Mtazamo wa Rais Samia kuhusu Mashirika ya Umma si sahihi

kmbwembwe

JF-Expert Member
Aug 16, 2012
10,428
7,216
Serikali ya Samia eti inatazama mashirika ya umma kama uwekezaji wa kibiashara ambapo serikali haistahili tena kuwekeza ila watu binafsi. Msimamo huo sio sahihi kwa sababu mashirika ya kibiashara ya umma yalikwisha binafsishwa yote tangu awamu ya Mkapa. Yale yaliyobakia ni yale ya kimkakati kwa maendeleo ya nchi hayawezi kupewa watu binafsi.

Mashirika kama TANESCO, TTCL, TRC, Air Tanzania, mashirika ya kuzalisha na kusambaza maji, TPA, etc etc. Ili mashirika ya kimkakati kua na tija na kufikia malengo ya uwepo wake lazima serikali iwe na utashi wa kuyasimamia vema.

Serikali inayoruhusu vigogo wake wale kwa urefu wa kamba zao kwa vyovyote itakua na muelekeo wa kuwaacha vigogo kupora kutoka mashirika ya kimkakati ya umma na hatimae kujidai kuyabinafsisha huku ni uporaji wa mali ya umma.

Hatuna haja kuonesha kwa nini mashirika ya kimkakati kwa maendeleo ya nchi yawepo. Na tukisema maendeleo ya nchi tunamaanisha maendeleo ya umma wa wananchi na sio tabaka fulani.

Tuliwahi kubinafsisha TRC, TTCL, na air tanzania na tulichokiona kama matokeo ilibidi kuyarudisha mashirika hayo mkonono mwa umma kwa maana ya kumilikiwa na serikali.

Reli tuliibiwa na wahindi mali zote zisizohamishika kama majumba na viwanja kwa maana walipiga hela wao na mwisho hadi karibu kuibiwa uwezo wa kujitegemea kwa wao kuanza kupeleka vichwa vya treni india kwa matengenezo ambapo karakana na wafanyakazi wenye ujuzi na uwezo walibakia kinywa wazi.

Kuhusu Air Tanzania vivyo hivyo makaburu wakatuadhibu vibaya.

Kinachotakiwa ni Samia kuwa makini na ajue sera na itikadi za CCM bado ni relevant asituchanganyie ulaji kwa urefu wa kamba wakati ni uporaji wa umma.

Kinachotakiwa ni usimamizi imara wa mashirika ya kimkakata na kuacha kufanya uteuzi kishikaji ambapo wapigaji na watu wasio na weledi na uzalendo kupewa kuendesha mashirika hayo.
 
Serikali ya samia eti inatazama mashirika ya umma kama uwekezaji wa kibiashara ambapo serikali haistahili tena kuwekeza ila watu binafsi. Msimamo huo sio sahihi kwa sababu mashirika ya kibiashara ya umma yalikwisha binafsishwa yote tangu awamu ya mkapa. Yale yaliyobakia ni yale ya kimkakati kwa maendeleo ya nchi hayawezi kupewa watu binafsi.

Mashirika kama tanesco, TTCL, TRC, air tanzania, mashirika ya kuzalisha na kusambaza maji, TPA, etc etc. Ili mashirika ya ki
Mimi naona serikali iruhusu ushindani kwenye hayo mashirika kama ilivyo kwenye simu, benki, mafuta, elimu, afya, usafirishaji na kadhalika.
 
Hoja nzuri, uandishi unachosha!

Kwenye mada, pengine tungetafuta jinsi ya kuendesha maisha yetu bila kujali CCM wanafanya nini! Binadamu waliopata kuwepo ndani ya CCM hawazidi watano, na sidhani kama wapo tena.

