kwa upole sana
Member
- Feb 4, 2017
- 64
- 81
Daa leo naenda fanya utalii wa ndani temeke, mpaka nijue hayo maeneo yote korofi
Cha msingi walipe kodi tuu
Yeshata kama wanavunja sheria???
c kweli hayo mambo zamani sana ila sasa hv yamepungua sana kiukweli miaka ya 2003 to 2014 palikua hapafai ila nowdays yamepungua Sanaa yapo ila kwa uchache sana. temeke wailes ,mtongani ,mitaa ya kombora,kwa aziz ali ,kwa kabuma ,kitomondo,dabo kibini.Ukifika Temeke kuna mtaa unaitwa Mji mpya ndani yake kuna kamtaa korofi kanaitwa KINDANDE.
Kindande kuna maskani maarufu inaitwa Lebanon.
Huu mtaa kwa kindande ni mtaa ambao unaogopeka kupita bila taadhari kwa saa 24..Mambo yote maovu yapo hapo kuanzia wizi kukaba mchana umalaya uvutaji bangi ulio kubuhu.
Katika maisha yangu yote sijawai kuona wanawake wanavuta bangi kupita wanaume ni mewaona kwa Kindande.
Mabinti wa kwa Kindande wanatabia ya kukaa nje wakikuomba hela ukakataa kutoa hayo matusi yake ni balaaha.
Mabinti wa kwa Kindande wanaongoza kucheza vigodoro wakiwa uchi sometimes wanakodishwa kwenda kusasambua kwenye vigodoro vya majirani zao Mtongani,Tandika,Wailes, na Mbagala.
Hawa mabinti wana tabia ya kukodi boda boda usiku mishale ya saa 7 usiku na kuendelea wana tegesha sehemu za starehe ukijiroga ukampakia mkifika tu kwa Kindande kuna makaburi mitaa hiyo litakuja kundi litakupiga piki piki inaondoka.
Kwa Kindande ukimpenda demu ukichepuka kazi unayo utapigwa na kundi lake plus matusi juu hila yeye kuchepuka ruksa.
Wana maskani yao inaitwa Lebanon hiyo na polisi ni kufukuzana kila siku hapo unawapata madogo wa miaka 12 waliopinda wapiga bangi hatari.
Huku unakuta dogo naye ni baba vibinti vidogo navyo ni single mother.
Huu mtaa unaongoza kwa matusi kwa lika zote hakuna heshima kwa mkubwa wala mdogo.
Hiki kimtaa kimepakana na Tandika Kwa Aziz Ally Temeke mwisho na Mtoni mtongani.
Kama sio mtu wa vulugu usipange mtaa huu...
sana sana kile kituo ni cha kishenzi wamekaa kirushwa rushwa.Tandika kilimahewa ni habari nyingine mkuu, nadhan huijui vzr bado.
Sent using Jamii Forums mobile app
Yah, upo sahihi kwa 100%! Enzi kwa Kindande pako moto hata kwa Azizi Ally pale kituoni kupita usiku ni hadi uwe mwenyeji... enzi Kilwa Rd ni barabara moja iliyojaa mashimo kibao, na kituoni kwa Azizi Ally full vibanda!! Ile Madafu yenyewe ilikuwa full utata! Ukienda Sifa, kwa Kabuma, Relini taabu tupu. Temeke Mwisho yenyewe unaibiwa mchana ng'ombe anakula majani..c kweli hayo mambo zamani sana ila sasa hv yamepungua sana kiukweli miaka ya 2003 to 2014 palikua hapafai ila nowdays yamepungua Sanaa yapo ila kwa uchache sana. temeke wailes ,mtongani ,mitaa ya kombora,kwa aziz ali ,kwa kabuma ,kitomondo,dabo kibini.
Kile kituo kila muhuni ana afande wake.sana sana kile kituo ni cha kishenzi wamekaa kirushwa rushwa.
Siku nyingine kama una hela tafuta mabosi wao (lazima kunakuwa na mabosi ambao ni wazoefu)wape ofa!!! Umemaliza kazi. Utalindwa na kupewa dili mbalimbaliUsipo wapa ushirikiano uswazi utaiona ngumu
"Hakuna Muhuni Ambae Hana Utu"Mwaka 88 baada ya kupata kazi idara moja ya serikali nilipata chumba maeneo ya Manzese Midizini, wezi wote wa kwenye mitumba walikua wanakaa midizini. Nilikua nikirudi saa kumi sitoki ndani mpaka kesho yake kwa kuogopa vibaka. Siku moja kaja dogo mmoja kuniambia, shoferi usipende kukaa ndani kama dem. Njoo nikuyembeze. Basi nikatoka nae break ya kwanza kwenye banda la gongo. Enzi zile kituo cha polisi cha karibu ni urafiki. Basi nikaagiza kijeti kilipoisha nikaagiza cha pili. Wahuni walikunywa mpaka wakasema shoferi basi. Kuanzia hapo niliyembea Manzese yote mida yoyote bila kuulizwa na mtu. Ila wakikuomba kistaarabu kifanta au fegi wape tu. Nikaja kugundua kwamba kumbe hakuna mhuni ambae hana utu.