MTANZANIA MWENZANGU IJUE VIZURI ( ESCROW)
Ndugu zangu watanzania napenda nichukue fursa hii niwakumbushe machache kuhusu hili sakata la Escrow maana tumedanganywa sana sasa tuseme inatosha maana ata vitabu vitakatifu vinaeleza bayana kwamba watu wangu wemeangamia kwa kukosa maarifa
Ndugu zangu ninavyojua bwana Rugemalira alikua mtanzania pekee aliyekua na haki katika fedha za Tegeta Escrow Kama mmiliki wa asilimia 30% za IPTL.
Akashawishiwa na serkali kumuuzia bwana Singa Singa kwa madai ya serkali ya awamu ya nne kwamba Singasinga ni mwekezaji mkubwa ataboresha mtambo, Rugemalira akakubali akamuuzia kwa makubaliano waliyofikia ya dola 75 million
Bwana Rugemalira akalipwa asilimia 10% na kuendelea kuisubiria asilimia yake 90% katika siku 60 kwa mjibu wa mkataba .
Cha ajabu sasa!!! Singasinga na washirika wake walikua hawana nia njema na Rugemalira na wala hawakua na mpango wa kumlipa hiyo asilimia 90% walichokua wanahitaji ni kumtumia Rugemalira kuzifikia pesa pale Bank kuu (B.O.T)
Kibaya zaidi Rugemalira anasubiria kulipwa pesa zake kumbe watu washabeba hizo pesa kutoka Bank kuu na kugawana wakiwa na mikokoteni, rumbesa na vifurushi pale STANBIC bank mimi nawewe tujiulize hii bank mbona watu hawaizungumzii na waliochukua pesa kwa mikokoteni, rumbesa n.k hawatajwi Zitto, Lissu na kafulila watwambie
Rugemalira kuona hivyo ndo akaamua kwenda mahakamani kushitaki nakumbuka aliwashitaki wafuatao:-
1. Gavana wa Bank kuu kwa kuruhusu kutoa pesa hizo
2.PAP
3.STANBIC kwa kupokea fedha hizo na
4.Bank moja ya wapakistani iliyopokea kiasi fulani Cha fedha hizo za Escrow
Hapa sasa ndugu zangu ndo kimbembe, fitini na paniki dhidi ya bwana Rugemalira kuona anaendelea kupambana kupata haki yake ndo zilianza, watu wakatengeneza chuki dhidi yake inasemekana walishirika wa singasinga walikataa kumlipa bwana Rugemalira na kupanga kumuondoa kwa njia nyingine wajuazo wao.
Lakini inasemekana Gavana wa benki akaogopa sana na kusema hawafikii popote na hiyo GRAND FRAUD kwa hiyo ni bora wakubaliane kumlipa Rugemalira haki yake ili mambo yaishie hapo.
Na ndo hivyo Rugemalira alivyolipwa fedha zake kwa amri ya mahakama ya tarehe 17/ 01/ 2014 ambayo hadi sasa imefichwa kwa siri kubwa je!! ?? Zitto kabwe na Lissu hawajui hili Mimi na wewe tujiulize na tutafakari kwa kina!!!??
Na katika hiyo furaha ya kupata fedha zake kutoka mikononi mwa wanyanganyi Rugemalira akaamua kutoa sadaka na mgao kwa watu mbali mbali wakiwemo viongozi wa serkali na dini akiwataka wafungue akauti benki ya mukombozi inayomilikiwa na kanisa katoliki je kuna kosa gani apo na pesa amepewa kwa amri ya mahakama kwa tafsiri nzuri hiyo pesa ni Mali yake.
Kibaya ni pale wanaoujua ukweli huu wanaamua kudanganya watanzania kwa kujipambanua na kusema waliopewe pesa na bwana Rugemalira ndio wezi kumbe waongo na wazandiki ukweli wanaujua na ndo maana Zitto alikataa kutia sahihi kwenye ripoti iliyowasilishwa bungeni na kamati sasa kwa nini asemi ukwelii!!! Mimi na wewe tujiulize!!??
Sasa hii ndo ngumu kumeza naomba Zitto na Lissu watutajie waliochukua fedha benki kuu na kugawana pale STANBIC wakibeba hizo pesa kwenye mikokoteni, rumbesa, vifurushi n.k ni akina nani hao tuwajue!!??
Vile vile niwape angalizo watanzania magazeti yasitupotoshe kazi kubwa kuandika waliopewa mgao na Rugemalira hii inaonesha watu waliohusika na kukwapua hizo pesa Bank kuu na kugawana pale STANBIC wanaendelea kujificha na kuhonga magazeti ili yaendelee kutupotosha watanzania alafu kwanini hii Bank ya STANBIC watu hawaizungumzii wakati hii benki ndo imehusika kutorosha pesa kutoka Bank kuu( B.O.T)
Mwisho nipende kumpogeza Raisi wetu kipenzi Cha watanzania hasa sisi maskini JPM kwa hizi hatua anazozichukua tunamshukru Mungu kwamba kupitia yeye tutayajua mengi na bahati nzuri JPM nimpenda haki sana na mwenye hofu na Mungu, Lissu anayejifanya kupinga kila kitu na kujiona yeye ndo mjuzi wa kila jambo mimi nasema kwa serkali hii tukufu atachelewa sana na unafiki wao ndo umefika mwisho hatudanyanyiki tena wanajifanya wanaguswa sana na hili swala kumbe nia yao ni kutupotosha watanzania
Mungu ibariki nchi yetu Tanzania
Mungu mbariki Raisi wetu JPM
Niwatakie siku njema
Magufuli Captain ( CCM mpya)
CCM Halisi kama kina Lusinde and Co.
