Msuya atueleze aliko Sokoine

Msuya atueleze aliko Sokoine

Nafikili wakina msuya mtakuwa mnawaonea. Muulizeni aliyekuwa raisi wakati ule.ndiye mwenye mujibu. Kwani kama Msuya alishiriki kwanini hakuadhibiwa na raisi wetu mpendwa wakati ule. Au kwanini uchunguzi haukufanyika kwa amri ya raisi wa wakati ule. Raisi ndiye top wa kila kitu.
 
Hivi mnafaamu Imran Kombe the late and former Intelligence Chief.? R.I.P SOKOINE.
 
mzee wako alichukiwa na kinana kwa rushwa zake akamuanzishia skendo ya tembo,,sasa naona baada ya mzee msuya kuusema ukweli mmemuanzishia ya sokoine,,, eti dawa kuwafunga watu midomo wasimguse mzee ambae ni mgonjwa,,,,kazi mnayo kuuza nyanya mbovu itakaaa kwenye friji hadi lini?? nasikia ata kamba za viatu haoni hadi avalishwe
 
Karibia na uchaguzi mkuu mwaka 2010, Jenerali Ulimwengu alipata kuandika kuwa tunapoelekea uchaguzi mkuu tutarajie mengi. Watu wenye heshima zao ndani ya jamii na elimu isiyo na shaka watasimama na kuongea mambo ya hovyo kabisa kuliko neno lenyewe "hovyo" linavyomaanisha. Si kwamba hatakuwa hawaelewi kuwa wanaongea upuuzi, bali watafanya hivyo ili kutimiza haja za matumbo yao.

Alilolisema Jenerali Ulimwengu takribani miaka mitano iliyopita linajirudia leo! Watu wazima wanaongea upuuzi tu bila kujali chochote! Huyu anaongea hili yule anaongea lile yaani ujinga ujinga!

Wewe uliyeleta huu uzi bila shaka unatumia kiuno kufikiri na kama si hivyo basi tumbo lako ndilo linalokuongoza kuleta huu uozo! Sokoine kafariki lini? wakati wote huo ulikuwa wapi kuiibua hii hoja yako? Mnapenda kuleta viroja kujibu hoja nzito. so hutaki Msuya akemee ufisadi? Unataka kumchafua Msuya kisa anakemea ufisadi wa bwana wako? Mlimchafua Salim Ahmed Salim na sasa mnamchafua Msuya!

Mnapokosa hoja tulieni na sio kuleta vioja.
Mbona povu linakutoka hivyo! Wewe kaa pembeni mwache Msuya aeleze anachokielewa kuhusu kifo cha Sokoine.
 
Binafsi huwa sina tabia ya kutetea majitu kama Msuya. Usimpuuze anayemhoji huenda anafahamu zaidi yako maana Msuya kweli amejaa upuuzi tu. Mwizi, fisadi wa kueleweka.

labda anadhani wanaofahamu undani wake ni marehemu. Tupo na tunamfahamu kwa upuuzi wake.
Secretary wa Msuya, dada mmoja wa Kipare, alikuwa bado kijana tu, akisali pale Temeke Luth Church.
Dada huyu alikuwa na pacha mwenziwe, ALIPOTEA na asionekane tena katika uso wa dunia.
Sasa ni zaidi ya miaka 30 dad huyu hajaonekana.
 
Secretary wa Msuya, dada mmoja wa Kipare, alikuwa bado kijana tu, akisali pale Temeke Luth Church.
Dada huyu alikuwa na pacha mwenziwe, ALIPOTEA na asionekane tena katika uso wa dunia.
Sasa ni zaidi ya miaka 30 dad huyu hajaonekana.

Unataka kutuambia ni sahihi kwa Msuya kwa vile alivyoitwa "kidole cha damu"?
 
Uanjua watu wanasemaga vitu bila kujua kuna siku vitakuja kuleta maswali.

Kama kuna mtu anasema Sokoine alikuwa akiwa njiani kuelekea Morogoro, nani alithibitisha kifo cha Sokoine? Kulikuwa na Daktari kwenye ile gari aliyempima na kujua alifia njiani wakienda Morogoro?

Nini ilikuwa sababu ya kumpitisha Morogoro Regional Hospital Ikiwa walikuwa wanajua alifilia njiani hata kabla hajafika Morogoro?

Ni vizuri wakanyoosha maelezo.

