MTEGO wa DR.ULIMBOKA uko tayari...

MTEGO wa DR.ULIMBOKA uko tayari...

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Serikali imeshakamilisha mtego wa kumzima kabisa Dr.Ulimboka. Mtego huo umeratibiwa na Usalama wa Taifa na Polisi kupitia kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Eliezer Feleshi. Mtego huo ni upi? Ni hivi:kuna 'Jambazi' la kikenya lililofikishwa Mahakamani kwa tuhuma za kumteka na kumtesa Dr.Ulimboka. Kesi iko Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Sasa,kuna taarifa kuwa Dr.Ulimboka anaendelea kupata nafuu na ameshaanza kufanya mazoezi mepesi. Ni habari ya kutia moyo. Lakini,Dr.Ulimboka atakaporudi nchini,atatamani akutane na Waandishi wa Habari na kuzungumzia sakata lake. Hilo hatafanikiwa kulifanya.Na akilifanya atashtakiwa kwa kuidharau Mahakama. Kivipi?

Serikali kupitia Jeshi la Polisi litamuwahi kwa kumwambia kuwa suala analotaka kulizungumzia liko Mahakamani. Dalili za kusimamia mtego huo zimeshaanza kuonekana Bungeni.Ni juzi tu Bajeti ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ya Mambo ya Ndani ilizuiwa(baadhi ya kurasa zake) kwa kisingizio hichohicho. Swali litakalobaki ni je,mambo hayo ndio yataishia kwa 'Jambazi' la Kikenya?
 
Vyovyote vile haki lazima itasimama tu,haijalishi mitego ni mikubwa kama ya kumnasa tembo.God is just
 
Dr Uli atazuiwa kama nani? yeye ni muhimili gani katika hii mihimili mitatu? Mbona kesi ya Kombe magazeti na watu walikua wanizungumzia na wakati ipo mahakamani?
 
Ushaona wapi mtu anayefanya mambo kihuni huni akafika anakotaka kwenda?
 
Huu sasa ni uhuni mbona JK aliliongelea Suala la Uli kwa speech yake while ilo Suala likiwa kwa Mahakama
Naona Mahakama sasa inatumika Kama Kichaka cha kuficha mambo
 
Serikali imeshakamilisha mtego wa kumzima kabisa Dr.Ulimboka. Mtego huo umeratibiwa na Usalama wa Taifa na Polisi kupitia kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Eliezer Feleshi. Mtego huo ni upi? Ni hivi:kuna 'Jambazi' la kikenya liliofikishwa Mahakamani kwa tuhuma za kumteka na kumtesa Dr.Ulimboka. Kesi iko Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Sasa,kuna taarifa kuwa Dr.Ulimboka anaendelea kupata nafuu na ameshaanza kufanya mazoezi mepesi. Ni habari ya kutia moyo. Lakini,Dr.Ulimboka atakaporudi nchini,atatamani akutane na Waandishi wa Habari na kuzungumzia sakata lake. Hilo hatafanikiwa kulifanya.Na akilifanya atashtakiwa kwa kuidharau Mahakama. Kivipi?

Serikali kupitia Jeshi la Polisi litamuwahi kwa kumwambia kuwa suala analotaka kulizungumzia liko Mahakamani. Dalili za kusimamia mtego huo zimeshaanza kuonekana Bungeni.Ni juzi tu Bajeti ya Kambi Rasmi ya Upinzanzi Bungeni ya Mambo ya Ndani ilizuiwa(baadhi ya kurasa zake) kwa kisingizio hichohicho. Swali litakalobaki ni je,mambo hayo ndio yataishia kwa 'Jambazi' la Kikenya?

Kweli huyu jamaa according to experience, ni bingwa wa hii kitu.
Lakini moto huu wa petrol, hakuna ataeweza uzima....hadi kieleweke baba..
 
Waandishi wa habari wamfuate huko huko ,kama wale waandishi wa Kimataifa wanaweza kuifanya kazi hiyo ,au hata madaktari wanaweza kumfanyia mazungumzo na kuhusisha masuali mazito kwake ,kama anawafahamu waliomteka ,kuwataja majina kiasi ya kuelezea kisa kizima kwa yale anayoyakumbuka na kuwa yenye usaili wa kideo sio audio.
 
Nimerudi kutoka kwenye burn,serikali haina namna ya kumzuia mpiganaji Uli kwakuwa yeye sio muhimili na vyombo vya habari si muhimili.
 
Waandishi wa habari wamfuate huko huko ,kama wale waandishi wa Kimataifa wanaweza kuifanya kazi hiyo ,au hata madaktari wanaweza kumfanyia mazungumzo na kuhusisha masuali mazito kwake ,kama anawafahamu waliomteka ,kuwataja majina kiasi ya kuelezea kisa kizima kwa yale anayoyakumbuka na kuwa yenye usaili wa kideo sio audio.

hakuna haja ya kungoja kuja Tz. Azungumze huko huko na vyombo vya hapa kwetu vinukuu tu yale yaliyosemwa. Video clip iwekwe katika mtandao kazi ya kuisambaza itakuwa imekamilika.
 
Sasa,kuna taarifa kuwa Dr.Ulimboka anaendelea kupata nafuu na ameshaanza kufanya mazoezi mepesi. Ni habari ya kutia moyo. Lakini,Dr.Ulimboka atakaporudi nchini,atatamani akutane na Waandishi wa Habari na kuzungumzia sakata lake. Hilo hatafanikiwa kulifanya.Na akilifanya atashtakiwa kwa kuidharau Mahakama. Kivipi?

We nani kakuambia Ulimboka ana mpango wa kurudi Tanzania kwa sasa kabla usalama wake haujahakikishwa?! Ulimboka ni mkimbizi kwa sasa mpaka hali iatakaporuhusu kurudi nchini...meaning 'mtandao' wa serikali hii utakapotoka madarakani!
 
Hebu tufafanulie kidogo mkuu, hapo Usalama wa Taifa wanahusika vipi?

Usalama wa Taifa ni maajenti wa kupanga Dili zote za kuangamiza Wananchi wa Tanzania hasa wale wanaodai haki na kusema ukweli kuhusiana na Serikali Dhurumati inayoongoza Tanzania.

Hivyo kwa kuwa ni maajenti lazima kwa taarifa kuwa Ulimboka anaendelea vizuri wanakuna vichwa namna ya kummaliza kwa njia yoyote endapo atarudi salama ili asiweke mambo hadharani.



MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
Back
Top Bottom