Mtei amefilisika kimawazo - Zitto

Mtei amefilisika kimawazo - Zitto

Well sasa unataka mjadala uwe wa dini maana naona tunapelekana ambako sintopenda zaidi kuingia. Kwanza kabisa nimeshasema kwamba swala la mahakama ya kadhi lipo kikatiba na kisheria maana tunafuata mfumo wa kisheria wa cultural law na ndio unaotambulika hata ktk ndoa za waislaam, mirathi na kadhalika kisheria. Sio kwamba hakuna kitu hiki kipo isipokuwa walicholalamika waislaam ni kwamba sheria hazifuatwi inavyopaswa kwa sababu baadhi ya hukumu zimefuata secular wakati ndoa ilikuwa ya kiislaam.

Zipo kesi za madai hata za wakristu ktk ndoa ama talaka ambazo zimeamuliwa ki secular wakati waliofunga ndoa ni wakatoliki ambao dini inawakataza kuachana isipokuwa kwa zinaa (kama sijakosea)..waumini wanaweza kulalamikia sheria na maamuzi ya korti zetu na ikaswihi, Hivyo hata Kanisa linaweza kabisa kuiomba serikali inapofikia maswala la kuvunja ndoa za waumini wake, mirathi au yaliyopo ktk cultural law wapelekwe mahakimu wanaoijua sheria ya dini yao. wakristu hawakatazwi kufanya hivyo ila maadam siku hizi tunapuyanga tu mambo mengi ya dini yamepuuzwa. Hakuna kosa kisheria na hakuna mahala waislaam wanakiuka katiba ila ndivyo ilivyotakiwa kuwa. Binafsi napingana na mahakama ya kadhi kwa sababu waislaam wenyewe wanafanya mengi kinyume cha imani ya dini leo utaka kuwahukumu baada yaa.

Mkuu wangu memorundum of Association ni kinyume cha sheria, na ndio maana ikaitwa makubaliano ya muafaka ambayo kisheria yanakosa nafasi. Hakuna mkataba baina ya serikali na serikali na ndio maana ikaitwa Muafaka kama ulivyofanywa wa CUF na CCM. Nionyehse mahala poppote ktk katiba kunaporuhusu vyama viwili kuandaa mbele ya uchaguzi jinsi ya kuongoza Zanzibar. Nionyeshe hata kipengele kimoja cha katiba yetu kinachoruhusu hivyo?. BTW nenda katazame tafsiri ya Muafaka (Memorundum of Association) halafu rudi tujadili hapa.

Unarudi kulekule. Hakuna mtu anayesema kuwa waislamu hawana haki ya kujiamulia mambo yao yenyewe. Tunachopinga ni kudai kuwa Mahakama hiyo iingizwe katika mfumo wa serikali. Ingawa wakatoliki hawatambui talaka lakini wahusika wanaweza kwenda serikalini na ndoa yao ikafanywa batili. Msimamo wa kidini hauingilii utendaji wa serikali. Ndivyo ilivyo. Na ndivyo inavyotakiwa kuwa. Hukumu kila siku inatakiwa kuwa secular katika nchi isiyo na dini bila kujali imani ya wahusika.

Wakatoliki wanakataa talaka, period. Umeoa au umeolewa basi utakuwa hivyo hadi kifo kitakapowakuta. Hawaangallii zinaa, ukatili au kitu kingine. Itakapofika Kanisa kuomba wao watoe hukumu katika masuala yanayowahusu wale waliobatizwa nao, nao tutawapinga. Katika nchi ambamo tumeoaniana, wengi kuwa wenye dini jina, na wengine wenye imani tofauti, hiyo tutaona ndio mwanzo wa kuigeuza nchi hii kuwa theocracy. Tutawapinga kama tunavyopinga Mahakama ya Kadhi ndani ya serikali.

Mkuu, mbona unachanganya Memorandum of Understanding (MoU) iliyopo baina ya mashirika ya kikristu na serikali na Memorandum of Association ambayo inaelekea iko kati ya CUF na CCM. Ni vitu viwili tofauti. MoU si mkataba bali ni makubaliano yasio na uzito wa kisheria. Hauwezi kumpeleka mtu Mahakamani kwa kutotekeleza yaliyopo kwenye MoU. MoA ni makubaliano ya ushirikiano ambayo ni ya kisheria. Ni mkataba wakati MoU si mkataba. Lakini hata hivyo sioni tatizo kwa vyama viwili kukubaliana kabla ya uchaguzi jinsi watakavyoshirikiana kama watashinda. Kama wananchi wanaona hivyo sivyo basi kwenye uchaguzi ujao watawaadhibu. Mbona Liberal Democrats wanashirikiana na wahasibu wao Conservatives huko Uingereza? na unaona jinsi wapiga kura wanavyowaadhibu?

