Muhongo anaivuruga TANESCO, Magufuli yuko wapi?

Muhongo anaivuruga TANESCO, Magufuli yuko wapi?

Sijawahi kufikiria Kama kuna mtu atakuwa na nguvu ya kuleta uzi wa kuitetea TaNesco jamani hawa kweli walikuwa na CEO au Ni mausanii ya karne na karne Leo mtu anatumia kivuli cha Waziri sijui nini kuitetea TaNesco na uongozi mzima sijui tunataka marekebisho wapi sisi watanzania inawezekana kweli huyo mnaemsema msomi ana mapungufu yake lakini bora ungemtafutia kisa Hata Kwenye madini huko migodini na kwingineko Sio Tanesco please wote tunajua tumeteseka na bado tunateseka na urasimu plus huduma mbovu na mlolongo wa kishenzi kabisa unaofanywa na watumishi wa tanesco hadi Leo bado Tanesco haijakaa vizuri. Waziri awe na maringo kiburi sijui dharau hivyo umeviona wewe personally ila Tanesco watanzania wote tunajua madharau Yao viburi vyao matusi Yao majibu Yao mabaya na mauchafu Yao yote tuache kutafuta vitu vidogo vidogoo Kwenye hatua zinazochukuliwa kuondoa kero za wateja wa Tanesco ambao Ni Mimi na wewe Kama wewe mleta uzi Ni mtumishi wa Tanesco basi ujue hamkuwa wazuri Hata chembe hadi sasa mnabadilishwa tabia zenu kinguvu na mnaumia kuziacha tabia zenu mbaya zimewaganda Kama ngozi vile


Soma vizuri hakuna sehemu nimeitetea Tanesco
nimesema kama ana shida na menejimenti afanye mabadiliko
ateue ingine.....

Two wrongs do not make it right....
kama Tanesco kuna shida ya menejimenti itafutwe menejimenti ya kufaa
sio waziri kuwa 'de facto ceo'
sijui kama unaelewa tofauti yake
 
Wasomi wengi wako narrow

A PhD holder huwa anafocus kwenye a very narrow and highly specialized study area... watu jamii ya Muhongo huongozwa na maksi alizopata kwenye kujibu swali ambalo si ajabu lilikua hypothetical

it is a fact kwamba Muhongo ni loose fuse na damage yake kwenye system itakuja kugundulika when its too late

Kwa bahati mbaya sana, mfumo mzima wa Tanesco nao ni kama hauna qualities, pamoja na wengi kusomeshwa na kuwa na uwezo, the organizational culture ya tanesco inawanyima uwezo wa kuwa na maamuzi ya kujenga... wamekua more of watu wa kuangalia ya leo

Ushauri... Muhongo agundue kwamba wizara yake ni kubwa sana kuliko tanesco...

Mkuu inashangaza wewe umesoma na kuelewa tatizo
watu wengine kwa uwezo wao finyu wa kuelewa mambo wanafikiri ninasema
Tanesco iko perfect na isiguswe...

Watu hawajui hasara ya mtu kama Muhongo kujifanya CEO wa taasisi yeyote ile
 
Kweli umelalamika lakini agizo lake la kusema umeme ushuke bei na service charge itolewe ni agizo muhimu na lenye maslahi na Watanzania

Biashara hazitolewi maagizo na wanasiasa
jiulize mbona sukari haijashuka?
 
Ili la kushusha bei lilishangaza, mpaka EWURA wanakuwa na wasiwasi kuhusu punguzo linaloombwa! Lakini tunashangaa nini kwa stahili ya sasa tunaiona mawaziri, wakuu wa mikoa, wilaya n.k. wote wanafuatilia 'utendandaji' hadi kwa maofisa wasiowajibika kwao na tena kwa kuruka mamlaka zinazowahusu maofisa hao. Wanawawajibisha bila mamlaka zao kujua au hata kujulishwa - wanazisikia bombani!


Sasa wewe mwenyewe hushangai?
kipi kina faida? kushusha bei au kuzuia isipande kwa mda mrefu?
Siasa ndo zinaongoza haya mambo now
 
Nami nimeliona ilo Prof anajisahau sana nadhani huwezi toa order kwa zonal managers/regional managers wa TANESCO moja kwa moja unless umepitia kwa mabosi wao otherwise inakuwa ni KUMUNDERMINE kwa CEO wa TANESCO.
In a long run iyo italeta mtafaluku manake wapo ambao wataharibu na watasema tuliambiwa na waziri meanwhile wao wanareport kwa CEO.
Apo chain of command inakuwa ndivyo sivyo

Mkuu inashangaza watu wenye brain kama yako hapa JF siku hizi ni kama hakuna kabisa
mtu nampa hadi link aone Waziri akitoa majukumu kama yeye ndo CEO na still haelewi
 
Kama waziri anaruhusiwa kutoa maagizo pale inapofaa. Mnataka akae nyuma awe anaangalia tu? Wananchi wanapotoa malalamiko lazima achukue hatua. Chain my foot.
Kiutawala ina madhara iyo uonapo kitu wasiliana na CEO yeye ndo awashukie watu wake otherwise hao zonal na regional managers wataanza kujiona matawi na kuanza mbypass CEO na in a long run kutakuwa mvulugano .Kama ulishawai kuwa ktk ngazi ya utawala unaweza nielewa.Dunia ya sasa imeenda mbali mpaka mtu wa chini yako wanapotaka kumuajiri HOD lazima uwepo maana atareport kwako so lazima ujue aina ya mtu ambaye utafanya nae kazi.
 
Pamoja na kusifiwa usomi uliotukuka lakini nina tatizo moja na huyu mtu, huyu ni wale type ya superiority complex kujiona na kujifanya anajua kila kitu na wengine ni wapuuzi tuu
Muhongo ni kiburi ana dharau majivuno na ubabe....ngoja tuone mwisho wake
profesa Hashauruki!
 
Mkuu inashangaza wewe umesoma na kuelewa tatizo
watu wengine kwa uwezo wao finyu wa kuelewa mambo wanafikiri ninasema
Tanesco iko perfect na isiguswe...

Watu hawajui hasara ya mtu kama Muhongo kujifanya CEO wa taasisi yeyote ile
Boss

Tanzania kuna mbayuwayu wengi sana... unakumbuka jinsi walivyokua wamampinga Kagame na Rwanda humu?? check leo wanavyojihemusha kama kanga pori!!

Take it from me, Muhongo anabidi arudi juu, awe strategist na sio micro manager wa vitu vidogo vidogo, itafika siku atashindwa kuwajibisha watu kwasababu he was part of the decision and execution plan

Kwa humu, wanaopinga watakua wengi, simply because JF ni free for all, hakuna mental test, IQ test wala minimum requirements/criteria ya kuwa member

CCM has benefitted a lot from mbayuwayu
 
Boss

Tanzania kuna mbayuwayu wengi sana... unakumbuka jinsi walivyokua wamampinga Kagame na Rwanda humu?? check leo wanavyojihemusha kama kanga pori!!

Take it from me, Muhongo anabidi arudi juu, awe strategist na sio micro manager wa vitu vidogo vidogo, itafika siku atashindwa kuwajibisha watu kwasababu he was part of the decision and execution plan

Kwa humu, wanaopinga watakua wengi, simply because JF ni free for all, hakuna mental test, IQ test wala minimum requirements/criteria ya kuwa member

CCM has benefitted a lot from mbayuwayu


Mkuu hili la watu waliokuwa wanampinga Kagame leo watu hao hao wanamshabikia
simply sababu Magufuli kawa rafiki nae linadhihirisha jinsi watu wengi hapa JF ni lay men...
 
Mkuu fuatilia tu media
Hata TANESCO kupunguza bei ya kuunga umeme lilikuwa agizo lake
kwa masharti kuwa serikali itatoa ruzuku
ni kweli inatoa ruzuku but haitoshelezi
na ina maana kuwa TANESCO isijiendeshe kwa faida na isijitegemee
kuishi kwa ruzuku......na mwisho ndo hayo kwenda kukopa na deni kuongezeka....

Soma hata ile hotuba ya Zitto siku ile anafunga ishu ya ESCROW
aliitaja deni la TANESCO before Muhongo lilikuwa bilioni 50
now zaidi ya bilioni 300....

