Wewe unaona kiongozi wa juu kabisa wa chama kudanganya baba ni issue ndogo hiyo? Mwacheni ajibu mwenyewe kama alivyojibu kuwa anamili kadi ya CCM. Mbona mke alipoguswa aliibuka na kusema yeye ni wa ukweli na kuwadhalilisha akina ROSE KAMILI na CECILIA PARRESSO.
Yeye kudanganya baba ama mzazi (kama mnavyotaka tuamini), ndo kumeifanya nchi hii kuwa masikini wa kutupwa kiasi hiki? Ndo kumesababisha migogoro ya kidini iliyozuka hivi sasa? Ndo kumesababisha matokeo ya kidato cha nne kuwa mabaya kupindukia? Ndo kunasababisha kutamalaki kwa wizi na ufisadi nchini? Ndo kunaifanya seroikali ya nchi hii kuwa dhaifu kiasi ya kwamba inashindwa hata kutatua matatizo yetu? Ama ndo kumelifanya bunge letu kuwa kichaka cha wahuni wanaotetea maslahi ya matumbo yao na chama chao, na kuwasahau wananchi waliowachagua?
Ndo kumemfanya mwenyekiti wako na chama chako kwa ujumla kuwatelekeza watanzania, kuamua kuhubiri migawanyiko na chuki za kidini, kimakabila na kikanda? Ndo kumewafanya mshindwe kabisa kutekeleza hata robo ya ilani yenu ya uchaguzi mpaka sasa?
Hebu jaribuni kujikita kwenye mambo ya msingi na yenye tija kwa taifa hili.
Hii nguvu mnayoitumia na kupotea bure mngetumia kutafuta majawabu ya matatizo yanayotukabili kama taifa, naamini tungekuwa na uchumi imara na maisha bora kama MAREKANI!
Dr Slaa sio mgeni wa siasa za taifa hili, hajaibuka jana yupo tangu miaka ya 90....Huko kote mlikuwa wapi sio unafiki na UMA.L.A.YA wa kisiasa huu?
Hebu tuache kujitoa nguo hadharani ndugu zangu.....Kwa hali hii tunawakosea wazazi wetu waliotulea kwa staha, heshima na uadilifu, tunawakosea hata walimu wetu waliotufudisha,tunaudhihirishia umma wa watanzania kuwa tulihudhulia shule na vyuo lakini HATUJAELIMIKA.
Tunadhalilisha hata vijana wenzetu ili mwaisho wasiku jamii ituone kuwa tu wapuuzi, hatufai kukabidhiwa dhamana za kuongoza!