Badala ya kulalamikia MoU ambayo inaipunguzia serikali mzigo wa kutoa huduma za kijamii basi na nyie mngeingia kwenye MoU yenu ili sote tufaidike. Kama vile mnavyowapeleka watoto wenu St. Joseph University nasi tunawapeleka watoto wetu Feza.

Amandla.....
 
Wote tunajua kuwa huko visiwani kuna Mahakama ya Kadhi na hawana tatizo nayo. Hawa si watahitaji mmoja tu kutoka Bara kulazimisha hoja hii? Na hivyo hivyo kwa masuala mengine mengi yenye kuwagusa waislamu.

Fundi Mchundo,
Kwa hiyo una tatizo na hoja yenyewe au tatizo ni hoja/dai hiyo kuwasilishwa na waislam?

Mtei ni muasisi wa Chama na hana cheo katika chama, kwa hali hiyo hawezi kuwa msemaji wa Chama. Zitto ana nafasi katika Chama kwa hiyo analosema lina uzito kichama kuliko alilosema Mtei. Sasa mbona yeye kusema hauoni kama kunatosha hadi viongozi wengine waseme?

....Nae kama angeonekana kwenda kinyume na msimamo wa chama, bila shaka mmoja wa viongozi wenzake wangemsema. Kama alivyofanya yeye kwa Mtei. Ndio demokrasi.

Mkuu,nadhani kuna kitu muhimu unakikosa au hukijui kuhusu Chadema. Mtei hana cheo katika chama?Na unaamini hivyo katika mtazamo gani? Kutokuwepo kwenye formal structure ya kichama haitoshi kumfanya asiwe superior kwenye maamuzi ya chama mkuu.Labda nikukumbushe kitu kimoja,baada ya Nyerere kung'atuka madarakani,alibaki kuwa mwanachama wa CCM bila cheo,lakini ushawishi na nafasi yake katika chama ilikuwa hata ni zaidi ya Mwenyekiti wa chama. Na ndivyo hivyo kwa Mtei.
Au kwa tafsiri yako,akisema jambo Zitto na kisha Mtei akakosoa ndio unakuwa msimamo wa chama,lakini akisema Mtei na kisha Zitto akakosea,hapo anakuwa amekiuka maadili ya chama na ynakuwa ni mtazamo binafsi? Double standards katika chama!!
Labda jikumbushe,Zitto alipotoa msimamo wake kuhusu suala la umri na urais,na mtazamo wake kuhusu kugombea iwapo atapendekezwa na chama chake,Mtei alitoa kauli gani? Kama kweli unaamini analosema Zitto lina uzito katika chama zaidi ya Mtei? Chadema ni double standards mkuu!
 
Unarudi kulekule. Hakuna mtu anayesema kuwa waislamu hawana haki ya kujiamulia mambo yao yenyewe. Tunachopinga ni kudai kuwa Mahakama hiyo iingizwe katika mfumo wa serikali. Ingawa wakatoliki hawatambui talaka lakini wahusika wanaweza kwenda serikalini na ndoa yao ikafanywa batili. Msimamo wa kidini hauingilii utendaji wa serikali. Ndivyo ilivyo. Na ndivyo inavyotakiwa kuwa. Hukumu kila siku inatakiwa kuwa secular katika nchi isiyo na dini bila kujali imani ya wahusika.

Wakatoliki wanakataa talaka, period. Umeoa au umeolewa basi utakuwa hivyo hadi kifo kitakapowakuta. Hawaangallii zinaa, ukatili au kitu kingine. Itakapofika Kanisa kuomba wao watoe hukumu katika masuala yanayowahusu wale waliobatizwa nao, nao tutawapinga. Katika nchi ambamo tumeoaniana, wengi kuwa wenye dini jina, na wengine wenye imani tofauti, hiyo tutaona ndio mwanzo wa kuigeuza nchi hii kuwa theocracy. Tutawapinga kama tunavyopinga Mahakama ya Kadhi ndani ya serikali.

