Mtoto wangu mtukutu mno! Naombeni ushauri

Mtoto wangu mtukutu mno! Naombeni ushauri

Huyo mtoto sio bure kuna ujumbe anatoa kwa wahusika lakini nyie hamjui??
Yawezekana kabisaa hiyo sio dam yenu??
Hapo kuna baba feki hapo kama wewe ni mzazi wa kiume kaa ukijua unalea dam ambayo sio yako.

Nina mengi sana ya kukueleza tena kwa ushahidi lakini kama huamini mambo ya mila mila itakuwa kazi bure.na ushahidi na mifano hai ya kutosha.

Ss mtoto kama huyo kunadawa anapewa na kama sio wa dam yenu anazurika nayo
Kwa nini kosa la mzazi aadhibiwe mtoto? Mtoto hajimbambika kwenye ukoo wenu, sasa inakuwaje yeye ndo adhurike. Kwa nini asidhurike yule aliwabambikia. Nafikiri inabidi muitafakari vizuri hiyo njia yenu.
 
Renegade Asante kwa ufafanuzi mzuri. Wakati mwingine hizi mada za JF tunazijibu kwa utani kumbe mwenzetu ana tatizo kweli. Kwa kuongezea kwenye ufafanuzi huo, wakati mwingine tabia mbaya ya mtoto ni matokeo ya yale maneno yaliyotamkwa na baba au mama wakati wa mimba huska. Ilimtokea rafiki yangu, yeye na mke wake walikuwa wameamua watazaa watoto watatu tu, na waliamua kufuata kalenda. wakiwa ndani ya mkakati wao wa kufuata kalenda mwanamke kapata mimba. yule jamaa alimfokea sana mke wake kwa nini karuhusu ile hali. Mimba miezi tisa wiki 40, mtoto hatoki. Wiki 42, mama kafanyiwa maombi ndo mtoto kazaliwa.
Mtoto kakua lakn kila akishikwa na baba lazima aliye sana. Hadi miaka miwili hali hiyo hiyo. Miaka minne, baba hawezi hata mkumtuma kitu. Fimbo haikusaidia. Baba akaanza kuhisi mtoto si wake.
Kama bahati akahudhuria semina ya maisha ya kiroho, bahati nzuri akafundishwa somo la toba. Ile semina ikampa mwanga. Baada ya semina jamaa alienda moja kwa moja hadi nyumbani. Kafika kamnyanyua mtoto na kumbeba kifuani kwake. Mtoto anakawa anajitahidi kujinasua mikononi mwake ila jamaa kamung'ang'ania, huku akitamka maneno ya kuomba msamaha kama alivyoelekezwa kwenye semina. Ilikuwa jioni, wakalala ikawa asubuhi. Mtoto alikuwa wa kwanza kumuamsha na kumsalimia: 'Baba shikamoo'. Hicho ni kitu alikuwa hajawahi kupata kutoka kwa huyo mtoto. Tokea hapo, mtoto akabadilika baba yake ndo akawa kipenzi chake kuliko hata mama. Kwa hiyo basi huenda tatizo likawa kwenye meneno yaliyotamkwa juu ya ile mimba. Wazazi waulizwe vizuri circumstances za hiyo mimba.

Superstition mkuu. Hii ni malezi wala sio hicho ulichosema
 
Kwa yeyote anaye weza toa msaada wa aina yoyote kwa mjukuu wangu ni mtukutu, shule hataki matukio ya udokozi, michezo mingi haishi kwake.

Anasumbua sana ashapigwa sana na kwa sasa ukimpiga anakwambia nichome moto ukimwambia njoo nikuchome anakuja na kujivisha tairi yani acheni tu.

Kwa anaye jua kituo ama dawa anisaidie.

Mi sitatoa coment mpaka mtoa uzi huu atuambie full background ya mtoto huyo kwani maelezo yake hayatoshi kwa mtu kuelewa namna gani ushauri. Mi naomba anieleze kiufupi kuanzia mimba kutungwa je ilikuwaje mpaka anazaliwa. Ndo nitampa ushauri.
 
Si uliona raha kulea mjukuu amekushinda unaomba ushauri .................muache aendelee kudokoa sisi hatutamuita njoo uchomwe moto bali tutachoma bila kumuita kama unavyomuita.
 
Huyo ana kipaji cha wizi...inabd ukiendeleze anaweza kuwa jambazi na akawatoa katika lindi la umasikin...KIPAJI KUTOKA MOYONI.
 
Kuna umuhimu wa mtoto kulelewa na wazazi wawili; baba na mama hata kama mmoja kati yao ni wa kufikia...

Amekosa mapenzi na malezi ya baba...anaweza akawa anafanya afanyayo kwa kuwa kuna anachofikiri...anaweza akawa anahisi abandoned na baba yake...kwa nini haukai na mtoto wako...tena mtoto wa kiume? Unategemea atamtumia nani kama role model wake?

Kwa ufupi hapa solution ni ngumu kwa sababu wewe si unayekaa na mtoto na hujui anapata malezi gani na ana experience nini.

Na ni bahati mbaya sana wana saikolojia wanasema mtoto ufunzwa kuwa na tabia unayotaka akiwa below 7 years...in other words kwa sasa ni too late.
 
Very true.
Adhabu kubwa kabisa ni kumuambia mtoto 'watoto wa Mungu hawafanyi hivyo na mama hapendi kabisa'. Kwa upole bila kupandisha sauti.
  • Expect good behavior from your children
​Children must know what you expect from them and what they can expect from you. When children can predict how you will behave in reaction to them, they will make better behavioral choices themselves
 
Kwa yeyote anaye weza toa msaada wa aina yoyote kwa mjukuu wangu ni mtukutu, shule hataki matukio ya udokozi, michezo mingi haishi kwake.

Anasumbua sana ashapigwa sana na kwa sasa ukimpiga anakwambia nichome moto ukimwambia njoo nikuchome anakuja na kujivisha tairi yani acheni tu.

Kwa anaye jua kituo ama dawa anisaidie.

mhhhhhhh!
 
Simpo..kama hapo Dar mnunulie bodaboda..baada ya wiki 2 utaletewa habar za kuaminika
 
Huyo mtoto sio bure kuna ujumbe anatoa kwa wahusika lakini nyie hamjui??
Yawezekana kabisaa hiyo sio dam yenu??
Hapo kuna baba feki hapo kama wewe ni mzazi wa kiume kaa ukijua unalea dam ambayo sio yako.

Nina mengi sana ya kukueleza tena kwa ushahidi lakini kama huamini mambo ya mila mila itakuwa kazi bure.na ushahidi na mifano hai ya kutosha.

Ss mtoto kama huyo kunadawa anapewa na kama sio wa dam yenu anazurika nayo

Mmmh mwingine ni unyama,kisa cha kumpa dawa mtoto asiye na hatia adhulike kwa kosa la mama maana yake nini?so unfair
 
Pole Mkuu, STOP STOP now, acha kumpiga tena kwani keshakuwa sugu... Just mpapase kichwani all the time, Niuvumilivu wako unahitajika na Mpe attension yako zaidi ya mambo yako mengine !! ikishindikana Kuna maombi na Dua'a fulani asomewe na maji yaliyosomewa. In-ShaAllah atapona na utoto utapita nakuwahandsome and clever child.
Good luck Ubarikiwe
muelekeze hizo dua ili atafute sheikh amsomee inawezekana ikawa solution nzuri kuliko kupiga, anaweza mtia mtoto kilema.
 
kaka@mfamaji anaishi na bibi na mama ake

Baba wa mtoto u wapi? inawezekana alimtaka mkamng'ang'ania so amefanyala kufanya ili msiwe na amani, mtafuteni muongee naye anaweza akawa na solution nzuri.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom