Mtoto wa Mke wangu: Sheria inasemaje?

Mtoto wa Mke wangu: Sheria inasemaje?

Hasira za kutopigiwa pasi unazihamishia kwa mtoto?
 
Poleni wana ndoa.kwa hilo naona na kuhisia kuna shida kubwa kwenye ndoa yako.nayo ni jeuri ww ni jeuri na mkeo pia.mtoto hana kosa.jiulize angekuwa wako na mkeo amnyanyase ungejisikiaje.
Kweli umelonga,sisi wote hakuna anayeshindwaga....si vizuri lakini!
 
Wanaume wengine wavivu kupiga tu pasi nayo ni kazii
Kama humpendi mtoto wangu hata mie kuna vitu sitovifanya kwa ukamilifu,inauma sana kuona mwanao kabaguliwaaa.inaonyeshaa kuna vitu ushamuonyeshea huyo mkeo kwa mtoto wakee
Jamani uchungu unaumaaa mnoo hata ukizaa bogaa utalipenda mpaka kufa kwako

Mama shughuli zangu niko bize mno, naamka saa 11 alfajiri, narudi nimechoka nimepigika, na ndio maana nikapata hasira kwa nini nipige pasi mwenywe ingawa we unaona sio kazi ngumu.
 
Mama shughuli zangu niko bize mno, naamka saa 11 alfajiri, narudi nimechoka nimepigika, na ndio maana nikapata hasira kwa nini nipige pasi mwenywe ingawa we unaona sio kazi ngumu.

Ee sawaa ila ungemalizana nae kiistaarabu tu we haujui usiku ulivyo mrefu akikubaniaa usije kulalamika hapaa
 
According to dini ya kiislamu: Mtoto wa mkeo ni mtoto wako, na anastahili malezi yote kutoka kwako including mirathi.
Mtoto wa mumeo (kama wewe ni mwanamke) SIO mtoto wako na hatambuliki kisheria.


duh.....changu chako....chako chako mwenyewe.....safi sana....
 
Mimi kwanza nikushauri kuhusu ndoa yako. Kwenye ndoa kama ilivyo kwenye uhusiano wowote "Revenge" ni kitu kibaya na matunda yake ni lazima uhusiano uvunjike. Atakataa kukupigia pasi, utakataa kumpa mtoto pocket money, atakununia na wewe utamnunia, kisha atakunyima unyumba na wewe utatoka nje...ukitoka na yeye anatoka. Sasa huko nje kuna atakayerudi na mimba na mwingine hiv...Kuna atakayekolea hatimaye divorce proceedings zikaanza na mtatengeneza watoto wa kambo watakaoenda kusababisha majanga kwenye ndoa nyingine. Now tell me, Where r we heading?

Never ever ever think of doing something bad to a person to counter for something bad done to u unless u want an enemy out of them.

Kingine, Kama wewe ni baba wa ukweli kabisa. Huyo mtoto ulitakiwa uwapatanishe hao wazazi wake na mtoto akalelewe full na baba-haijalishi utatumia mbinu gani kufanikisha hilo. Baba yake akimkataa wewe kama kichwa cha nyumba unatakiwa kumchukua under ur wing. Anakuwa mwanao jukumu lako kabisa kama hao wengine.

Kataa kuwa baba wa kushikiza, mkeo anajifanyia tu maamuzi yake na mtoto analipiwa na ndugu za mkeo. Mwishowe mtoto akuletee dharau uone kama utaweza kuwa baba hapo nyumbani! Tena unamtumia kumtisha mkeo? Thats too low man!

Kama hataelewa hapa basi tena. Naona amejionyesha kuwa too low with character. Mwanaume anatakiwa aact with integrity hata kama mke anakigeugeu. Yani nae anaingia kwenye malumbano ya kanga? really mtoto wa watu anahusikaje.

Mkuu kama unataka kuchukiwa basi onyesha dalili za masimango kwa huyo mtoto. Na duniani hapa tenda wema uende zako, sijui huyo mkeo anakuvumiliaje kutokumlipia ada na matunzo mwanae. So long as yupo kwako mtreat kama mtoto wako bila kujali atashukuru au La . Unakumbuka msemo "ukipenda boga---Penda na ua lake" . Nimeona familia nyingi tu baba anatunza watoto wa mke (and vice versa) hata kama baba zao wapo hai so long as hao watoto wanaishi nyumba moja na baba aliyemuoa mama yao. Hapa mkuu nimekudharau eti unampa malazi na chakula?? hata shemeji zako watakuwa wanakushangaa .
 
Napenda wenye ufahamu wanisaidie kuhusu hili.
Nina mke wangu wa ndoa ambaye kabla sijamuoa nilimkuta na mtoto wa kiume wa miaka mitatu, mtoto huyo sasa hivi mkubwa na ameingia form one sekondari.
Mtoto huyu ana baba yake ambaye ni mtu mwenye uwezo mkubwa tu, lakini kutokana na jeuri ya mama yake (mke wangu) hataki kumshirikisha mtoto upande wa babake kwa jambo lolote, yaani hataki hata mtoto ajue kuna babake. Ada ya shule silipi mimi ila mjomba wa mtoto yaani kaka wa mke wangu.
Chakula, mavazi, uniform, nauli ya kwenda shule ya boarding na matumizi ya shule vyote natoa mimi.
Katika kukorofishana baada ya yeye kukataa kunipigia pasi nguo zangu kwa madai kupiga pasi ni option tu hufanyika akipenda yeye sio lazima na mimi nikamjibu ku supply education materials kwa mwanao ni option tu sio lazima kwani mtoto huyo ana baba yake aliye hai , labda asingekuwa naye (amekufa) ndo ingekuwa lazima!
Niliongeza kuwa wajibu wangu kwa mtoto wake huyo ni kumpa chakula ale na kumpa malazi alale tu na sio vitu vingine.
Swali langu sheria inasemaje kuhusu wajibu wetu kwetu sisi akina baba wenye watoto wa aina hii?