Ninachokifahamu mimi, waliompeleka Hospital ya Morogoro walikataa asipimwe kwamba alishakufa. Ni jambo dogo lakini ni vizuri kuliangalia kwa upana. Pale Morogoro hakuna Daktari alimpima Sokoine kuthibitisha amekufa ama la. Dr. Materu, aliyekuwa zamu pale, aliye wapokea hakuruhusiwa ampime.

Kama ni report iliandikwa ilikuwa ni kwa formalities na kutokana na maelezo waliyokuwa wanayapata.

Ninaogopa kusema zaidi kwa hofu ya kuambiwa naandika uchochezi.

Imetosha.
Kwanini sasa "nduguzetu" walimbeba Prof Shaba kutoka New Africa Hotel kumrudisha kwake chapchap baada ya kunywa whisky na kuanza kusema "Sokoine hakufa kifo...alikuwa na matundu ya..."
Searching....
 
Uanjua watu wanasemaga vitu bila kujua kuna siku vitakuja kuleta maswali.

Kama kuna mtu anasema Sokoine alikuwa akiwa njiani kuelekea Morogoro, nani alithibitisha kifo cha Sokoine? Kulikuwa na Daktari kwenye ile gari aliyempima na kujua alifia njiani wakienda Morogoro?

Nini ilikuwa sababu ya kumpitisha Morogoro Regional Hospital Ikiwa walikuwa wanajua alifilia njiani hata kabla hajafika Morogoro?

Ni vizuri wakanyoosha maelezo.

Ninachokifahamu mimi, waliompeleka Hospital ya Morogoro walikataa asipimwe kwamba alishakufa. Ni jambo dogo lakini ni vizuri kuliangalia kwa upana. Pale Morogoro hakuna Daktari alimpima Sokoine kuthibitisha amekufa ama la. Dr. Materu, aliyekuwa zamu pale, aliye wapokea hakuruhusiwa ampime.

Kama ni report iliandikwa ilikuwa ni kwa formalities na kutokana na maelezo waliyokuwa wanayapata.

Ninaogopa kusema zaidi kwa hofu ya kuambiwa naandika uchochezi.

Imetosha.
vifo vingi ktk jamii za ki Africa hata kwenye ngazi ya kaya au familia zinakuwa na hisia au imani za ajabu ajabu hasa kwa watu kama wewe na mleta hoja. Hata mtu muone anaumwa EBOLA mtasena alikuwa na ugomvi na fulani. HEBU TOKENI HUKO JAMANI. Tupo ulimwengu mwingine sasa
 
Mwili wa marehemu kufanyiwa ama kutokufanyiwa uchunguzi, nalo ni swala la imani kiongozi?

Tafadhali tofautisha imani, ambayo ni hakika ya mambo yatarajiwayo na bayana ya mambo yasiyoonekana, na swala halisi kama la kupima ama kutokupima kama mtu kafa ama yuko hai. Hapo kweli kuna imani?

Please be realistic!.
 
Tunapokaribia kuadhimisha miaka 30 tangu kilipotokea kifo kilichojaa utata cha aliyekuwa Waziri Mkuu Ndg.Edward Moringe Sokoine,ni wakati mwafaka sasa kumhoji Mh.Cleopa Msuya juu ya tuhuma za kuhusishwa na kifo cha Mh. Sokoine;kwa sababu Mh. Msuya kwa siku za karibuni amejitokeza kukemea maovu mbalimbali yanayofanywa na viongozi wa CCM bila shaka pia atakuwa na ujasiri wa kujitokeza na kutolea ufafanuzi wa tuhuma hizi.

Mnataka kuuleta yale mambo yenu ya kupakazia kama mlivyo mpakazia salimu ahmedi alimua karume.
 
Ndugu zake Sokoine kina nani waliombeba Prof Shaba kutoka New Arusha Hotel?

Mimi ninajua Sokoine hakuwa na ndugu wa kwenda kustarehe New Africa Hotel. Wote walikuwa pale msibani including watoto wake, Joseph and Lazaro, na ukoo wote. Hadi yule ngombe mwusi anachinjwa, wanapaka mafuta yake mwili yake, hatukuwa na ndugu yake anakaa New Africa anaitwa Profesa Shaba 1984.

Nilikaa pale Munduli juu Mwezi mzima baada ya mazishi kabla sijaenda Munduli jeshini.

Naomba kama kuna point sijakupata nielewshe.

