Mtu anawezaje kulenga watu saba gizani...

Mtu anawezaje kulenga watu saba gizani...

Wajuzi mtuambie.. Mana inaonekana gari haikuharibika sana kwa risasi ikiharibika kutokana na kupinduka ukiachia tundu la risasi lililopiga kioo kwa mbele...
kama ni swala la mkuranga basi aliyekwambia ni gizani alikudanganya... haikuwa gizani bali ilikuwa ni saa 12 jioni.. aliyekuwa wa kwanza kulengwa alikuwa dereva na gari ikapoteza muelekeo maana ilikuwa kwenye mwendo hivyo kwenda kutumbukia kwenye mtaro na hivyo wale wahalifu kutumia mwanya huo kuwashambulia askari kirahisi maana gari lilipata ajali...
 
........kwa hiyo hao walikuwa hawana rushwa ya kutoa bali risasi !? ....unashirikisha ubongo au mat.ako kufikiri !?
Umemuelewa ni kwa nini ameandika hivyo?..Au unamtusi tu bila kujua alichokimaanisha.
 
Mkuu hayo yote si rahisi kuyafahamu hasa sisi raia wa kawaida.. Tunabaki kushangaa tu... Vp polisi wengine walishindwa kutake cover?
Endelea kushangaa tu, shangaaaaaaa.


2013 miili ya askari jwtz 9 wakiwa opp UN sudan ililetwa baada ya kufanyiwa ambush na waasi,je walishindwa kabisa KUTAKE COVER??

Lengo langu nataka ujue kuanzia sasa, siraha kama siraha moja ile unayoiona inaweza kupindua nchi kabisaa, swala tu ni kwamba imetumikaje.ndio maana ikitoweka mikono salama TAHARUKI.nashangaa tunakenua tu humu sababu waliokufa ni wanaotupora vihera vyetu.

Huyu muuaji ametumia akili ya kawaida kabisa kujua kwamba gari ikiwa kwenye mwendo cha kushambulia 1)dereva 2)tairi 3)abiria. Sasa nikuulize inahitaji utaalam gani kurenga hivyo vitu??

Mrio wa risasi+gari kuanza kuyumba+mpaka kuanguka askari wanatake vip cover!!!!wakati adui yao yupo pembeni anasubiri wa kwanza kutoka???aliyepona inasemekana alirushwa mbali baada ya gari kuanguaka.ikawa bahati kwake wala sio uaskari.

Wakati mwingine tuwe tunatuliza akili kwanza kabla tu ya kuanza kuandika.
 
Hata Wewe pia kama unazijua ungeweza tu kumwekea pia na wala kusingeharibika kitu ILA kwakuwa unawashwa na aina yangu kubwa ya ' Uelewa ' na ' Ufahamu ' wa mambo mbalimbali ambayo kimsingi huwa kila siku yanakuchukiza ukaamua kuja na aina yako hii ya response ya ' Kipumbavu ' kabisa Kwangu. Narudia tena kukuambia utaendelea kuichukia 24/7 hii ID ila zawadi ya Kipekee ya kuwa ' Talented and Charismatic ' niliyopewa na Mwenyezi Mungu ' kamwe ' hutoweza kuwa nayo na yawezekana pia hata katika ' Koo ' zako zote mbili hakuna ambaye anathubutu tu kufikia robo yangu.
Mimi nikajua jamaa hapo juu anakusingizia!!.Kumbe kweli una masifa,tena ya KIJINGA.
 
Namashaka na style ya wauaji kuwa ya ustadi mkubwa,bila woga,kufahamu mda vizuri na malengo mahususi.
Wanaweza kuwa maaskari wenzao wanao wafahamu vizuri!
Jeshi la polisi lifanye uchunguzi wa kina na madhubuti!Familia nane kwa wakati mmoja kwenye kambi moja ni hatari sana,hata kwa waliobaki kambini hapo.
Hao wanaovamia Studio na kutishia watu kwa bastola si wakupuuzwa na kuchekewa.Kuna kitu lazima.Tunalazimishiwa woga bila sababu ya msingi.Fanyeni kazi yenu kwa WELEDI walinzi wetu wa amani.USALAMA wa raia upo shakani
 
