Muhongo anaivuruga TANESCO, Magufuli yuko wapi?

Muhongo anaivuruga TANESCO, Magufuli yuko wapi?

Nionavyo mimi kwa muda huu ni bora Muhongo aiongoze TANESCO kwa namna anavyoona yeye kama mtalaamu kwa sababu Shirika hili limekuwa na makandokando kwa muda mrefu na kufanya huduma ya kupata Umeme iwe matajiri au kujuana zaidi kwa sababu hizi hapa:
1. Kupata uunganishwaji wa Umeme imekuwa ni gharama kubwa sana ambapo nguzo zimekuwa zikiuzwa hadi milioni moja.
2. Swala la Service Charges ni jipu la muda mrefu na bado liko kwenye taasisi nyingi za Serikali ikiwemo idara ya maji. Kama kuna mtu anaweza kujustify mstumizi halisi ya pesa za Service Charge kwa mteja ambaye hata nguzo, waya na mita alijinunulia mwenyewe, basi atuambie hapa. Hata upande wa Idara za maji tunalipa sh 2500 kila mwezi kama service Charge. Izingatiwe kuwa ukitaka kupata maji siku hizi wanakuja nawapima umbali toka chanzo cha maji hadi nyumbani kwako then unapewa bill yote hata ile ya gharama za bomba kubwa unalundikiwa wewe. Kama haitoshi, bomba lako likipasuka na ukawaita mafundi toka idara ya maji, jiandae pesa ya connectors, usafiri na ufundi. Je haya sio majipu? Hao wakurugenzi wa Bodi ya TANESCO ni majipu tu watumbuliwe maana miaka yoote ni polojo tu hatuna umeme wa uhakika. MUHONGO Tumbua majipu hayo haraka na mshauri yule waziri wa maji naye aanze na issue ya Connection na Service charges za maji ni majipu yameiva yanasubiri mtumbuaji tuuu.
 
Hivi huyu mtu anayefuta maoni yangu yeye ni nani? Si uungwana hata kidogo kuzuia fikra za watu wengine. Nimesema kama na ninyi ni jipu basi mtumbuliwe tuu
 
Amewekwa hapo ili kuwakomesha wapinza na sio kufanya kazi . tutegemee kuona uchafu mwingi Wa huyu prof
 
Nionavyo mimi kwa muda huu ni bora Muhongo aiongoze TANESCO kwa namna anavyoona yeye kama mtalaamu kwa sababu Shirika hili limekuwa na makandokando kwa muda mrefu na kufanya huduma ya kupata Umeme iwe matajiri au kujuana zaidi kwa sababu hizi hapa:
1. Kupata uunganishwaji wa Umeme imekuwa ni gharama kubwa sana ambapo nguzo zimekuwa zikiuzwa hadi milioni moja.
2. Swala la Service Charges ni jipu la muda mrefu na bado liko kwenye taasisi nyingi za Serikali ikiwemo idara ya maji. Kama kuna mtu anaweza kujustify mstumizi halisi ya pesa za Service Charge kwa mteja ambaye hata nguzo, waya na mita alijinunulia mwenyewe, basi atuambie hapa. Hata upande wa Idara za maji tunalipa sh 2500 kila mwezi kama service Charge. Izingatiwe kuwa ukitaka kupata maji siku hizi wanakuja nawapima umbali toka chanzo cha maji hadi nyumbani kwako then unapewa bill yote hata ile ya gharama za bomba kubwa unalundikiwa wewe. Kama haitoshi, bomba lako likipasuka na ukawaita mafundi toka idara ya maji, jiandae pesa ya connectors, usafiri na ufundi. Je haya sio majipu? Hao wakurugenzi wa Bodi ya TANESCO ni majipu tu watumbuliwe maana miaka yoote ni polojo tu hatuna umeme wa uhakika. MUHONGO Tumbua majipu hayo haraka na mshauri yule waziri wa maji naye aanze na issue ya Connection na Service charges za maji ni majipu yameiva yanasubiri mtumbuaji tuuu.

Si bule kichwa chako kitakuwa hakifanyi kazi vizuri.

Kila huduma ina service charge, watanzania tumekuwa watu wa hajabu sana TATIZO la TANESCO limesababishwa na wanasiasa wenyewe.

Mikataba mibovu waliyoingia kwa nini hawataki kuifafanyia review?

Ni vipi Capacity charge itasimishwa tusiendelee kuilipa?Wabunge na Waziri wa Nishati Mtafanya nini kuokoa janga hili?Tuache kila kukicha ni Capacity charge Richmond Symbion ipatikane Solution.Wadanganyika tunadaganyika kweli.Profesa Muhogo Waziri wa Nishati njoo mbele utupe Suluhisho Tunakuaminia ktk Sekta hii uliyobobea.

SOMA HII ITAKUSAIDIA, iliwekwa na Pasco wa JF

Wanabodi, hii nimeikuta kule fb, kama imeishaletwa humu, iunganishe kule ilipo!.

Hillary Was Scheduled To Meet Privately With Crony Lobbying Her For Africa Business
Hillary Clinton's State Department schedule includes an entry for a meeting with former Ambassador Joseph Wilson in December 2009, just a month after the…
DAILYCALLER.COM

Maria Sarungi-Tsehai
12 hrs ·
Jamani hii imeandikwa na gazeti la huko Marekani siyo sisi waafrika na ma-conspiracy theory zetu! Sasa tunaona kumbe MCC yote huku inahusiana na Clinton na Symbion. Dah! Hebu someni article yote kwanza Dan Nkurlu Evarist Chahali Lusajo Lazarus Mwaisaka Mbaraka Islam Mimi Mwanakijiji Zitto Kabwe Maxence Melo
Months after Wilson contacted Clinton about Symbion, a small, quasi-federal agency called the Millennium Challenge Corporation (MCC) granted the company $100 million in ....
See More

My Take.
Maria Sarungi-Tsehai, Sisi Tanzania tulichotaka ni umeme, bila kujali kampuni ni nani, ni ya wapi na inamilikiwa na nani!. Tangu ilipokuja nchini kwa jina la Richmond, na baadae Dowans, na kutuletea umeme kwa kutucharge capacity charge ya shilingi milioni 152 kwa siku, ilikutwa ni kampuni hewa!, Tume ya Mwakyembe ilipobaini hayo madudu, tukamtoa kafara Lowassa, tukavunja mkataba na tukahakikishiwa hakuna madhara!. Zitto Kabwe akashauri tuinunue mitambo hiyo, akagomewa!, tena tukaona bora kuwasha mitambo ya IPTL ambayo ni chakavu mara 100 kuliko Richmond, uzalishaji wa umeme kidogo, kwa gharama kubwa na uchafuzi mkubwa wa mazingira, lakini watu bungeni walijiapiza kuliko kutumia Richmond, "Over my dead body!". Tukapelekwa mahakamani, tukashindwa na kudaiwa tozo ya Dowans, watu wakasema hatulipi!. Wenye pesa zao wakainunua na kuibadili jina to Simbion. Ukweli ni kuwa ile tozo tumeilipa kimya kimya na tunaifidia kwenye bili za umeme!, Richmond ndio ile ile Dowans, na ndio hii hii Simbion. There is no any justification at all, kama tuliikataa Dowans na kuikubali Simbion!, mitambo ni ile ile, umeme ni ule ule tulioukataa, na capacity charge ni ile ile milioni 152 kwa siku na tunalipa mpaka kesho!. Watu wale wale walioilaani Richmond, na kujiapiza "over my dead body!", ndio wale wale waliokuwa waki dance na Mama Clintoni pale Siombion!. Ukweli ni kampuni hewa, na wamiliki hewa yenye usajili hewa, ila mitambo ni mitambo ya ukweli, inafua umeme wa ukweli, tunacholipia sisi ni ile mitambo na ule umeme!. .Tukiambiwa sisi Watanzania ni watu wa ajabu sana, tunajifanya kushangaa!, Hata Magufuli hii kasi aliyoanza nayo ni nguvu tuu ya soda, CCM bado ni ile ile juzi, jana, leo na hata milele!.

Pasco
 
Mkuu The Boss,ni vema kama hao wataalam wa Tanesco wakajiuzulu kama wanaona wanaingiliwa katika maamuzi
Kupunguza umeme hakuepukiki baada ya gharama za uzalishaji kushuka na uzalishaji kuongezeka mpaka sasa tuna ziada ya megawati 100,na bado zitashuka zaidi kinyerrezi III itakapoanza kazi

Hizi ni SIASA gharama ya uzalishaji bado ipo juu, unafahamu mpaka sasa TANESCO inazalisha megawati ngapi?

Unafahamu matumizi ya nchi kwa ujumla inahitaji megawati ngapi?

SIASA na utalamu vitu viwili tofauti, pengine unatumika KISIASA ama AKILI YAKO inamapungufu katika kufikilia
leo tumeelewana kwamba lengo ni ufanisi zaidi bila kujali who oversee it. safi sana mzalendo mwenzangu.
 
Mkuu fuatilia tu media
Hata TANESCO kupunguza bei ya kuunga umeme lilikuwa agizo lake
kwa masharti kuwa serikali itatoa ruzuku
ni kweli inatoa ruzuku but haitoshelezi
na ina maana kuwa TANESCO isijiendeshe kwa faida na isijitegemee
kuishi kwa ruzuku......na mwisho ndo hayo kwenda kukopa na deni kuongezeka....

