Mtangazaji Jonijoo atoka Wasafi FM/TV na kuhamia ETV/EFM

Jonijoo amekuwa branded na Wasafi na si Radio yoyote wala Youtube.

Umma wa watanzania walio wengi wamemjulia wasafi, anajadiliwa kwa sababu alikuwa wasafi vinginevyo hakuna ambaye angemjadili.
Binafsi nimemjua Jonijoo muda sana na mdogo wangu ameshafanya interview nae (ni mwanamuziki) ila kumjua kwangu kitambo hakuleti maana watanzania wengi walikuwa wanamfahamu tayari.

Mtu wa Kigoma, Mwanza, Tabora, Shinyanga, Mara, Katavi, Kagera, Singida, Dodoma, Moro town, Iringa, na hata Morogoro angemjuaje John na hasikilizi Radio?
Hiyo wasafi hii mikoa uliyoitaja hapa inasikika? Au unabwabwaja tu
 
We mdingi Ni wa ajabu Sana unachuki na mtu ambaye hata kuonana nae kwa ujawahi hiv nikuulize kipi kizuri kilichofanywa na diamond umawahi kutoa comment nzuri?
Punguza jazba alafu vumilia tu haya maswala ya watangazaji kuhama vituo yataendelea kuwepo usijipe vidonda vya tumbo maana tangu Jonijo kahama umegoma kunywa uji.
 
Wasafi ilianza vizuri lakini inaharibiwa na usajili..tengeneza base nzuri kwa kuwatumia wakongwe...radio ina shikwa na vipindi vikuu vitatu...Taarifa ya habari...Michezo..then Vipindi vya burudani...wanachokosea wasafi kwanza sina uhakika kama wanae program manager mwenye anayefit nafasi hiyo..kama yupo basi anakosa ubunifu..ukishapata wakongwe watatu kwenye vipindi mhimili hivyo vitatu...then tafuta vipaji vipya ....lipo tatizo jingine lq media za bongo kuigana kwa kila kitu..huwa tunaigana timing ya muda wa vipindi ili kugombania wasikilizaji au watazamaji lakini watangazaji wengi wanaiga mpaka contents za redio au tv shindan mwisho wa siku vipindi vinapyaya vinakosa mvuto..unakuta mtangazaji anataka kuiga mpaka sauti ya mtangazaji wa redio shindani au tv ni ujinga..ubunifu ndo silaha kubwa

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii nimeiona America kwenye kila kitu.
Hautengenezi kipindi eti ili kionekane ni idea mpya no ile ni investment inapaswa kulipa.

Hadhira ya media za Tz kubwa ni vijana uwawekee bakurutu kama Radio one they won't listen, uwawekee singeli wasukuma, wagogo, na wanyakyusa they won't waste their precious time.

CMG wanachokifanya ndicho Tz kinapendwa kwa asilimia kubwa, kuna Radio inaitwa Miami Radio hii vipindi vyake ni sawa na kusikiliza Radio yoyote nyingine ila wanazidiana majonjo tu.

Content haziigwi ziko hapo miaka na miaka kipindi na zinafundishwa darasani.
Kwenye Ubunifu hapa you got a point
 
Hongera Jonijo,

Kuondoka kwako kuna watu wamepata homa ya mapafu,
Lol.

Corona Virus: Stay Home the only Medicine found.
 
Hahaha mkuu sijui umesoma shule gani kwamba umaarufu wa mtu(mfanyakazi)unazidi umaarufu wa kampuni duuh?
Media kwa kipindi hiki zinaitaji mapresenter wazuri mfano mzr nazitaja radio mbili tu RFA na ebony ya iringa watangazaji wazr walivo ondoka na zenyewe zimefifia
Ukiwa under 23 huwezi elewa ninajosema
Ukubwa wa media unachangiwa kwa kiasi kikubwa na watngazi wano wamiliki
Kwa hili haliitaji bachelor niakili ndogo tu inayo itajika
 
Media kwa kipindi hiki zinaitaji mapresenter wazuri mfano mzr nazitaja radio mbili tu RFA na ebony ya iringa watangazaji wazr walivo ondoka na zenyewe zimefifia
Ukiwa under 23 huwezi elewa ninajosema
Ukubwa wa media unachangiwa kwa kiasi kikubwa na watngazi wano wamiliki
Kwa hili haliitaji bachelor niakili ndogo tu inayo itajika
Mimi sio under 23, mkuu hakuna mtu anaweza zidi umaarufu taasisi au kampuni refer David Beckham, enzi za Man U, lakini hadi leo Man U ipo, sasa Radio haiwezi kufa kisa mtangazaji ameondoka mfano dhahiri ni EAST Africa radio watu wengi sana wamepita EA radio na walikua na majina lakini bado kituo kinasonga mbele tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom