Mtoto MCHANGA AOKOTWA LEO -Kimara/Baruti

Mtoto MCHANGA AOKOTWA LEO -Kimara/Baruti

MaxShimba

Platinum Member
Joined
Apr 11, 2008
Posts
36,008
Reaction score
4,093
[h=3]MTOTO MCHANGA ALIYEOKOTWA ASUBUHI YA LEO[/h]


Wasamaria wema wakikifuta uchafu kichanga kilichokutwa kimetupwa maeneo ya Kimara Baruti Bondeni karibu na maeneo ya Ubungo Kibangu.Yawezekana mtoto huyo alitupwa asubuhi kwasababu amekutwa akiwa hai na bado akiwa na damu.Baada ya polisi kufika eneo la tukio Wasamaria wema walimuwahisha mtoto huyo hospitali ya Palestina Sinza.

Kichanga hicho baada ya kufutwa futwa na kufunikwa.Mmoja wa wasamaria wema amenambia kuwa kichanga hicho cha kiume anaendelea vizuri baada ya kupatiwa huduma katika hospitali ya Palestina na amepelekwa hospitali ya Mwanyamala ambapo ndo kuna kitengo cha kuhifadhi watoto wachanga.


Inasikitisha sana jamani vyombo vya sheria vitoe adhabu kali kwa wanaofanya vitendo hivi ili kukomesha tabia hii.
 
Nimefurahi huyo mtoto kuwa mzima.Kuna sehemu nilisoma kwamba wanaotoa mimba au kutupa watoto,huwa baadae wanawakumbuka na kujuta.
 
Tunamshukuru Mungu huyu mtoto kupatikana akiwa hai na salama.
 
[h=3]MTOTO MCHANGA ALIYEOKOTWA ASUBUHI YA LEO[/h]


Wasamaria wema wakikifuta uchafu kichanga kilichokutwa kimetupwa maeneo ya Kimara Baruti Bondeni karibu na maeneo ya Ubungo Kibangu.Yawezekana mtoto huyo alitupwa asubuhi kwasababu amekutwa akiwa hai na bado akiwa na damu.Baada ya polisi kufika eneo la tukio Wasamaria wema walimuwahisha mtoto huyo hospitali ya Palestina Sinza.

Kichanga hicho baada ya kufutwa futwa na kufunikwa.Mmoja wa wasamaria wema amenambia kuwa kichanga hicho cha kiume anaendelea vizuri baada ya kupatiwa huduma katika hospitali ya Palestina na amepelekwa hospitali ya Mwanyamala ambapo ndo kuna kitengo cha kuhifadhi watoto wachanga.


Inasikitisha sana jamani vyombo vya sheria vitoe adhabu kali kwa wanaofanya vitendo hivi ili kukomesha tabia hii.
Ainasikitisha sana kwa kitendo wanachofanya mama/dada zetu.ila tusiangalie upande mmoja tuu tuangalie na upande wa pili yani jamii iliyo mzunguka na maingira aliyokuwa nayo mama kabla.tusiishie katika matunda ya dhambi tuu
 
Mungu ni mwema hakika amemnusuru
Nina hakika aliyemtupa atajutia tendo lake.
Yuko hai ni wazi atakuwa vema
Watu wanatafuta watoto usiku & mchana.
 
hizo picha ni vyema zikawekwa kwenye kumbukumbu kwa sababu nacho amini Mungu atatenda miuujiza kwa mtoto huyo na atakuja kuwa maarufu hapa duniani na hizo picha aje kuzishuhudia....jinsi alivyo okotwa kwenye mazingira ya ajabu hakika Mungu ni mwema siku zote
 
Mungu aliye Mkuu atamfanya mtoto huyu kuwa maarufu duniani na ipo siku mama yake kwa kuwa hakutegemea kuwa atakutwa hai atajitokeza na kumdai mwanaye, na mama huyu hiyo ndiyo itakuwa laana kwake hatapata mtoto mwingine tumboni mwake.
 
jamani hivi kwanini lakini, wengine wanatafuta hata radha ya mtoto kukaa tumboni hawaipati, wengine wanatupa, inasikitisha sana, Mungu ashukuliwe kwa kumeweka hai mtoto.
 
Alaaniwe mama aliye fanya unyama huo... Na pia naenda mbali zaidi mpaka kwa mzazi mwenza kama alichangia naye alaaniwe pia...... Namuombea mtoto huyo aendelee kuwa poa
 
Hizi ni mimba zisizo tarajiwa, wanaume mkiwapa mimba mabinti msiwakimbie, wasaidieni na kulea hivi viumbe!
 
Hivi we mama uliyetupa huyo mtoto roho haikuumi? Siku akiwa maarufu ndio unajitokeza eti mi ndio mama yako?? kudadeki nakutoa nduki. Mwenyezi Mungu ni mwingi wa rehema naamini atamkuza tu.
 
Hizi ni mimba zisizo tarajiwa, wanaume mkiwapa mimba mabinti msiwakimbie, wasaidieni na kulea hivi viumbe!

Wanaume tu sehemu ya tatizo. Ila inawezekana huyu mama hajui hata baba wa mtoto, fikiria usiku kapata dozi toka kwa mtu 3.
 
Inasikitisha sana, kuna watu ninawajua wana miaka zaidi ya ishirini katika ndoa na hawajaawahi hata kupata mimba, wanasali kila siku ili wapate mtoto, wengine wanawatupa jalalani.
 
Wanaume tu sehemu ya tatizo. Ila inawezekana huyu mama hajui hata baba wa mtoto, fikiria usiku kapata dozi toka kwa mtu 3.

Muache kukojoa kojoa hovyo kama hamuwezi kufuatilia hayo mashimo manamomwaga, matokeo yake ndio haya!
 
kama amepelekwa mwnanyamala sidhani kama atasalimika huyu .Mungu wangu hapo wameshamuuza huyo hao mabeduli wa hapo,watamla nyama hiyo ni hospitali ya ibilisi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom