‘Mtego wa madeni’ ni nyenzo ya propaganda inayotumika na jopo la washauri bingwa wa nchi za Magharibi

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG111349383245.jpg


Mwaka huu ni wa 10 tangu Pendekezo la Ukanda Mmoja, Njia Moja lilipotolewa na rais wa China Xi Jinping. Katika miaka hii 10, ushirikiano kati ya China na nchi zilizo katika njia ya Ukanda Mmoja na Njia Moja zimefaidika kwa kiasi kikubwa.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Ukanda Mmoja na Njia Moja ya nchini Sweden, Stephen Brawer, amezungumza na gazeti la Global Times la China, na ameeleza uelewa wake wa Pendekezo la Maendeleo ya Dunia, Pendekezo la Usalama wa Dunia, na Pendekezo la Ustaarabu wa Dunia, ambayo yametolewa na China.

Bw. Brawer anasema dunia imeyapokea mapendekezo hayo, na kuonyesha mabadiliko katika mwelekeo wa sera ya dunia, na kwamba, mapendekezo hayo ni muhimu sana kwa maendeleo ya dunia. Amesema ingawa Marekani na Kundi la Nchi 7 (G7) kwa sasa haziko tayari kukubali ama kuelewa mapendekezo haya, jambo hili halitazuia nafasi ya China na dunia kuendelea katika mwelekeo mwingine.

Akizungumzia madai yaliyotolewa na vyombo vya habari vya nchi za Magharibi kuwa kasi ya Pendekezo la Ukanda Mmoja, Njia Moja inapungua pamoja na kile walichokiita ‘mtego wa madeni’, Bw. Brawer amesema kauli hizo hazina msingi wowote, na ni nyenzo ya propaganda inayotumiwa na majopo ya washauri bingwa katika nchi za Magharibi kubadili ukweli wa mambo, na pia ni sehemu ya kauli zenye msingi wa kudumisha wazo la nguvu ya nchi za Magharibi na kutarajia kuwa dunia nzima itakubaliana nalo. Anasema dunia mpya inaibuka, na ni kwa maslahi ya watu wa Ulaya na Marekani kutopinga hatua hii kwa migogoro na mivutano, bali kuikumbatia na kushiriki, sio tu kwa manufaa ya jamii ya kimataifa, bali pia kusaidia kufufua uchumi wa nchi za Magharibi. Ameongeza kuwa huu ni wakati wa kuungana pamoja na kushinda mawazo ya kwamba, Marekani ni nchi yenye nguvu zaidi, kwani hiyo ilikuwa historia.

Tukizungumzia Pendekezo la Ukanda Mmoja, Njia Moja, kwa upande wa nchi za Afrika tunaweza kusema kuwa Pendekezo hilo limekuwa na manufaa makubwa kwa nchi zilizojiunga. Hii ikiwa ni tofauti na madai yanayotolewa na nchi za Magharibi, kuwa China inaziwekea nchi za Afrika kile wanachokiita, ‘mtego wa madeni.’ Tukichukulia Kenya kwa mfano, reli ya SGR inayofanya safari za abiria na mizigo kati ya mji wa pwani wa Mombasa na mji mkuu wa nchi hiyo, Nairobi, imekuwa na faida kubwa kwa wananchi. Sio tu kwamba reli hiyo imesaidia kupunguza muda wa safari kati ya miji hiyo miwili, bali pia imeweza kutoa fursa za biashara katika maeneo inayopita, na hivyo kuinua kipato cha wananchi katika maeneo hayo.

Kupitia Pendekezo hilo, China imeweza kuhamisha teknolojia zake za ubora wa juu kwa nchi nyingine zinazoendelea, ikiwemo teknolojia ya kilimo na kuzuia jangwa. Katika nchi za Afrika ikiwemo Madagascar, mpunga chotara kutoka China umekuwa ni mkombozi kwa wakulima na walaji, na kusaidia kupunguza hatari ya njaa.

Madai kwamba China inaziwekea baadhi ya nchi zinazoendelea, hususan za Afrika, ‘mtego wa madeni’, ni madai ambayo hayana msingi, na ni njama inayotumiwa na baadhi ya nchi za Magharibi, ikiwemo Marekani, kujaribu kuondoa ushawishi wa China katika jamii ya kimataifa, na ni madai ambayo yanapaswa kupuuzwa.

China imekuwa ni nchi kubwa inayoendelea, na nchi ya pili kwa uchumi duniani, lakini inachukua nafasi hiyo kuzisaidia nchi nyingine zinazoendelea, hususan za Afrika, kujipatia maendeleo kwa njia inayoendana na nchi husika, bila kulazimisha ama kuweka masharti yoyote yanayoingilia mambo ya ndani ya nchi husika, tofauti na inavyokuwa kwa nchi za Magharibi.
 
Back
Top Bottom