Mtoto wa Mke wangu: Sheria inasemaje?

Mtoto wa Mke wangu: Sheria inasemaje?

Napenda wenye ufahamu wanisaidie kuhusu hili.
Nina mke wangu wa ndoa ambaye kabla sijamuoa nilimkuta na mtoto wa kiume wa miaka mitatu, mtoto huyo sasa hivi mkubwa na ameingia form one sekondari.
Mtoto huyu ana baba yake ambaye ni mtu mwenye uwezo mkubwa tu, lakini kutokana na jeuri ya mama yake (mke wangu) hataki kumshirikisha mtoto upande wa babake kwa jambo lolote, yaani hataki hata mtoto ajue kuna babake. Ada ya shule silipi mimi ila mjomba wa mtoto yaani kaka wa mke wangu.
Chakula, mavazi, uniform, nauli ya kwenda shule ya boarding na matumizi ya shule vyote natoa mimi.
Katika kukorofishana baada ya yeye kukataa kunipigia pasi nguo zangu kwa madai kupiga pasi ni option tu hufanyika akipenda yeye sio lazima na mimi nikamjibu ku supply education materials kwa mwanao ni option tu sio lazima kwani mtoto huyo ana baba yake aliye hai , labda asingekuwa naye (amekufa) ndo ingekuwa lazima!
Niliongeza kuwa wajibu wangu kwa mtoto wake huyo ni kumpa chakula ale na kumpa malazi alale tu na sio vitu vingine.
Swali langu sheria inasemaje kuhusu wajibu wetu kwetu sisi akina baba wenye watoto wa aina hii?

Kwani hapo mwanzo wakati mnaoana mlikubalianaje kuhusiana na huyu mtoto? Naanza kupata picha kuwa umeshaanza kumchukia mtoto kwa makosa ya mama yake. Swala la kupiga pasi nguo haliwezi kuwafikisha hadi kwenye maswala ya msingi ya mtoto, hadi ije ipelekee hatimaye mtoto mumuathiri kisaikolojia halafu aharibike aache kufanya maswala ya msingi na hatimaye aanze kuvuta bangi. Achilia mbali mtoto wa mke wako, hata kama angekuwa mtoto mwingine tu ambaye hata huwajui ndugu zake ila umeamua kukaa naye, kumsaidia na kumsomesha, haiingii akilini ukija kumtelekeza katika latter stage kama hii. Halafu kitu cha msingi unapokuwa unatoa msaada kwa mtu, katika hali ya kawaida na ubinadamu, huwa tunachukulia kuwa huko mbele atakuja kukupa tafu kwa aina moja ama nyingine, ila sasa ninachoshauri hapa ni kuwa ni vizuri ukachukulia kuwa unatoa msaada ambao hautakuja kukurudia kwa namna yeyote ile huko mbele, ili kusudi ikitokea huyo uliyemsaidia akakukumbuka, basi uchukulie kama "previledge" kwako. Ukimsaidia ukiwa na malengo ya wewe kuja kusaidiwa pia, utajenga akilini kuwa una "rights" fulani kwake (wakati siyo) ambazo siku ukija kuzikosa, unafrustrate na unaweza kumfrustrate yeye pia. Sasa hivi naona kama unataka kuwa discouraged kumsaidia mtoto kwa sababu unaona mama yake anakuwa na kiburi na unaanza kujiuliza maswali, huyu mtoto atakuja kunijali kweli huko mbele? Una "assumed rights debts" kwake ambazo unadhani lazima aje azilipe na asipofanya hivyo hutaelewa.

Halafu huyu mwanamke naye amepata wapi maneno ya kijinga ya kuwa anamjibu mme wake namna hiyo? Fanya uchunguzi ila tahadhari kubwa, usi-link matatizo ya mama na attitude yako ya kumsaidia mtoto, yaani anatakiwa mama asibadilishe kabisa attitude yako kwa mtoto.
 
According to dini ya kiislamu: Mtoto wa mkeo ni mtoto wako, na anastahili malezi yote kutoka kwako including mirathi.
Mtoto wa mumeo (kama wewe ni mwanamke) SIO mtoto wako na hatambuliki kisheria.

Kuna vitabu haviwezi kupass hata kwenye simple logic of perspective. Ni heri hata utumie encyclopedia.
 