Soma hata ile hotuba ya Zitto siku ile anafunga ishu ya ESCROW
aliitaja deni la TANESCO before Muhongo lilikuwa bilioni 50
now zaidi ya bilioni 300....

Now ameteuliwa tena na Magufuli anakuja na maagizo tele ya dizaini hiyo
Unaposhusha gharama za kuunganisha umeme, in the SHORT RUN ni burden kwa shirika but in the LONG RUN ni faida kwa shirika-- si ama watu wafanye long run or short run planning!

Ingawaje kwenye milango yetu hatusimamiwi na polisi lakini bado watu wanakwepa kutumia majiko ya umeme kv umeme ni VERY expensive.

Umeme ni very expensive coz high investment and operation costs za TANESCO zinakuwa distributed among FEW service users waliounganishiwa umeme. Na moja ya sababu zinazofanya watu wachache wawe wameunganishwa ni kutokana na gharama kubwa za kuletewa umeme.

Now, ikiwa serikali inaamini kwamba uzalishaji wa umeme utaongezeka maradufu basi wanatakiwa kuwa na plan in advance za kuuza huo umeme. Ili kuuza umeme mwingi zaidi lazima uandae wateja wengi zaidi in advance. Na kv gharama za kuunga umeme zilikuwa barrier basi lazima upunguze au kuondoa hiyo barrier!

Sasa kama una umeme mwingi sana na una wateja wengi sana; zile investment and operation costs za TANESCO zitakuwa distributed among MANY ( from FEW) service users. Kushuka kwa unit production cost kunaweza kuifanya TANESCO washushe bei coz' wasipofanya hivyo watakuwa na umeme mwingi kwenye stock usiotumika kv wateja wengi waliopo wataishia kutumia umeme kwa vitu vidogo vidogo kwa kuogopa bili! Kinyume chake, ukishusha watu wengi hawataogopa tena kutumia majiko, pasi, heaters, mafriza n.k!! Na kv TANESCO watakuwa na umeme wa kutosha wala hutawasikia wakisisitiza watu watumie umeme kwa kubana! Leo hii wanasisitiza kila cku coz wanafahamu watu wakianza kuvurumisha majiko na mafriza, wao watashindwa ku-afford!

Sasa wakati watu wengi na wengi zaidi mnaposhindana kununua majiko na mafriza; hatimae hiyo inageuka kuwa opportunity ya kuongezeka mauzo ya units za TANESCO and eventually kuongeza mapato na faida.
 
Ni kwa nini Waziri Muhongo ndiye naweza kusema Waziri anayechukiwa na kupigwa labda klk Mawaziri wote wa Awamu ya tano na Upinzani? Hivi kosa lake hasa ni lipi? Ni lipi kubwa alilolifanya kuweza kustahili hii chuki?

Je kuna kitu labda wengi wetu hatufahamu? Kwa maana siwezi kuamini kwamba watu kama Zito kabwe, chadema &Co. wanamchukia Waziri Muhongo kwa manufaa ya Taifa letu, aidha itakuwa mambo ya mikataba ya umeme (Symbion) ambapo Waziri Muhongo amekuwa mwiba na anataka kusitisha mikataba au itakuwa kwenye Madini ambapo kote huko Upinzani wako kwenye payroll ya Wafanyabiashara wanaoinyonya nchi hii, vinginevyo haingii akilini kwa maana sioni kosa la Waziri Muhongo mpaka leo hii!
 
Ni kwa nini Waziri Muhongo ndiye naweza kusema Waziri anayechukiwa na kupigwa labda klk Mawaziri wote wa Awamu ya tano na Upinzani? Hivi kosa lake hasa ni lipi? Ni lipi kubwa alilolifanya kuweza kustahili hii chuki?

Je kuna kitu labda wengi wetu hatufahamu? Kwa maana siwezi kuamini kwamba watu kama Zito kabwe, chadema &Co. wanamchukia Waziri Muhongo kwa manufaa ya Taifa letu, aidha itakuwa mambo ya mikataba ya umeme (Symbion) ambapo Waziri Muhongo amekuwa mwiba na anataka kusitisha mikataba au itakuwa kwenye Madini ambapo kote huko Upinzani wako kwenye payroll ya Wafanyabiashara wanaoinyonya nchi hii, vinginevyo haingii akilini kwa maana sioni kosa la Waziri Muhongo mpaka leo hii!

arrogance.

it's a thing most people cant stomach.
 
Daah hivi kuna ufisadi wowote uliowasilishwa bungeni na mbunge wa ccm? symbion,epa,iptl ni upinzani ndio wameleta.Sasa itakuaje watake kukata mrija unaowalisha?
 