Kuna nduguyangu kafaa miongoni mwa waliowawa cha ajabu yeye ni police FFU Morogoro na hata familia yake iko Morogoro sasa huko Pwani sijui ilikuaje. Anyway deadman tell no tale
 
Ndugu itakuwa bado hujakutana na sharp shooters. Inaonekana jamaa alikuwa good marksman maana one bullet ilitoboa kioo usawa wa kifua cha dereva the other ones tatu pia on target kwenye passenger seat.
Giza sio shida kabisa ilimradi target yako unaijua ilipo
Umenikumbusha Pini Moja kali sana la SHARP SHOOTERS AKA SAUTI YA MIUJIZA NA PINI LAO LA UBANDIDU 1998 HIYO.
 
Hivi hizi mada za hovyo watu wameuliwa tena wana usalama wetu
unakuja kubwabwaja!!
 
Mimi nikajua jamaa hapo juu anakusingizia!!.Kumbe kweli una masifa,tena ya KIJINGA.

Sasa kama Wote Wewe na Yeye mna ' akili ' tu za kujitawaza chooni, kukomboleza mboga na za kuvukia barabara kwanini mnadhani nisijisifu kuwa nina ' upeo ' mkubwa kuliko nyie ' hopeless creatures ' wawili? Tena hujakosea Mkuu yaani hakuna kitu ninachopenda duniani kama sifa na kujisifu halafu nikusaidie tu inakupasa ukiwa ni Mtu wa namna hiyo basi kweli hata kiuhalisia uwe hivyo hivyo na bahati nzuri GENTAMYCINE naendana na ' mijisifa ' yangu. Nakusubiri kwa hamu uje na ' upupu ' wako mwingine ili niiharibu ' Pasaka ' yako togwa nilitie inzi.
 
Wajuzi mtuambie.. Mana inaonekana gari haikuharibika sana kwa risasi ikiharibika kutokana na kupinduka ukiachia tundu la risasi lililopiga kioo kwa mbele...
Inawezekana maana hawa ni wale Vijana waliokwenda Somalia kupigana na alshabab wanapotemwa wanarudi kuturudi! Snipers
 
........unajua maana ya 'ambush' !? (kijeshi) umewahi kupiga hata kwata ?(JKT)
Ambush zote zinatakiwa 99% successfull na si kitu cha kubahatisha, bali hupangwa. Unakumbuka ambush waliopigwa wakenya na Al Shabab mpaka wakavunja kambi ?
Mkuu uko sahihi mia kwa mia. Hii ilikuwa ni ambush ambayo hupangwa kwa kuongezea tu kwa sisi yuliopita JKT, ambush ina eneo linaloitwa "killing ground" ambalo nalo huandaliwa mapema. Na kwa kuwa ni tukio la kupangwa ambush zote huwa zina maafa makubwa sana kama hili lilivyotokea. Hata katika historia iko hivyo. Wajerumani waliingia kwenye ambush ya Wahehe walipoteza askari 300. Kwa wajuzi wa hizi ambush ni kuwa dawa yake huwa ni kukimbia tu lakini tukio limekuwa complicated kwa kuwa wapendwa wetu walikuwa kwenye gari.
Hapa cha kujiuliza ni kuwa waliopanga haya si watu mbumbumbu. Walijua wanachofanya na matokeo yake bila ya shaka waliyatarajia. Ni wakati Polisi watumie weledi wao hata ikibidi waombe msaada po pote pale kwa kuwa ni dhahiri huyu adui ana mipango ya muda mrefu. Mwenyezi Mungu awape nguvu wafiwa katika kipindi hiki kigumu. RIP polisi wetu.
 
Mbona inawezekana apo ni kwamba wamewahiwa yan huyo mshambuliaj inaonekana kama anauzoefu hiv na alifanya kwa haraka isingekua rahis wao kujibu mashambulizi
 
Kuna nduguyangu kafaa miongoni mwa waliowawa cha ajabu yeye ni police FFU Morogoro na hata familia yake iko Morogoro sasa huko Pwani sijui ilikuaje. Anyway deadman tell no tale
mengi yatasemwa, lakini kikosi kilikuwa na askari kutoka kwenye kambi mbalimbali
 
Back
Top Bottom