Ndugu yangu Mleta mada angalia tena vyanzo vyako vya habari kuhusu Kifo cha Marehemu Sokoine,Hizi taarifa unaloleta humu zinasababisha usumbufu kwa baadhi ya ndugu na jamaa wa Marehemu na sisi wengine ambao tunawafahamu hao Wazee wote na utumishi wao Serikalini.Jioni ile ya Jumatano,April 12/1984 pale Wami-Dakawa katika wilaya ya Mvomero,Mzee Sokoine alikufa katika ajali ya kawaida kabisa ya gari? Nasema hivi kwa sababu tulikuwa katika msafara ule.Kulikuwa na makosa yaliyofanywa na gari lililokuwa linakuja upande wa pili,ambalo lilikuwa linaendeshwa na Mkimbizi Dumisani Dube.Gari hilo liliserereka na kugonga gari la Waziri Mkuu,Upande aliokuwa amekaa Sokoine,na wakati huo inasadikiwa Marehemu alikuwa amelala.Mara tu baada ya ajali ile Mkimbizi yule alishikiliwa na vyombo vya usalama.Marehemu Sokoine aliiingizwa kwenye gari Jingine na kukimbizwa Hospitali ya Mkoa,Morogoro mjini.Hakuna aliyeweza kusema pale kwenye ajali ambayo ilitokea saa 10 jioni kama Waziri Mkuu alikuwa Hai au Amekufa.Habari za kifo zilithibitishwa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro na maelezo yake yalisema Waziri Mkuu alifariki kwenye ajali.
Hizi habari unazoziandika hapa kwamba Mzee Msuya anahusika kwa namna moja ama nyingine hazina ukweli wowote.Marehemu Sokoine alifariki katika ajali ya barabarani.Kuandika habari kama hii unaleta sintofahamu,umemuhusisha Mzee Msuya na tukio jingine la kupotea kwa secretary wake karibu miaka 30 iliyopita,siwezi kulisemea hilo kwa sababu ni mara yangu ya kwanza kulisikia.Lakini naomba usielekeze tuhuma hizi nzito kwa sababu tu ya misimamo tofauti ya Kiitikadi.Mzee Msuya kama wewe anaweza kusema lolote kuhusu hizi harakati za baadhi ya Watanzania kuwania nafasi ya Urais, hana upendeleo wowote kwenye mchakato huu,mwisho wa siku ana kura yake moja tu.Nipo wazi kukosolewa lakini nimeamua kuandika hili kwa makusudi ili tusiifanye forum kama kijiwe cha kuchafua Watanzania wenzetu!