Mtoto wangu mtukutu mno! Naombeni ushauri

Mtoto wangu mtukutu mno! Naombeni ushauri

Kwa yeyote anaye weza toa msaada wa aina yoyote kwa mjukuu wangu ni mtukutu, shule hataki matukio ya udokozi, michezo mingi haishi kwake.

Anasumbua sana ashapigwa sana na kwa sasa ukimpiga anakwambia nichome moto ukimwambia njoo nikuchome anakuja na kujivisha tairi yani acheni tu.

Kwa anaye jua kituo ama dawa anisaidie.
Keshakuwa sugu huyo!!Mtoto hafundishwi kwa kipigo hata kama ni mtukutu!!Inawezekana ana ugonjwa unaoitwa ADHD(Attention Deficit Hyperactivity Disorder) anakuwa hyperactive!!
 
kaka@mfamaji anaishi na bibi na mama ake

Kusema kweli hilo ndio tatizo la msingi. Most of childs wanaolelewa kwa mpango huo huharibika. Mchukue kaa nae karibu umfanyie cancelling anawezaa kubadilka. Pia kuna shulle za watoto watukutu huko wanasaidiwa pia kubadilika
 
Shule ya watoto watundu iko Mbulu kama sikosei. Unaweza kuuliza Wizarani upate uhakika zaidi
 
Shule ya watoto watundu iko Mbulu kama sikosei. Unaweza kuuliza Wizarani upate uhakika zaidi

Huko ndo anakwenda kuharibaka kabisa, akirudi huko maskani yake itakuwa kule soko la samaki (Ferry).
 
Hili ndio limekuwa tatizo kubwa kwa sasa lililoikumba Afrika na hasa kusini mwa Jngwa la Sahara i.e majibu mepesi kwa mambo magumu,...eti maombi...ddduuuuuuuh!!!!!!!!!!!!!!!...sijui nani katuroga.

Wewe lazima utakuwa mpinga Kristo! wengine maombi ndio kimbilio letu kwa issue zote hata zile zilizo katika uwezo wetu tunamtanguliza Mungu naye amekuwa anafanya! ameelaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu (ongeza na pesa) bali amebarikiwa mtu yule amtegemeyaye Mungu!
 
Naungana na Mwanunu. motto huyo apelekwe katika maombi hata mimi naweza kukuelekeza mahali sahihi maana hutapoteza kitu kama ukienda ni kama vile ulivyokuja humu jf na kuomba ushauri.
 
Huyo mtoto sio bure kuna ujumbe anatoa kwa wahusika lakini nyie hamjui??
Yawezekana kabisaa hiyo sio dam yenu??
Hapo kuna baba feki hapo kama wewe ni mzazi wa kiume kaa ukijua unalea dam ambayo sio yako.

Nina mengi sana ya kukueleza tena kwa ushahidi lakini kama huamini mambo ya mila mila itakuwa kazi bure.na ushahidi na mifano hai ya kutosha.

Ss mtoto kama huyo kunadawa anapewa na kama sio wa dam yenu anazurika nayo
 
Ikiwezekana fanya mpango sekondari umpeleke makuyuni ile shule ya jeshi manyara huko. Atabadilika atake asitake.
 
Tatizo la kubambikiziwa watoto hilo, muulizeni vizuri mama yake.
Hapa kuna ukweli sana,Katika Ulimwengu wa roho huwa kuna madai,Wanadamu wengi hawajajua nguvu iliyopo katika Damu, damu inafuatilia ndio maana unaweza kuwa na watoto wengi halafu unakuta mtoto mmoja ana tabia tofauti na wenzake japo umewalea wote katika missing ileile.
ltk mtoto huyu anamaudhi yaani basi maombi kisha fanyiwa saaaaana dawa saaaana
Mkuu Imani huwa hazichangamani , unaamua moja katika mbili aidha Kulia au Kushoto na sio Shoto- Kulia. Ukimpeleka kwa mganga basi baki kwa mganga, huwezi kumpelelka kwa mganga na kanisani.
Nina uzoefu wa kuhudumia watoto kupitia maombi, watoto wana Vita sana, inatakiwa kila mara kuwaombea watoto wetu. Nimehudumu kwenye mashule ya sekondari hapa Dar, Nilikuwa nakutana na matatizo sana ya vijana, lakini kupitia maombi walikuwa wanafunguliwa sana.


Shule ya watoto watundu iko Mbulu kama sikosei. Unaweza kuuliza Wizarani upate uhakika zaidi
Aisee usimpeleke huko ataaribika, atakukasirikia na kuona kuwa umemtenga. Kama unahamini katika maombi usichoke.
 
Kwa yeyote anaye weza toa msaada wa aina yoyote kwa mjukuu wangu ni mtukutu, shule hataki matukio ya udokozi, michezo mingi haishi kwake.

Anasumbua sana ashapigwa sana na kwa sasa ukimpiga anakwambia nichome moto ukimwambia njoo nikuchome anakuja na kujivisha tairi yani acheni tu.



Kwa anaye jua kituo ama dawa anisaidie.

Ushauri nasaba tu
Pia jaribu dini (maombi)
Ingawa miye naiamini njia ya ushauri
Na kuwa rafiki yake zaidi

Bazazi!
 
Renegade Asante kwa ufafanuzi mzuri. Wakati mwingine hizi mada za JF tunazijibu kwa utani kumbe mwenzetu ana tatizo kweli. Kwa kuongezea kwenye ufafanuzi huo, wakati mwingine tabia mbaya ya mtoto ni matokeo ya yale maneno yaliyotamkwa na baba au mama wakati wa mimba huska. Ilimtokea rafiki yangu, yeye na mke wake walikuwa wameamua watazaa watoto watatu tu, na waliamua kufuata kalenda. wakiwa ndani ya mkakati wao wa kufuata kalenda mwanamke kapata mimba. yule jamaa alimfokea sana mke wake kwa nini karuhusu ile hali. Mimba miezi tisa wiki 40, mtoto hatoki. Wiki 42, mama kafanyiwa maombi ndo mtoto kazaliwa.
Mtoto kakua lakn kila akishikwa na baba lazima aliye sana. Hadi miaka miwili hali hiyo hiyo. Miaka minne, baba hawezi hata mkumtuma kitu. Fimbo haikusaidia. Baba akaanza kuhisi mtoto si wake.
Kama bahati akahudhuria semina ya maisha ya kiroho, bahati nzuri akafundishwa somo la toba. Ile semina ikampa mwanga. Baada ya semina jamaa alienda moja kwa moja hadi nyumbani. Kafika kamnyanyua mtoto na kumbeba kifuani kwake. Mtoto anakawa anajitahidi kujinasua mikononi mwake ila jamaa kamung'ang'ania, huku akitamka maneno ya kuomba msamaha kama alivyoelekezwa kwenye semina. Ilikuwa jioni, wakalala ikawa asubuhi. Mtoto alikuwa wa kwanza kumuamsha na kumsalimia: 'Baba shikamoo'. Hicho ni kitu alikuwa hajawahi kupata kutoka kwa huyo mtoto. Tokea hapo, mtoto akabadilika baba yake ndo akawa kipenzi chake kuliko hata mama. Kwa hiyo basi huenda tatizo likawa kwenye meneno yaliyotamkwa juu ya ile mimba. Wazazi waulizwe vizuri circumstances za hiyo mimba.
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom