Oscar Oscar atua rasmi Wasafi FM

Zawadi B Lupelo

JF-Expert Member
Jul 19, 2015
2,549
3,722
IMG_7307.jpeg


Aliyekuwa Mtangazaji wa EFM Oscar Oscar AKA mzee wa Kaliua ametambulishwa rasmi Wasafi FM ambapo sasa atakuwa na kipindi chake kitakachokuwa kinaitwa Jana na leo, kikiruka muda uliokuwa wa kipindi cha Mgahawa yaani siku za wiki kuanzia Saa 11 jioni hadi Saa 2 usiku
 
View attachment 2633477

Aliyekuwa Mtangazaji wa EFM Oscar Oscar AKA mzee wa Kaliua ametambulishwa rasmi Wasafi FM ambapo sasa atakuwa na kipindi chake kitakachokuwa kinaitwa Jana na leo, kikiruka muda uliokuwa wa kipindi cha Mgahawa yaani siku za wiki kuanzia Saa 11 jioni hadi Saa 2 usiku
Sijaelewa. Kwahiyo kile kipindi cha Mgahawa kinaondolewa au hichi kipindi kipya cha Oscar kitakuwa weekend tu ?.
 
Oscar Oscar,Kitenge na Gerald Hando hawa ni wafanyakazi watiifu wa EFM, mda wowote wanaweza kurudi walipotoka. Nashanga kuona kipindi cha Mgahawa kimeondolewa, Yani badala ya kumtoa baba Revo wao wanakifuta kipindi kizima. Ujinga mtupu.
Maulid kitenge huo utiifu hana time nao,Hando hakupenda kuondoka EFM ila Majizo kwa kujishtukia kwake ndipo kumemfanya Hando aondoke kwani alishindwa kumtetea, halafu ile issues hata walisokosolewa na Hando (tena jamaa alitumia maneno ya kawaida) hawa kireact bali kujishtukia kwake labda kwa Oscar.

Sasa hivi kamuweka yule Madenge jamaa anaibuaga mijadala mizito ya kukosoa na hata comments zake tweeter zinakuwaga za moto,sasa sijajua na huyu atamfunga speed gavana maana Madenge anapenda kuwa free.

Halafu watangazaji kuondoka ni kitu cha kawaida, cha msingi ni kutengeneza misingi ya kuandaa wengine au kama una mzigo na ww unaenda kumvua mwengine na ndivyo hata kampuni za simu zinafanya hivyo.
 
Kipindi cha mgahawa ndio kipindi kizur sanq kwa Wasafi.

Baba Levo kajitahidi sana kuweka ucheshi, yule jamaa elimu hana ila anajua kuongea ukweli hasa ktk mada zilizonyooka.

Kuondoa kile kipindi kitashushq brand sana unless huyu mpya awekeze nguvu ktk ubunifu zaidi.
Kile kipindi cha Mgahawa bila Baba Levo kilikuwa kimepooza sana

Huyu jamaa wangemuongeza palepale kwenye Mgahawa awe na Baba Levo, Sekioni David na yule Adela Tillya

Ngoja tuone labda kimebadilishwa jina tu
 
Back
Top Bottom