Now ameteuliwa tena na Magufuli anakuja na maagizo tele ya dizaini hiyo
Hivi kupunguza bei ulitaka nani aseme. Mambo kama kupunguza bei ni siasa yaani ilani ya walioshinda. Mwanasiasa anayetekeleza sera na ilani ni waziri katika wizara kwa niaba ya Rais na chama.
Kingine ndugu yangu ikumbukwe wazi hiyo TANESCO ilishafeli kupita kiasi ndio maana bila booster ya wanasiasa ingekwisha kabisa. Sasa hilo deni la ESCROW Muhongo kalifanyaje tena?
 
Wakome wametufanyia nini cha zaidi tangu tupate uhuru zaidi ya kutujazia mi services charge na kutuunguzia vifaaa majumbani, he is better than them
 
Aisee katika hili kama mhongo atapita humu na kusoma hapa kuna kitu ndani ya nafsi yake atajifunza, alafu watu wameomba kuachia ngazi wao wanakuja kujitangaza wanatumbua jipu mmmh hii ni kuhadaa wananchi hapa ndio nilianza kuona kumbe hizi ni movie tu. Anyway anachokifanya huyu mtu ndani ya Tanesco Mungu ndiye anayejua na anajitengenezea jipu mwenye maana watu hawajui tu lakini kuna bonge la mvutano huko but still mambo ni vuguvigu ngoja yawe hot ndio wataelewa
 
Kiutawala ina madhara iyo uonapo kitu wasiliana na CEO yeye ndo awashukie watu wake otherwise hao zonal na regional managers wataanza kujiona matawi na kuanza mbypass CEO na in a long run kutakuwa mvulugano .Kama ulishawai kuwa ktk ngazi ya utawala unaweza nielewa.Dunia ya sasa imeenda mbali mpaka mtu wa chini yako wanapotaka kumuajiri HOD lazima uwepo maana atareport kwako so lazima ujue aina ya mtu ambaye utafanya nae kazi.
Hahahahahah eti waziri anapotaka toa agizo kwa watu wa chini yake atoe kwanza kwa ceo, hivi hujiulizi mbona maagizo kama hayo hatoi kwa taasisi nyingine anazosimamia ni tanesco tu??? Sisi wananchi tunamuomba profesa Muhongo aendelee kutoa maagizo mpaka pale TANESCO itakapoamua kutoa huduma kwa wananchi bila shuruti.
 
Mkuu inashangaza wewe umesoma na kuelewa tatizo
watu wengine kwa uwezo wao finyu wa kuelewa mambo wanafikiri ninasema
Tanesco iko perfect na isiguswe...

Watu hawajui hasara ya mtu kama Muhongo kujifanya CEO wa taasisi yeyote ile

Tunaendelea kufuatilia Media Wanashusha tena

mobile.mwananchi.co.tz/Habari/Tanesco-wajiandaa-kushusha-umeme-2017/-/1597580/3149624/-/format/xhtml/-/1ku21h/-/index.html
 
Tanesco Shirika pekee ambalo huwa Lina sababisha mawaziri kuachia madaraka Na kumlazimu Rais kuvunja Baraza la mawaziri
 
Uo uhungwana = uungwana uko wapi? Wa kupunguza bei ya umeme ili kuishi kwa ruzuku? Huoni kuwa anatafuta sifa na kuiua Tanesco?
 
Aliteuliwa na kupewa uwaziri kutoka kwenye utafiti wa miamba, akajiuzuru kwa kashfa . Akagundua siasa ni utajiri akagombea ubunge fedha za Escrow zikampa kick akashinda.
Kwa maamuzi haya taifa litaona makubwa
 
Wewe mtoa mada unalako jambo au umetumwa? mimi sioni tatizo lolote kwa Prof. Muhongo zaidi ya utendaji ulio tukuka. tatizo tulilonalo watanzania ni kwamba akitokea kiongozi ambaye anahatarisha maslahi yetu lazima tumletee figisufigisu na hili ndilo linalo fanyika
 
Nimewahi kuweka thread za Waziri Muhongo kuja na sera zake binafsi za kuinyang'anya TANESCO 'uzalishaji na kubinafsisha' so far ni kama amepigwa stop ameacha kuzungumza hayo lakini sasa anachokifanya kwa TANESCO ni hatari zaidi.