Kwanini sasa "nduguzetu" walimbeba Prof Shaba kutoka New Africa Hotel kumrudisha kwake chapchap baada ya kunywa whisky na kuanza kusema "Sokoine hakufa kifo...alikuwa na matundu ya..."
Searching....
 
Mtu kufa kwa risasi nayo ni imani ya kiafrica? mbona naona unataka kuutumia vibaya uafrica?

Hallucinations ni za kiafrica?

Mtu kupatwa na hallucinations akatafuta njia za kumfanya a relax no matter ni za namna gani nao ni uafrica?

Taratibu kiongozi.

vifo vingi ktk jamii za ki Africa hata kwenye ngazi ya kaya au familia zinakuwa na hisia au imani za ajabu ajabu hasa kwa watu kama wewe na mleta hoja. Hata mtu muone anaumwa EBOLA mtasena alikuwa na ugomvi na fulani. HEBU TOKENI HUKO JAMANI. Tupo ulimwengu mwingine sasa
 
Mtu kufa kwa risasi nayo ni imani ya kiafrica? mbona naona unataka kuutumia vibaya uafrica?

Hallucinations ni za kiafrica?

Mtu kupatwa na hallucinations akatafuta njia za kumfanya a relax no matter ni za namna gani nao ni uafrica?

Taratibu kiongozi.
Ukiambiwa uthibitishe kuwa mwili ulikuwa na matundu ya....utakubali!!? Au wewe ndiye ulihusika kwenye Postmortem. Halafu Je mlikuwa wapi kumuuliza Julius maana ndiye alikuwa Mkulu kabisa. Je ni nani alikuwa IGP, Intelligence chief , Home Affair minister nk.
Nasema mna imani za kichawi kwa kuwa kati ya hoja zenu eti kwavile alikuwa anapata mauzauza.!!! Sasa hii inahusika vip.!!!? NDIO MAANA NASEMA TOKENI HUKO kwenye fikra za ajabu ajabu.
Otherwise mpo hapa KISIASA ZAIDI. but be very careful unapoamua kumchafua mtu huwa inarudi na wewe ipo siku utahusishwa na kifo cha mtu hata kama hujahusika. ACHENI SIASA MAJI TAKA
 
Jamani ninahitaji kupata hotuba za Sokoine (R.I.P).Ziwe za. Audio, video , ama maandishi. Hotuba 15 za mwanzo kila moja nitailipia 20000. Malipo yatapitia kwa Invisible. Nichukue furusa hii kumuomba Invisible kulishughulikia hili.
Utaratibu, Tuma hotuba hiyo kwa Private message kwa kutumia account yako Ya JF kwa Invisible. Na mimi nikapata hotuba hiyo kupitia kwake. Nitakuwa nalipa kwa idadi ya hotuba nitakazopokea. Itakuwa kuwa vizuri zikipatikana za audio au video. Nimeamua zipitie kwa Invisible kwa ajiri ya kuzihakiki kama ni fake ama genuine.

Hotuba hizi nitazitoa hapa JF moja baada ya nyingine kwenye ule mwezi wa kumbukumbu ya kuzaliwa (siyo kufa ) Edward Moringe Sokoine.
 
Last edited by a moderator:
Nakumbuka kwenye kipindi cha majira (RTD) tarehe 10/4/1984 - siku mbili kabla ya Sokoine "kuuliwa", Ben Kiko aliripoti kuwa Mh. Sokoine alitamka hivi (kwenye kikao cha CCM) :-

"...Na wale Ma-Padri tuliowakamata kwenye uhujumu uchumi tutawapeleka kwa Baba Askofu wao... pia kikao kijacho tutawawajibisha viongozi wa juu wa chama na serikali ambao watabainika kuhusika na uhujumu uchumi..."

Siku mbili baadaye... Sokoine was GONE...GONE Forever....!

Kwa wale ambao mlikuwa hamjazaliwa:-

nashukur sana kwa kunipa uelewa
 
Secretary wa Msuya, dada mmoja wa Kipare, alikuwa bado kijana tu, akisali pale Temeke Luth Church.
Dada huyu alikuwa na pacha mwenziwe, ALIPOTEA na asionekane tena katika uso wa dunia.
Sasa ni zaidi ya miaka 30 dad huyu hajaonekana.

taarifa gani ilitolewa kupotea kwa binti huyo? au aliuawa au unadhan kitu gani kilimtokea huyo secretary
 
Back
Top Bottom