Mkuu, mbona unachanganya Memorandum of Understanding (MoU) iliyopo baina ya mashirika ya kikristu na serikali na Memorandum of Association ambayo inaelekea iko kati ya CUF na CCM. Ni vitu viwili tofauti. MoU si mkataba bali ni makubaliano yasio na uzito wa kisheria. Hauwezi kumpeleka mtu Mahakamani kwa kutotekeleza yaliyopo kwenye MoU. MoA ni makubaliano ya ushirikiano ambayo ni ya kisheria. Ni mkataba wakati MoU si mkataba. Lakini hata hivyo sioni tatizo kwa vyama viwili kukubaliana kabla ya uchaguzi jinsi watakavyoshirikiana kama watashinda. Kama wananchi wanaona hivyo sivyo basi kwenye uchaguzi ujao watawaadhibu. Mbona Liberal Democrats wanashirikiana na wahasibu wao Conservatives huko Uingereza? na unaona jinsi wapiga kura wanavyowaadhibu?

Badala ya kulalamikia MoU ambayo inaipunguzia serikali mzigo wa kutoa huduma za kijamii basi na nyie mngeingia kwenye MoU yenu ili sote tufaidike. Kama vile mnavyowapeleka watoto wenu St. Joseph University nasi tunawapeleka watoto wetu Feza.

Amandla.....
Nenda tena kasome katiba na sheria halafu rudi inienyeshe mahala katiba inakatazam sheria ya dini kutumika na mahakama zetu wanachoomba waislaam upo ktk muhimili wa Mahakama ambao sio kuingia serikalini. Soma na jaribu sana kuelewa sio kubisha ili mradi unabisha tu. kuhusu Memorundum of Association, nakubali nilifanya kosa la kimaandishi na nilirekebisha mapema kabla sema wewe umeamua tu kuturudiha nyuma kwa sababu huna hoja.

Bado nakutaka nenda katazame maana na tafisri ya memorundum of understanding.., kisha tutaendelea. Mimi sijazungumzia wakristu bali wana Chadema wanaomuunga mkono Mtei kwa sababu za Ukristu wao. Nina hakika wapo wakristu wengi tu hawakubaliani na Mtei haiwafanyi wao wasaliti wa dini ama imani..

Hakuna sababu ya kuendelea kubishana juu ya Uislaam na Ukiristu kwa moto alouwasha Mtei bali ni kuitazama haki imesimama wapi. Tulimkosoa Jussa kwa kutaka kutugawa kwa Udini na sii kosa kumkosoa Mtei hata kidogo. Mbona nilimuwasha Jussa na leo namtetea Nyerere kwa maamuzi yake kupambana na Udini?..

Ya Uingereza lazima utambue kwamba taifa hilo lilipatikana kwa Ukristu, ni Ukiristu ndio unaongoza hata kikatiba lazima watazame Biblia inasema nini kabla ya kupitisha hata baadhi ya sheria zao.. Kanisa ni sehemu ya utawala wa Uingereza toka enzi wakitawala makoloni yake, hatuwaigi wala kuwafuata wao..
 
Nenda tena kasome katiba na sheria halafu rudi inienyeshe mahala katiba inakatazam sheria ya dini kutumika na mahakama zetu wanachoomba waislaam upo ktk muhimili wa Mahakama ambao sio kuingia serikalini. Soma na jaribu sana kuelewa sio kubisha ili mradi unabisha tu. kuhusu Memorundum of Association, nakubali nilifanya kosa la kimaandishi na nilirekebisha mapema..

Bado nakutaka nenda katazame maana na tafisri ya memorundum of understanding.., kisha tutaendelea. Mimi sijazungumzia wakristu bali wana Chadema wanaomuunga mkono Mtei kwa sababu za Ukristu wao. hakuna sababu ya kuendelea kubishana juu ya Uislaam na Ukiristu kwa moto alouwasha Mtei bali ni kuitazama haki imesimama wapi. Tulimkosoa Jussa kwa kutaka kutugawa kwa Udini na sii kosa kumkosoa Mtei hata kidogo.
JF ni tanuru inatakiwa itwange kotekote without fear or favour. Mtu akikosea akosolewe; Kumkoma Nyani Giladi.
 