Mkuu hapo kwenye sheria mimi sina la kuchangia lakini kitendo cha wewe baba mzima wa nyumba kukosa subira na kuyamtaka uliyotamka ni udhaifu wa hali ya juu. Usingethubutu kuhamishia hasira zako kwa mtoto wa watu. Na kama alivyosema huyo mwanamke hajakosea kwani wewe hujaoa kibarua kukupikia na mengine wayafanyayo wanawake ni huruma yao kwa waume zao. Jicontrol ndoa ni mtihani. Wewe ni muislamu mkuu nitoe somo linahusiana na imani yetu ili usihangaike kwenye hizi za kina TAMWA NA TAULA?
 
Mwambiee banaa mkeo sio housegirl maana kazi yake ni kukupa raha na kuzaa tu!!

Upande wangu sipo tayari mtu yeyote aguse nguo ya aina yoyote ya mme wangu,wala kumpikiaa hata kama sijui tutarekebishanaa labda bint wa kazi aoshe vyombo na kufua nguo za watoto
Kama hakuna binti au uwezo haupo mke lazima ujishughulishee
 
Yaan unagombana na mkeo unataka kusitisha huduma kwa mtt asiye na hatia.inavyoonyesha ww umechoka kukaa na huyo mtt ulikua unatafuta sababu tu,kama ndivyo ww mweleze tu ampeleke kwa huyo mjomba anaemlipia ada ya shule.ww ubaki unalea wakwako tu,
 
hahahahahaaaa, dah, mkuu ndiyo maana wewe ni HUNIJUI!!!
yan ningekuwa mimi nisingeongea chochote ningekuwa naondoka asbuhi cjanyoosha naingia kwenye gari naondoka na jion narud zmenyooka vzuri. Siku nikiona vp narud nimebadilisha nguo kabisa. Angepata adabu

Umekosea kumhusisha mtoto. Epuka kujibizana na mwanamke ndani ya ndoa. ukiona umemwambia hajakuelewa fanya kwa vitendo kimyakimya.
 
Last edited by a moderator:
Mwanaume kama wewe siwezi kuishi na wewe unavisasi umelelewa vibaya kujibiwa vibaya kuhusu pasi ndo umsimange kuhusu mtoto inaonekana kilikuuma toka zamani hapo ndo ukapata pa kulitolea dukuduku lako kama unamsaidia msaidie mtoto ni malaika
 
pole sana aisee.omba siku zote za maisha yako Mungu akupatie mke / mke wa kuelewana nae.

Mie nimepita huko napaelewa sana ila namshukuru Mungu kwa kila jema.
 
Napenda wenye ufahamu wanisaidie kuhusu hili.
Nina mke wangu wa ndoa ambaye kabla sijamuoa nilimkuta na mtoto wa kiume wa miaka mitatu, mtoto huyo sasa hivi mkubwa na ameingia form one sekondari.
Mtoto huyu ana baba yake ambaye ni mtu mwenye uwezo mkubwa tu, lakini kutokana na jeuri ya mama yake (mke wangu) hataki kumshirikisha mtoto upande wa babake kwa jambo lolote, yaani hataki hata mtoto ajue kuna babake. Ada ya shule silipi mimi ila mjomba wa mtoto yaani kaka wa mke wangu.
Chakula, mavazi, uniform, nauli ya kwenda shule ya boarding na matumizi ya shule vyote natoa mimi.
Katika kukorofishana baada ya yeye kukataa kunipigia pasi nguo zangu kwa madai kupiga pasi ni option tu hufanyika akipenda yeye sio lazima na mimi nikamjibu ku supply education materials kwa mwanao ni option tu sio lazima kwani mtoto huyo ana baba yake aliye hai , labda asingekuwa naye (amekufa) ndo ingekuwa lazima!
Niliongeza kuwa wajibu wangu kwa mtoto wake huyo ni kumpa chakula ale na kumpa malazi alale tu na sio vitu vingine.
Swali langu sheria inasemaje kuhusu wajibu wetu kwetu sisi akina baba wenye watoto wa aina hii?
\
1. Hivi wewe ni baba kweli?
2. unajua ya kesho ?
Wakati unamuoa huyo mwanamke ulifahamu fika kuwa kuna mtoto [most likely hawakuoana] na ulikubali kumuoa na kumtunza mke pamoja na mtoto huyo na watoto wengine wajao.
Huyo ni mwanao [regardless baba yake anauwezo au la] na unawajibika kumhudumia kama unavyofanya kwa watoto wengine.
 
Mama shughuli zangu niko bize mno, naamka saa 11 alfajiri, narudi nimechoka nimepigika, na ndio maana nikapata hasira kwa nini nipige pasi mwenywe ingawa we unaona sio kazi ngumu.

Mmh baba, kwani yeye si mwajiriwa? Vitu vingine ni kusaidiana ujue...na hakukuwa na ulazima kiviiilee kumuingiza mtoto kwenye huo msuguano...
 
Back
Top Bottom