Serikali ni familia yao! Ndugu wakigombana.
Kwa ufupi tuwazirie shamba la mahindi nyani
 
Serikali ya samia eti inatazama mashirika ya umma kama uwekezaji wa kibiashara ambapo serikali haistahili tena kuwekeza ila watu binafsi. Msimamo huo sio sahihi kwa sababu mashirika ya kibiashara ya umma yalikwisha binafsishwa yote tangu awamu ya mkapa. Yale yaliyobakia ni yale ya kimkakati kwa maendeleo ya nchi hayawezi kupewa watu binafsi.

mashirika ya kimkakata na kuacha kufanya uteuzi kishikaji ambapo wapigaji na watu wasio na uzalendo kupewa kuendesha mashirika hayo.
Uchumi umeusomea wapi? Nawasiwasi umwsoma soviology ndo mana we ni mweupe kichwani. Au umesoma engineering. Kumbuka mwiguli ni first macroeconomist hata imf inamjua
 
Serikali ya samia eti inatazama mashirika ya umma kama uwekezaji wa kibiashara ambapo serikali haistahili tena kuwekeza ila watu binafsi. Msimamo huo sio sahihi kwa sababu mashirika ya kibiashara ya umma yalikwisha binafsishwa yote tangu a.
Leo hii Kuna makundi ya mamia ya wasomi wamerundikana mtaani hawana ajira na tatizo hili alilitengeneza jpm kwa kukumbatia mashitika ya uma na kuua biashara au sector binafsi. Wawekezaji potenti wote waligukuza wafanyakazi ambao Leo ni mamia kwa maelefu mtaani mbaya zaidi hata walimu hawana ajira tofauti na mtazamo wa kipindi Cha jk kwamba ukitaka ajira ya haraka sana somea ualimu na ikuwa kweli kipindi chake hakuna mwalimu alikuwa mtaani. Jpm akaja kuua kila kitu. . Mama anajaribu kurescue hi wimbi la vijana kihangaika mtaani. Au wewe unafurahia tatizo hili?
 
Yale yaliyobakia ni yale ya kimkakati kwa maendeleo ya nchi hayawezi kupewa watu binafsi.

Mashirika kama tanesco, TTCL, TRC, air tanzania, mashirika ya kuzalisha na kusambaza maji, TPA, etc etc. Ili mashirika ya kimkakati kua na tija na kufikia malengo ya uwepo wake lazima serikali iwe na utashi wa kuyasimamia vema.

.
Haya unayoyasema yapo pale tu kwa nia njema tu ya Marais waliopita na huyu aliyepo. Siku ikitokea akaja Rais mwingine mwenye msimamo kama ule wa awamu ya tatu, utayasikia hewani tu
 
Kuna mashirika yapo yanafaa mengine hayana maana,
Kingine serikali iuze hisa ibaki na hisa 20-30% kama ilivyofanya NMB na CRDB, mashirika kama cereal Board, TTCL wabaki na mkonga,
NBC tuuze hisa tubaki na 30, tuuze hisa TCB, Lakini pia shirika la reli libaki kuwa shirika la reli, treni waachie mashirika binafsi
 
Serikali ya samia eti inatazama mashirika ya umma kama uwekezaji wa kibiashara ambapo serikali haistahili tena kuwekeza ila watu binafsi. Msimamo huo sio sahihi kwa sababu mashirika ya kibiashara ya umma yalikwisha binafsishwa yote tangu awamu ya mkapa. Yale yaliyobakia ni yale ya kimkakati kwa maendeleo ya nchi hayawezi kupewa watu binafsi.

Mashirika kama tanesco, TTCL, TRC, air tanzania, mashirika ya kuzalisha na kusambaza maji, TPA, etc etc. Ili mashirika ya kimkakati kua na tija na kufikia malengo ya uwepo wake lazima serikali iwe na utashi wa kuyasimamia vema.

Serikali inayoruhusu vigogo wake wale kwa urefu wa kamba zao kwa vyovyote itakua na muelekeo wa kuwaacha vigogo kupora kutoka mashirika ya kimkakati ya umma na hatimae kujidai kuyabinafsisha huku ni uporaji wa mali ya umma.

Hatuna haja kuonesha kwa nini mashirika ya kimkakati kwa maendeleo ya nchi yawepo. Na tukisema maendeleo ya nchi tunamaanisha maendeleo ya umma wa wananchi na sio tabaka fulani.

Tuliwahi kubinafsisha TRC, TTCL, na air tanzania na tulichokiona kama matokeo ilibidi kuyarudisha mashirika hayo mkonono mwa umma kwa maana ya kumilikiwa na serikali.

Reli tuliibiwa na wahindi mali zote zisizohamishika kama majumba na viwanja kwa maana walipiga hela wao na mwisho hadi karibu kuibiwa uwezo wa kujitegemea kwa wao kuanza kupeleka vichwa vya treni india kwa matengenezo ambapo karakana na wafanyakazi wenye ujuzi na uwezo walibakia kinywa wazi.