JF ni tanuru inatakiwa itwange kotekote without fear or favour. Mtu akikosea akosolewe; Kumkoma Nyani Giladi.
Mbona sijakataa kukosolewa, mimi huandika kama navyofikiria bila kuandaa pembeni. Ukianza kunitazama kwa makosa ya kimaandishi basi utakesha maana yapo mengi sana. Nisome, jaribu kunielewa ukishindwa uliza na sio kutaka kubadilisha hoja.. Fundi Mchundo amekuta MoU ni kinyume cha sheria sasa anatafuta pa kutokea tu.
 
Mtei hana cheo katika chama?

Kwa ufafanuzi tu, Mtei ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA. Hicho ni cheo kikubwa sana kuliko Mbunge ndani ya Chama. Propaganda za kuwa Mtei hana Cheo kwenye Chama haziwezi kubadilisha ukweli kuwa CHADEMA imeshindwa kuonyesha ujasiri wa kuwakosoa wazee wake na badala yake kutoa kauli za kisiasa za kujitenga na kauli zao. Tanzania inahitaji viongozi jasiri wanaoweza kuona kosa na kusema hili ni kosa, bila kujali nani amelifanya. Angalau Zitto ameonyesha ujasiri, lakini tamko la chama limekaa kisiasa tu...
 
Fundi Mchundo,
Kwa hiyo una tatizo na hoja yenyewe au tatizo ni hoja/dai hiyo kuwasilishwa na waislam?


Mkuu,nadhani kuna kitu muhimu unakikosa au hukijui kuhusu Chadema. Mtei hana cheo katika chama?Na unaamini hivyo katika mtazamo gani? Kutokuwepo kwenye formal structure ya kichama haitoshi kumfanya asiwe superior kwenye maamuzi ya chama mkuu.Labda nikukumbushe kitu kimoja,baada ya Nyerere kung'atuka madarakani,alibaki kuwa mwanachama wa CCM bila cheo,lakini ushawishi na nafasi yake katika chama ilikuwa hata ni zaidi ya Mwenyekiti wa chama. Na ndivyo hivyo kwa Mtei.
Au kwa tafsiri yako,akisema jambo Zitto na kisha Mtei akakosoa ndio unakuwa msimamo wa chama,lakini akisema Mtei na kisha Zitto akakosea,hapo anakuwa amekiuka maadili ya chama na ynakuwa ni mtazamo binafsi? Double standards katika chama!!
Labda jikumbushe,Zitto alipotoa msimamo wake kuhusu suala la umri na urais,na mtazamo wake kuhusu kugombea iwapo atapendekezwa na chama chake,Mtei alitoa kauli gani? Kama kweli unaamini analosema Zitto lina uzito katika chama zaidi ya Mtei? Chadema ni double standards mkuu!

Mimi sina tatizo na hoja kuwasilishwa bali tunachotaka ni kuwa, itapowasilishwa itazamwe bila upendeleo wowote. Kwa vile hatuwezi kuwaona watu mioyoni mwao basi tungependa pawe na parity kaika uwakilishi ya wakristu na waislamu.

Mtei si Nyerere. Hata Nyerere baada ya kung'atuka hakuwahi kudai kuwa ndie msemaji wa chama. Alipinga kujiunga kwa Zanzibar kwenye OIC lakini ni waliokuwa kwenye uongozi wakati ule ndio waliokataa rasmi. Angekuwa na cheo kwenye chama basi angemuagiza Mwenyekiti wake asijiunge lakini yeye alipinga bila kuagiza. kama ilivyokuwa haki yake kama raia.

Akisema Zitto kama Naibu Katibu Mkuu tunachukulia kama msimamo wa chama hadi hapo waliojuu yake watakapominga. Akisema Mtei, ni mtazamo wa raia aliye mwanachama wa Chadema na hata kama hatakosolewa kamwe hautakuwa msimamo wa Chama hadi hapo upate baraka za uongozi au kiongozi mmoja.

Kwani Zitto na Januari walipotoa misimamo yao kwenye kongamano basi uliona kuwa tayari CCM na Chadema wameingia Muafaka kuhusu umri wa mgombea urais?

Usitake kulazimisha mambo.

Amandla.....
 
Kwa ufafanuzi tu, Mtei ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA. Hicho ni cheo kikubwa sana kuliko Mbunge ndani ya Chama. Propaganda za kuwa Mtei hana Cheo kwenye Chama haziwezi kubadilisha ukweli kuwa CHADEMA imeshindwa kuonyesha ujasiri wa kuwakosoa wazee wake na badala yake kutoa kauli za kisiasa za kujitenga na kauli zao. Tanzania inahitaji viongozi jasiri wanaoweza kuona kosa na kusema hili ni kosa, bila kujali nani amelifanya. Angalau Zitto ameonyesha ujasiri, lakini tamko la chama limekaa kisiasa tu...

mafisadi wa ccm sasa wamepata pa kutokea

aloanzisha udini ni Kikwete kwa kuteua tume yenye waislam 23 kati ya 30

mengine yote haya mnayoandika ni ngonjera tu
 
Kwa ufafanuzi tu, Mtei ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA. Hicho ni cheo kikubwa sana kuliko Mbunge ndani ya Chama. Propaganda za kuwa Mtei hana Cheo kwenye Chama haziwezi kubadilisha ukweli kuwa CHADEMA imeshindwa kuonyesha ujasiri wa kuwakosoa wazee wake na badala yake kutoa kauli za kisiasa za kujitenga na kauli zao. Tanzania inahitaji viongozi jasiri wanaoweza kuona kosa na kusema hili ni kosa, bila kujali nani amelifanya. Angalau Zitto ameonyesha ujasiri, lakini tamko la chama limekaa kisiasa tu...
Mkuu wangun hapa sintokubaliana na wewe maana ukimsoma Mnyika utaelewa kwamba chama kimejitenga na Mtei kwa kutumia busara kubwa sana. Huwezi kumkemea mzee Mtei kwa sababu ameandika kile alichodhania yeye ni haki yake japokuwa kinachonganisha wananchi. Sema Zitto kaingiwa na jazba kwa sababu anapigwa vita sana na wazee hawa hawa ndani ya chama kama msaliti na anapopata nafasi kama hizi inampa picha kinachoendelea nyuma ya pazia. Na hata ukimuuliza yeye nadhani atakwambia kwa uhakika Mzee Mtei kachoka na ndio maana yeye na kina Mbowe walikichukua chama na kuunda dira tofauti na ile iliyoasisiwa na mzee Mtei.

Mbona Mwinyi alipigwa kibao na kijana au Mkapa kuzomewa haya ni ya kawaida kabisa kwa wazee wetu kukosea na wakakosolewa isipokuwa inahitajika sana busara ktk kutoa majibu. CUF wameshindwa kabisa kumkataza Jussa na hata Lipumba alipokuja alizungumza juu juu biola kumnyoooshea kidole, ndio siasa mkuu wangu.
 
Mbona sijakataa kukosolewa, mimi huandika kama navyofikiria bila kuandaa pembeni. Ukianza kunitazama kwa makosa ya kimaandishi basi utakesha maana yapo mengi sana. Nisome, jaribu kunielewa ukishindwa uliza na sio kutaka kubadilisha hoja.. Fundi Mchundo amekuta MoU ni kinyume cha sheria sasa anatafuta pa kutokea tu.

Mbona uongo mtu mzima wala haupendezi? Itakuwaje MoU iwe kinyume ya sheria wakati haisimamiwi na sheria? Tuonyeshe palipo na mkataba kati ya mashirika ya kikristu na serikali ndio tutaanza kukuelewa kidogo.

Amandla....
 
Kwa hali hii basi itakuwa ni kamati ya ajabu ambayo haitaangalia muingiliano wa dini katika taifa letu. Ili pawe pana dhana ya haki kutendeka, basi kuna haja ya kuhakikisha kuwa pande hizo zenye usongo basi ziwakilishwe ipasavyo. Lakini hili haliwezekani ilhali Zanzibar wanapewa parity katika uwakilishi wa kamati hii ambayo inazungumzia katiba ya nchi ambayo wengi wa wawakilishi wao hawachelei kuonyesha kuwa haitaki (kama si kwa maneno basi vitendo). Ndio maana wengine tunasema kuwa badala ya kukazania mjadala wa Katiba basi tuanze kwa kuungalia Muungano wetu na uwakilishi katika vyombo vyetu. Tutakachokubaliana ndicho kitakachoongoza upatikanaji wa nchi itakayokuwepo au zitakazokuwepo.

Kukimbilia kudai alichokisema Mtei ni mfano wa udini wa Chadema ni sawa na wale wanaohusisha kutamkwa kwa Takbir kwenye mikutano ya CUF kama ushahidi wa uislamu wa chama hicho.
Mtei ameongea kama raia na ajibiwe kama raia mwengine na si vinginevyo.Amandla........
Nakubaliana nawe kabisa kuwa kamati hiyo ni lazima iangalie nchi kwa ujumla na kila kinachotuunganisha au kututenganisha kwa masilahi na mustakabali wa taifa.