Suala la kupasi nguo ni wajibu wake ungelimaliza pasipo kuchanganya mambo ya mtoto hukupaswa kujibu hivyo kabla ya kumuowa ulijua nakulipokea na ni wajibu ni mtoto pia sio sahihi kumuingiza kwenye magomvi yenu yanamhusu pia huwezi kujua mbeleni akakuthamini kushinda watoto wako wakuzaa endeleza wema wako mungu atakusaidia
 
Inaonyeshaa humpendi yule mtoto ndio maana jibu lako lilikua moja kwa moja kwa mtoto .ukimuoa mwanamke ana mtoto somesha huyo mtoto,kama hukutaka hivyo ungeoaa ambae hana mtotoo
 
Wanaume wengine wavivu kupiga tu pasi nayo ni kazii
Kama humpendi mtoto wangu hata mie kuna vitu sitovifanya kwa ukamilifu,inauma sana kuona mwanao kabaguliwaaa.inaonyeshaa kuna vitu ushamuonyeshea huyo mkeo kwa mtoto wakee
Jamani uchungu unaumaaa mnoo hata ukizaa bogaa utalipenda mpaka kufa kwako
 
Inaonyeshaa humpendi yule mtoto ndio maana jibu lako lilikua moja kwa moja kwa mtoto .ukimuoa mwanamke ana mtoto somesha huyo mtoto,kama hukutaka hivyo ungeoaa ambae hana mtotoo

Jwa nini usomeshe mtoto wa mtu na Baba yake yupo hai na uwezo wa cover expenses za mtoto wake anazo?

Jeuri ya mwanamke kwa mzazi mwenzake isiyo burden kwa mtu mwingine, msiangalie hivi vitu kiushabiki.
 
Inaonyeshaa humpendi yule mtoto ndio maana jibu lako lilikua moja kwa moja kwa mtoto .ukimuoa mwanamke ana mtoto somesha huyo mtoto,kama hukutaka hivyo ungeoaa ambae hana mtotoo

Umefikiaje hitimisho la hovyo nmna hii??
 
Wanaume wengine wavivu kupiga tu pasi nayo ni kazii
Kama humpendi mtoto wangu hata mie kuna vitu sitovifanya kwa ukamilifu,inauma sana kuona mwanao kabaguliwaaa.inaonyeshaa kuna vitu ushamuonyeshea huyo mkeo kwa mtoto wakee
Jamani uchungu unaumaaa mnoo hata ukizaa bogaa utalipenda mpaka kufa kwako

Hakuna kosa kubwa kama kuwaza na kufikia hitimisho tu kwa kuamini namna ulivyokuwa unafikiria ni sahihi

Mwanamke yoyote anajua majukumu yake kwa mume
Ni hatari sana kwa mwanamke kutokujua hili

Kwanza kama ungekuwa na tafakuri ndogo tu ungeona kuwa huyo mke ni wa hovyo sana,kwa kule tu kutokutaka mwanae ajue kama ana baba ni ishara tosha ya kuonesha namna alivyo wa hovyo

Kumgharamia mwanao ni jukumu lako na sio la mwingine,huyo mwanamke anatakiwa ajue kuwa huyo mtoto ni lazima agharamiwe na baba yake labda angekuwa hayupo [Kafariki]

Lakini huyo jamaa kumhudumia ni hisani tu ...!!!!!!!
 
Umeonyesha fadhila kwa kulea tangu 3 yrs mpaka seko, sasa kujibishana na mama mambo yenu wawili huyo mtoto anahusikaje? Wewe umegombana na mkeo baada ya kukataa kupasi nguo zako, swala la mtoto halipo hapo. Ingekuwa mmeachana labda ndio ningeona pointi ya kuhusu mstakabali wa mtoto.
 
Napenda wenye ufahamu wanisaidie kuhusu hili.
Nina mke wangu wa ndoa ambaye kabla sijamuoa nilimkuta na mtoto wa kiume wa miaka mitatu, mtoto huyo sasa hivi mkubwa na ameingia form one sekondari.
Mtoto huyu ana baba yake ambaye ni mtu mwenye uwezo mkubwa tu, lakini kutokana na jeuri ya mama yake (mke wangu) hataki kumshirikisha mtoto upande wa babake kwa jambo lolote, yaani hataki hata mtoto ajue kuna babake. Ada ya shule silipi mimi ila mjomba wa mtoto yaani kaka wa mke wangu.
Chakula, mavazi, uniform, nauli ya kwenda shule ya boarding na matumizi ya shule vyote natoa mimi.
Katika kukorofishana baada ya yeye kukataa kunipigia pasi nguo zangu kwa madai kupiga pasi ni option tu hufanyika akipenda yeye sio lazima na mimi nikamjibu ku supply education materials kwa mwanao ni option tu sio lazima kwani mtoto huyo ana baba yake aliye hai , labda asingekuwa naye (amekufa) ndo ingekuwa lazima!
Niliongeza kuwa wajibu wangu kwa mtoto wake huyo ni kumpa chakula ale na kumpa malazi alale tu na sio vitu vingine.
Swali langu sheria inasemaje kuhusu wajibu wetu kwetu sisi akina baba wenye watoto wa aina hii?

Mtoto unampa huduma kila kitu kama mwanao halafu hataki kufanya wajibu ambao ni wajibu wa mtoto kwa wazazi wake bado mwanamke haoni kosa kwa huyo mwanae? Huyo mwanamke na mwanae hawana shukrani ndio maana hawa wanawake wenye watoto ni kuangalia sana kwasababu wao huwa hawajui kuangalia kosa wapi wanapenda kuwa upande wa wanao maana wako na ile kuwa mwanae anaonewa badala ya kuangalia kosa liko wapi kwanza.
 
Inaonyeshaa humpendi yule mtoto ndio maana jibu lako lilikua moja kwa moja kwa mtoto .ukimuoa mwanamke ana mtoto somesha huyo mtoto,kama hukutaka hivyo ungeoaa ambae hana mtotoo

kazi ipo napita tu hapa, Dinazarde unaonekana una mtoto nini? maana unajibu kwa jazba
 
we bana hebu sovu issue zako na mkeo!
kama hukuwa tayari kulea huyo mtoto toka mwanzo ungesema abaki kwa mjomba wake we uchukue mke!


ulishindwa kuweka misingi y kunyooshewa nguo toka mnaoana leo uje kulalamika ?
kwa mfano mkeo akiwa anakunyooshea
-itaondoa ukweli kuwa baba wa huyo mtoto ana uwezo?
-itaondoa ukweli kuwa mkeo hataki kumtambulisha mtoto kwa babake?
-itaondoa ukweli kuwa mkeo ana kiburi(kwa tafsiri yako kutotaka mawasiliano na baba wa mtoto ni kburi?eheheh sijui kama unajua unachokiwish)


hebu fanya homework yako!

dah umeongea kwa hisia!!
 
Jwa nini usomeshe mtoto wa mtu na Baba yake yupo hai na uwezo wa cover expenses za mtoto wake anazo?

Jeuri ya mwanamke kwa mzazi mwenzake isiyo burden kwa mtu mwingine, msiangalie hivi vitu kiushabiki.

Boraa uoe mwanamke ambae hajazaaa
 
Umefikiaje hitimisho la hovyo nmna hii??

Sawa ni wajibu tu wa mwanamke kumfanyiaa mmewee kama kumnyoosheaa pasi,
Lakin kwanin ugomvi wa kunyooshewaa nguo tu mpaka amjibu vile inaonyesha anaishi na yule mtoto kwa kinyongoooo
 
Jwa nini usomeshe mtoto wa mtu na Baba yake yupo hai na uwezo wa cover expenses za mtoto wake anazo?

Jeuri ya mwanamke kwa mzazi mwenzake isiyo burden kwa mtu mwingine, msiangalie hivi vitu kiushabiki.

Na ni kwanini aoe mwanamke ambae ana mtoto,hakuwaona ambao hawana watoto
Mbona wengine wanaoaa mwanamke ambae ana watoto kuanzia wawili na anawasomesha pia kuwalea kama watoto wakee
Ukiona huwezi kua na moyo mpana na roho iliyojaa uchoyo na roho mbayaa dawa ni kuoaa mwanamke ambae hamna mtoto una waachia wanaowezaa
 
Sawa ni wajibu tu wa mwanamke kumfanyiaa mmewee kama kumnyoosheaa pasi,
Lakin kwanin ugomvi wa kunyooshewaa nguo tu mpaka amjibu vile inaonyesha anaishi na yule mtoto kwa kinyongoooo

Unaendelea na mahitimisho yasiyofaa

Kwanini tu usifikirie kuwa huyo jamaa alifikia hivyo baada ya kuchishwa na karaha za mkewe kwa sababu ameshasema kuwa ana tabia ya ukorofi?
 
Baba paroko Eiyer toaa ushauri bana maana mleta mada kaletaa mada nusu mengine kafichaaa
Tena mtoto anasomeshwa na mjomba wake kapunguziwaa mzigoo bado tu kumlisha na kumvishaa anaumiaa lollll
 
Jwa nini usomeshe mtoto wa mtu na Baba yake yupo hai na uwezo wa cover expenses za mtoto wake anazo?

Jeuri ya mwanamke kwa mzazi mwenzake isiyo burden kwa mtu mwingine, msiangalie hivi vitu kiushabiki.

Hii ndio point ya mśingi. Mianamke kama hii ni ya kuitimulia mbali na mitoto yao.
 
Back
Top Bottom