Kuhusu Air Tanzania vivyo hivyo makaburu wakatuadhibu vibaya.

Kinachotakiwa ni Samia kuwa makini na ajue sera na itikadi za CCM bado ni relevant asituchanganyie ulaji kwa urefu wa kamba wakati ni uporaji wa umma.

Kinachotakiwa ni usimamizi imara wa mashirika ya kimkakata na kuacha kufanya uteuzi kishikaji ambapo wapigaji na watu wasio na uzalendo kupewa kuendesha mashirika hayo.
Amedanganyika na mabeberu. Ili uweze kuwaelewa mabeberu inabidi uwe intelligent kweli kweli. Mabeberu wanaweza wakasema shirika fulani ni private owned kumbe ni private geresha, private hewa, private danganya toto.
Je, sisi tunaweza kuwa na private geresha? TISS inaweza kumiliki mashirika makubwa kibiashara? JWTZ inaweza kumiliki mashirika makubwa kibiashara? Je, magereza yetu? Uhamiaji? Je, Matajiri wetu wanabebeka kimkakati? Mashirika yakaitwa ya private na yakaorodheshwa baadhi ya hisa zao katika Dar es Salaam Stock Exchange?
 
Serikali ya samia eti inatazama mashirika ya umma kama uwekezaji wa kibiashara ambapo serikali haistahili tena kuwekeza ila watu binafsi. Msimamo huo sio sahihi kwa sababu mashirika ya kibiashara ya umma yalikwisha binafsishwa yote tangu awamu ya mkapa. Yale yaliyobakia ni yale ya kimkakati kwa maendeleo ya nchi hayawezi kupewa watu binafsi.

Mashirika kama tanesco, TTCL, TRC, air tanzania, mashirika ya kuzalisha na kusambaza maji, TPA, etc etc. Ili mashirika ya kimkakati kua na tija na kufikia malengo ya uwepo wake lazima serikali iwe na utashi wa kuyasimamia vema.

Serikali inayoruhusu vigogo wake wale kwa urefu wa kamba zao kwa vyovyote itakua na muelekeo wa kuwaacha vigogo kupora kutoka mashirika ya kimkakati ya umma na hatimae kujidai kuyabinafsisha huku ni uporaji wa mali ya umma.

Hatuna haja kuonesha kwa nini mashirika ya kimkakati kwa maendeleo ya nchi yawepo. Na tukisema maendeleo ya nchi tunamaanisha maendeleo ya umma wa wananchi na sio tabaka fulani.

Tuliwahi kubinafsisha TRC, TTCL, na air tanzania na tulichokiona kama matokeo ilibidi kuyarudisha mashirika hayo mkonono mwa umma kwa maana ya kumilikiwa na serikali.

Reli tuliibiwa na wahindi mali zote zisizohamishika kama majumba na viwanja kwa maana walipiga hela wao na mwisho hadi karibu kuibiwa uwezo wa kujitegemea kwa wao kuanza kupeleka vichwa vya treni india kwa matengenezo ambapo karakana na wafanyakazi wenye ujuzi na uwezo walibakia kinywa wazi.

Kuhusu Air Tanzania vivyo hivyo makaburu wakatuadhibu vibaya.

Kinachotakiwa ni Samia kuwa makini na ajue sera na itikadi za CCM bado ni relevant asituchanganyie ulaji kwa urefu wa kamba wakati ni uporaji wa umma.

Kinachotakiwa ni usimamizi imara wa mashirika ya kimkakata na kuacha kufanya uteuzi kishikaji ambapo wapigaji na watu wasio na uzalendo kupewa kuendesha mashirika hayo.

Kuna tetesi kuwa hoteli zilizokuwa zinamilikiwa au zina hisa za serikali huko kwenye mbuga....
 
Ile ikulu pia ni taasisi ya kibishara, tumeishindwa, tuwape DP world waisimamie
Dunia ya kisasa inahitaji vichwa vyetu vifanye kazi kisasa zaidi. India wamewapa DP World bandari yao waiendeshe, ina maana na wao wameshindwa kujiendesha?, mbona wanatupa misaada ya sekta ya matibabu kila kukicha?.

Kuna utando wa ujamaa vichwani mwetu, tufanya kile tuwezalo tuuondoe ili tubakie watu wenye fikra huru.
 
Back
Top Bottom