Ninatumaini kuwa uweledi, busara na elimu ndivyo vinapaswa kuwaongoza hao wanakamati.
Kwa muktadha huyo kuwepo kwa uwiano ni njia ya makato ya kusema tupige kura ninyi simba sisi yanga, this will defeat the whole purpose of 'tume'

Sina uhakika na walioandika katiba iliyotufikisha miaka 50 kama taifa licha ya matatizo yatokanayo walichaguliwa kwa uiwano gani. Sina uhakika ile kamati iliyokaa Motel Agype kuunda Chama cha mapinduzi chanye watu wa aina zote ilikuwa na uwiano gani. Mimi nasema haya mambo yafanywe kitaalamu na si kuangalia wajihi au wasifu

Nakubaliana nawe pia katika mambo yanayonishangaza ni hili la wzbar, kwanza kwa uwiano na pili je wanataka kitu wanachoshiriki kukiandika? Hawa wameshaonyesha chuki za wazi kabisa hadi 'xenophobia' kwa wabara, sasa tulitakiwa tuanze na hili la muungano.

Isije ikatokea wakaandika katiba na kesho wakaondoka zao kama wanavyopanga halafu wakatuachia mzigo wa marekebisho tena. Na isije ikatokea wakaingiza interest zao kwa kitu wasichokiamini. Kosa hili nimelisema sana, tunatakiwa tuweke farasi mbele ya mkokoteni na si mkokoteni mbele ya farasi.
Hata uundwaji wa tume hii sikubaliani nao kwasababu haikutokana na wenye katiba (wananchi)
Hakika umesema,kuuangalia muungano ndiyo dira ya katiba yetu.

Ninatofautiana nawe kuhusu Mtei. Mzee Mtei ni Mbunge wa Zamani, Gavana wa Benki kuu ya Tanzania na Waziri wa fedha. Kwa katiba iliyokuwepo wakati wake, yeye alikuwa ni mmoja wa 'watarajiwa wa urais' yangetokea yasiyotarajiwa.

Nina maana sifa zake za elimu, uzoefu wake, pamoja na kuwa waziri mwandamizi (senior minister)
Mzee Mtei ni mwanasiasa na mwanzilishi wa Chadema. Sifa za mzee wetu zinamweka mahali tofauti sana na rai kama wewe na mimi. Edwin Mtei yenyewe ni habari kabla ya habari.

Kauli zake zinapewa uzito sana ndiyo maana unaona badala ya kujadili katiba watu wanabadilishana kashfa utadhani tupo katika makanisa na misikiti, utadhani tunaandika biblia na misahafu.
Hali isingekuwa hivyo kama kauli hiyo ningeitoa kapuku mimi, lakini ni upele na sasa umewapata wenye kucha

Ni kutokana na influency yake kitaifa kauli alizozitoa zinapaswa zilinganiwe na yeye mwenyewe. Ima azitolee ufafanunuzi au kama hana aombe radhi. No more no less

Lau basi angetumia uzooefu wake kama Mbunge,Gavana au Waziri kuonyesha kile anachodai tungemwelewa.
Alipaswa atuonyeshe wakati akiwa Gavana alileta vipi uwiano, wakati akiwa waziri alileta uwiano vipi.
Ana uzoefu mwingi tu wa kutusaidia nao. Kauli rahisi ya 'waislam ni wengi kuliko wakristo' ni ya 'uchochezi'. Haku propose ilitakiwa iweje Hata kama kuna ukweli lakini hakuuwakilisha katika viwango vya hadhi yake.

Mimi narudia tena na tena, kamati yenyewe sikubaliani nayo kwasababu haikuundwa na sisi na suala la muungano lingetangulia katiba ili tujue tunaandika katiba ya nani na kwanini. Haya ya udini yanazidi kutuondoa kwenye tatizo,Mzee Mtei sijui anajisikiaje akiona yanayosomeka ! Aje afafanue au aombe radhi kinyume chake ameitia doa kubwa historia na heshima yake.
 