Muhongo yeye ni waziri lakini ni zaidi ya CEO wa TANESCO anaingilia utendaji wa kila siku now anatoa maagizo yeye mwenyewe moja kwa moja kwa mameneja wa TANESCO wa kanda mameneja wa wilaya mameneja wa mkoa na watedaji wengi wa TANESCO.

Kilichopo now TANESCO ni kama chaos chochote menejimenti ya TANESCO ikiamua, Muhongo anaagiza wafanye kinyume chake au vile anavyoona yeye inafaaa. Yeye ni kama 'de facto CEO' wa TANESCO ieleweke kuwa yeye Muhongo hajawahi kuongoza chochote huko nyuma kabla ya kuwa Waziri na baadhi ya maamuzi yake na 'amri' zake kwa TANESCO yamepelekea deni la TANESCO liongezeke mara 5 zaidi na mtu yeyote mwenye akili anajua 'athari' za taasisi kubwa kama TANESCO kuwa wanapokea maagizo ambayo mengi siyo ya kitaalamu ni ya kisiasa kwa mtu nje ya shirika.

Ushauri wangu kwa Magufuli kama wana tatizo na menejimenti ya TANESCO ni bora kuibadili kuliko hii ya sasa ambapo menejimenti ipo lakini maamuzi yote anafanya waziri sababu mwisho mambo yakiharibika itakua uonevu mkubwa kuipa lawama menejimenti.

Vikao vya Muhongo na mameneja wa kanda na mikoa wa TANESCO vinaripotiwa hadi na media wakati mwingine vikao hivyo Waziri Muhongo anafanya bila kushirikisha menejimenti ya shirika na maamuzi ni amri tu.

Magufuli anayajua yote haya?

Huu ni mfano mmoja tu wa interference ya waziri kwa menejimenti: Muhongo kutimua mameneja Tanesco

Huu mchango wa member mmoja humu nauweka hapa kwa faida ya wengi;
The boss sioni haya kusema uvivu wa
Nimewahi kuweka thread za Waziri Muhongo kuja na sera zake binafsi za kuinyang'anya TANESCO 'uzalishaji na kubinafsisha' so far ni kama amepigwa stop ameacha kuzungumza hayo lakini sasa anachokifanya kwa TANESCO ni hatari zaidi.

Muhongo yeye ni waziri lakini ni zaidi ya CEO wa TANESCO anaingilia utendaji wa kila siku now anatoa maagizo yeye mwenyewe moja kwa moja kwa mameneja wa TANESCO wa kanda mameneja wa wilaya mameneja wa mkoa na watedaji wengi wa TANESCO.

Kilichopo now TANESCO ni kama chaos chochote menejimenti ya TANESCO ikiamua, Muhongo anaagiza wafanye kinyume chake au vile anavyoona yeye inafaaa. Yeye ni kama 'de facto CEO' wa TANESCO ieleweke kuwa yeye Muhongo hajawahi kuongoza chochote huko nyuma kabla ya kuwa Waziri na baadhi ya maamuzi yake na 'amri' zake kwa TANESCO yamepelekea deni la TANESCO liongezeke mara 5 zaidi na mtu yeyote mwenye akili anajua 'athari' za taasisi kubwa kama TANESCO kuwa wanapokea maagizo ambayo mengi siyo ya kitaalamu ni ya kisiasa kwa mtu nje ya shirika.

Ushauri wangu kwa Magufuli kama wana tatizo na menejimenti ya TANESCO ni bora kuibadili kuliko hii ya sasa ambapo menejimenti ipo lakini maamuzi yote anafanya waziri sababu mwisho mambo yakiharibika itakua uonevu mkubwa kuipa lawama menejimenti.

Vikao vya Muhongo na mameneja wa kanda na mikoa wa TANESCO vinaripotiwa hadi na media wakati mwingine vikao hivyo Waziri Muhongo anafanya bila kushirikisha menejimenti ya shirika na maamuzi ni amri tu.

Magufuli anayajua yote haya?

Huu ni mfano mmoja tu wa interference ya waziri kwa menejimenti: Muhongo kutimua mameneja Tanesco

Huu mchango wa member mmoja humu nauweka hapa kwa faida ya wengi;
Tanesco ni kichefuchefu. Muhongo Fanya kazi yako wananchi tuko nyuma yako.
 
Back
Top Bottom