Pamoja na hali hiyo pia aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), Profesa Mark Mwandosya, alipinga hatua ya fedha hizo kuitwa ni mali ya IPTL na kuhoji
inakuwaje kama fedha hizo zingekuwa mali ya mtu binafsi kwa nini ilikaguliwa katika vitabu vya BoT.
Profesa Mwandosya alimpa pole Zitto kutokana na makombora alitokuwa akirushiwa huku akimtaka kutokata tamaa na asimame imara kwani Taifa litakumbuka mchango wake siku moja.
Wakati akisema hayo
Lissu, alisema watu waliopewa fedha hizo ni wezi na hawastahili kutetewa kwani baada ya kuona kuna hatari ya suala lao kugeuka waliamua kugawa fedha kwa baadhi ya wabunge na watendaji wa Serikali.
Mbali na hao pia aliyekuwa Mbunge wa Nzega, Dk. Hamis Kigwangalla, alisema kuwa Profesa Muhongo, alikuwa muongo kwani imekuwa ni kawaida yake kutetea uongo mara kila wakati.
WALIOTETEA UCHOTWAJI FEDHA
Pamoja na Kamati ya PAC kuwasilisha ripoti yake juu ya suala hilo ambapo ilijiridhisha kuwa sehemu ya fedha hizo ni za Serikali, baadhi ya wabunge na mawaziri walipinga hatua hiyo na kusema kuwa fedha hizo hazikuwa za umma bali ni mali za IPTL.
Mmoja wa mawaziri waliosimama bungeni kutetea suala hilo ni aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ambaye alizungumza kwa kujiamini kuwa fedha hizo si mali ya umma.
LUSINDE
Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde (CCM), akichangia ripoti hiyo ya PAC bungeni, alisema hata Zitto ambaye ni mwenyekiti wa kamati alipokea fedha kutoka kwa Sethi.
“Zitto ni rafiki yangu mkubwa na aliwahi kunisaidia nilipokuwa na tatizo, lakini katika hili lazima niseme kwamba ulipokea fedha kutoka kwa Sethi, atupe jibu isije kuwa tunakaa hapa kumbe walaji wako wengi. Kwa nini Tibaijuka anapopewa inakuwa fedha haramu, lakini kwa Zitto ni halali?
“Na Zitto anahusika, Kafulila naye anakuja hapa ohh eti taarifa ya siri imevuja tujadili,
tujadili kwani ninyi Mungu?” alihoji Lusinde.
MOHAMED CHOMBO
Mbunge wa Magomeni, Zanzibar, Mohamed Chombo (CCM) alisema:
“Nimesikiliza ripoti ya PAC na Serikali, lakini jambo hili lipo wazi kwamba hizi fedha hazikuwa za umma, zilikuwa za IPTL zimelipwa na Tanesco.”
RICHARD NDASA
Mbunge wa Sumve, Richard Ndassa
(CCM), alisema kumezuka mtindo wa kusingiziana na kwamba wabunge wa aina wamwogope Mungu.
“Tusiwavunje moyo wizara, wamefanya kazi kubwa, tushauri pale kwenye tatizo tuseme sasa fukuza huyu halafu nini kinafuata?
“Tukiwa na utaratibu wa kufukuzana itaendelea hivyo hivyo, tumwogope Mungu, lakini nafsi zetu zitatusuta kwa sababu ya matendo yetu. Hivi sasa kamezuka mtindo wa kusingizia mtu huyu kala, huyu kapewa mtu akipewa asimame hapa aseme amepewa, lakini tusiwasingizie,” alisema Ndassa.
MARIAM KISANGI
Mbunge wa Viti Maalumu, Mariam Kisangi
(CCM), alisema
upinzani baada ya kuona kwamba chama tawala kinapeta wakaamua kuwakoroga na Escrow.
“Tuangalie utendaji wa watu na
ninawaambia hatoki Muhongo wala Maswi, CCM kitapita na hiyo ndiyo njama zenu upinzani kutukoroga. Mmekaa mkao na CCM inapeta, mkajisemea hawa tuwakoroge na nini ndio mkaja na Escrow mara EPA, nawaambia njama zenu hazisaidii.
“Zile fedha si za umma. Tanesco ina madeni mengi, inadaiwa Sh bilioni 700. Waziri ameeleza vizuri, kwa hiyo tusipotezeane muda hapa,” alisema mbunge huyo.
SIMBACHAWENE
Aliyekuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini na Mbunge wa Kibakwe,
George Simbachawene, naye alitumia mbinu zote kutetea ufisadi huo na wakati mwingine alijenga hoja ili watuhumiwa waweze kupenya.
Chanzo: Gazeti la Mtanzania.
Ndio maana mimi husema siamini katika CCM katika suala la maendeleo ya Tanzania ama dhati ya wao kushughulika na hujuma au ufisadi dhidi ya Taifa.