Mkuu wangun hapa sintokubaliana na wewe maana ukimsoma Mnyika utaelewa kwamba chama kimejitenga na Mtei kwa kutumia busara kubwa sana. Huwezi kumkemea mzee Mtei kwa sababu ameandika kile alichodhania yeye ni haki yake japokuwa kinachonganisha wananchi. Sema Zitto kaingiwa na jazba kwa sababu anapigwa vita sana na wazee hawa hawa ndani ya chama kama msaliti na anapopata nafasi kama hizi inampa picha kinachoendelea nyuma ya pazia. Na hata ukimuuliza yeye nadhani atakwambia kwa uhakika Mzee Mtei kachoka na ndio maana yeye na kina Mbowe walikichukua chama na kuunda dira tofauti na ile iliyoasisiwa na mzee Mtei.

Mbona Mwinyi alipigwa kibao na kijana au Mkapa kuzomewa haya ni ya kawaida kabisa kwa wazee wetu kukosea na wakakosolewa isipokuwa inahitajika sana busara ktk kutoa majibu. CUF wameshindwa kabisa kumkataza Jussa na hata Lipumba alipokuja alizungumza juu juu biola kumnyoooshea kidole, ndio siasa mkuu wangu.

Kaka,
Hivi mara hii umeshasahau kuwa Zitto alipotoa maoni yake kwenye media kuhusu ku walk out on President Bungeni alitakiwa kwenda kujieleza. Mbona Shibuda ameshutumiwa kwa kutoa maoni yake. Hivi Mtei ana haki zaidi ya kutoa maoni yake kuliko hawa wengine?
Hivi mbona Rostam anaposhutumiwa kwa ufisadi shutuma hizo zinaelekezwa kwa CCM? Kwa nini isitumike fikra hiyohio kuwa Rostam ni tabia yake kama yeye. Kwa hiyo kosa likifanywa na mwana CCM ni kosa la CCm, likifanywa na mwana CHADEMA ni kosa lake binafsi. This is very interesting...
 
Mbona uongo mtu mzima wala haupendezi? Itakuwaje MoU iwe kinyume ya sheria wakati haisimamiwi na sheria? Tuonyeshe palipo na mkataba kati ya mashirika ya kikristu na serikali ndio tutaanza kukuelewa kidogo.

Amandla....
Labda nikusaidie hivi, Memorundum of understanding sio Mkataba. Ukisha elewa tunachozungumzia rtudi tena..

1. Memorandum of understanding (MoU)
is a document describing a bilateral or multilateral agreement between parties. It expresses a convergence of will between the parties, indicating an intended common line of action. It is often used in cases where parties either do not imply a legal commitment or in situations where the parties cannot create a legally enforceable agreement. It is a more formal alternative to a gentlemen's agreement..

2. Contract
A contract is an agreement entered into voluntarily by two parties or more with the intention of creating a legal obligation..

 
Kaka,
Hivi mara hii umeshasahau kuwa Zitto alipotoa maoni yake kwenye media kuhusu ku walk out on President Bungeni alitakiwa kwenda kujieleza. Mbona Shibuda ameshutumiwa kwa kutoa maoni yake. Hivi Mtei ana haki zaidi ya kutoa maoni yake kuliko hawa wengine?
Hivi mbona Rostam anaposhutumiwa kwa ufisadi shutuma hizo zinaelekezwa kwa CCM? Kwa nini isitumike fikra hiyohio kuwa Rostam ni tabia yake kama yeye. Kwa hiyo kosa likifanywa na mwana CCM ni kosa la CCm, likifanywa na mwana CHADEMA ni kosa lake binafsi. This is very interesting...
Nitakujibu kwa ufasaha zaidi.
Swala la Zitto lilikuwa msimamo wa pamoja ambao kura yake ama kuwepo kwake bungeni kunaondoa kura moja ya chama vile vile Shibuda yaani athari yake ni kupoteza UMOJA wa chama ktk maamuzi yanayopinga muswada ama sera lakini Makosa ya Rostam yanahusishwa na chama kwa sababu chama kinamlinda yeye. Ufahamike kwamba sio tu Rostam anapingwa na Chadema au CUF bali hadi wananchi kwa sababu athari zake hazipo kwa chama chake. Tofauti na wengine Rostam ni bingwa wa kutuibia sisi na kukinufaisha chama hivyo ni sawa na kanisa au msikiti unapokea fedha za mwizi. Kisheria wao CCM ni wahusika vile vile.
 
Nitakujibu kwa ufasaha zaidi.
Swala la Zitto lilikuwa msimamo wa pamoja ambao kura yake ama kuwepo kwake bungeni kunaondoa kura moja ya chama vile vile Shibuda yaani athari yake ni kupoteza UMOJA wa chama ktk maamuzi yanayopinga muswada ama sera lakini Makosa ya Rostam yanahusishwa na chama kwa sababu chama kinamlinda yeye. Ufahamike kwamba sio tu Rostam anapingwa na Chadema au CUF bali hadi wananchi kwa sababu athari zake hazipo kwa chama chake. Tofauti na wengine Rostam ni bingwa wa kutuibia sisi na kukinufaisha chama hivyo ni sawa na kanisa au msikiti unapokea fedha za mwizi. Kisheria wao CCM ni wahusika vile vile.

Kwa hiyo kaka Mkandara unachotaka kutuambia ni kwamba swala la kupinga kauli za udini sio la kichama ndani ya CHADEMA, kwamba hilo limeachwa kila mtu aamue anavyotaka? Maana sioni tofauti kati ya mtu anayepinga maamuzi ya pamoja ya kutokumsikiliza Rais na yule anayepinga maamuzi ya pamoja ya kutetea umoja ya kitaifa?
Kauli ya mtei inatosha kumfanya ahitajike kujiudhuru, ila kwa sababu watanzania tumeshaamua kuwa mambo yetu ni substandard ndio maana hii kauli inaachwa inaeleaelea tu.
Unadhani ni sahihi kwa kiongozi wa chama kutoa kauli tata halafu anaingia mitini bila kutoa ufafanuzi wowote hata baada ya kuona kauli yake imesababisha mtafaruku. Mtei hana nidhamu kwa jamii na CHADEMA imeshindwa kumhandle Mtei.
 
Mawazo kweli kabisa tatizo linakuwa ikifika kuingilia CUF utakuwa very different;

Hapo ndipo mnapoficha ajenda zenu hadi Mungu anaumbua kama alivyofanya kwa Mzee Mtei;

Mtei ni mdini na mkabila wa kuogopwa Tanzania; ikulu si kanisani

unamaanisha nini unaposema ikulu si kanisa kwahiyo ikulu ni msikiti?
Kwani waislamu wawe wengi kwenye tume? Au wao ni wasomi sana? Au wao ni wengi sana Tanzani kuliko wengine.usipotambua kwamba wahusika wakuu yaani kikwete na shein ni wadini wewe ni kilaza.
 
Nguruvi3,
Unajua tunataka zsana kurefusha mpira ambao ukikatika utarudi machoni..Nina hakika sana hata Wazanzibar wenyewe wana mashaka na uchaguzi huu kwa sababu wote hawa waliochaguliwa ni pro Muungano. Ikumbukwe tu kwamba muswada uliopita na kuwa sheria ulisisitiza Muungano kuwepo na kwamba hautavunjwa, sasa wale wote wanaopinga muungano lazima watakuja na kashfa ya uchaguzi huu kwa sababu hawataki Muungano (UMOJA) wetu, hawa ni sawa kabisa na Mtei na wapo wanaitazama tume hii kama kikwazo kwao. Wapo CCM na CUF wanasubiri tu wakati muafaka kuanzisha vurugu zao.

Katiba yetu ya mwaka 1977 ndio ilomjengea chuki Nyerere kwa sababu alipigana na Udini, Ukabila, rushwa na kusema wazi kwamba nchi hii ni ya wakulima na wafanyakazi.. Wafanyabiashara wote walimwona mbaguzi na bahati mbaya wakati huo waislaam wengi (wenye asili ya kiarabu) ndio walikuwa wafanyabiashara pamoja na wahindi.. This is the fact kwa nini Nyerere alichukiwa zaidi na waislaam baada ya Azimio la Arusha.

Mimi nachowaomba wote wanaolalamikia uchaguzi wa wajumbe wa Zanzibar wanipe list yao ya watu wanaowajua wao kama wanaswihi kuingia ktk tume hii maana jamani tusiwe wajinga kiasi hicho. hao wabunge wa Zanzibar ktk bunge la Muungano lina wakristu wangapi? Baraza la Mapinduzi lina wakristu wangapi?. hata serikalini mawaziri na manaibu kutoka Zanzibar kuna wakristu wangapi? siku zote tusilalamike ila leo, iweje swala la wajumbe wa Zanzibar liwe tatizo kwetu ilihali hawa watu ni asilimia 99 waislaam. Na hawa wajumbe wanawakilisha upande wa Zanzibar ktk muungano wetu kikatiba. How are we gonna avoid that?
- Tupeni list yenu kutoka Zanzibar mjadala ufungwe..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom