbaya kimeo changu hakikuwa na technologia ya kubloc so niliteseka kwa muda hadi nikafikiria sijui nimtegee nimwombe tukutane kisha nimwendee na police maana ndoa yangu ilikuwa inashake haswa kwa ajili yake (whoever he was). Maana sikuwa naweza kuzima simu usiku au kuimute -nitaambiwa nina mambo yangu ati. So nikaanza kumchunia, akibeep nakaa kinywa na Mr akirauka nakaa kimya nikaambiwa nina dharau, kiburi, jeuri na kila kisifa kilichonifaa. But alikujachoka mwenyewe akaacha yaani hadi niliicremugi ile namba!!
So what I want to write here ni kuwa usimlemaze huyo if he daa want to understand you kiutuuzima, mwaga mboga kabla hajamwaga ugali. And the more you delay ndo unarise maswali kwa Mr right wako