Kosa la mihongo ni kuziba mianya ya ufisadi na kutakaa kwake kubuluzwa na madalali
 
Ni kwa nini Waziri Muhongo ndiye naweza kusema Waziri anayechukiwa na kupigwa labda klk Mawaziri wote wa Awamu ya tano na Upinzani? Hivi kosa lake hasa ni lipi? Ni lipi kubwa alilolifanya kuweza kustahili hii chuki?

Je kuna kitu labda wengi wetu hatufahamu? Kwa maana siwezi kuamini kwamba watu kama Zito kabwe, chadema &Co. wanamchukia Waziri Muhongo kwa manufaa ya Taifa letu, aidha itakuwa mambo ya mikataba ya umeme (Symbion) ambapo Waziri Muhongo amekuwa mwiba na anataka kusitisha mikataba au itakuwa kwenye Madini ambapo kote huko Upinzani wako kwenye payroll ya Wafanyabiashara wanaoinyonya nchi hii, vinginevyo haingii akilini kwa maana sioni kosa la Waziri Muhongo mpaka leo hii!
Ni fisadi tu
 
Nimewahi kuweka thread za Waziri Muhongo kuja na sera zake binafsi za kuinyang'anya TANESCO 'uzalishaji na kubinafsisha' so far ni kama amepigwa stop ameacha kuzungumza hayo lakini sasa anachokifanya kwa TANESCO ni hatari zaidi.

Muhongo yeye ni waziri lakini ni zaidi ya CEO wa TANESCO anaingilia utendaji wa kila siku now anatoa maagizo yeye mwenyewe moja kwa moja kwa mameneja wa TANESCO wa kanda mameneja wa wilaya mameneja wa mkoa na watedaji wengi wa TANESCO.

Kilichopo now TANESCO ni kama chaos chochote menejimenti ya TANESCO ikiamua, Muhongo anaagiza wafanye kinyume chake au vile anavyoona yeye inafaaa. Yeye ni kama 'de facto CEO' wa TANESCO ieleweke kuwa yeye Muhongo hajawahi kuongoza chochote huko nyuma kabla ya kuwa Waziri na baadhi ya maamuzi yake na 'amri' zake kwa TANESCO yamepelekea deni la TANESCO liongezeke mara 5 zaidi na mtu yeyote mwenye akili anajua 'athari' za taasisi kubwa kama TANESCO kuwa wanapokea maagizo ambayo mengi siyo ya kitaalamu ni ya kisiasa kwa mtu nje ya shirika.

Ushauri wangu kwa Magufuli kama wana tatizo na menejimenti ya TANESCO ni bora kuibadili kuliko hii ya sasa ambapo menejimenti ipo lakini maamuzi yote anafanya waziri sababu mwisho mambo yakiharibika itakua uonevu mkubwa kuipa lawama menejimenti.

Vikao vya Muhongo na mameneja wa kanda na mikoa wa TANESCO vinaripotiwa hadi na media wakati mwingine vikao hivyo Waziri Muhongo anafanya bila kushirikisha menejimenti ya shirika na maamuzi ni amri tu.

Magufuli anayajua yote haya?

Huu ni mfano mmoja tu wa interference ya waziri kwa menejimenti: Muhongo kutimua mameneja Tanesco

Huu mchango wa member mmoja humu nauweka hapa kwa faida ya wengi;
Karma has started hitting back!.
P.
 
Pamoja na kusifiwa usomi uliotukuka lakini nina tatizo moja na huyu mtu, huyu ni wale type ya superiority complex kujiona na kujifanya anajua kila kitu na wengine ni wapuuzi tuu
Muhongo ni kiburi ana dharau majivuno na ubabe....ngoja tuone mwisho wake
dah mshanaJr GT na kweli tumeona mwisho wake
 
Pamoja na kusifiwa usomi uliotukuka lakini nina tatizo moja na huyu mtu, huyu ni wale type ya superiority complex kujiona na kujifanya anajua kila kitu na wengine ni wapuuzi tuu
Muhongo ni kiburi ana dharau majivuno na ubabe....ngoja tuone mwisho wake
Mwisho wake leo
 
Tunasubiri Magufuli ...karma yake itakapofika
itafika tuu kwa sababu karma haina mswalie Mtume, ila inaweza is hit back kama mtu ana i reverse, yaani baada ya kufanya maovu, au mabaya, halafu kabla karma hai hit back, akafanya mambo mema mengi na makubwa kuliko yalemaovu, hivyo ile positive karmic forces zikawa stronger kuliko negative karmic, hizo positive zina reverse the negative ndio maana kuna watu niliwaeleza humu, kuwa siku ya siku, unaweza kushangaa kuwakuta Osama, Saddam na Qaddafi peponi, halafu Bush, Blair na Obama motoni!.

P.
 
Back
Top Bottom