Idimulwa
Platinum Member
- May 27, 2011
- 6,205
- 5,283
Wakuu taratibu tupo msibani.... ingawa bado ni tetesi
RIP...
Msiba feki?
Wakuu taratibu tupo msibani.... ingawa bado ni tetesi
RIP...
Huyo kajitakia pia liwefundisho kwa wote wanaobeba hela nyingi kizembe
source yako ni wapi?
Tatizo sio majambazi, serikali imebadilika kuwa jambazi na kuwadhulumu raia wake kwa wizi wa wazi wazi, unategemea nini kutoka kwa hawa wezi wa kuku. Hakuna amani, wananchi wanalipa kodi ili kuona serikali inakuwa na jeshi madhubuti la polisi matokeo yake viongozi wa juu kabisa serikalini wanatumia pesa hizo kwa shopping nchi za nje na kuwaacha walipa kodi solemba. Aibu kuwa na rais dhoofu.
Ni aibu Sana jiji la Dar kukosa CCTV camera. Kama zingekuwepo saizi Kova na watu wake wangekuwa wameishaona sura za waliomuua huyo jamaa na kazi ingebaki kuwatafuta tu. Pia nchi haina vitambulisho ya taifa, haina biometric data za watu wake ambayo pia ingesaidia watu wa Forensic kuwajua wauaji kwa kutrace vitu kama finger prints, hairs nk...
Tunaongozwa na jamaa limetokea Msoga, kule wanacheza ngoma za kienyeji na kunywa ile pombe ya mnazi, halina mawazo ya kuweka vifaa vya kiteknolojia ya kisasa kumaliza kadhia kama hizi. Watu kwa mamia wameuwawa, wamemwagiwa tindikali, wameporwa Mali lakini polisi hawajui waanzie wapi wanaishia kufanya kazi kama waganga wanaopiga ramli. Hakuna hata kuwawajibisha polisi kwa mrundikano wa UNSOLVED MURDER CASES. Wakishaenda kuchungulia eneo la tukio na kupiga picha wanaondoka zao, hakuna msukumo wa kuwanasa wauaji, labda kuwe na presha za kisiasa au kidini Kova anakamata watu feki na kusingizia ndio wauaji baada ya kuwatesa kule SITAKISHARI na kila mtanganyika anaridhika. Ndio maana tunawaambia kila siku ikataeni hii CCM, tuweke hata jiwe lituongoze tuanze upya. Nairobi Kuna CCTV, sisi tunashindwa nini?
Hili ni tatizo sana.
Lakini tusimlaumu mkulu kwa hili kwani hili ni jukumu la waziri ambae anashughulikia usalama wa raia na wizara ya mambo ya ndani.
Kwa uzoefu wangu suala la CCTV, biometric fingerprinting na mambo yote yanayohusu forensics katika nchi zilizoendelea yanafanywa kuwa kuwashirikisha wananchi ambao wamesomea mambo hayo na wanaendesha taasisi zinazoshughulikia mambo hayo kwa ushirikiano na polisi na wizara husika ya mambo ya ndani.
Lakini kwa nchi kama Kenya au Rwanda wao wameweza kwa sababu kuna uadilifu kwenye kazi hizi ambazo zinahusu kubeba na kushughulikia data za raia na kwa Tanzania kuna hatari ya UFISADI kuingizwa kwenye eneo hilo na ndio maana haiwezekani kuwa na ushirikiano huo ambao utaitwa kwa kiingereza "Ad- hoak" au improvised events, yaani ni ushirikiano usodumu kwa muda mrefu.
Nchi zilizoendelea zenyewe zimejipangia utaratibu ambao ni dedicated kabisa na ikitokea incident sehemu basi kila mtu anafahamu jukumu lake la ku-attend ile incident kuanzia polisi, CID, ambulance na watu wa forensics.
Mkuu elewa kwamba CCTV sio kitu ya gharama, haitofautiani Sana na gharama za taa za barabarani. Lakini kwa vile tunaongozwa na vipofu hawazungumzii kabisa na hata kuweka kwenye mipango yao. Ni aibu kwa jiji la Dar kukosa CCTV camera, hizo pikipiki boxer zote zingemulikwa. Pili umiliki wa Leseni za udereva hapa kwetu ni wa hovyo, nchi za wenzetu kuwa na leseni ni kazi ya ziada na inakuwa linked na makazi ya mmiliki wa leseni na hata gari unayoendesha. Ukifanya kosa unaletewa faini kwenye address yako. Pia leseni za madereva wa Boxer zingesaidia kuwapata hawa jamaa. Suala la usalama wa raia kwa teknolojia ya kisasa liko integrated Sana, lakini starting point ni vitambulisho vya taifa na biometric database ambayo CCM Wanapiga danadana isiwepo kwa vile ufisadi wanaofanya wa kumilikisha Mali kwa watu hewa ungejulikana tu kwa vile fingerprints hazidanganyi